Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Kuelekea Furahiday

Najua mmekuwa na siku nzuri na zaidi ni siku nzuri kwa sababu tunaelekea kuitafuta Ijumaa. Na kwa wote waliofunga na mimi ninayefunga usiku ninapolala na kufungulia mchana naamini leo zimebaki siku hazijai kiganjani nifungulie. Au ninaweza kufunga hata zile sita kama hali itaruhusu. Una tatizo na hili?

Habari za kuuawa polisi kule Kibiti hazivutii hata kidogo, hakuna kifo kidogo wala kikubwa lakini ni tatizo kubwa sana pale askari wa polisi anapouawa. Hakuna jambazi anayeua polisi, amini hilo nakwambia. Ikitokea polisi anauawa basi tambua kuwa kuna zaidi ya ujambazi. Pole kwa familia za askari polisi waliuouawa wakitimiza wajibu wao. Maneno haya hayamaanishi nawapenda polisi, namchukia anayeua polisi wetu, hii si sawa hata kidogo. Hili ulijue pia na sitojali utatafasiri vipi, polisi wanatulinda na tuko salama sana kwa sababu wao wapo hata kama wana makandokando kibao yanayokera. Hongera kwetu tunaowachukia polisi wachache wanaonyanyasa raia ila tunalaani kwa nguvu zote polisi wetu wazuri kuuawa na maharamia tunayokaa nayo mtaani.

Sina mengi leo ila leo nimeamka kipinzani pinzani tu utasema sijui ni diwani wa kata gani sijui. Hivi ni sahihi kabisa kusema binti/mtoto wa kike anapopata mimba asisomeshwe? Naamini hii si sawa na ninaweza kukubaliana kutokubaliana nawe kuwa kila mtoto ana haki ya kusoma maana ni haki ya msingi ya kila mmoja, anayechepuka na kuchepukia. Tumuache mwanafunzi anayebahatika kupata mimba asome akiwa na uwezo wa kusoma. Tuna mengi ya kukarabati, mimba za mwanafunzi si tatizo la kutufanya tupayuke kama mpagawa.

Maslahi hapa, nina binti mdogo na nitajitahidi kumfanya (umri ukifika)ajue kuwa kupata mimba si jambo baya na la kulaaniwa au kukoseshwa fursa ikiwemo elimu. Nitamsisistiza kuwa kuna umri na kupanga ni kuchagua

Muziki ni furaha na kesho ndo hiyo tena, burudika na huyu mdada machachari wa enzi zake diana King, binafsi napenda wimbo wake wa Tenderness lakini siuweki leo huo nakuwekea reggae/dancehall iliyobamba miaka hiyo.

Uwe na wakati mzuri Kapuku mwenzangu


Asante kwa music kiongozi Obe
 
Muziki: Kuelekea Furahiday

Najua mmekuwa na siku nzuri na zaidi ni siku nzuri kwa sababu tunaelekea kuitafuta Ijumaa. Na kwa wote waliofunga na mimi ninayefunga usiku ninapolala na kufungulia mchana naamini leo zimebaki siku hazijai kiganjani nifungulie. Au ninaweza kufunga hata zile sita kama hali itaruhusu. Una tatizo na hili?

Habari za kuuawa polisi kule Kibiti hazivutii hata kidogo, hakuna kifo kidogo wala kikubwa lakini ni tatizo kubwa sana pale askari wa polisi anapouawa. Hakuna jambazi anayeua polisi, amini hilo nakwambia. Ikitokea polisi anauawa basi tambua kuwa kuna zaidi ya ujambazi. Pole kwa familia za askari polisi waliuouawa wakitimiza wajibu wao. Maneno haya hayamaanishi nawapenda polisi, namchukia anayeua polisi wetu, hii si sawa hata kidogo. Hili ulijue pia na sitojali utatafasiri vipi, polisi wanatulinda na tuko salama sana kwa sababu wao wapo hata kama wana makandokando kibao yanayokera. Hongera kwetu tunaowachukia polisi wachache wanaonyanyasa raia ila tunalaani kwa nguvu zote polisi wetu wazuri kuuawa na maharamia tunayokaa nayo mtaani.

Sina mengi leo ila leo nimeamka kipinzani pinzani tu utasema sijui ni diwani wa kata gani sijui. Hivi ni sahihi kabisa kusema binti/mtoto wa kike anapopata mimba asisomeshwe? Naamini hii si sawa na ninaweza kukubaliana kutokubaliana nawe kuwa kila mtoto ana haki ya kusoma maana ni haki ya msingi ya kila mmoja, anayechepuka na kuchepukia. Tumuache mwanafunzi anayebahatika kupata mimba asome akiwa na uwezo wa kusoma. Tuna mengi ya kukarabati, mimba za mwanafunzi si tatizo la kutufanya tupayuke kama mpagawa.

Maslahi hapa, nina binti mdogo na nitajitahidi kumfanya (umri ukifika)ajue kuwa kupata mimba si jambo baya na la kulaaniwa au kukoseshwa fursa ikiwemo elimu. Nitamsisistiza kuwa kuna umri na kupanga ni kuchagua

Muziki ni furaha na kesho ndo hiyo tena, burudika na huyu mdada machachari wa enzi zake diana King, binafsi napenda wimbo wake wa Tenderness lakini siuweki leo huo nakuwekea reggae/dancehall iliyobamba miaka hiyo.

Uwe na wakati mzuri Kapuku mwenzangu


ASANTE OBE...SPEECHLESS...UBARIKIWE
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom