Muziki: Jumatatu ya Teknolojia
Ninajiaminisha kuwa Kapuku, yes, wewe unayenisoma muda huu, umekuwa na Jumatatu nzuri kabisa na hasa kwa kuwa kuanzia Ijumaa ilikuwa ni mapumziko mazuri ya Eid ambayo kiukweli hayakuendana na mialiko tuliyoizoea awamu zilizopita. Yote kheri tu na maisha yanasonga.
Asante kwa wote mnaolifanya Jukwaa hili kuwa sehemu nzuri ya kufurahia, kujifunza, kufundishana na zaidi kupata maarifa, tunafanya vizuri hadi nahisi tukiendelea hivi majukwaa mengine yatakufa. Ha ahahaha, unacheka kwa sababu unajua haiwezekani, lol, inawezekana sana tu maana kuwepo kwako hapa ni sababu tosha kabisa ya kuyatia 'joto' majukwaa mengine. Asante kwa kuwepo hapa.
Muziki sasa, teknolojia ina mammbo mazuri lakini usisahau kuwa inaweza leta mambo yasiyosahihi cha msingi ni wewe mtumiaji kujitambua na kuifanya teknolojia. Kwanini ninaandika haya, mnajua napenda kushare, well, sio kuwapa nilichonacho bali nawajulisha tu nimenunua Samsung Galaxy new model, naamini suala la emoji halitanisumbua tena. Ungana nami kwenye kufurahia manunuzi ya simu mpya, na kama unajua kujiunga na kifurushi cha chuo please nielekeze