Makapuku Forum

Makapuku Forum

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 15 AZIZ HASHIM
ILIPOISHIA:
“Aisee! Mbona hii inaonekana kuwa ngoma nzito?”
“Ni ngoma nzito kwelikweli, halafu kuna huyu kijana ameingizwa kwenye mtego bila mwenyewe kujua chochote, mpaka namuonea huruma.”
SASA ENDELEA…

“Kwa akili zako unafikiri huyu kijana atakuwa ameingia kwenye mtego mwenyewe akiwa hajui chochote?”
“Hajui chochote, hata maelezo aliyokuwa anayatoa, yanaonesha kabisa hakuna anachokijua.”
“Unafikiri inawezekana mtu akaingizwa kwenye kumi na nane za Loris kama hana umuhimu? Hata kama mwenyewe hajui naamini lazima kuna jambo ambalo limefanya aingizwe kwenye huu mtego.”
“Lakini hajaingizwa na Loris mwenyewe isipokuwa binti yake.”
“Nani ambaye hajui kwamba Loris amekuwa akimtumia mwanaye kwenye kazi zake, hasa pale anapoona mambo yameanza kuwa magumu kwake?”
“Yote yanawezekana lakini taarifa za ndani zinaonesha kwamba huyu binti mwenyewe ameshachoka kumtumikia baba yake na ndiyo maana unaona anaandamwa na matatizo makubwa!”
“Unataka kusema ndiyo maana anatishiwa kuuawa?”
“Inawezekana kabisa, nahisi kuna jambo kubwa analolifahamu lakini hataki kueleza ukweli kwa sababu hata ukifuatilia maelezo aliyokuwa anayatoa, anazungumza vitu nusunusu sana.”
“Mh! Kweli hii ngoma nzito! Kwa hiyo tunafanyaje?”
“Inabidi tuwasiliane kwanza na mkuu, si unajua mtandao wa Loris unahusisha mpaka viongozi wetu?”
***
Raya alishika taulo nililokuwa nimejifunga na kulivuta kisha akalitundika pale alipoweka khanga yake, tukabaki saresare maua! Akanisogelea jirani kabisa kiasi cha kila mmoja kuanza kuzisikia pumzi za mwenzake, tukawa tunatazamana machoni huku ‘Jamal’ wangu naye akianza kufura kwa hasira.
“Quench my thirst dear Jamal! I’m in deep love with you, take me and let me feel like a real woman!” (Nikate kiu yangu mpenzi wangu Jamal! Nipo kwenye penzi lenye kina kirefu na wewe, nichukue na unifanye nijihisi kuwa mwanamke niliyekamilika!) alisema Raya kwa sauti iliyokuwa ikisikika kama ya mtoto mchanga.
Bado sikuwa najua nifanye nini kwa sababu sitaki kusema uongo, ukiachilia mbali ukweli kwamba sikuwa na hisia za kimapenzi dhidi yake, Raya alikuwa ni msichana mzuri sana ambaye mwanaume yeyote aliyekamilika, asingeweza kumuacha, hasa katika mazingira kama yale tuliyokuwepo.
Akionesha kuwa na shauku kubwa, alinikumbatia kwa nguvu na tukagusanisha ndimi zetu, nikahisi kama mwili wangu umepigwa na shoti kali ya umeme.
Kwa kutumia mkono mmoja, alifungua bomba la maji, yakawa yanatumwagikia mithili ya watu waliokumbatiana kwenye mvua kali, hali iliyonizidishia msisimko mkali kwani japo maji yalikuwa ya baridi, joto la mwili wake lilinifanya nijihisi kama nipo kwenye ulimwengu wa tofauti kabisa.
Alifunga bomba na kuchukua sabuni, ingawa tayari nilishakuwa nimeoga, alianza upya kunipaka sabuni mwili mzima, nikazidi kusisimka pale mikono yake laini ilipokuwa ikinipaka sabuni, alipomaliza alitaka na mimi nifanye kama vile. Nikaanza kumpaka sabuni mwili mzima, kusema ukweli hakuna siku ambayo nilisisimka kama siku hiyo.
Baada ya kumaliza, alifungua tena maji, tukaoga huku mara kwa mara tukigusanisha ndimi zetu, tulipomaliza alichukua taulo na kunifuta kwa mahaba mazito kisha akanifunga kiunoni, na yeye akachukua khanga yake moja na kujifunga bila hata kujifuta.
Kwa kuwa mwili wake ulikuwa na maji, khanga ile ilishikana na ngozi ya mwili wake na kulifanya umbo lake lionekane vizuri, hasa maeneo ya kiunoni kwa nyuma ambayo yalikuwa si haba! Kwa makusudi kabisa, akatangulia mbele na kuanza kutembea kwa maringo kuelekea chumbani kwake.
Nilijikuta nikiwa kama kondoo anayepelekwa machinjioni, nikawa namfuata nyumanyuma huku macho yangu yakiwa hayabanduki kwenye mwili wake, nikimeza mate kama fisi aliyeona mfupa. Sikuelewa kilichofuatia zaidi ya kujishtukia tukiwa juu ya kitanda chake kikubwa.
Hata sikukumbuka taulo langu nililivua muda gani, achilia mbali khanga yake, zaidi ya kujikuta wote wawili tukiwa kama tulivyoletwa duniani, hakukuwa na mazungumzo tena, kilichosikika kilikuwa ni miguno ya hapa na pale wakati joto la huba likizidi kupanda kwenye mtima wa kila mmoja.
Dakika kadhaa baadaye, kila mmoja alikuwa tayari kwa pambano la kirafiki lisilo na jezi wala refa, Raya akionesha kuukamia mchezo kuliko kawaida. Kabla hata kipyenga cha kuashiria mpambano kuanza hakijalia, tayari Raya alishamkamata ‘Jamal’ wangu na kumuelekeza kwenye lango la kuingilia ngome kuu, nami nikawa mtiifu kwa kila alichokuwa anakifanya Raya.
Tofauti kabisa na nilichokuwa nimekitegemea, ‘Jamal’ wangu alikutana na ukuta mgumu wa ngome hiyo, ikabidi nimuongezee nguvu ya kusonga mbele, nikamuona Raya akiuma meno na kufumba macho yake, zoezi lililosindikizwa na miguno ambayo sikuelewa kama ilikuwa ya raha au maumivu.
Miguno ile iliniongezea hamasa, huruma zikaniishia kabisa, nikaongeza nguvu na muda mfupi baadaye, tayari tulikuwa tukielea kwenye ulimwengu mwingine tofauti kabisa, ambao kwa Raya ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kuufikia. Nikiri kwamba kwa mara ya kwanza, nilijikuta nikiijutia nafsi yangu kwa kushindwa kumuelewa Raya mapema na kumpa nafasi ndani ya moyo wangu.
Haikuwa rahisi kwa msichana mrembo kama yeye, kwa umri wake, elimu yake na uwezo wa familia yao, kuwa bado hajaguswa mpaka siku hiyo. Kwangu niliiona ni zaidi ya bahati na nikaendelea kujilaumu kwa kuchelewa kusoma alama za nyakati. Tuliendelea kusakata kabumbu kwa zaidi ya dakika ishirini, Raya akijitutumua kadiri ya uwezo wake ili asionekane mgeni kabisa kwenye sanaa hiyo ya kikubwa.
Mpaka kipyenga kinalia kuashiria kumalizika kwa mpambano huo, dimba lote lilikuwa halitamaniki, ungeweza kufananisha na machinjio ya Vingunguti au ya Pugu.
“Ahsante, ahsante sana Jamal, hatimaye ndoto zangu za muda mrefu zimetimia, umenifanya nijione mwanamke niliyekamilika!” alisema Raya kwa sauti iliyokuwa inasikika kama ya mtoto mchanga, machozi yakiulowanisha uso wake. Akawa ananibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu.
Kwa kuwa dimba lilishachafuka, ilibidi turudi tena bafuni, tukarudia tena kuogeshana, safari hii kwa hisia kali kuliko mwanzo kisha tukarudi kwenye chumba cha wageni ambacho kimsingi ndiyo nilichotakiwa kulala. Raya akaniganda kama ruba na hatimaye, tukajikuta tukiingia tena dimbani kwa ngwe ya lala salama. Kipyenga kilipolia kuashria kumalizika kwa dakika tisini, tulipitiwa na usingizi wa pono.
Mimi ndiyo nilikuwa wa kwanza kuzinduka, alfajiri ya siku ya pili ambapo kilichonizindua, ilikuwa ni mlio wa simu yangu iliyokuwa inaita mfululizo. Kwa taabu niliichukua simu na kutazama namba ya mpigaji. Moyo ukanilipuka baada ya kugundua kuwa alikuwa ni Shenaiza.
Nilimtazama Raya aliyekuwa bado amelala juu ya kifua changu, nikajiuliza mara mbilimbili kama nipokee au la. Mpaka simu inakata, sikuwa nimeamua nini cha kufanya, ikaanza tena kuita mfululizo ambapo nililazimika kuipokea, sauti ya Samantha ikasikika upande wa pili, ikinipa taarifa ambazo zilinishtua mno.
“Unasemaaa?” nilijikuta nikiuliza kwa sauti ya juu, iliyomzindua Raya usingizini.
Je, nini kitafuatia?
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 16 AZIZ HASHIM
ILIPOISHIA:
Nilimtazama Raya aliyekuwa bado amelala juu ya kifua changu, nikajiuliza mara mbilimbili kama nipokee au la. Mpaka simu inakata, sikuwa nimeamua nini cha kufanya, ikaanza tena kuita mfululizo ambapo nililazimika kuipokea, sauti ya Samantha ikasikika upande wa pili, ikinipa taarifa ambazo zilinishtua mno.
“Unasemaaa?” nilijikuta nikiuliza kwa sauti ya juu, iliyomzindua Raya usingizini.
SASA ENDELEA…

Wamekuja tena hapa hospitalini wanataka kuniua na wametishia kwamba wanahisi na wewe unahusika kwenye hiki kinachoendelea kwa hiyo wameapa kufanya kila kinachowezekana kuhakikisha wanatupoteza wote wawili.
“Lakini Shenaiza, hivi ingekuwa wewe ndiyo upo kwenye nafasi yangu ungejisikiaje? Yaani unajikuta tu upo katikati ya mambo ya hatari, maisha yako yanawindwa usiku kucha lakini hata huelewi chanzo ni nini, ungejisikiaje?”
“Ningejisikia vibaya Jamal lakini si nilishakwambia nitakueleza kila kitu? Wala huna haja ya kuwa na haraka wala kukasirika.”
“Utaniambia lini? Unajua kilichonitokea nilipoondoka hapo hospitalini? Bado kidogo ningekufa leo, kibaya ni kwamba sijui hasa kinachoendelea, sijui chochote kuhusu wewe wala matatizo yako ambayo sasa yameshakuwa yangu pia.”
“Huu sio muda wa kulaumiana Jamal, nakuomba kama ulivyofanya mara ya kwanza, njoo unitoroshe tena hospitali na nakuahidi safari hii tukitoka tu, nitakueleza ukweli wa kila kitu.”
“Hapana! Siwezi Shenaiza, tafuta mtu mwingine wa kuifanya kazi hiyo, sipo tayari.”
“Jamani Jamal, kwa hiyo upo tayari kuona nakufa wakati uwezo wa kunisaidia unao? Tena asubuhi hii ndiyo muda mzuri, watu wakija kuwaletea wagonjwa chai na sisi tunatumia muda huohuo kutoroka, nipo chini ya miguu yako,” alisema Shenaiza kwa sauti iliyoonesha alikuwa akilengwalengwa na machozi.
Nilishindwa cha kumjibu, nikamuona Raya naye ambaye bado alionesha kuwa na usingizi, akijigeuza pale kitandani na kunikumbatia tena ikiwa ni ishara kwamba hakufurahishwa na kitendo cha mimi kuzungumza na Shenaiza alfajiri ile.
“Ok, basi sawa nitajua cha kufanya,” nilijibu harakaharaka kisha nikakata simu. Nililazimika kumkatisha kwa sababu sikutaka kuendelea kumkasirisha Raya.
“Good morning baby!” (Habari za asubuhi mpenzi) alisema Raya huku akijinyoosha mwili kwa uchovu, akanibusu mdomoni na kunikumbatia tena.
“Ulikuwa unaongea na nani kwenye simu?” aliniuliza swali ambalo nilijua kwamba majibu yake anayo ila anataka kunitega.
“Si huyu Shenaiza, asubuhi yote hii anaanza kuleta matatizo mengine!”
“Mh! Anasemaje tena?”
“Ananiambia kuwa wale watu wanaotaka kumuua, wameanza kunitafuta na mimi na wamemuapia kuwa ni lazima watufanye kitu kibaya, mimi na yeye.”
“Ooh! Mungu wangu, nakuomba Jamal uachane na huyo msichana, achana kabisa na mambo yake, kama ni matatizo ni yake wala wewe hayakuhusu, isitoshe mtu mwenyewe ndiyo kwanza mmejuana, achana naye nakuomba,” alisema Raya kwa hisia za hali ya juu.
Japokuwa alikuwa na hoja kwa alichokuwa anakizungumza, akili zangu zilikuwa ni kama zimezingirwa na ukungu, nikawa sielewi nataka nini maishani mwangu. Niliona kama matatizo yaliyokuwa yanamkabili Shenaiza, yalikuwa yananihusu sana na ni mimi pekee ndiye niliyekuwa na uwezo wa kumsaidia.
Japokuwa kuna wakati mwingine nilikuwa nikiona kama nabebeshwa mzigo nisioustahili, bado niliona ninayo nafasi ya kumsaidia. Ilibidi niamke na kuelekea bafuni, Raya naye akaamka na kunifuata, tukaoga pamoja huku Raya akionesha kufurahishwa mno na ukaribu wangu.
Tulirudi chumbani ambapo wakati mimi nikijiandaa, Raya alienda jikoni kuandaa kifungua kinywa. Nilipomaliza kujiandaa, tayari kifungua kinywa kilikuwa tayari, Raya akiwa ndani ya khanga moja tu, akanikaribisha mezani.
Mwenyewe alitamani asubuhi hiyo tuendelee kukaa kimahaba kama ilivyokuwa usiku lakini akili zangu zilikuwa zikienda mbio sana, nikapata kifungua kinywa harakaharaka kisha nikamuaga.
Haikuwa rahisi kwake kuniruhusu, ikabidi nimdanganye kwamba nitarudi muda mfupi baadaye na sitatoka tena siku hiyo mpaka usiku. Ilibidi aniruhusu kwa shingo upande lakini akanitaka kuwa makini sana kwa kila kitu nitakachokuwa nakifanya.
Tulikumbatiana, nikambusu kwenye paji la uso wake kisha nikatoka, hatua kadhaa mbele niligeuka na kumtazama, nikamuona machozi yakimlengalenga, sikuwa na cha kufanya zaidi ya kuendelea na safari yangu.
Nilitoka na kwenda moja kwa moja mpaka hospitalini alikokuwa amelazwa Shenaiza, bado ilikuwa ni mapema sana na ndugu, jamaa na marafiki wa wagonjwa wengi walikuwa wakiwapelekea vifungua kinywa.
Ilibidi na mimi niingie kwenye mgahawa mmoja ulikuwa nje ya hospitali na kuchukua kifungua kinywa kwa ajili ya Shenaiza. Nilifanya hivyo ili isiwe rahisi kwa walinzi na madaktari kunihisi vibaya. Saa kumi na mbili kamili nilikuwa nikiingia kwenye mlango wa wodi aliyokuwa amelazwa Shenaiza.
Niliingia kimyakimya bila kuonekana na mtu yeyote mpaka pembeni ya kitanda cha Shenaiza, nikamuinamia na kumsemesha kwa sauti ya chini.
“Shenaiza! Shenaiza!”
“Ooh! Jamal, ahsante kwa kuja mpenzi wangu,” alisema Shenaiza ambaye kwa ilivyoonesha, hakuwa amelala bali aligeukia ukutani tu, akanikumbatia na kunibusu kwa hisia nzito huku akionesha mwili wake kuwa kwenye maumivu makali.
“Ni wewe pekee ndiye unayeweza kunisaidia kwa sababu hata polisi nao naona wanasuasua tu, najua nakubebesha mzigo mzito lakini nakuhakikishia wema wako hautapita bure, usichoke kunisaidia,” alisema Shenaiza kwa sauti ya chini akijaribu kujikakamua na kuinuka pale kitandani.
Nilimsaidia kufanya hivyo, akakaa juu ya kitanda na kuanza kuangaza macho huku na kule.
“Huu ndiyo muda mzuri, inabidi tuondoke kabla hawa mashetani hawajafika,” alisema Shenaiza, nikawa naitika kila kitu alichokuwa ananiambia. Japokuwa nilikuwa najua kwamba ninachokifanya ni kosa jingine kubwa, nilijikuta nikiwa sina cha kufanya zaidi ya kutii kile Shenaiza alichokuwa anakitaka.
Tukatoka mpaka nje ya hospitali hiyo bila kugunduliwa na mtu yeyote, sikutaka kufanya makosa kama yale niliyoyafanya siku ile nilipomtorosha Shenaiza kule Amana, tukaenda mpaka kwenye kituo cha daladala na kupanda iliyokuwa inaelekea Makumbusho.
Ili kuzidi kupoteza ushahidi, nilimwambia Shenaiza ajifunike khanga yake, na mimi nikavaa kofia kubwa ya pama, tukatulia kwenye siti ya watu wawili. Abiria wengine waliendelea kuingia na baada ya gari kujaa, safari ilianza huku moyoni nikisali kusitokee jambo lolote baya.
“Sidhani kama tutafika salama huko tunakokwenda, moyo wangu unasita sana,” alisema Shenaiza kwa sauti ya kutetemeka. Sijui alikumbwa na nini mpaka aanze kuzungumza maneno yake, nikawa nampa moyo kwamba asiogope chochote.
Safari iliendelea mpaka tuklipofika Magomeni ambako kulikuwa na foleni kubwa sana asubuhi hiyo, jambo ambalo halikuwa la kawaida.
“Nimekwambia kwamba sijui kama tutafika salama, umewahi kuona asubuhi namna hii kunakuwa na foleni kama hii?” alisema Shenaiza huku akizidi kuonesha hofu kubwa ndani ya moyo wake, nikawa nazidi kumtuliza.
Je, nini kitafuatia?
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 17
ILIPOISHIA:
Safari iliendelea mpaka tulipofika Magomeni ambako kulikuwa na foleni kubwa sana asubuhi hiyo, jambo ambalo halikuwa la kawaida.
“Nimekwambia kwamba sijui kama tutafika salama, umewahi kuona asubuhi namna hii kunakuwa na foleni kama hii?” alisema Shenaiza huku akizidi kuonesha hofu kubwa ndani ya moyo wake, nikawa nazidi kumtuliza.
SASA ENDELEA…

Tulikaa kwenye foleni kwa zaidi ya dakika ishirini, magari yakiwa hayaendi mbele wala hayarudi nyuma. Nilitegemea kwamba muda mfupi baadaye askari wa usalama barabarani (trafiki) watafika na kusaidia kuondoa foleni hiyo lakini haikuwa hivyo.
Madereva wengine walipochoka, walianza kupiga honi kwa nguvu, huku wengine wakiteremka kwenye magari yao na kusogea upande wa mbele kujaribu kuangalia kilichokuwa kinasababisha foleni hiyo.
“Nasikia kuna ajali huko mbele, hapa hatuwezi kuondoka sasa hivi mpaka trafiki waje, wapime ajali yenyewe, wayatoe magari yaliyopata ajali unafikiri itakuwa sasa hivi?” kondakta wa daladala tuliyopanda, alisema na kutufanya abiria wote tuishiwe nguvu.
“Sasa tutafanyaje?”
“Inabidi tushuke tutembee kwa miguu, kule hospitali wakishtukia kwamba nimetoroka wanaweza kuanza kutufuatilia na huenda wakatukamata hapahapa, tuondoke,” alisema Shenaiza huku akisimama kwenye siti aliyokuwa amekaa, na mimi nikasimama, tukamlipa kondakta nauli yake kisha tukashuka.
“Inabidi tutembee mpaka upande wa pili tukachukue Bajaj au bodaboda,” alisema Shenaiza huku akizidi kujitanda ushungi wake ili isiwe rahisi kwa mtu yeyote kumtambua, na mimi nilishusha kofia yangu ya pama, tukawa tunatembea kuelekea kule kwenye Bajaj.
Tukiwa tunatembea katikati ya tuta la barabara lililokuwa linatenganisha barabara mbili za lami, ghafla tulishtushwa na muungurumo mkali wa pikipiki kubwa mbili zilizokuwa zinakuja upande wetu, tukiwa hata hatujui zimetokea wapi.
“Tulijua lazima tutakupata tu, wewe ndiyo unajifanya kimbelembele kuingilia ishu za watu si ndiyo?” alisema mwanaume mmoja kwa sauti ya kukwaruza, wote wakiwa wamesimamisha pikipiki zao kubwa huku na kule na kutufanya mimi na Shenaiza tubaki katikati, hofu kubwa ikanitanda ndani ya moyo wangu.
Cha ajabu zaidi, wakati wakiwa wametuzunguka pale barabarani, foleni ilianza kutembea, magari yakaanza kuondoka huku abiria waliokuwa wameshuka, nao wakiingia kwenye magari na kuendelea na safari.
“Leave him alone, what wrong has he done? (Mwacheni, kwani kuna jambo gani baya amefanya?) Kama mnanitaka mimi nichukueni lakini siyo huyu kijana wa watu,” alisema Shenaiza lakini hakuna aliyemsikiliza, ukichanganya na kelele za magari na vyombo vingine vya usafiri vilivyokuwa vikiondoka baada ya foleni kuanza kutembea, hakuna mtu aliyejua kilichokuwa kinaendelea.
“Siku nyingine hutakiwi kuingilia mambo yasiyokuhusu,” alisema mwanaume mmoja huku akinisogelea, nikawa nazidi kutetemeka kwani kwa jinsi hali ilivyokuwa, wangeweza kunifanya chochote wanachokitaka bila mtu yeyote kujua kilichokuwa kinaendelea.
“Nimesema muacheni?” alisema Shenaiza lakini kabla hata hajamalizia, mmoja kati ya wale wanaume wanne, alimtwanga ngumi nzito ya usoni, akapepesuka na kutaka kudondoka lakini mwingine alimdaka na kumsimamisha.
Hofu niliyoipata ilikuwa haielezeki, kama Shenaiza, mwanamke mrembo kiasi kile alipigwa ngumi nzito kiasi kile, mimi je? Nilijiuliza huku nikizidi kutetemeka, tayari nilishaanza kusikia harufu ya mauti.
Ghafla iliibuka pikipiki nyingine ambayo tofauti na zile nyingine, yenyewe ilikuwa na mtu mmoja tu, tena mwanaume aliyeonesha kuwa na umri mkubwa kuliko wale wengine, akafunua kioo cha kofia ngumu (helmet) aliyokuwa ameivaa, akanitazama kwa ukali, macho yangu yakagongana na yake.
Nilichokigundua, hakuwa Mtanzania na kwa kiasi kikubwa, alikuwa na sura inayofanana na Shenaiza kwa mbali, jambo lililonifanya niamini kwamba lazima atakuwa na uhusiano wa kindugu na msichana huyo, aliendelea kunitazama bila kuzungumza kitu chochote.
Nikiwa bado naendelea kutetemeka, magari yaliyokuwa kwenye foleni yakiwa yamepungua kabisa na eneo lote kurejewa na hali yake ya utulivu, nilimuona yule mwanaume akiwapa ishara fulani wale watu waliooonesha kuwa ni wafuasi wake, Shenaiza ambaye sasa alikuwa akivuja damu nyingi puani, akabebwa juujuu na kupakizwa kwenye pikipki ya yule mwanaume kisha akaondoka kwa kasi kubwa na kutokomea.
“Hili litakuwa funzo kwako na kwa watu wengine wenye tabia kama yako, usipende kuwasogelea wanawake usiowajua,” alisema mmoja kati ya wale wanaume, nikashtukia nikipigwa na kitu kizito kichwani, nikadondoka mzimamzima kama gunia. Sikuweza hata kupiga kelele za kuomba msaada.
Nikiwa pale chini, kwa taabu nilimuona mwanaume mmoja akichomoa kisu kikubwa na kunikalia, akakinyanyua na kukishindilia upande wa kushoto wa kifua changu bila huruma. Siwezi kuyaelezea maumivu ambayo niliyasikia, nikafumbua mdomo ili kupiga kelele za kuomba msaada lakini sauti haikutoka, nikasikia wale watu wakipongezana kisha wakapanda kwenye pikipiki zao na kuondoka kwa kasi.
Damu nyingi zilikuwa zinanitoka upande wa kushoto wa kifua changu kiasi cha kunifanya nilowe chapachapa. Nilijitahidi kuinuka pale nilipokuwa nimelala huku damu nyingi zikiendelea kunitoka lakini maumivu makali yalinirudisha chini.
Kwa kutumia mikono yangu miwili, nilijaribu kuminya pale kwenye jeraha kubwa ili kuzuia damu isiendelee kunimwagika lakini nilijikuta mikono ikikosa nguvu, kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo nilivyokuwa nazidi kuishiwa nguvu.
Watu wengi walianza kukimbilia pale nilipokuwa nimeanguka na kunizunguka, niliwasikia wengine wakishindwa kuficha hisia zao na kuanza kuangua vilio. Nadhani hali waliyoniona nayo iliwafanya waamini kwamba siwezi kabisa kupona kutokana na damu zilivyokuwa zinaendelea kunimwagika mithili ya bomba lililopasuka.
Nikiwa kwenye maumivu makali, nilijigeuza na kuanza kutazama angani, upeo wa macho yangu ukagota kwenye mawingu meupe na ya bluu yaliyokuwa yakilipendezesha anga, nikabaki nimetulia nikiwa kwenye hali hiyo.
Kelele za watu wengi waliokuwa wanazidi kuongezeka eneo la tukio kunishangaa, zilianza kupungua taratibu masikioni mwangu, zikazidi kupungua na baadaye nikawa nasikia kama watu wananong’ona. Kwa mbali nilisikia mlio wa ving’ora ambavyo hata hivyo sikujua ni vya nini.
Nikiwa naendelea kutazama angani, taswira ndani ya mboni za macho yangu ilianza kufifia taratibu na kadiri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele ndivyo nayo ilivyozidi kufifia, japokuwa ilikuwa ni asubuhi, kigiza kikaanza kutanda kwenye macho yangu.
Nakumbuka neno la mwisho nililofanikiwa kulisema, ingawa ilikuwa ni kwa taabu kubwa kutokana na midomo yangu kuwa mizito, ilikuwa ni: Mungu nisaidie! Nikafumba macho na giza totoro likatawala kila sehemu, sikuelewa tena kilichoendelea baada ya hapo!
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 18
ILIPOISHIA:
Nakumbuka neno la mwisho nililofanikiwa kulisema, ingawa ilikuwa ni kwa taabu kubwa kutokana na midomo yangu kuwa mizito, ilikuwa ni: Mungu nisaidie! Nikafumba macho na giza totoro likatawala kila sehemu, sikuelewa tena kilichoendelea baada ya hapo!
SASA ENDELEA...

Katika hali ambayo sikuitegemea na ambayo mpaka leo huwa siwezi kuifafanua, muda mfupi baadaye nilijikuta nikizinduka lakini nikiwa kwenye hali ya tofauti kabisa. Nilizinduka nikiwa palepale nilipokuwa nimelala awali lakini katika hali ya ajabu, nilikuwa mwepesi sana.
Nikajikuta nikianza kupaa taratibu kuelekea juu. Nikiwa juu kidogo, niligeuka na kutazama pale nilipokuwa nimeangukia, nikashangaa kuona bado mwili wangu ulikuwa umelala palepale, damu nyingi zikiendelea kutoka kwenye jeraha la kifuani, tena safari hii zikitoka kwa mabongemabonge.
“Mungu wangu! Hiki ni kitu gani tena?” nilijikuta nikisema kwa sauti ya chini, ungeweza kudhani nilikuwa kwenye ndoto lakini haikuwa hivyo. Nilijiuliza kama mwili wangu bado ulikuwa pale chini, mimi niliyekuwa napaa nilikuwa ni nani? Sikupata majibu.
Niliendelea kupaa kuelekea juu mpaka nikafikia umbali wa mita kadhaa, ulioniwezesha kuona vizuri kila kitu kilichokuwa kinaendelea eneo la tukio. Niliwaona watu wakizidi kumiminika kwa wingi eneo la tukio, wengine wakishika vichwa vyao baada ya kuuona mwili wangu ukiwa kwenye hali ile.
Hali hiyo ya ajabu iliendelea kunitokea, nakumbuka niliendelea kushuhudia kila kitu kilichoendelea, jinsi mwili wangu ulivyochukuliwa kutoka eneo la tukio na kukimbizwa mpaka hospitali ambako nako niliona madaktari walivyokuwa wakichakarika kuokoa maisha yangu.
Niendelee kusisitiza kwamba wakati haya yote yakitokea, katika ulimwengu wa kawaida sikuwa na fahamu hata kidogo, nilikuwa nimefumba macho na kulala pale kitandani kama maiti, nikiwa nimeunganishwa na mashine ya kunisaidia kupumua lakini katika ulimwengu mwingine ambao hata sijui niuiteje, nilikuwa nimesimama kwenye pembe moja ya ile wodi, nikishuhudia kila kilichokuwa kinaendelea.
Kazi ya kuokoa maisha yangu iliendelea, madaktari na manesi wakawa wanapishana huku na kule, huyu kabeba dawa, huyu kabeba chupa ya damu, huyu mikasi na sindano, ilimradi kila mmoja alikuwa bize.
Nilijisikia ahueni kubwa ndani ya moyo wangu kuona watu ambao pengine hata hawakuwa wakinijua, wakipigana kuokoa maisha yangu. Niliendelea kuwatazama wanavyohangaika, kuna wakati machozi ya uchungu yalikuwa yakinitoka kwa sababu ya kilichotokea, nikawa naendelea kujiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.
Narudia tena, mpaka leo huwa napata sana ugumu kuelezea hasa kile kilichotokea ni nini, yaani mimi niliyekuwa nashuhudia hayo yote nilikuwa nani na ule mwili ambao watu wote walikuwa wakiamini kwamba ni mimi, ulikuwa kitu gani?
Jambo pekee ninaloweza kusema, ni kwamba kila jambo linatokea maishani linatokea kwa sababu maalum na kuna mambo mengi sana yanayoendelea kutokea hapa duniani ambayo mimi na wewe hatuyajui. Huenda mimi nilitokewa na haya ili leo nije kutoa ushuhuda kwa watu ambao huwa ni wagumu kuamini kwamba kuna maisha mengine zaidi ya haya tunayoyajua.
Maisha haya ya kawaida ya binadamu tulio wengi, yamejawa na mambo mengi sana ambayo kwa akili za kawaida huwezi kuyaelewa na nilichojifunza ni kwamba mambo mengi humu duniani, hayapo kama ambavyo tumezoea kufikiria yapo. Kwamba hakuna jambo ambalo linatokea kwa bahati mbaya! Hata hizi ajali ambazo wengi huwa tunaona kwamba zimetokea kwa bahati mbaya, huwa hazitokei tu!
Waingereza wana msemo mmoja maarufu kwamba ‘everything is predestined’ wakimaanisha kila kinachotokea maishani tayari kilishapangwa! Nasisitiza hakuna kitu kinachotokea kwa bahati mbaya.
Yawezekana hata wewe usinielewe kwa sasa lakini napenda kukuhakikishia kwamba mambo mengi sana ambayo tunayajua na kuyaamini, hayapo vile ambavyo kwa miaka mingi tumekuwa tukiyaamini. Nikisema dunia nzima imejaa vitu vingi ambavyo havipo kama tulivyozoea kuviona, huenda ukawa hunielewi kwa urahisi lakini mimi nasimulia mambo ambayo yamenitokea mwenyewe.
Ukitaka kuamini, kuanzia sasa, anza kutazama kila kitu kwa jicho la tatu! Hata lile jambo ambalo ulikuwa unaamini kwamba unalijua au ulikuwa unaamini kwamba ni ukweli, hebu anza kulitazama kwa namna nyingine na jiulize maswali katika kila jambo, kuanzia kuhusu wewe mwenyewe, kwamba wewe ni nani, kwa nini upo duniani, umetoka wapi na unaelekea wapi na mambo yote yanayokuzunguka, utaanza kuelewa ninachokimaanisha.
Basi nikiwa nimesimama palepale kwenye pembe moja ya ile wodi, nikishuhudia kila kilichokuwa kinaendelea kwenye mwili wangu uliokuwa umelazwa pale kitandani ukiwa hauna fahamu hata kidogo, nilishtuka baada ya kuhisi upepo mkali ukianza kuvuma mle ndani ya wodi.
Sikuelewa ule upepo umetokea wapi kwa sababu milango na madirisha yote yalikuwa yamefungwa, baadhi ya vifaa vilivyokuwa mezani, vilianza kudodondoka, vikiwemo vichupa vya dawa na vifaa vingine vya kidaktari, manesi wakawa na kazi ya kuviokota na kuviweka sawa.
Ghafla nilihisi kama nashikwa na mtu mwenye nguvu sana, nikanyanyuliwa kutoka pale nilipokuwepo, kufumba na kufumbua, nikajikuta nipo kwenye mazingira mengine tofauti kabisa, mahali ambapo hata sijui nipaelezeeje. Kulikuwa na giza totoro kila upande, kiasi kwamba hata ukisogeza kidole jirani kabisa na jicho lako, usingeweza kuona kitu chochote.
Yule mtu ambaye alikuwa amenishika na kunitoa kule wodini, ambaye nasema ni mtu kwa sababu mikono yake ilikuwa ya kibinadamu kwa sababu na mimi nilimshika nikitaka kumjua ni nani lakini nikashindwa hata kumuona kwa sababu ya giza, aliniachia, nikajikuta nimesimama sehemu ambayo sikujua mbele ni wapi wala nyuma ni wapi, giza lilikuwa nene kikwelikweli.
“Jamal!” nilisikia sauti nzito, iliyokuwa ikisikika kama mwangwi, ikiliita jina langu. Umewahi kuingia kwenye sehemu ambayo ina uwazi mkubwa halafu ukatamka neno lolote na kusikia likijirudiarudia? Basi hivyo ndivyo ilivyokuwa kwangu, ile sauti nzito ilijirudiarudia mara kadhaa.
“Mungu wangu, hiki ni nini tena?” nilijisemea moyoni kwa hofu kubwa lakini tofauti na nilivyotegemea, wakati mimi nikiamini kwamba najisemea moyoni, niliisikia sauti yangu ikisikika utafikiri niliyatamka maneno yale mdomoni wakati ukweli ni kwamba niliyasemea moyoni.
Nikajikuta nikitetemeka kuliko kawaida, hofu kubwa ikiwa imeukumba moyo wangu ambao sasa ulikuwa ukidunda kwa nguvu kiasi cha mapigo yake kusikika vizuri kabisa hata kwa mtu aliyekuwa pembeni yangu.
“Jamal!” ile sauti ilisikika tena lakini tofauti na mwanzo, safari hii ilisikika ikionesha aliyeitoa alikuwa amesogea mbali kabisa na mimi, nikawa natamani kuitikia lakini nilishindwa kutokana na hofu kubwa iliyokuwa imenizingira.
“Jamal!” ile sauti ilisikika tena kwa mara ya tatu, safari hii ikionesha kwamba aliyekuwa akiniita alikuwa mbali zaidi. Katika hali ambayo siwezi kuielezea, nilijikuta nikianza kutembea kuelekea kule sauti ile ilikokuwa inazamia. Kwa mbali nikaanza kusikia sauti kama za watu wanaougulia maumivu makali, sauti za watoto wachanga waliokuwa wakilia na sauti za kutisha za wanyama ambazo nyingine hata sijawahi kuzisikia tangu nizaliwe.
Kuna wakati hofu ilinizidi na kutaka nigeuze nilikotoka lakini kitu ndani ya moyo wangu kikaniambia nizidi kusonga mbele. Kadiri nilivyokuwa nazidi kusonga mbele ndivyo zile sauti zilivyokuwa zinazidi kuongezeka, nikazidi kutetemeka kwa hofu huku nikiwa sijui nini itakuwa hatma yangu.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom