BlessedHope
JF-Expert Member
- Jan 29, 2016
- 7,988
- 32,649
KWA UNAYESIKIA UMEVUNJIKA MOYO,KWA USIKIAE KUWA NA MZIGO MZITO KWA MAPITO YAKO YALIYOSABABISHWA LABDA NA UNYANYASAJI FULANI,YAKABIDHI KWA MUNGU MKUU UPATE SULUHU LA KUDUMU;YAKABIDHI HAYO KWA KRISTO YESU AKUSAIDIE;
Mathayo 11:28.
28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
MTAFUTE MUNGU,
Zaburi 34:4-5.
4 Nalimtafuta Bwana akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote.
5 Wakamwelekea macho wakatiwa nuru, Wala nyuso zao hazitaona haya.
MTWIKE YEYE FADHAA ZAKO ZOTE(YAKUSUMBUAYO);
1 Petro 5:7
7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
MTEGEMEE MUNGU PEKEE(MUNGU WA AMANI);
Isaya 26:3-4.
3 Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea Katika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini.
4 Mtumainini Bwana siku zote Maana Bwana YEHOVA ni mwamba wa milele.
USIZITEGEMEE AKILI ZAKO;
Mithali 3:5-6.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6 Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.
MTUMAINI MUNGU;
Zaburi 42:11.
11 Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.
UBARIKIWE,
Shalom.

