Muziki: Kutokubaliana Sio Ugomvi
...nijiaminishe tu kuwa umekuwa na wikend nzuri, well, ilikuwa nzuri na wiki ndo hii imeanza, wiki ya karibu na December. Mwaka unaelekea kuisha na ni suala la kukumbushana tu kuwa kuna mengi yanakuja December, kifupi december haijawahi kumuacha mtu makini salama. Unajua ninachosema.
Nimepiga na story na anko wangu majuzi, ujue nini (hili neno nilistuka kuwa Shedede anasema linatumiwa sana na mdada anayevutiwa naye)mimi na anko tunatofautiana sana kimitizamo, yeye anatabia jumlisha za King Mswati na Bob Mugabe hapo unampata anko wangu. Kisiasa tunakubaliana kutokubaliana kiasi cha kufikia hata kunitishia kuwa nisiende kwake kunywa juice na kumsalimia aunt yangu. Huwa ni jasira tu tunaposhindwa kukubaliana. Nachofurahia ni kuwa tuna namna yetu ya kiukoo kutatua mgogoro pale tunaposhindwa kukubaliana kwa hoja. Tunajiaminisha kuwa tunapokubali kutokubaliana juu ya kitu huwa hatugombani, tunakaaa chini na kufurahia tofauti zetu na kuzivumilia. Ila mimi huwa sivumilii tabia yake ile mnayoifahamu humu, ile ya anko nyumba nyingi.
Muziki sasa, nikushukuru sana
Shunie kwa kuweka magazeti humu, asante BH kwa sala na asante
Shadrack K. Lwila kwa kusogoza leo humu. Sijakusahau anko wangu
Lyon Lee kwa UF, ooh, nilitaka kujisahau mwenyewe, mnishukuru kwa kudhamini magazeti