Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Kuhama Mtaa

Ninyi ni watu wema sana, huwa nakuwa na wakati mzuri sana nikiwa hapa na hili si uongo wala makidai, Ndo ukweli na ukweli siku zote hata ukifukiwa futi sita chini utaibuka tu, huwa ni suala la muda tu na wala si kitu kingine. Hongera kwetu tunaojitahidi angalau kusema kweli japo mara chache kuliko nyingi za uongo. Sisi ni binadamu.

Nimefurahia segment ya Makapuku TV, hii itakuwa ni bomb, hoping itapangwa muda mzuri ili zisiingiliane na nyingine.

Jana nilipotea, yeah, ni vizuri nikashare nanyi maana tangu mwenye nyumba aanze kunisalimia kila siku (salamu maana yake anakumbushia nilipe kodi ya nyumba, ni haki yake lakini si kwa salamu zinazozidi kipimo). Nimeamua kuhama, naamu nahama maana kwanza nimesikia tetesi anaongeza kodi ya nyumba. Ni nyumba yake afanye analotaka na kodi ni yangu naamua navyotaka.

Mnakumbuka mwezi jana ulikuwa wa neema kwangu, kwanza nilinunua saa mpya, solar automatic. Then, baadaye yaani after that nikapewa simu ya tachi na funga kazi sasa nimeingiza flat scrini ndani na hapo sasa ndo maneno yalipoanza na vituko. Dirisha la chumbani limechwana mtindo wa sambusa, walitaka kupora simu wakaondoka na chaja, kama kuna member yeyote anakodisha chaja aweke tangazo, au vipi aniazime bila kuweka sharti la kurudishiwa. Mkopaji jeuri.

Nisikuchoshe bhana maana najikuta naongea sana. Kuna mtu aliniambia naongea sana kwa sababu nilichelewa kutembea, sio kosa lake maana ndo aliyenizaa.

Muziki na kuhama leo, nimekupigisha sound mvua hapo juu lakini lengo langu nataka tu umsikize Shaggy, yeah Mr Lavalava. Enzi hizo miziki ya kutengenezwa studio ndo inawika sanaa na japo huu wimbo ni wa studio lakini nimewahi kuwaona jamaa hapa mjini wanaucheza live gitaa nyingi na vinanda, utapenda.

Hadi hapo wakati mwingine Makapuku ni sehemu nzuri kwa sababu tu wewe u sehemu yake



Tahadhari: Muziki huu raha yake uwe na simu zile za kichina zenye spika nane na subufa, wenye Samsung, LG, Iphone na nyingine za makabila ya original inabidi muwe wataulivu sisi wenye Samsing, Itel6, Yutong4 tufaudu
 
Kama ndo yule jamaa mpya afadhali tu ushemeji ufe. Nilifikiri kuwa baada ya brother Shedede ungekuwa angalau na kipindi cha ku-cool off kidogo na kuangalia upepo unakwendaje. Kumbe unaunganisha tu ka treni lisilo na breki from one relationship to another. Goodluck mama japo nahisi kama safari hii umelamba gharasha


Kila siku nasema hizi fitna nazopigwa lazima kuna mkono wa mtu tu, hii si kawaida jameni
 
Aaaargh !!!
d14163adc02b4d7dd85640b28c508d61.jpg
Shemeji shimba VP tena?!
 
Muziki: Kuhama Mtaa

Ninyi ni watu wema sana, huwa nakuwa na wakati mzuri sana nikiwa hapa na hili si uongo wala makidai, Ndo ukweli na ukweli siku zote hata ukifukiwa futi sita chini utaibuka tu, huwa ni suala la muda tu na wala si kitu kingine. Hongera kwetu tunaojitahidi angalau kusema kweli japo mara chache kuliko nyingi za uongo. Sisi ni binadamu.

Nimefurahia segment ya Makapuku TV, hii itakuwa ni bomb, hoping itapangwa muda mzuri ili zisiingiliane na nyingine.

Jana nilipotea, yeah, ni vizuri nikashare nanyi maana tangu mwenye nyumba aanze kunisalimia kila siku (salamu maana yake anakumbushia nilipe kodi ya nyumba, ni haki yake lakini si kwa salamu zinazozidi kipimo). Nimeamua kuhama, naamu nahama maana kwanza nimesikia tetesi anaongeza kodi ya nyumba. Ni nyumba yake afanye analotaka na kodi ni yangu naamua navyotaka.

Mnakumbuka mwezi jana ulikuwa wa neema kwangu, kwanza nilinunua saa mpya, solar automatic. Then, baadaye yaani after that nikapewa simu ya tachi na funga kazi sasa nimeingiza flat scrini ndani na hapo sasa ndo maneno yalipoanza na vituko. Dirisha la chumbani limechwana mtindo wa sambusa, walitaka kupora simu wakaondoka na chaja, kama kuna member yeyote anakodisha chaja aweke tangazo, au vipi aniazime bila kuweka sharti la kurudishiwa. Mkopaji jeuri.

Nisikuchoshe bhana maana najikuta naongea sana. Kuna mtu aliniambia naongea sana kwa sababu nilichelewa kutembea, sio kosa lake maana ndo aliyenizaa.

Muziki na kuhama leo, nimekupigisha sound mvua hapo juu lakini lengo langu nataka tu umsikize Shaggy, yeah Mr Lavalava. Enzi hizo miziki ya kutengenezwa studio ndo inawika sanaa na japo huu wimbo ni wa studio lakini nimewahi kuwaona jamaa hapa mjini wanaucheza live gitaa nyingi na vinanda, utapenda.

Hadi hapo wakati mwingine Makapuku ni sehemu nzuri kwa sababu tu wewe u sehemu yake



Tahadhari: Muziki huu raha yake uwe na simu zile za kichina zenye spika nane na subufa, wenye Samsung, LG, Iphone na nyingine za makabila ya original inabidi muwe wataulivu sisi wenye Samsing, Itel6, Yutong4 tufaudu

Naielewa sana hii ngoma na nakubali sana ngoma za Shaggy japo ule wild tonight aliomshirikisha Olivia huwa naupenda kuliko yoote
 
*dah!! mapenzi yanavotesaga wengi wanafikigiaga hata hatua ya kunywa sumu*
*mi mwenyewe juzi tu nimetoswa nililia hadi nikaamua kunywa FANTA*

_ulitaka nife_??



ha hahahahaaaa, hebu ukipata nafasi isome news ya huko Marikani ambayo jamaa kajiua kwa sababu mpenzi wake alikuwa akimuandikia texts akimsihi ajiue wawe kama Romeo and Juliet
 
Kama ndo yule jamaa mpya afadhali tu ushemeji ufe. Nilifikiri kuwa baada ya brother Shedede ungekuwa angalau na kipindi cha ku-cool off kidogo na kuangalia upepo unakwendaje. Kumbe unaunganisha tu ka treni lisilo na breki from one relationship to another. Goodluck mama japo nahisi kama safari hii umelamba gharasha
Yule sio km unavyofikiliA shemeji mi niko single now yule ni mpendwa tu nothing happened
 
Naielewa sana hii ngoma na nakubali sana ngoma za Shaggy japo ule wild tonight aliomshirikisha Olivia huwa naupenda kuliko yoote


Yeah, umetulia sana huo wimbo, enzi hizo naenda disco na patner wangu kavaa nguo ya kumpa uhuru anapocheza. Sio siku hizi disco si wanaume wala wanawake wamevaa jinsi hata kina Shululu wanaohesabu wanashindwa kuzihesabu
 
Hivi hii biologia kweli,ni kukosa hofu ya Mungu na kujisahau..kuna siku mkuu Bitoz alielezea jambo kuwa waangalifu sana na vitu vinavyopostiwa(kupiga picha na kupost)kumbukumbu inabaki milele hawa vijana hata kama wanaigiza si kwa umbali huu,
HOSEA 4

6.Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa;kwakuwa wewe umeyakataa maarifa,mimi nami nitakukataa wewe ,usiwe kuhani kwangu mimi;kwakuwa umeisahau sheria ya Mungu wako mimi
nami nitawasahau watoto wako

7.Kadri walivyzidishwa ,na kadri hiyohiyo walinitenda dhambi;nami nitageuza utukufu wao kuwa AIBU.

8.Hujilisha dhambi ya watu wangu,hujifurahisha moyo kwa uovu wao

9.Hata itakuwa kama walivyo watu ndivyo atakavyokua kuhani,nami nitawaadhibu kwa ajili ya njia zao,na kuwalipa kwa matendo yao.

10.Nao watakula lakini hawatashiba,watafanya zinaa lakini hawataongezeka,kwa sababu wameacha kumwangalia BWANA.

11.Uzinzi na divai na divai mpya huondoa fhamu za wanadamu

Hofu ya MUNGU NI TIBA TUWASAIDIE WATOTO VIJANA KUMJUA MUNGU KUMPENDA KUMHESHIMU ITAWASAIDIA KUEPUSHA KUIGA MAMBO YASIYO FAA

METHALI 22

6.Mlee mtoto katika njia impasayov,Naye hataicha mpaka atakapokuwa mzee

Tumuombe Mungu atusaidie na awasaidie watoto wetu,wadogo zetu,vijana wafuate njia ya Mungu na wajue kusudi l Mungu kuwaleta duniani

Shalom
Ni kweli kabisa Blessed, japo kuna watoto wanaoharibika kutokana na mazingira wanayokulia pamoja na wale wanaowazunguka, lakini wengi wao huwa ni matokeo ya wazazi wao kushindwa kuwafunza yapi maadili mema na yapi ni maadili yasiyofaa.

Unakuta wazazi wengine hata hawawapeleki watoto wao makanisani au misikitini kulingana na imani zao, wala kufuatilia maendeleo yao kiimani, ambako mtoto atafundishwa mambo mbalimbali pamoja na kumfanya mtoto kuwa na hofu ya Mungu.

Kwahiyo linapokuja swala la mtoto kufanya maamuzi ya lipi ajifunze na lipi aachane nalo wakati wa makuzi yake, imani aliyonayo (ambayo ilipaswa kujengwa na wazazi wake) ndiyo itakayomuwezesha kufanya uchaguzi wa yanayompasa na yasiyompasa kufanya.

Wazazi ndio chanzo kikubwa cha mtoto kuharibika au kufanikiwa kimaadili, kuondoa wale watoto wachache ambao labda hawana wazazi au vinginevyo.
Labda neema ya Mungu tu imfunike mtoto husika.
Kwakweli tuwaombee sana na kuwajengea misingi mizuri tangu wakiwa wadogo, hii itawasaidia sana.

Inasikitisha sana kwakweli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom