Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muwe na usiku mwema kwenu mlindwe na damu ya Yesu Kristo toka msalabani
ae4cce5b797326db4fb383a00670698c.jpg
 
Muziki: Jumatatu ya Teknolojia

Ninajiaminisha kuwa Kapuku, yes, wewe unayenisoma muda huu, umekuwa na Jumatatu nzuri kabisa na hasa kwa kuwa kuanzia Ijumaa ilikuwa ni mapumziko mazuri ya Eid ambayo kiukweli hayakuendana na mialiko tuliyoizoea awamu zilizopita. Yote kheri tu na maisha yanasonga.

Asante kwa wote mnaolifanya Jukwaa hili kuwa sehemu nzuri ya kufurahia, kujifunza, kufundishana na zaidi kupata maarifa, tunafanya vizuri hadi nahisi tukiendelea hivi majukwaa mengine yatakufa. Ha ahahaha, unacheka kwa sababu unajua haiwezekani, lol, inawezekana sana tu maana kuwepo kwako hapa ni sababu tosha kabisa ya kuyatia 'joto' majukwaa mengine. Asante kwa kuwepo hapa.

Muziki sasa, teknolojia ina mammbo mazuri lakini usisahau kuwa inaweza leta mambo yasiyosahihi cha msingi ni wewe mtumiaji kujitambua na kuifanya teknolojia. Kwanini ninaandika haya, mnajua napenda kushare, well, sio kuwapa nilichonacho bali nawajulisha tu nimenunua Samsung Galaxy new model, naamini suala la emoji halitanisumbua tena. Ungana nami kwenye kufurahia manunuzi ya simu mpya, na kama unajua kujiunga na kifurushi cha chuo please nielekeze


Asante Obe kwa music
 
Uliiona wapi shemela
Yaan shemela tulikua wadogo kuna rafiki yetu mmoja tulienda kwao akatuambia baba kanunua kanda ya video ya popo bawa akaiiba tuione nje

Kipindi hiko hakunaga DVD basi kututolea sijui inasema popo bawa kaonekaa znz ni ya maelezo yake tu sasa sisi kuonyeshwa cover popobawa anaruka hivi ana jicho moja acha tukimbie shemela utoto bana
 
Yaan shemela tulikua wadogo kuna rafiki yetu mmoja tulienda kwao akatuambia baba kanunua kanda ya video ya popo bawa akaiiba tuione nje

Kipindi hiko hakunaga DVD basi kututolea sijui inasema popo bawa kaonekaa znz ni ya maelezo yake tu sasa sisi kuonyeshwa cover popobawa anaruka hivi ana jicho moja acha tukimbie shemela utoto bana
Haaaaahaaaa kweli utoto shemela, ilikuwa mwaka gani huyo shemela
 
Shemela si unakumbuka kipindi cha saa mpya lakini tutakoma na hiyo galaxy sijui galaxy gani binamuuuu ukuje naomba picha mie halaf uniambie ni galaxy gani


mmmh, ile saa acheni tu jamani, sasa usisahau kumtaarifu BH kuhusu mimi kuwa mmiliki wa Samsung Galaxy.

Sijajua ni toleo gani, haya mambo bhana inahitaji muda? Afu ujue inaweza kufanya screenshot, unabonyeza cha kuzimia na kuongezea sauti mara unasikia chwaaaaaa, ndo tayari tena

Natest tu mitambo kwa sasa hivi
🙂😉😀😵

Umeona
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom