MKE JEURI
(The Wife's Tyrant)
Sehemu Ya 38..... MWISHO
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←
"boss.... Kumbe ulikuwa na tatizo kubwa la kifamilia na ulikuwa kimya tu"
Aliongea saidi huku akiwa anaendesha gari
"saidi.. Katika dini yangu ya Kiislamu hua hairuhusu mwanandoa yeyote kutoa siri ya kifamilia... Na ndio mana nilikuwa msiri sana"
"kumbe ndio mana kila mara ulikuwa na mawazo kazini"
"aahhh yote ni maisha tu.. Na kikubwa ni kwamba nashukuru kila mtu keshalijua hili"
Sheby na wafanyakazi wake walifika kazini na kuendelea na kazi, ikiwa ni bado mapema sana....
"enheee tuendelee na maongezi yetu boss"
Alikuwa ni saidi akiwa na boss wake ofisini,
"ivi tulikuwa tunapiga story gani vile"
"ahahahah mambo ya wake"
"aahhh tuachane nayo hio mada... "
Sasa wakiwa bado wanaendelea na stori, ghafla simu ya sheby ikaingia meseji, akatoa simu mfukoni kisha akaifungua ile meseji, ilikuwa inatoka kwa mke wake...
"sheby mume wangu... Siwezi kuishi na hawa watoto... Ni aibu kubwa sana nimeona bora nife nao pamoja, ni watoto wangu wacha nife nao.. Usikose kuja kutuzika"
Heee sheby alitoa macho baada ya kusoma hio meseji...
Mara moja alimpigia simu,... Lakini simu iliita mpaka ikakata. Akarudia tena kwa bahati nzuri ikapokelewa
"halooo mwai, unataka kufanya nini"
"ndio hivyo... Siko tayari kulea vilema... Naomba uchague moja.. Niwapeleke hawa watoto kwa baba yao, afu nirudi tuendeleee kuishi kama kawaida... Au nife na watoto wangu uje kutuzika tu"
ENDELEA.......
Kijana sheby alishtuka sana kuskia hivyo, na pia alihisi labda ni utani wa mwai, na asingeweza kufanya hivyo katika maisha yake hivyo hata sheby kushtuka kwake ni kwamba anamjua mwai kwa jinsi anavyo yapenda maisha ya kidunia, ni ngumu kufa na wale watoto
"wewe mwai wewe usifanye hivyo.. Na duka lako la lipstick utamwachia nani"
"sheby mume wangu, naomba usilichukulie jambo hili kuwa mzaha, mimi sipo tayari kulea watoto wa aina hii... Mimi nimekamilika itakuwaje marafiki wa familia yangu wakigundua mimi nimezaa vilema"
"lakini ni watoto wako hao.. Muite baba yao mkae chini myajenge, na kama hana uwezo wa kuwatibia au kuwalea, mimi nitawalea hao watoto, kikubwa tu akubali"
"na akikubali mimi narudi kwenye ndoa yangu,.. Mimi bado ni mke wa mtu"
"kama nitakuwa na akili finyu we rudi, lakini kama akili zangu ni timamu, basi kuendelea na wewe kuwa mke wangu sahau"
Sheby aliongea hivyo kisha akakata simu,...
Wakati huo sasa huku kwa mwai baada ya sheby kukata simu, mwai katafuta jina la jemsi na kumpigia, mana anajua hawezi kuruhusiwa kutoka na hali ya uzazi aliokuwa nayo, alimpata jemsi mwenye hao watoto kisha akawa anaongea nae kupitia simu
"baby... Hivi una taarifa gani wewe"
"taarifa.... Sina taarifa yeyote ile"
"beibeee... Una watoto wawili mapacha"
"Weeeeeee, acha utani baby"
"heeee njoo home uwaone"
"heeeee nije kwenu? Na wazazi wako watanionaje"
"heeeee jemsi, ama kweli wewe huna taarifa,.. Mimi nimeshaachana na yule bwege, na sasa hivi wazazi wangu wanajua kuwa baba wa watoto ni wewe,.. Na licha ya hivyo wenyewe wanatamani wakuone"
"weweeeeee mwai acha utani lakini"
"we njooo... Tena njoo sasa hivi"
"sawa basi nakuja"
"ok poa... Usije ukaacha kuja mana hawa watoto wakikuwa afu wazazi wangu hawakujui hutokaa kuwaona na usijijue kama una watoto kwangu"
"nakuja mama watoto wangu"
Jemsi alifurahi sana kuskia mpenzi wake kajifungua watoto mapacha,.. Sasa kumbe mwai kacheza tu kamchezo cha kumuita aje amshikishe watoto wake,
"mama... Yule mshenzi anakuja, naomba akiingia tu milango ifungwe apewe watoto wake"
Aliongea mwai huku akiwa na watoto wake tena kawafunga vizuuuri kabisa wanaonekana sura tu, hivyo hata jemsi akija hawezi kujua chochote kile juu ya watoto hao
"ivi mwai mwanangu, we ulizani ni rahisi mtoto wa kiume kukaa na watoto wadogo kiasi hiki"
"mama atajua mwenyewe huko... Mimi akija hapa nampa watoto awabembeleze huku tukitoka nje, akitoka tu tufunge geti"
"hapana, kwa hali hii hawa watoto hawatokuwa... Kiukweli hata mimi roho ya imani imenijia, na najuta ni kwanini nilowafukuza wale vilema siku ile... Kweli waswahili walisema usitukane mamba ingali hujauvuka mto,.. Tuliwafukuza wale vilema ingali we una mimba..."
"lakini mama, ile sherehe ilikuwa haiwahusu, walifuata nini na ile sherehe ni watu wenye hadhi yetu, mimi bado sijaona kosa lolote lile"
"ivi unajua kuwa sheby mume wako ndio aliwaleta wale watu"
"ati nini"
"tena baada ya kuwafukuza yeye aliwapeleka hotelini na kuwapa mikuku"
"lakini yeye kawatoa wapi"
"si huko barabarani"
Baada ya siku hio kupita, leo ni siku nyingine tena, kijana sheby akiwa nyumbani kwao na wazazi wake wakiwa wanashauriana jambo fulani,
"kiukweli mwanangu nakupa pole sana kwa yaliokukuta ndani ya ndoa yako, nisamehe sana baba"
"lakini baba, kwanini ulifanya hivyo na kunifanya nikose raha siku zote hizo"
"mwanangu sheby.... Huijui siri kubwa ya maisha yangu ila leo wacha nikuambie ili ujue sababu ya kukulazimisha umuoe binti wa Mohamed,... kabla hujazaliwa wewe mimi nilikuwa maskini wa kutupwa,.. Nikiwa na mama yako huyu, na dada yako huyu akiwa kadogo sana,... Mtoto anahitaji kula, mimi sina kazi wala kibarua chochote nilichokuwa nategemea,.. Nilikuwa natamani nipate hata kazi ya kulipwa elfu hamsini kwa mwezi, lakini pia nilikosa ningelipata wapi,.. Miaka hio niliadhilika sana baba yako nikiwa katika jiji hili hili la Arusha... Kwa bahati nzuri bwana Mohamed alihamishwa kikazi kutoka jijini Dar es Salaam kuja arusha,.. Na kazi aliokuwa akifanya ni kazi ya heshima na alikuwa akilipwa kiasi kikubwa cha fedha, mimi nilikuwa simjui hata chembe, lakini siku anahamishwa mimi ndio nilikuwa pale stendi nikizurura tu... Ndio nikapata kazi ya kumbebea vitu vyake vya ndani vyote na mkokoteni,.. Na hapo ni mtu mzima haswa... Yule bwana alinipatia kiasi cha elfu 50, baada ya kumaliza kazi yake,.. Pesa niliotamani kulipwa kwa mwezi leo nimeipata kwa masaa... Kipindi hicho kupata elfu 50 ni kazi na pia ilikuwa kubwa sana,.. Hapo ndipo nilipojua kuna matajiri duniani,.. Lakini bwana Mohamed hakuishia hapo alipenda hata kuja kumtembelea mana mimi ndio nilikuwa mwenyeji wake niliemseidia vitu vyake,.... Nakumbuka kuna siku nilikutana nae njiani akiwa na gari yake, ndani kuna mtoto wake wa kike na mkewe,.. Wakati huo wewe hujulikani utatungwa lini, nilikuwa na mtoto mmoja tu ambae ni huyu dada yako rehema,.. Bwana Mohamed alinipa lifti mpaka nyumbani kwake, nilipofika tu kwake kanikaribisha vizuri hata kuingia nilikuwa Naogopa sana mana alikuwa akifanya kazi serikalini ni mtu mkubwa sana... Kwakua mimi nilikuwa na shida na kazi, aliniambia nimtafutie kijana wa kutengeneza gadeni hapo nyumbani kwake,.. Sikuweza kufanya hivyo badala yake nikaitaka mimi ile kazi mana hata mimi nilikuwa nina shida.. Nakumbuka bwana Mohamed aliniambia hii kazi ni ya vijana wadogo, sio sisi watu wazima.. Subiri mimi nitakufanyia mpango kwenye kampuni yetu ya kifamilia ufanye kazi... Kiukweli nilishukuru sana kwa hisani alioifanya,.. Kweli nilimtafuta yule kijana wa gadeni, kisha baada ya wiki nikapelekwa kwenye kampuni yao, mana hata wao walikuwa na pesa kwenye familia yao..... Sasa kwakuwa nilipelekwa na boss mkubwa, yaani kwenye hio kampuni bwana Mohamed ndio mkubwa wao... Nilipewa nafasi ya juu sana kwasababu nililetwa na mkubwa wao.. Nililipwa kiasi cha shilingi laki tatu kwa mwezi, ambapo kwa malipo ya sasa ni kama milioni 3 za kitanzania,... Japo humo humo kina wanaolipwa zaidi ya hio yangu.. Lakini lakini tatu kwangu nilikiona ni kipato kikubwa sana.. Na hapo ndipo safari yangu ya maisha mazuri ikaanzia hapo.. Kila nikihitaji mkopo wa laki tano ambayo ni kama milioni tano kwa sasa, bwana Mohamed alikuwa akiniongezea laki tano nyingine,.. Jumla ninakuwa na milioni moja ambapo kwa sasa ni sawa na millioni kumi za kitanzania.... Hapo ndipo nami nikaacha kubweteka, nikawa bahali ili na mimi niwe kama yeye.... Nakumbuka siku namwambia mafanikio yangu, alifurahi sana, nilipomwambia nami naandaa kampuni yangu ya usafirishaji... Alifurahi sana tena akaniuliza katika kampuni yako kuna kitu kimepungua.. Nikamjibu hapana... Kiukweli mzee mwenzangu alinipenda sana.... Na sikuwa na cha kumlipa chochote zaidi ya kutoa shukrani zangu kwake..
Ndipo juzi hapa sasa ndio kanijia na kutaka wewe umuoe binti yake, na aliniomba kwamba nimtolee aibu mana wazee wenzake wote wameozesha mabinti zao, lakini wakwake haolewi kwa tabia za mtoto wake,.. Aliniambia kabisa tabia za mtoto wake ni mbaya sio za kupata mume kabisa, hivyo kaniomba kama mzee mwenzie nitumie sauti ya ubaba naye atumie sauti ya ubaba ili muoane wewe na mtoto wake.. Nikikumbuka fadhila alizonifanyia miaka hio, kiukweli sikuwa na pingamizi juu ya hilo japo moyo ulikuwa ukiniuma kwa hilo.. Lakini nikaona wacha nilipe fadhila alizonifanyia huyu bwana.... Ndipo mkaoana kwa lazima na kuishi kwa lazima...... Hivyo ndivyo ilivyokuwa mwanangu nisamehe, ubusara wangu ndio uliokutesa mwanangu.. Nisamehe sana baba yako..."
Mzew Rashidy aliongea mengi sana mpaka kila mmoja alichoka, lakini mama anayajua hayo yote, lakini sheby yeye hayajui mana pesa kazikuta hivyo hajui mateso alioyapitia baba yake.... Sasa sheby ndio kujumlisha na ile picha alioiona kule kwenye kabati la baba yake siku ile... Walipiga picha pamoja lakini baba yake alionekana kuchoka sana yaani alikuwa hana mbele wala nyuma, kumbe hivyo ndivyo ilivyokuwa...
"sasa wazee mimi ngoja nitoke kidogo mana kichwa hakijakaa sawa"
Sheby aliaga kihivyo lakini mama yake alimzuia
"wewe... Sasa hebu tuambie una mchumba, mana hatutaki tena uzoee maisha ya kibachela"
"ndio ninae"
Aliposema tu anae, baba kadakia
"sasa kama unae unasubiri nini, au huna pesa za kutosha baba"
"lazima nimwangalie tabia yake kwanza"
"ina mana humjui"
"namjua.. Na hata wewe unamjua ila humjui"
"mmmhhh sawa lakini mimi nisingetaka uishi bila mtu kwa sasa"
Basi kijana sheby alitoka hapo mpaka ofisini kwake....
"saidi vp"
"aaahh poa boss... Hujaonekana toka asubuhi hapa"
"aahhhh si unajua pilika pilika hizi"
"enhee niambie"
"ebu washa gari tukatulie mahali kwanza turefresh mind kidogo"
Saidi anavyopenda kutoka na boss, haikuchukuwa hata dakika gari imeshawashwa mpaka kwenye restaurant moja hivi hapo jijini na kuagiza vibaiti vidogo vidogo.... Sasa wakiwa wanaendelea kula ghafla shadi akatokea maeneo hayo, lakini hakuwaona ila saidi ndio kamuona shadi,... Sasa saidi kwa akili yake akajua sheby alimdanganya ile ishu ya yeye kiwa na mahusiano na mke wake ambae ni zaituni, hivyo akamwonyesha sheby kama anamjua shadi, mana kama hamjui basi ni mwongo lakini kama anamjua basi ni kweli...
"boss, unamjua yule dada"
Sheby kumwangalia vizuri alimjua ni shadi, rafiki yake na zaituni
"ina maana hata wewe humjui mshenga wako"
Aliongea kijana sheby huku akimwangalia saidi
"una maana gani kusema mshenga"
"we ulifikiri bila huyu ungempata zai"
Saidi hapo ndio kajua kweli boss wake hakumdanganya hata kidogo
"kweli boss leo ndio naamini kweli zaituni alikuwa mpenzi wako... Siamini kama nimeoa mtu uliekuwa nae Kimapenzi"
"kwanza zaituni sijawahi kumwingilia kimapenzi, japo nilikuwa namwogesha mwenyewe lakini sijawahi"
"acha kunidanganya boss, yaani uogeshe mwanamke mtu mzima na wewe ni kidume rijali afu uniambie hujalala nae"
"ndio.... Zaituni alikuwa kipofu, na niliapa kutokumgusa mpaka nitakapomuoa"
"aahhhhh kweli sijaona mwanaume kama wewe aiseee......... Shadi... We shadi"
Saidi alimwita shadi aliokuwa kaketi meza ya jirani
"haaaaaaa saidi kumbe upo hapa"
Shadi alikuwa bado hajamuona sheby mana alikuwa kajiinamia kwenye meza, hivyo hakufanikiwa kumwona sura, ila anajua saidi yupo na rafiki yake...
"mambo shem"
Alisalimia shadi huku akimpa mkono saidi..
"safi tu hali yako mtoto mzuri"
"waapi mzuri mkeo..... Mwaya kaka mambo"
Shadi alimsalimia sheby huku akinyoosha mkono wake lainiii... Sheby akainua kichwa na kuupokea mkono, lakini shadi alipomwona kumbe ni sheby alirudisha mkono na kuanza kuongea
"kumbe ni wewe.... Yaani siamini kama kweli kuna wanaume makatili kiasi hiki"
"shem vp tena, mbona umebadirika ghafla"
Aliuliza saidi huku akimsihi akae
"huyu ndie alienipa kazi yake ya kumshawishi zai awe malaya ili ajue kama anampenda,... Mimi nilifanya juu chini ile kazi iende sawa mana hata mimi nilikuwa nampenda huyu kijana kutokana na uchapakazi wake, lakini kumbe nae ni tajiri alitudanganya wote,.. Nikaimaliza kazi yake vizuri,.. Nikamwambia sheby mimi nakupenda na hali yako hio hio ya kuuza viazi, lakini akasema ngoja nifikirie mana alikuwa ana mawazo juu ya kumkosa zai... Nikaona wacha nimuache hizi siku mbili tatu... Heeeeeeee, kwani toka siku hio nilimuona.. Mpaka nikajikuta nayatamani maisha anayoishi zaituni, nami nikaingia huko huko aliko zai.. Roho inaniuma sana, nimemfanyia mwenzangu ukuadi mpaka kaolewa afu mimi nimebaki nahaha na wanaume tu.. Yaani namlaani sana huyu mtu"
Shadi aliongea mengi sana lakini sheby alimtuliza...
"Samahani sana kwa hilo shadi... Lakini hata mimi nilikutafuta sana, kila nikikupigia naambiwa simu inatumika... Nikaona wacha nikuache utanitafuta kama ulivyonitafuta mwanzo na kuniambia unanipenda,.. Ni bahati mbaya tu, naamini utapata mume bora"
"sio rahisi sheby... Mimi nilikupenda wewe na ndio maana nikafanya juu chini zaituni awe malaya ili uwe na mimi... Lakini kumbe malipo yangu ni hapa hapa duniani"
"pole sana... Ila kama unaendelea na kazi hio naomba uache.. Nitakupa mtaji ufanye biashara, achana na hio kazi"
Shadi kuskia mtaji kidogo hasira zikamtua....
"lakini boss, kweli ulichokifanya kwa zai sio kizuri... Mimi naamini zaituni angelikuwa mke wako sema tu hukumfanyia fea"
"aahxxxhhh saidi tuyaache hayo... Mi naona tuondoke hapa"
Baada ya wiki mbili kupita, sheby akiwa nyumbani kwake anapoteza muda kwa kumwagilia mauwa katika bustani yake... Ghafla mlango ulisukumwa na mtu kuingia...
"we vp, umefukuzwa huko kwenu"
Aliongea sheby huku akimsogelea, na hakuwa mwingine bali alikuwa ni mwai,..
"Si nimerudi kwa mume wangu"
"heeeeeeee ehehehehe halooooo.... Ahhh umeacha nimecheka kicheko cha kike kwa ujinga wako... Kwanza kabla ya yote watoto wakuwapi mana sijawahi hata kusikia matumizi wiki ya tatu hii sasa inaisha"
"watoto kawachukuwa baba yao"
"una uhakika kawakubali"
"ndio"
"ok sawa... Vp una njaa upikiwe"
"nikapike mwenyewe au nipikiwe"
"heeeeeeeee ivi kumbe hujui... Aahhhh nakumbuka kadi ziliisha hukupewa kadi wewe... Kiukweli nina siku ya nne sasa toka nioe"
"whaaaat... "
"ohoooo.... Unashngaa tena... Mimi nimeshaoa... We mama chidi"
Sheby alimwita mkewe atoke ili aamini kweli kaoa.... Laaaaa Haulaaa mwai kabaki mdomo wazi kwa mke aliomuona....
"mary.... Yaani umethubutu kuolewa na mume wangu mary"
"Eh eh samahani we mwanamke... Naitwa hadija bibie... Mimi sio mary.. Mary bado hajaolewa, naitwa hadija.. Mwanamke ninaejua thamani ya ndoa.. Wanawake wenzio wanaitafuta ndoa kwa udi na uvumba we waichezea nyoooo..... Wanaume wenyewe wa kuoa wako wapi?? Leo upate afu uchezeee... Eti zoba, zoba kwako, kwangu mume huyu"
Mary au hadija kwa jina ndoa aliongea kwa nyodo kali kumlingishia rafiki yake kipenzi kuwa sasa ni mume wa mtu
"mary yaani unanifanyia hivi kweli.. Mimi... Nani kawaleta kwenye huu mji"
"i Know ni wewe, lakini umeichezea ndoa mwenyewe... Wanaume wachache dunia hii... Umempata afu wamchezea loooo unalo ilo"
Ghafla mlango ukasukumwa na mtu mwingine kaingia, alikuwa ni rose...
"habari zenu jamani... Poleni kwa maumivu ya kupoteza ndoa wengine poleni kwa furaha ya kupata ndoa... We bibie mpoteza ndoa.. Unasubiriwa na askari hapo nje.. Naskia umeuwa"
"kauwa??"
Sheby kashangaa kuskia mwai kauwa
"ndio.... Vile vitoto kaviua"
"astakafilu lah jamani mwai.... Haya kisa ni nini"
"lakini hayupo peke yake.... Yupo na jemsi wake, wapo nae hapo nje kajaa pingu ngwi"
Rose alikuwa akiongea kwa mbwembwe nyingi sana mana maisha ni yao kwa sasa...
"rose kwanini hamkumbuki fadhila zangu lakini"
"heeeee we mfungwa vipi, ebu nenda uko... Umeyachezea mwenyewe sasa kayachezee mavi huko gerezani"
Rose alikuwa akitoa maneno shombo.. Ghafla geti likagongwa,.. Alikuwa ni askari
"afande, mwanamke mwenyewe ni huyu hapa"
"kamata huyo atatoa maelezo kituoni"
Sheby alitaka kuingilia kati anagalao kumtetea mwai, lakink alizuiwa na rose
"shem.. Hii kesi haikuhusu.. Tulia uifurahie ndoa yako..... Hadija mdogo wangu, nakuomba sana itunze ndoa yako mama... Ukiachwa utajiju... Mpaka sasa mimi mwenzio tayari nina mchumba na dini nabadirisha na mimi... Nami ndani ya ndoa mama.. Staki utani"
"unaolewa lini dada rose"
"wiki hizi hizi..."
Sheby akaingilia kati juu ya swala hilo
"mmeo anajiweza kuusu harusi... Mana kama hajiwezi niigharamikie mimi hio ndoa yenu"
"kiukweli shem hata yeye kashiba.. Sio mbaya na nadhani unamfahamu"
"ni nani huyo"
"jamali"
"heeeeeeeee na yule bwege nae anaoa"
Jamali ni mfanyakazi wake, ambae wanafanya nae kazi kampuni moja, nae kumbe kamuona rose kuwa kama mkewe...
"hadija... Binafsi kwa mimi namuomba mungu anifanye nitulie kwenye ndoa yangu.. Sasa hivi sitaxki starehe yeyote, sasa nafuata njia zako hadija... Sasa nimeamua kutulia, naomba tutulie hadija... Dunia hii haina wanaume.. Ukimpata mama tulia mlee watoto....... Shem"
Rose alimwita sheby
"ndio shem"
"nilikuja kuwatembelea tu.. Na kuwaonyesha hawa askari sehemu alipokimbilia mwai... Wacha nirudi si mnajua leo wikiende mume wangu yupo nyumbani... Naombeni niende"
Rose kabadirika sana kutoka kwenye maisha ya kidigitali mpaka kwenye maisha ya kidini, huezi amini rose sasa ni mtu wa hijabu hataki tena mambo ya sherehe....
"rose... Binafsi hata sisi tunakuombea ndoa njema... Nasi hatukuzuii mana unakwenda kuwa mke wa mtu"
"nashukuru sana... Nanyi muishi kwa amani"
Rose aliondoka zake tena alikuja na gari ya mchumba wake ambae ni jaxxmali.... Sheby kamuoa mary tena unaambiwa siku ya ndoa hata mary alikuwa hajui, kaenda kiburuzwa tu ofisini mpaka ukumbini na kukutana na shela la harusi.. Unaamniwa baada ya ndoa mary alizimia, mana alihisi ni ndoto kwake....
"ivi umepika wewe umekuja kuskiza umbea tu hapa nje"
Aliongea sheby kwa kumwambia mkewe
"heeeeeee mume wangu.. Chakula karibia kinapoa sasa"
"wacha bwana"
Sheby alimbeba mkewe mpaka ndani katika meza ya chakula...
MWISHO..........
JAMANI DADA ZANGU PUNGUZENI NYODO... DUNIANI KUNA PINGILI TATU ZA MAISHA... (1) KUZALIWA.... (2) KUOLEWA (3) NA KUFA.... KWAHIO JUA NI LAZIMA UOLEWE, SASA KWANINI ULETE NYODO MAMA... WANAUME NI WACHACHE SANA KWENYE HII DUNIA.. UKISKIA KASEMA ANATAKA KUKUOA, KAZANIA MANA NDOA USHACHANGULIWA HIVYO... ACHENI TAMAA ZA MAISHA.. TAFUTENI ZENU MZIFURAHIE SIO UTAMANI KUOLEWA NA TAJIRI WAKATI KAZITAFUTA MWENYEWE... ATAKUNYANYASA SANA MANA PESA ZAKE UMEZIKUTA... PUNGUZENI NYODO JAMANI KUOLEWA NI SHERIA TENA NI LAZIMA NA SIO OMBI.....