Tumosa
JF-Expert Member
- Jul 21, 2016
- 16,527
- 52,623
Nackia umetekwa maana hali ya hewa inaruhusuPambana na hali yako . ...![]()
![]()
![]()
Napatikana ndiooNikupigie kweli
Mimi weweHata sijui pambana na hali yako tu![]()
Hii ntaisoma baadae shem ..SEVEN DAYS IN HELL! (SIKU SABA KUZIMU)-1 MTUNZI AZIZ HASHIM
Damu nyingi zilikuwa zinanitoka upande wa kushoto wa kifua changu kiasi cha kunifanya nilowe chapachapa. Nilijitahidi kuinuka pale nilipokuwa nimelala huku damu nyingi zikiendelea kunitoka lakini maumivu makali yalinirudisha chini.
Kwa kutumia mikono yangu miwili, nilijaribu kuminya pale kwenye jeraha kubwa ili kuzuia damu isiendelee kunimwagika lakini nilijikuta mikono ikikosa nguvu, kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo nilivyokuwa nazidi kuishiwa nguvu.
Watu wengi walianza kukimbilia pale nilipokuwa nimeanguka na kunizunguka, niliwasikia wengine wakishindwa kuficha hisia zao na kuanza kuangua vilio wakilitaja jina langu. Nadhani hali waliyoniona nayo iliwafanya waamini kwamba siwezi kabisa kupona kutokana na damu zilivyokuwa zinaendelea kunimwagika mithili ya bomba lililopasuka.
Nikiwa kwenye maumivu makali, nilijigeuza na kuanza kutazama angani, upeo wa macho yangu ukagota kwenye mawingu meupe na ya bluu yaliyokuwa yakilipendezesha anga, nikabaki nimetulia nikiwa kwenye hali hiyo.
Kelele za watu wengi waliokuwa wanazidi kuongezeka eneo la tukio kunishangaa, zilianza kupungua taratibu masikioni mwangu, zikazidi kupungua na baadaye nikawa nasikia kama watu wananong’ona. Kwa mbali nilisikia mlio wa ving’ora ambavyo hata hivyo sikujua ni vya nini.
Nikiwa naendelea kutazama angani, taswira ndani ya mboni za macho yangu ilianza kufifia taratibu na kadiri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele ndivyo nayo ilivyozidi kufifia, japokuwa ilikuwa ni mchana, kigiza kikaanza kutanda kwenye macho yangu.
Nakumbuka neno la mwisho nililofanikiwa kulisema, ingawa ilikuwa ni kwa taabu kubwa kutokanana midomo yangu kuwa mizito, ilikuwa ni: Mungu nisaidie! Nikafumba macho na giza totoro likatawala kila sehemu, sikuelewa tena kilichoendelea baada ya hapo!
Katika hali ambayo sikuitegemea na ambayo mpaka leo huwa siwezi kuifafanua, muda mfupi baadaye nilijikuta nikizinduka lakini nikiwa kwenye hali ya tofauti kabisa. Nilizinduka nikiwa palepale nilipokuwa nimelala awali lakini katika hali ya ajabu, nilikuwa mwepesi sana.
Nikajikuta nikianza kupaa taratibu kuelekea juu. Nikiwa juu kidogo, niligeuka na kutazama pale nilipokuwa nimeangukia, nikashangaa kuona bado mwili wangu ulikuwa umelala palepale, damu nyingi zikiendelea kutoka kwenye jeraha la kifuani, tena safari hii zikitoka kwa mabongemabonge.
“Mungu wangu! Hiki ni kitu gani tena?” nilijikuta nikisema kwa sauti ya chini, ungeweza kudhani nilikuwa kwenye ndoto lakini haikuwa hivyo. Nilijiuliza kama mwili wangu bado ulikuwa pale chini, mimi niliyekuwa napaa nilikuwa ni nani?Sikupata majibu.
Niliendelea kupaa kuelekea juu mpaka nikafikia umbali wa mita kadhaa, ulioniwezesha kuona vizuri kila kitu kilichokuwa kinaendelea eneo la tukio. Niliwaona watuwakizidi kumiminika kwa wingi eneo la tukio, wengine wakishika vichwa vyao baada ya kuuona mwili wangu ukiwa kwenye hali ile.
Niliwaona watu kadhaa ambao nilikuwa nikiwafahamu wakiwa na nyuso za huzuni kali, wengine wakiangua vilio kwa nguvu. Nilimuona rafiki yangu na mfanyakazi mwenzangu ambaye muda mfupi kabla ya tukio nilikuwa naye, Justice akiwa analia kwa uchungu mno huku akilitaja jina langu.
Nilimuona pia Raya, msichana ambaye naye tulikuwa tukifanya naye kazi na ambaye alikuwa anapenda sana kuwa karibu na mimi ingawa mara kwa mara nilikuwa nikimkwepa (nitaeleza zaidi kuhusu msichana huyu baadaye), naweza kusema yeye ndiye aliyekuwa na hali mbaya kuliko watu wengine wote kwani alikuwa akilia kwa sauti ya juu huku akilitaja jina langu kiasi cha kusababisha muda mfupi baadaye aanguke na kupoteza fahamu.
Niliwaona pia baadhi ya watu wakiupiga picha mwili wangu kwa kutumia simu zao za mikononi, niliwaona pia waandishi kadhaa wa habari ambao nao walikuwa wakipiga picha nyingi eneo la tukio, za mnato na za video.
Muda mfupi baadaye, walifika askari wanne waliokuwa wamepakizana kwenye pikipiki mbili, maarufu kama tigo ambao niliwaona wakianza kuwarudisha watu nyuma kutoka pale mwili wangu ulipokuwa umelala.
Mmoja wao alisogea jirani kabisa, nikamuona akiuchunguza mwili wangu kisha akaugusa shingoni kama anayesikiliza mapigo ya moyo, nikamuona akiinuka na kuwasogelea wenzake, wakawa wanazungumza jambo ambalo sikuelewa ni nini. Mmoja akatoa simu ya upepo (radio call) na akawa anazungumza na upande wa pili.
Nikiwa bado naendelea kushangaa kwani kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, nilianza kusikia ving’ora kwa mbali, nikakumbuka kwamba kabla sijapoteza fahamu kutokana na kutokwa na damu nyingi, nilivisikia tena ving’ora hivyo lakini tofauti yake ni kwamba sasa nilikuwa na uwezo wa kuona kila kilichokuwa kinaendelea.
Lilikuwa ni gari la kubebea wagonjwa (ambulance) ambalo lilikuwa likija kwa kasi eneo lile mwili wangu ulipokuwepo. Nyuma yake lilikuwa limeongozana na difenda ya polisi ambayo niliitambua kwa urahisi kutokana na namba zake za usajili na maandishi yaliyokuwa ubavuni yaliyosomeka ‘Police’.
Wale askari waliokuwepo eneo la tukio waliwatawanya watu upande ule ile ambulance ilikokuwa inatokea, gari likasogea mpaka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo.
Likasimama ambapo manesi wanne waliovalia nguo nyeupe waliteremka wakiwa na machela, sambamba na askari kadhaa waliokuwa kwenye ile difenda, wote wakasogea na kuuzunguka mwili wangu.
Wakasaidiana kuuinua mwili wangu pale chini na kuulaza kwenye machela kisha wakauingiza kwenye ambulance. Nilimuona Justice naye akipanda. Raya yeye alipakizwa kwenye lile gari la polisi akiwa hajitambui.
Gari likaondoka kwa kasi kubwa likifuatiwa na difenda kwa nyuma, wale askari wa pikipiki waliendelea kuwepo pale eneo la tukio kwa dakika kadhaa wakiwa makini kuwasikiliza watu walichokuwa wanakisema huku wakiwahoji wengine kadhaa.
Kwa muda wote huo, bado nilikuwa najiuliza kilichotokea bila kupata majibu, sikuelewa nipo kwenye hali gani kwa sababu kama ni mwili wangu, tayari ulishapakizwa kwenye ambulance na kukimbizwa hospitali lakini nilishangaa mimi bado nipo eneo lile nikielea angani.
Nilijiuliza ule mwili wangu unapelekwa wapi lakini pia sikupata majibu. Ghafla nilipata wazo la kuifukuzia ile ambulance ili nijue wanaupeleka wapi mwili wangu. Wazo nililoona linafaa, ilikuwa ni kushuka chini na kuchukua bodaboda kwani niliamini kutokana na foleni iliyokuwepo na kasi ya ambulance, ni usafiri huo pekee ndiyo unaoweza kuniwahisha.
Nilishuka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo muda mfupi uliopita, watu wakawa wameshaanza kutawanyika huku wengine wakijikusanya vikundivikundi pembeni na kujadiliana kuhusu kilichotokea. Nilimsikia mzee mmoja akiwaambia wenzake: “Kwa hali aliyonayo, hawezi kupona, lazima afe.”
Nikashtuka sana kusikia kauli hiyo kwa sababu sikujua wanamzungumzia nani kwamba lazima afe wakati mimi bado nilikuwa hai na nilikuwa nawasikia wanachokisema.
Sikutaka kupoteza muda, harakaharaka nilisogea pembeni ya barabara na kupunga mkono kusimamisha bodaboda, japokuwa dereva alikuwa akija upande wangu, nilishangaa akinipita kama hajaniona. Akaja wa pili naye licha ya kumpungia mkono kwa nguvu hakusimama, akanipita kwa kasi.
Nilijitazama vizuri mwilini kwani nilihisi huenda wanaogopa kusimama kutokana na mwili wangu kulowa damu lakini kituambacho pia nilishindwa kukielewa, shati nililokuwa nimevaa halikuwa na hata tone la damu. Lilikuwa ni shati lilelile ambalo mwili wangu wakati unatolewa eneo lile lilikuwa halitamaniki kwa damu.
Nilishindwa kuelewa ni nini hasa kimetokea, nikajitazama vizuri mwili wangu na kugundua kwamba ulikuwa na hali fulani kama ya kung’aa kusiko kwa kawaida, nilijishika pale kifuani lakini hapakuwa na alama kwamba nilikuwa nimejeruhiwa vibaya, nikazidi kuchanganyikiwa.
Ilibidi nisogee mpaka kwenye maegesho ya bodaboda nikiamini pale itakuwa rahisi kuzungumza na dereva yoyote ili aniwahishe kabla ile ambulance haijapotea kabisa. Nilipopiga hatua moja nilijiona kuwa mwepesi sana halafu tambo lilikuwa refu sana tofauti na kawaida. Sehemu ambayo ningetembea hata hatua ishirini, nilipiga hatua mbili tu, nikawa nimeshafika pale kwenye bodaboda.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Unataka kuongea na me shem kwaniNapatikana ndioo
Yaaan bandika banduaNackia umetekwa maana hali ya hewa inaruhusu
Aiseee mambo za kuquote story nzima yaan mood ya kuendelea kuweka imeniisha mimiHii ntaisoma baadae shem ..
Mimi ndioooWewe![]()
Weka moja moja tupate mda wa kusoma shemILIPOISHIA:
NILISHANGAA kugundua kwamba ukiachilia mbali meseji mbili za rafiki zangu, Justice na Prosper, nyingine zote zilikuwa zimetoka kwa yule msichana aliyekosea namba ya simu, nikashusha pumzi ndefu na kuanza kuzisoma, moja baada ya nyingine nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kuona ameandika nini.
SASA ENDELEA…
YA kwanza ilisomeka: “Samahani kaka Jamal naomba tuchati kama hutajali.” Nikaisoma na kuirudia zaidi ya mara mbili, sikuelewa maana ya yeye kuomba tuchati ni nini kwa sababu tayari nilishamwambia amekosea namba na mwenyewe akakiri hilo.
Hakuishia hapo, meseji nyingine ikasomeka: “Nina tatizo kubwa nilikuwa nahitaji mtu wa kumshirikisha ndiyo maana nikawa nimempigia simu ndugu yangu mmoja aitwaye Moses lakini baada ya kusikia sauti yako, naamini na wewe unaweza kuwa na busara na kunisaidia nini cha kufanya.”
“Mbona hunijibu?” ilisomeka meseji nyingine, nikawa naendelea kuzisoma moja baada ya nyingine ambapo msichana huyo alianza kulalamika kwamba nimemdharau ndiyo maana nilikuwa sitaki kujibu meseji zake, mwisho akaniambia nisimfikirie vibaya na kama ameniudhi anaomba nimsamehe.
Nilishusha pumzi ndefu baada ya kumaliza kusoma meseji zote, nikatafakari kwa kina nikiwa sijui lengo la msichana huyo ni nini hasa. Sina desturi ya kumdharau mtu hata mara moja, hasa anaponiambia ana matatizo. Huwa naamini kwamba hata kama huwezi kumsaidia mtu kwa namna nyingine, ushauri wa kimawazo unaweza kuwa msaada tosha kwake.
Ilibidi nichukue simu yangu na kupiga namba ya yule dada aliyeniambia kwamba anaitwa Shenaiza. Ilipoanza kuita tu, harakaharaka alipokea, nikamueleza kwa nini nilichelewa kujibu meseji zake.
“Nilikuwa na kazi naifanya ndiyo maana sijakujibu, nisamehe kwa hilo,” nilimwambia, harakaharaka akaniambia nisijali na anashukuru kwa kuwa nimempigia kwani tayari alishaanza kujisikia vibaya ndani ya nafsi yake. “Umeniambia una tatizo, naweza kukusikiliza tafadhali,” nilimuuliza kwa sauti ya kiungwana, nikamsikia akishusha pumzi ndefu kisha akaniuliza mahali nilipo.
“Nipo nyumbani, Mikocheni.”
“Mimi nipo Ilala, tunaweza kuonana tafadhali kama hutajali.”
“Mh!” niliguna, nilishindwa kuelewa msichana huyo anataka nini. Haikuwa kawaida yangu kuonana na watu nisiowajua, yaani dakika chache zilizopita mtu anakupigia simu na kukueleza kwamba amekosea namba, muda mfupi tena baadaye anakueleza kwamba ana shida muhimu na anataka kuonana na wewe? Nilijiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.
Nimewahi kusikia visa vya watu wengi hasa jijini Dar es Salaam ambao walitekwa na kwenda kufanyiwa vitu vibaya baada ya kutegeshewa wanawake. Wengi wanaamini ni wanaume wachache sana wanaoweza kuepuka kishawishi cha mwanamke anayekupigia simu na kuomba kuonana na wewe, hata kama hamfahamiani.
“Hapana, haitawezekana dada’angu, tuzungumze tu kwa simu, leo nina kazi sana,” nilimkatalia kijanja. Msichana huyo aliendelea kung’ang’ania akitaka kuonana na mimi lakini kwa sababu za kiusalama, niliendelea kushikilia msimamo wangu.
Alipoona nimekuwa mgumu, aliniomba basi nipange siku na mahali ambapo tutaonana kwa sababu anahisi kwamba huenda nina wasiwasi naye, nikamwambia asiwe na wasiwasi siku nitakayokuwa na nafasi nitamtaarifu.
“Ila naomba iwe haraka, nina tatizo kubwa mwenzio,” alisema huku sauti yake ikionyesha kwamba alikuwa na huzuni kali ndani ya moyo wake. Nilikata simu na kujilaza kitandani, nikashusha pumzi ndefu na kuendelea kujiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.
Kwa muda mfupi tu niliozungumza naye, tayari tulikuwa kama watu ambao tumefahamiana miaka mingi iliyopita. Sauti yake ilionyesha alikuwa na jambo zito ndani ya moyo wake lakini sikutaka kuwa mwepesi na kujiingiza kichwakichwa, nilikuwa tayari kutoa msaada wowote ambao angeuhitaji lakini pia nilihitaji kuwa na uhakika na maisha yangu.
Muda uliendelea kuyoyoma, kwa kuwa siku hiyo nilikuwa mapumziko nyumbani baada ya kazi za wiki nzima, niliutumia muda wangu mwingi kufanya usafi ndani kwangu, kufua nguo za kazini pamoja na za kushindia na baada ya kumaliza, nilirudi na kuendelea kutazama muvi. Jioni nilitoka na kwenda kwenye mgahawa uliokuwa jirani na pale nilipokuwa naishi, japokuwa nilikuwa nimekamilika kimaisha, nilikuwa mvivu sana kwenye suala zima la kupika kama walivyo vijana wengi ambao hawajaoa.
Kwa hiyo shughuli nyingine zote nilikuwa nikizifanya kwa mikono yangu isipokuwa jambo moja tu; kupika. Japokuwa nilikuwa na umri ambao ningeweza kuwa na msichana wa kunisaidia majukumu madogomadogo ya nyumbani, namaanisha mpenzi lakini nilikuwa nimeamua kuishi ‘single’ hasa kutokana na maumivu makubwa ya moyo niliyoyapata katika uhusiano wangu uliopita.
Tangu nilipoanza kuwa na akili za kikubwa, nilikuwa nimetoka na wasichana wawili tu, tena kwa nyakati tofauti lakini mambo niliyokutana nayo, yalinifanya nisitamani tena kuwa na mpenzi. Nikaamua kutuliza moyo mpaka umri wa kuoa utakapofika na huo ndiyo ulikuwa msimamo wangu.
Baada ya kupata chakula cha jioni, nilirudi nyumbani kwangu na kuendelea na mapumziko yangu. Majira ya kama saa tatu za usiku, yule msichana alinitumia tena ujumbe akinitakia usiku mwema, nami nikamjibu na tukawa tumeishia hapo kwa siku hiyo.
Kesho yake asubuhi, niliwahi kuamka na kuanza kujiandaa kuelekea kazini kama kawaida. Mahali nilipokuwa nafanya kazi, hapakuwa mbali sana na nyumbani kwangu kwa hiyo nilikuwa nikipanda daladala au wakati mwingine nikiwa na fedha za ziada, nakodi Bajaj au bodaboda.
Nilikuwa nikifanya kazi kwenye kampuni ya ukandarasi ya Collins Constructors & Civil Engineering, Mbezi Beach nikiwa kwenye kitengo cha usanifu wa ramani za majengo au kwa Kiingereza Architecture.
Sikuwa nimeanza kazi muda mrefu kwa sababu ndiyo kwanza nilikuwa nimehitimu masomo yangu ya chuo kikuu. Nikiwa kazini, niliendelea na majukumu yangu kama kawaida, ilipofika majira ya kama saa nne, muda ambao kwa kawaida huwa tunapumzika dakika chache kwa ajili ya kifungua kinywa, Shenaiza alinipigia simu kwa lengo la kunijulia hali, tukazungumza kawaida tu kisha akakata simu.
Niliendelea na kazi na kutokana na ubize wangu, sikushika tena simu mpaka saa kumi na moja jioni, muda ambao kwa kawaida huwa tunatoka kazini. Niliposhika simu yangu, nilikutana na ‘missed calls’ nyingi za Shenaiza na ujumbe mmoja ulionishtua sana moyo wangu. Aliniambia kwamba anahisi anakaribia kufa.
Ujumbe uliishia hivyo tu, nikashindwa kuelewa alikuwa anamaanisha nini? Ilibidi nimpigie, simu yake ikawa inaita tu bila kupokelewa. Nilipiga tena na tena lakini hakukuwa na majibu, nikapatwa na wasiwasi mkubwa ndani ya moyo wangu.
Sikujua msichana huyo amepatwa na nini, nikajihisi kuwa na hatia kwa sababu pengine kama ningekubali kuonana naye jana yake alipotaka nifanye hivyo, ningeweza kuelewa nini kinachomsumbua na pengine ningeweza kumsaidia.
Niliondoka kazini nikiwa ni kama nimechanganyikiwa, sikuwa namjua Shenaiza lakini sijui kwa nini nilihisi kama matatizo yake yalikuwa yakinihusu sana. Nikiwa kwenye kituo cha daladala nikiendelea kusubiri usafiri, ujumbe mfupi uliingia kwenye simu yangu, ulisomeka:
“Mwenye simu hii amelazwa Hospitali ya Amana, Ilala. Hali yake ni mbaya, hawezi kuzungumza.”
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue