Makapuku Forum

Makapuku Forum

Upo sahihi
Kila nmoja ana umuhimu
Nilizungumzia watu wa mambo ya Intelejensia kama jamaa(Elyer) ndo wapo wachache ndo maana michango ya aina hiyo ipo michache
.......


Swadakta mdau, inawezekana nilielewa tofauti.

Michango ya member wa hapa haiji tu kwa kuwa mtu anataka kuandika, au aonekane kaandika.
Hata sentensi moja inayoeleweka ikiandikwa hapa hutokana na mtu kupata maarifa fulani na kisha kuyatumia kupitia ujuzi ili mwingine aelewe.

Hakuna kipya kinachoandikwa sasa, tunakuja na njia rahisi tu ya kueleweshana. Ndiyo maana unapoweka UF au zile kumi bora nia ni kufikisha maarifa kwa mwingine ambaye naye anagawa maarifa kwa namna yake. Hii ndiyo intelijensia.

Unapoandika kitu kieleweke lazima ufikiri (tasking the brain-reasoning) na hii ndo intelligence.
 
Swadakta mdau, inawezekana nilielewa tofauti.

Michango ya member wa hapa haiji tu kwa kuwa mtu anataka kuandika, au aonekane kaandika.
Hata sentensi moja inayoeleweka ikiandikwa hapa hutokana na mtu kupata maarifa fulani na kisha kuyatumia kupitia ujuzi ili mwingine aelewe.

Hakuna kipya kinachoandikwa sasa, tunakuja na njia rahisi tu ya kueleweshana. Ndiyo maana unapoweka UF au zile kumi bora nia ni kufikisha maarifa kwa mwingine ambaye naye anagawa maarifa kwa namna yake. Hii ndiyo intelijensia.

Unapoandika kitu kieleweke lazima ufikiri (tasking the brain-reasoning) na hii ndo intelligence.
Sawa mdau
Ufafanuzi wako ni kuntu
Nimependa hapo kila mtu huabdika kwa kufikiri
.......
 
Muziki: Unapendeza Ukiwa Hapa

Siku inaelekea kuisha na unajua kabisa ulikuwa na mchana wa namna gani leo. Naamini umepangilia vema namna kesho itakavyokuwa, usikonde Kapuku muheshimika, kwanza nakusalimia na kisha nasema kesho jua litawaka tena. Siku ngumu huashiria mwisho mzuri, hujachelewa.

Unajua nini mdau wa KF, huwa mara zote nashukuru na napenda kuacknowledge wote wanaochangia hapa kwa majina, wakati mwingine huwa ni ngumu, nasahau na hii haimaanishi mchango wako haujaonekana. KF kuwepo hadi kufikia ilipo leo, yes wapo waasisi walioiweka hapa, heshima kwao. Lakini jua kitu kimoja kama kiongozi lazima awe na wafuasi ambao hawajioni tofauti na kiongozi (hii ni dhana ya utawala wa kibiashara-FYI). Maarifa tunayoyapata hapa ni makubwa sana, yeah, makubwa na hayakuzuii au kutuzuia kuyasaka maarifa mahala pengine. Inasemwa mtafute elimu hadi uajemi/uchina.

Muziki sasa, leo tumwangalie Mopao, msomi mwenye shahada ya uzamili na alijikita kwenye hesabu, tunajuana tusiopenda hesabu, ha hahahahaa> natamani kuweka hesabu ya kujumlisha kutoa sijui magazijuto lakini kama sina jibu hata kama umekosea nitaona umepatia.
Burudika mdau maana umuhimu wako hapa ni wa kipekee sana na unapendeza ukiwa hapa

 
Muziki: Unapendeza Ukiwa Hapa

Siku inaelekea kuisha na unajua kabisa ulikuwa na mchana wa namna gani leo. Naamini umepangilia vema namna kesho itakavyokuwa, usikonde Kapuku muheshimika, kwanza nakusalimia na kisha nasema kesho jua litawaka tena. Siku ngumu huashiria mwisho mzuri, hujachelewa.

Unajua nini mdau wa KF, huwa mara zote nashukuru na napenda kuacknowledge wote wanaochangia hapa kwa majina, wakati mwingine huwa ni ngumu, nasahau na hii haimaanishi mchango wako haujaonekana. KF kuwepo hadi kufikia ilipo leo, yes wapo waasisi walioiweka hapa, heshima kwao. Lakini jua kitu kimoja kama kiongozi lazima awe na wafuasi ambao hawajioni tofauti na kiongozi (hii ni dhana ya utawala wa kibiashara-FYI). Maarifa tunayoyapata hapa ni makubwa sana, yeah, makubwa na hayakuzuii au kutuzuia kuyasaka maarifa mahala pengine. Inasemwa mtafute elimu hadi uajemi/uchina.

Muziki sasa, leo tumwangalie Mopao, msomi mwenye shahada ya uzamili na alijikita kwenye hesabu, tunajuana tusiopenda hesabu, ha hahahahaa> natamani kuweka hesabu ya kujumlisha kutoa sijui magazijuto lakini kama sina jibu hata kama umekosea nitaona umepatia.
Burudika mdau maana umuhimu wako hapa ni wa kipekee sana na unapendeza ukiwa hapa


Daah binamu asante aisee nilikua mdogo hii nyimbo jaman umenikumbusha mbali jaman
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom