Muziki: Happy Birthday Nyagei
...nimeiona humu ndani na kwa vile
Nyagei ni mtaasisi mwenzangu, nimeiona isiwe shida nikitumia kipengele hiki kumtakia hongera nyingi wakati anapokumbuka tarehe ya leo miaka anayoijua yeye alipozaliwa. Leo ni siku yako mdau na hongera sana. Ujue wewe ni mtu mzuri sana na unaposheherekea leo basi jua kabisa KF iko pamoja na wewe.
Jamani tusimsumbue Nyagei, leo yupo kwenye siku yake ya mwezi wa december. Hongera zaidi kwa wote ambao mnaona siku zenu mwezi wa 12. Siandiki mengi kwako maana kwanza kabisa najua, ulituweka wazi humu kuwa muziki unaopenda ni wa Jazz na George Benson ni mwanamuziki unayemfurahia, hongera tena na tena.
Muziki sasa, kusindikiza Birthday ya mdau mwenzetu tundomboleke na kisha tutulie kwa jazz
Happy bord-date Nyagei, Jukwaa hili ni zuri sana kwa kuwa wewe upo hapa
na huyu ni GB unayevutiwa naye zaidi