Makapuku Forum

2/Dwayne Johnson

Alizaliwa mwaka 1972 tarehe 2 Mei
Yeye anajiita The Rock yaani mwamba
Kwenye mieleka ni kama vile hana mpinzani na ni mwamba kweli we waulize akina John Cena ,Triple H ,Hulk Hogan watakwambia jamaa mgumu kama mwamba wa kule Mahenge ambayo kuipasua hata kwa baruti ni mbinde
Kwenye filamu jamaa pia anafanya vizuri haswa muvi za kibabe
Pia anavuta mkwanja kupitisma mikataba ya kibiashara/matangazo Ana utajiri wa USD 145 Milioni
......
 
Weeee kumbe huyu naye alikua mcheza mieleka? Wallah nilikua sjui nampenda huyu mbaba sana

Madame S
 
Movie za huyoo jamaa ni sheeedaa.... Huwa sichoki kuziangalia
 
1/Vince McMahon
Akiwa na Stephanie
Alizaliwa Agosti 24 mwaka 1945
Ndiye baba wa Diva wa miekeka Stephanie McMahon ambaye kwa sasa kwa wanawake hana mpinzani
Alikuwa ni mcheza miekeka nguli enzi zake licha ya kuwa na umbile la kawaida
Baada ya kustaafu akaanzisha kampuni za mieleka ambazo yeye ndiyo anazoziongoza kama CEO sasa unapomuona ulingoni kashika kipaza sauti usifikiri anauza sura pale yupo kwenye biashara zake ujue
Pia keshawahi kucheza filamu kibao tu
Ana utajiri wa USD 800 Milioni
.
.
.
.
.
.
.
Shukrani kwa mliosapoti mada
Niwatakie Usiku Mwema
Tukutane Jumatatu
Mwisho
...............
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…