
*KINYWA CHA YESU*
Kinywa cha Yesu kilijawa na

Neno la Uzima

Neno la Faraja

Neno la Hekima

Neno la Maarifa

Neno la Haki

Neno la Hukumu

Neno la Rehema

Neno la Upendo
Katika haya machache neno kuu
Lililo kinywani Mwa Bwana Yesu
Ni maneno mawili tu nayo ni

*Neno la Rehema*

*Neno la Upendo*
Katika maneno haya mawili lililo
Kuu zaidi ni *Upendo* ndilo neno
Lililo jawa ndani ya Mungu Mwana
Neno hili la *Upendo* ni Neno liletalo
Faraja kwa kila amwaminiye Yesu
Kristo kuwa ni Bwana na Mwokozi
Wa Maisha yake.
Ndiyo maana leo watu hukusanyika
Katika nyumba za ibada ili kupata
*Neno la Faraja* kutoka katika
*vinywa vya watumishi wa Mungu*
Najua unahitaji *Neno la Faraja*
Basi usifanye moyo wako kuwa
Kama mgumu, ilihali njia ipo
Ya kupata *Faraja*
Kama ilivyo andikwa



Mathayo 11:28-30
[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
*[29]Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;*
[30]kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.
Penda kuwa mwanafunzi wa Yesu
Hudhuria mafundisho ya Yesu
Kila wakati na kila Siku
Nawe utapata raha Nafsini mwako
Na moyo wako uta msifu Bwana.
*Neno la Faraja*