Bitoz
JF-Expert Member
- Aug 27, 2015
- 30,823
- 126,632
MARIA & CONSOLATA WAFAULU FORM VI WAPATA DIV II PTS 10
....................................................
Hujafa hujaumbika na siku zote Mungu ni mwema na Mungu ana makusudi yake ni wa ajabu kwa sababu maajabu yake ni makubwa na ukuu wa Mungu unajidhihirisha katika muujiza wa watoto mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana kiwili wili Consolata na Maria Mwakikuti ambao sasa wana ndoto ya kujiunga chuo kikuu.
Ikumbukwe kuwa mapacha wengi wanaoungana hudumu kwa kipindi kifupi na wengine hupoteza maisha wakati madaktari wakijaribu kutumia ustadi wao wote kuwatenganisha ila wapo ambao Mungu huwaruhusu kuendelea na maisha na kuwapa mafanikio ya tele katika maisha yao
Hivyo miongoni mwa mapacha walioungana na ambao hadi sasa wanaishi na kufanya vizuri kwenye masomo yao Consolata na Maria ambao ni miongoni mwa watoto 6 kwenye familia ya Mwakikuti na Mungu, si tu, amewaruhusu kuendelea kuishi, bali pia ameanza kuonyesha maajabu yake kwa kuwapa mafanikio na kufanya vizuri kwenye masomo Mapacha hawa wameungana kuanzia kiunoni wanatumia miguu miwili ,mikono mine kila mmoja na yake na vichwa viwili kwa maana kila mmoja na kichwa chake ni wacheshi na wanaopendana kupita kiasi.
Ifahamike kuwa ingetegemewa kwamba katika dunia yao la utandawazi na uwingi wa vyombo vya habari, taarifa za kuzaliwa kwao zingepamba magazeti mengi, redio na televisheni.lakini haikuwa hivyo kwa Maria na Consolata ambao walizaliwa Hospitali ya Misheni ya Ikonda mwaka 1996. Ulemavu wao ulisababisha wafichwe na kwa wakati huo habari za kuzaliwa kwao hazikuenea sana.
Walianza kujulikana wakati walipojiunga na elimu ya msingi wakati wamisheni walipolazimika kuwahamishia watoto hao kwa mama mlezi wao na kwa wakati huo, walitafutwa walezi wawili.
Wakiwa na miaka mitatu, baba yao Alfred Mwakikuti alifariki dunia na walipofikia darasa la pili mwaka 2002, mama yao pia alifariki dunia hivyo kuwaacha wakiwa yatima. Mama yao mlezi anasema licha ya kuwa analipwa kiasi kidogo cha mshahara kutoka misheni kwa ajili ya kuwalea, bado maisha yao ni magumu sana na analazimika kulima ili aweze kukidhi mahitaji yao.
Mabinti hawa pacha walioungana kiwiliwili ambao ni yatima, Consolata na Maria Mwakikuti (19) wa Kijiji cha Ikonda wilayani Makete mkoa mpya wa Njombe, waliofanya mitihani ya kidato cha sita mwaka huu katika shule ya sekondari ya UDZUNGWA
Pacha hao walizaliwa wakiwa wameungana katika Hospitali ya Ikonda wilayani Makete, mkoani Iringa mwaka 1996.
Walifaulu mtihani wa darasa la saba mwaka 2010. Katika mtihani wa kidato cha nne kila mmoja alikuwa na namba yake ya mtihani (Maria-S. 283/0004 na Consolata S 283/0009) na walifaulu vizuri ndipo walichaguliwa kujiunga na kidato cha sita.
Pia Katika mtihani wao wa kidato cha sita kila mmoja alikuwa na namba yake (maria 0639/545 na consolata 0639/516 na wote wamefaulu kwa DIV. TWO ya point 10,,,,Wao wana ndoto za kwenda chuo kikuu kusomea ualimu.
hist-D
Kisw-C
Engl-C .
HONGERA SANA KWAO,, HAKIKA MUNGU ANA MAKUSUDI NA WATOTO HAWA.
NB;
Copied from Jf
Written by
NANGA WA DEPO
....................................................
Hujafa hujaumbika na siku zote Mungu ni mwema na Mungu ana makusudi yake ni wa ajabu kwa sababu maajabu yake ni makubwa na ukuu wa Mungu unajidhihirisha katika muujiza wa watoto mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana kiwili wili Consolata na Maria Mwakikuti ambao sasa wana ndoto ya kujiunga chuo kikuu.
Ikumbukwe kuwa mapacha wengi wanaoungana hudumu kwa kipindi kifupi na wengine hupoteza maisha wakati madaktari wakijaribu kutumia ustadi wao wote kuwatenganisha ila wapo ambao Mungu huwaruhusu kuendelea na maisha na kuwapa mafanikio ya tele katika maisha yao
Hivyo miongoni mwa mapacha walioungana na ambao hadi sasa wanaishi na kufanya vizuri kwenye masomo yao Consolata na Maria ambao ni miongoni mwa watoto 6 kwenye familia ya Mwakikuti na Mungu, si tu, amewaruhusu kuendelea kuishi, bali pia ameanza kuonyesha maajabu yake kwa kuwapa mafanikio na kufanya vizuri kwenye masomo Mapacha hawa wameungana kuanzia kiunoni wanatumia miguu miwili ,mikono mine kila mmoja na yake na vichwa viwili kwa maana kila mmoja na kichwa chake ni wacheshi na wanaopendana kupita kiasi.
Ifahamike kuwa ingetegemewa kwamba katika dunia yao la utandawazi na uwingi wa vyombo vya habari, taarifa za kuzaliwa kwao zingepamba magazeti mengi, redio na televisheni.lakini haikuwa hivyo kwa Maria na Consolata ambao walizaliwa Hospitali ya Misheni ya Ikonda mwaka 1996. Ulemavu wao ulisababisha wafichwe na kwa wakati huo habari za kuzaliwa kwao hazikuenea sana.
Walianza kujulikana wakati walipojiunga na elimu ya msingi wakati wamisheni walipolazimika kuwahamishia watoto hao kwa mama mlezi wao na kwa wakati huo, walitafutwa walezi wawili.
Wakiwa na miaka mitatu, baba yao Alfred Mwakikuti alifariki dunia na walipofikia darasa la pili mwaka 2002, mama yao pia alifariki dunia hivyo kuwaacha wakiwa yatima. Mama yao mlezi anasema licha ya kuwa analipwa kiasi kidogo cha mshahara kutoka misheni kwa ajili ya kuwalea, bado maisha yao ni magumu sana na analazimika kulima ili aweze kukidhi mahitaji yao.
Mabinti hawa pacha walioungana kiwiliwili ambao ni yatima, Consolata na Maria Mwakikuti (19) wa Kijiji cha Ikonda wilayani Makete mkoa mpya wa Njombe, waliofanya mitihani ya kidato cha sita mwaka huu katika shule ya sekondari ya UDZUNGWA
Pacha hao walizaliwa wakiwa wameungana katika Hospitali ya Ikonda wilayani Makete, mkoani Iringa mwaka 1996.
Walifaulu mtihani wa darasa la saba mwaka 2010. Katika mtihani wa kidato cha nne kila mmoja alikuwa na namba yake ya mtihani (Maria-S. 283/0004 na Consolata S 283/0009) na walifaulu vizuri ndipo walichaguliwa kujiunga na kidato cha sita.
Pia Katika mtihani wao wa kidato cha sita kila mmoja alikuwa na namba yake (maria 0639/545 na consolata 0639/516 na wote wamefaulu kwa DIV. TWO ya point 10,,,,Wao wana ndoto za kwenda chuo kikuu kusomea ualimu.
hist-D
Kisw-C
Engl-C .
HONGERA SANA KWAO,, HAKIKA MUNGU ANA MAKUSUDI NA WATOTO HAWA.
NB;
Copied from Jf
Written by
NANGA WA DEPO
