Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ametoa "hakikisho la 100%" kwa mashabiki kuwa kipa David de Gea atakuwepo Old Trafford msimu huu mpya. (Telegraph)
Deportivo la Coruna wamempa mkataba wa miaka kumi Lucas Perez katika jitihada za kumshawishi mshambuliaji huyo wa Arsenal kurejea katika klabu yake hiyo ya zamani. (DXT Campeon)
Mazungumzo ya uhamisho wa mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28 kwenda PSG yameporomoka kutokana na bei kubwa ya ada ya uhamisho na mshahara anaodai. (Le Parisien)
Chelsea wataongeza bidii katika kutaka kumsajili kiungo wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain, 23, wiki hii ingawa huenda wakakabiliwa na ushindani kutoka Manchester City. (Express)
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.