Makapuku Forum

Makapuku Forum

Nakumbuka uncle ila na wewe ulichokifanya kinajulikana na wote


...yeah, kwa kweli nilifanya kitendo cha kishujaa sana, hadharani. Hakuna aliyeamini hata uncle mkubwa alipigwa butwaa nilipojitokeza hadharani na cheti cha kupongezwa kama mfanyakazi mwenyenidhamu. Hakuna ambaye hakujua

giphy.gif
 
Mungu Baba ktk jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, ninakisogelea kiti chako cha rehema kwa moyo wa shukurani na taadhima kwa ulinzi ulio tufanyia usiku wa jana na leo hii siku ya Ijumaa, Baba ututakase kwa damu ya ukombozi ya mwanao Yesu Kristo kwa makosa yetu yote tuliyo kukosea kwa mawazo yetu, maneno na matendo.
Baba tunajikabidhi tena pamoja na shughuli zetu, kanisa lako, familia zetu,nchi yetu na watu wote.
Nimeomba haya pamoja na ambayo sijayaomba ktk jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo Aaamin

MBARIKIWE SANA

Asante BH kwa kuniombea
 
Muziki: Shika Shikamana

Ni masaa machache tu tuifikie Furahiday, na kama hujua basi jua leo kuwa hii ya kesho ni siku tu kama siku nyingine katika wiki. hakuna kitakachobadilika na salmu yangu kwako Kapuku mheshimika itabaki kuwa kama ya siku zote. Wewe ni mtu makini ndo maana uko hapa na uwepo wako humu Jukwaani tunaufurahia na unalijua hilo.

Asante sana shululu kwa kubadili avatar, oh sorry kwa magazeti, mjomba wangu Lyon Lee kwa UF bila kumsahau wangu, mi amor husna muba kwa Historia na picha, nasikitika mara nyingi nashindwa kuweka picha katika kipengele chako ulichokimudu kikamilifu. Asante BlessedHope kwa kutukumuka katika sala zako, ujue nini, hili ni very pasono from me to you, unatufanya tujisikie vizuri.

Hakuna KF bila wewe makaveli10 , Gentries , Tumosa , moneytalk , Transcend , mzeewakungoa , Shunie , Mndali ndanyelakakomu , Mkushi wa kusi , na wewe ambaye nimesahau kukutaja hapa, mjue nini, uwepo wenu hapa KF unanifanya najisikia salama sana kama nimekaribishwa polisi kwenda kuwasaidia. Si unaujua ule msemo wao wa tunakutafuta uje utusaidie upelelezi au tunamhifadhi kwa usalama wake. Asanteni sana nyie watu.

Muziki sasa, wiki la reggae hili na nani kakwambia kwenye reggae hubambii kama hujambabikiziwa. Ukishika shikamana, sijui kama ni kushika au kushikwa, utatafakari mwenyewe maana usiku sasa


Better late than never ..Asante Obe nafurahia sana Muziki hasa wako uchaguzi wako ni sahihi...Mungu akubariki sanasana ....siku njema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom