Makapuku Forum

Makapuku Forum

Bandika banduaa kama kawaidaa leoo ...uku mkiendelea kujibugia pilau sijui ndo mjazo au makinikia lakini yote sawaa.....ewaaaaah mimi nimemuwakilisha binamu kwa mama ashura ila msiulize Ashura ana miaka mingapi.....

Soon
 
SEHEMU YA 16

Lakini baada ya wiki chache toka niingie gerezani nililetewa barua. Ilikuwa siku hiyo tukiwa tunavunja mawe, niliitwa na afisa mmoja wa magereza na kunikabidhi barua. Barua ambayo sitokuja kuisahau kwani ilinitonesha zaidi na kuniliza. Barua iliyonisukuma kula kiapo kuwa sitozungumza na yeyote kuhusu yaliyonikuta. Niliamua kuishi maisha ya ukimya na ububu ndio ukazidi kuwa jirani nami. Naikumbuka sana barua ile. Kwa mwandiko tu wa nje ya ile barua nilijua fika imetoka kwa Mariam. Japo tulishaachana muda mrefu lakini hati yake niliielewa vizuri mno. Nilikumbuka mara ya mwisho kumuona na ile siku aliyokuwa analikimbilia karandinga huku akilia na kuionesha barua. Nilijua lazima ile barua ndiyo hii iliyo mikononi mwangu sasa.
Nilitulia kwenye kivuli na kuichana bahasha na kuitoa karatasi ya barua ambayo ilikuwa imeandikwa pande zote mbili kwa wino mweusi. Aaah! Macho yalinitoka na moyo kunidunda kila niliposoma neno moja baada ya lengine aliloandika Mamu.
||.........................||
"Mpendwa Hussein.
Najua sikustahili kusogea mbele ya macho yako kutokana na yale niliyokutenda siku za nyuma. Lakini naomba unisamehe ndani ya nafsi yako ili hata nitapokufa niwe nimejipunguzia walau uzito kidogo ndani ya mzigo wangu mkubwa wa dhambi. Ukweli nilikupenda lakini sikuwa mwanamke mwema kwako.
Nilikuwa msaliti wa penzi lako kwa shinikizo la maneno na ushauri wa rafiki zangu kuwa mwanaume mmoja hatoshi kwa mwanamke mrembo mwenye kuhitaji mambo mazuri kama mimi. Hivyo nilijikuta nakosa msimamo ingawa chaguo langu la kweli ulikuwa wewe. Sikuwa na mwanaume mmoja ingawa kila mwanaume aliyepata kuwa nami nilimfanya aamini yuko peke yake. Nilikuwa mwanamke muongo nisiyestahili kuigwa. Nisamehe sana kwa kile kilichotokea pale ufukweni.
Madhumuni ya barua hii si kukuumiza kwa kukukumbusha yaliyopita, bali ni kukutaka ujue kuwa una damu yako inayoishi uliyoitumbukiza tumboni mwangu miezi miwili kabla hatujatengana.
Lakini kwa bahati mbaya siku niliyokuja kwa nia ya kukwambia ukweli huu ndiyo ile siku tuligombana kwa sababu ya kile kipindi kilichosema wanawake sisi ni wauaji. Hakika nilikereka kwa kuwa mengine yalinigusa kabisa na kuniumbua moyoni. Tulipotengana nilikuchukia na kujaribu kuitoa ile mimba lakini ajabu ilishindikana na kuendelea kukua. Nilijaribu kuwasukumia wengine lakini kwa bahati mbaya miezi miwili iliyoingia mimba sikuwahi kushiriki tendo na mwanaume yeyote zaidi yako. Hesabu ya miezi iliniumbua na kuonekana sikuwa mwaminifu hata kwa yule mwanaume niliyemtegemea ambaye alikupiga pale ufukweni. Nilijikuta naachika na kubaki mwenyewe nikilea mimba yangu kubwa nyumbani. Ukipiga hesabu mwezi niliojifungua na umri wa mtoto utakumbuka kila kitu. Nilijaribu kukutafuta baada ya kujifungua ili unisamehe tuishi tena na mwanetu lakini nilipata habari tu ulihama na nikapata tetesi umeoa. Hapo nilikata tamaa ya kuwa nawe tena maishani japo nilishakula kiapo cha kuwa mwanamke mwema kwako. Lakini nilishachelewa nikajiona nisiye na bahati. Maisha yalikuwa magumu sana Hussein hasa baada ya mama kufariki ghafla. Sikuwa na chaguo zaidi ya kujiingiza kwenye biashara ya kuuza mwili wangu ili tupate kuishi vyema na kumlea mwanangu. Sikutaka tena kuwa na mwanaume mwengine wa kumpenda wala kumdanganya. Lakini mwaka mmoja baadae ndipo nikapatwa mshtuko kusikia habari juu ya kesi yako. Hakika nafsi imeniuma sana na sina imani kabisa kama kweli ulifanya mauaji.
Niliisikia sauti yako siku ile mahakamani uliposema kuwa Wanawake ni wauaji. Moyoni sikuchukia kama siku ile na nilikubaliana nawe kwa namna fulani nahisi hata kesi yako umeponzwa na mwanamke.
Nasikitika ninapomuangalia huyu mtoto ninayemuacha katika hali ya uyatima kwani hapa nilipo nami ni mgonjwa kufa. Nimegundulika nina kansa ya koo. Sitoweza kupona Hussein. Kwa mujibu wa vipimo vya madaktari wamegundua kuwa kansa yangu imesababishwa na uchafu wa mbegu za kiume uliokuwa unapenya kwenye vijitundu vya ulimi na kwenda kukaa chini ya koo. Uchafu huu ndio umetengeneza wadudu wabaya walioanza kushambulia koo pasipo mwenyewe kujua. Usishangae Hussein huo ndio ukweli. Na hii yote ilisababishwa na tabia yangu ya muda mlefu kupenda kunyonya tupu za wanaume tofauti mara kwa mara kwa lengo la kuwachanganya kimapenzi ili nipate kuwachuna vizuri. Tena wengine walimaliza haja zao mdomoni mwangu kabisa. Aaaah! starehe na ujinga wa muda mfupi leo umegharimu maisha yangu nikiwa bado nayahitaji. Najuta kumuacha mtoto ambaye najua hatomuona tena babaake kutokana na hukumu uliyopewa.
Nilikuja naye siku ile ya kesi yako na alilia sana pindi ulipotolewa kwa kusukumwa huku ukipigwa kuingizwa kwenye karandinga baada ya kusonya mahakamani.
Nakuombea Mungu akunyooshee mkono wa kheri na atende muujiza kifungo chako kiwe chepesi.
Mtoto huyu anaitwa Asha na kwa ajabu ya Mungu kukuthibishia ni mwanao, Naye nyuma ya shingo yake karibu na sikio amezaliwa na alama kama yako. Sasa ana miaka mitatu.
Japokuwa naye ni wa kike lakini huko ulipo naomba umuombee ili asije potezwa katika mkumbo na kuwa miongoni mwa Wanawake Wauaji.
Ahsante kwa kuisoma barua yangu.
Ni mimi mfu mtarajiwa MARIAM
||........................||
Nilitetemeka na kukakamaa kwa machungu machozi yakanitoka huku nikiikunjakunja ile barua ya Mamu na kuanza kugugumia kilio.
Moyo uliamini wazi kuwa huyo kweli ni mwanangu hasa baada ya kusikia kazaliwa na alama kama ile niliyokuwa nayo shingoni. Nilimkumbuka hata mwanangu wa kiume waliyemuua naye alizaliwa na alama hiyo pia na mimi nilizaliwa nayo nikiirithi toka kwa baba yangu. Niliwaza kwa kumsikitikia mwanangu ambaye nilijua fika kwa mazingira atayolelewa hatokuja kuwa kati ya wanawake wachache wema zaidi niliona kuna muuaji mwengine anaandaliwa aliyetoka kwenye mifupa yangu.
Akilini nilipagawa zaidi na kujikuta nanyanyuka na kucheka kwa sauti kubwa sana. Kicheko ambacho hakuna aliyekielewa maana yake. Lakini mwisho wa kicheko changu nilisema maneno matatu tu ambayo niliamini yanatosha kufikisha ujumbe bila maelezo. ''WANAWAKE NI WAUAJI''
Hapo ndipo nikazidi kuwa sipendi kuzungumza lakini kila mwezi nilipenda kuandika sehemu mbalimbali hadi kwenye miti maneno hayo ili hii iwe kumbukumbu na ujumbe mzuri kwa wanaume wengine wataokuja na kutoka jela hata kama nitakuwa nishakufa wakawasimulie wenzao kuwa kuna ujumbe uliachwa na mfungwa mmoja usemao wanawake ni wauaji. Niliamini kwa kufanya hivyo itatokea siku moja wanaume watatafuta maana ya huu usemi na watauelewa ukweli na kujifunza jinsi ya kuishi na wanawake hadi shetani atapohama vichwani mwao na kutokea kizazi cha wanawake wema na waliobarikiwa na hapo maumivu yote yataisha.
Lakini kwa sasa bado naona na naamini wanawake ni wauaji Kamishna.
Mimi si chizi wala si bubu kama wanavyosema. Ila kama watapuuzia haya na kuendelea kufuta maneno yangu niliyochora kwenye kila kuta, basi wajue fika wanaume wengi watazidi kuumia kwaa kuponzwa na wanawake. Pia hata wanawake wachache wema watazidi kutoweka kwa kuponzwa na hawa wauaji ambao ndio wengi sana ulimwenguni.
Na hiyo ndiyo hadithi ya kweli juu ya kisa kilichonifanya niwe hapa miaka yote na niwe hivi mwanangu. Nakushukuru kwa kuniita baba kwani sikuwahi kuitwa jina hilo wala kutegemea. Mwanangu walimuua akiwa mdogo na yule aliye hai sijawahi kupata salamu zozote. Sijapata taarifa yoyote toka kwa mtu yoyote aliyenijua. Si mjomba, si ba mkubwa hata yule rafiki yangu pia. Miaka yote hiyo sikuota kama siku moja nitakuja kunyanyua mdomo wangu kuhadithia ukweli huu ambao ulibaki kuwa siri gizani. Mungu akubariki sana mwanangu pia naomba ujifunze sana usije pata matatizo kwa sababu ya wanawake kwani namkumbuka yule mlemavu alisema 'sio lazima hadi uje uwe kilema kama mimi bali yanaweza kukukuta kwa mtindo tofauti na ukajuta'
Ona mimi yamenikuta hivi...! Je wewe ukizembea yatakukutaje? Ishi nao kwa umakini mwanangu. Sisemi kwamba uwachukie wanawake kama mimi, la hasha!! Kwa kuwa hayajakukuta unapaswa kuwapenda na kuwaonesha thamani kwa kukumbuka fadhila kuwa hawa ndio mama zetu. Tulikulia kwenye matumbo yao lakini kamwe imani isizidi upendo. Wapende sana lakini usiwaamini sana kwa kuwa wanaweza kukubadilikia pasipo hata kupanga wakubadilikie. Siku zote wanaponzwa na utashi wa fahamu zao. Hufikiri baada ya kitendo na wanapoamua lao hawarudi nyuma. Wapo wanawake wanaowaroga wanaume zao ili wazidi kuwapenda ndani ya nyumba. Wapo wanawake wanaowapa watoto baba ambao kiuhalisia wanajua si baba zao. Wapo watoto wenye baba zaidi ya wawili na wote wanahudumia pasipo kujua. Haya yote na mengine mengi yanatendwa na wanawake pasipo kufikiria athali ya baadae. Usimlaumu mwanaume anayemuua mwanamke kinyama ukamuona muuaji, wanawake wanakera wanaweza kukufanya mwanaume ufanye kitu ambacho hujawahi kufikiria. Wapo wanaume wanakosana hadi na familia kwa sababu ya wanawake. Daaah! wanawake ni viumbe wa ajabu sana mwanangu Kamishna. Siku zote ishi kwa kukumbuka kuwa WANAWAKE NI WAUAJI hapo utaishi nao vyema na hutozembea.

*____*____*
|||||||||||||||

Alimaliza babu Hussein bubu kumuhadithia mkasa wake kamishna Shaaban Mwinchande aliyebaki ameshika tama machozi yakimtoka. Walijikuta wamekesha baada ya kugundua ishatimu saa kumi na moja alfajiri. Kamishna alisimama na kumkumbatia Hussein huku akimfariji kwa maneno mazuri ya kutia moyo.
"Pole sana baba. Ila naomba ukumbuke kuwa jela haimaanishi sawa na kutokuwa duniani. Unachopaswa ni kumshukuru Mungu na kumtumaini yeye kwani hujui kilicho mbele yake. Mungu ni mwema na kila afanyalo ni kamilifu. Amini kama amekuandikia hutofia jela basi kuna maana kubwa ya kuwa hapa na lazima utatoka siku moja." Maneno ya Kamishna Shebby yalimfanya Hussein atoe machozi ya furaha na kumkumbata nae. Hakuamini Hussein kama siku moja atapata faraja ndani ya gereza kama ile anayoipata, tena kutoka kwa askari mwenye cheo kikubwa?!. Hakika hakuwahi kuiota wala kufikiria. Naye Kamishna Shebby alijiapiza moyoni mwake na kuweka naziri ya kumsaidia Hussein kwa kuutafuta ukweli wote uliojificha nyuma ya pazia. Kubwa lililomuumiza moyo ni habari za Mr. X ambaye hata Hussein hakujua alikuwa nani hasa?.....Pia kama Zai yuko hai kweli ama alikufa naye? Na kama yuko hai mwanamke aliyeuawa ni nani...?! Na kwanini baba mkubwa alibatilisha ahadi yake na kumsariti Hussein dakika za mwisho?......!!?
Hayo yalikuwa baadhi tu ya maswali mengi yaliyojaa kichwani mwa kamishna Shebby ambayo alijiapiza kuyatafutia majibu yake kwa udi na uvumba bila kujali miaka mingapi ilipita.

Je, ataweza?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom