Makanisa yavunje MoU na Serikali...

Makanisa yavunje MoU na Serikali...

Sikonge, Jasusi,

..mmeeleza kwamba kuna hospitali za Moravian na Menonite ambazo hazipati ruzuku toka serikalini.

..kutokana na ukweli huo hapo juu, mashirika ya Kikristo yasibweteke na MOU, badala yake yaonyeshe ubunifu kwa kutafuta vyanzo vingine vya fedha za kuendesha shughuli zao utoaji huduma kwa jamii.

..zaidi, it is about time they gave wananchi some explanation kuhusu suala la MOU. Haiyumkiniki watu wazunguke nchi nzima wakiipiga vita MOU lakini serikali na mashirika ya Kikristo yamekaa kimya tu.

..Mimi naona huo ni UZEMBE wa hali ya juu. Kwa maana nyingine hatuwezi kuwalaumu ndugu zetu Waislamu ikiwa wataamini kwa 100% yale yote wanayoelezwa na kundi la kina Ustaadh Ilunga Kapungu, Sheikh Ponda, na Maalim Basalehe.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkapa alitoa chuo cha Tanesco kama kiini macho pesa aliwapa makanisa kupitia pesa za Mou zinajenga yale kama 100
bila ya wasiwasi wowote na nyingine zikabaki.

Chama
Gongo la mboto DSM

Chama,
I respect you. Lakini kusema kuwa pesa za MOU zinatumika kujenga shule 100 za makanisa ni uwongo mtupu. Kwa hakika sijui ni hospitali ngapi ambazo serikali imeahidi kuzipa fedha kupitia MOU ambazo zinapokea fedha hizo, Kama alivyosema Sikonge, hospitali ya Moravian mpaka sasa inapokea zero money licha ya MOU. Na mimi naweza kukuthibitisha kuwa hospitali ya Shirati, as of July this year, ilikuwa haijapokea hata senti tano za serikali ingawa ni serikali hiyo hiyo iliomba hospitali ifanywe hospitali ya rufaa ya mkoa. Kwa hiyo dhana kwamba serikali inatoa MOU kwa taasisi za makanisa na makanisa kuzitumia kupanua himaya zake ni uwongo mtupu.
 
Hey kwani kuna kundi la watu au taasisi iliyozuiwa kuwa na MoU na serikali alimradi ni kwa faida ya kundi hilo na jamii kwa ujumla??? ni suala na ajabu kusema ivunjwe badala ya kusema nasi pia tuwe na the same MoU!!!
 
Kwanza nashukuru kwa kufunguka kuwa upo USA na siyo Gongolamboto kama unavyotuandikia.

Kwa kuwa unaishi huko, yanayotokea huku SIKONGE kwa kweli huyafahamu na unafikiri ni kama USA. Ni sawa na yule binti wa mfalme aliyesema "Kama watu wana njaa, si wale keki?"

Nilimjibu Barubaru kuwa kwa Sikonge hospital, Serikali inabidi ipeleke Tsh.20 milioni kwa mwezi ambazo ni sawa na Euro 10,000 sawa na mshahara wa Gavana wa BoT. Ila kwa sasa Sikonge Hospital inapokea Tsh. 00,000 milioni kwa mwezi.


Sikonge,

Labda utudadavulie hizo Tsh 20 Million zipelekwe hospital kwa kazi gani? Je kwa ajili ya Amin cost au Ops Cost?
 
Chama,
I respect you. Lakini kusema kuwa pesa za MOU zinatumika kujenga shule 100 za makanisa ni uwongo mtupu. Kwa hakika sijui ni hospitali ngapi ambazo serikali imeahidi kuzipa fedha kupitia MOU ambazo zinapokea fedha hizo, Kama alivyosema Sikonge, hospitali ya Moravian mpaka sasa inapokea zero money licha ya MOU. Na mimi naweza kukuthibitisha kuwa hospitali ya Shirati, as of July this year, ilikuwa haijapokea hata senti tano za serikali ingawa ni serikali hiyo hiyo iliomba hospitali ifanywe hospitali ya rufaa ya mkoa. Kwa hiyo dhana kwamba serikali inatoa MOU kwa taasisi za makanisa na makanisa kuzitumia kupanua himaya zake ni uwongo mtupu.

Mkuu Jasusi;
Labda nikuwekee wazi si hospitali zote za makanisa zinapokea pesa za MoU; wapokeaji wakubwa kwenye hizi pesa za MoU ni taasisi za Kikatoliki na Kianglikan; waashauri na waandishi wa MoU ni kutoka; nimewahi kusema huko nyumba MoU haziaathiri Waislamu pekee bali wapo Wakristo wa madhehebu mengine; mkuu jasusi labda kama unataka tukewekee figure tutakuwekea; MoU ni wizi wa pesa zetu za kodi; kama ambavyo tunapiga kelele kwenye mikataba mibovu ya madini na huu pia tutaupigia kelele; huwezi ukakubali kuhusu pesa za MoU ndio zimechangia makanisa kupanua himaya zake lakini huo ndio ukweli wenyewe. Mifumuko ya vyuo na mashule uliongezeka mara tu baada ya taasisi za makanisa kupokea pesa za MoU.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Zilikuwa, nasema tena Zilikuwa zisaidie kwenye Miashahara na madawa.

Ila sasa hivi ni kichekesho kujadili Amin coast au Ops Cost kwa sababu hizo pesa HAZIPO.

Hospital ya Moravian hapa SIKONGE, tangu mwaka 2006 inajiendesha yenyewe kwa kupokea misaada nje ya MoU.

Kwa hiyo hata mkiiuwa MoU, bado zitaendelea kuishi. Ila hazitatibu tena watu kwa bei nafuu kwa kisingizio kuwa Serikali INASAIDIA baadhi ya gharama.


chama, wizi unafanyika pote tu. Hata ukiuwa MoU zote, bado watu wataiba huko huko Muhimbili. Pesa za EPA pale BoT hazikuwa pesa za MoU au kanisa. Pesa walizoteka akina Nyoni pale Wizara ya Afya hadi zikaleta ugomvi na akina Ulimboka, hazikuwa pesa za Mou au kanisa.

Pesa za MEREMETA, DEEP GREEN, nk hazikuibiwa kwa kupitia MoU au Kanisa. Nilifikiri hili utaliona na kulisema kwanza.

Tatizo la Tanzania ni zaidi ya MoU na Kanisa. Kama una AKILI kweli, basi utaliona na kulifungulia Thread yake peke yake hapa JF. Ila kama utakalia kusema kuwa kuvunja MoU kutamaliza wizi wizara ya afya.......... Sanasana watu wa vijijini ambao ndiyo masikini zaidi, wataumia.

I wish kweli tungelivunja na Makanisa yaanze kuvuta WATEJA kwa kusema "Kama wewe Mkristo, utatibiwa kwa bei nafuu na kama wewe si Mkristo, utalipia gharama kamili......" Najua mtaanza kulalamika kuwa Wakristo wanabadilisha dini Waislaam kwa kutumia huduma za hospitals na mashule.

NGO watu wanaiba sana pesa na hilo nalijua. Ila kwa Tanzania, wapi hawaibi? Ndiyo maana wengi wanaona kwa sasa, as longer CCM bado ipo madarakani, serikali na chama ambacho kimeingia kwa RUSHWA, basi Rushwa na wizi utaendelea kuwepo. Watu wanaiba kila sehemu ili wapate fedha za UCHAGUZI.

Kuna kitu kinaitwa RULE OF LAW ambacho kinalalamikiwa sana na Chadema, UNAKIFAHAMU?
Sikonge,

Labda utudadavulie hizo Tsh 20 Million zipelekwe hospital kwa kazi gani? Je kwa ajili ya Amin cost au Ops Cost?
 
Mkuu Sikonge
Kwa pole sana kwa kumpoteza mzee wako kazi ya Mungu wote tupo njia moja Mungu amlaze mahala pema.
Turudi kwenye Mada husika; sijakataa hata siku moja taasisi iwe ya kidini au za kibinafsi; zisijitoleee; tunachokataa ni wizi wa rasimali zetu kwa kutumia mgongo wa dini; nilisema awali waathirika wa hizi pesa si waislamu tu; wapo wakristo wa madhebu mengine; waandishi wa MoU walikuwa ni watendaji wa serikalini kutoka madhehebu ya kikatoliki na waanglikana; jiulize kwanini Moravian na wasabato hawapewi? Mkuu binafsi kesho ukiniambia kuna mchango unahitajika wa kusaidia kuendesha hospitali ya Sikonge nitajitolea ni utashi binafsi; hata US nachangia shule kikatoliki ingawaje mimi si mkatoliki ipo kwenye maeneo ninayoishi na kuna wakati pia najitolea kwenye vijishughuli vidogo vidogo; mkuu sijawahi kuunga mkono wizi wa Marememeta; unakumbuka mzee jaji Warioba alivyozungukwa na kusaini kitu ambacho hakukijua hadi leo hana jibu kuhusu Merememeta; ndio hivyo hivyo mzee Mwinyi alivyozungukwa mkuu huu ni wizi nadhani unatetea kitu ambacho hukijui kaa chini tafuta data za hii kitu kinachoitwa MoU; mwanzoni nilikubaliana nazo baada ya kupata datas zake niliacha kinywa wazi; hapa hapana udini tunapigania maslahi ya taifa; yakishaundwa haya matabaka; zitakuwa vurugu ambazo kuzizima hatutaweza.

Chama
Gongo la mboto DSM
 

-Waislaam wawe wanalipia gharama kwa bei ya kawaida ya kusomeshwa kwenye Mashule ya Kanisa nk.


kuna kanisa linasomesha bure waislam..au kwa bei nafuu ??! :confused2: kanisa gani hilo...? au shule gani hiyo ya kanisa inasomesha waislam bure/ kwa bei ya kawaida ..? naomba mfano ...

 
Usiende huko!
Mahospitali,Makanisa,Shule vilivyojengwa na Mkoloni kwa hela ya Watanganyika wa dini zote viliachiwa Wakristo waendelee kuvimiliki baada ya Uhuru, Nyerere aliona mbali kuwa baadaye watu watakuja kuhoji hili hivyo akaleta ubabaishaji wa kujifanya kuvitaifisha baadaye kumuachia mwingine avirudishe!

MoU, Necta, Muungano ni vitu ambavyo Wakristo hawatokubali kwa gharama yoyote ile viingiliwe kwa sababu ndiyo mihimili yenyewe ya Mfumo Kristo

Kulijuwa hili ninalolisema angalia mtaharuki uliowapata wachangiaji hapa kuhusu hoja ya Kanisa kuvunja MoU na Serikali



Kuna maelezo mengine yatolewayo humu yakiachwa yabaki hivyo yalivyo yanapotosha ukweli uliopo. Wewe Bwana unayejiita Sideeq dhana yako kuwa Mahospitali, makanisa na shule zinazomilikiwa na Makanisa zilijengwa na Mkoloni kwa hela ya Watanganyika wote si ya kweli hata kidogo. Naomba nitoe maelezo ya Kanisa Katoliki. Makanisa, Hospitali, vituo vya afya, zahanati, shule za msingi na sekondari vilijengwa wakati wa Ukoloni wa Mwingereza katika Tanganyika. Katika kipindi hicho isingewezekana serikali ya kikoloni ya Waingereza ikawapa Wakatoloki fedha za kujenga majengo kwa ajili ya kutoa huduma nilizozitaja hapo juu. Ikumbukwe kuwa Waingereza (wakiwa na dhehebu lao la Anglikana) wasingetoa fedha kwa ajili ya washindani wa dhehebu lao. Kitu kingine ambacho Bwana Sideeq unapaswa kujua ni kuwa wakati Wamisionari wa Kikatoliki walipokuja hapa Tanganyika walikuja chini ya miavuli ya mashirika yao ambayo ingawa kwa sheria za kanisa yalikuwa chini ya Papa, lakini yalikuwa tofauti. Kuna sehemu walikwenda Holy Ghost, sehemu nyingine walikwenda Wabenediktini, sehemu nyingine Wamisionari wa Afrika (White Fathers), Wakonsolata, Wajesuiti na kadhalika. Wengine kati yao walikuwa ni Wamonaki.

Hawa wote walikuwa na karama na misisitizo tofauti katika huduma zao za kimwili na kiroho kutegemea na shirika lenyewe. Mashirika mama yao huko Ulaya yaliwategemeza kwa kila kitu wakiwa hapa. Kipato cha Watanganyika wakati huo kilikuwa cha chini sana.

Makanisa yao na shule zao yalijengwa kwa fedha kutoka makao makuu ya mashirika hayo. Fedha walizopewa na makao makuu ya mashirika yao zilitolewa na waumini wa Ulaya kwa lengo la kuinjilisha nchi ambazo zilikuwa bado gizani kiimani. Hiyo desturi ya kupewa fedha kutoka Ulaya na Marekani haikuishia wakati wa ukoloni bali imeendelea hadi sasa. Katika maeneo ambayo watu wake wana umaskini wa kipato bado Wamisionari wameendelea kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule, makanisa na vituo vya afya.

Kadri ninavyofahamu mimi, hiyo MoU si kwamba inalazimishwa na Kanisa Katoliki. Kwa miaka mingi hata kabla ya utaratibu wa kuingia na makubaliano na serikali Kanisa Katoliki limekuwa likitoa huduma hizo kwa kutoza kiasi kidogo cha fedha. Lengo lilikuwa si kufanya biashara bali kurudisha gharama ili huduma iwe endelevu. Hata hivyo katika sera ya afya ya nchi hii kuna aina ya huduma za afya hutolewa na serikali bila malipo. Huduma hizo ni kama chanjo kwa watoto chini ya miaka 5, huduma kwa mama na mtoto, hiduma ya tiba kwa wazee, huduma za VVU/UKIMWI, na kadhalika. Katika maeneo ambayo hakuna hospitali au vituo vya afya vya serikali ambavyo vingetoa huduma hizo lakini kulikuwepo hospitali binafsi ( za makanisa na wengineo) serikali iliamua kushirikiana na asasi hizo binafsi ili kuisaidia serikali kutoa huduma hizo. Huwezi kuwa na ushirikiano bila kuwa na makubaliano yatakayoonyesha mipaka ya majukumu kwa kila mshirika. Huu ndiyo mwanzo wa MoU.

Inawezekana kufuta makubaliano haya ya MoU. Matokeo ni kwamba huduma zitakazotolewa na asasi hizi za Kikatoliki hazitakuwa bure tena. Watalazimika kutoza fedha kidogo ili huduma ziwe endelevu. Itabidi sasa watoto wadogo na akina mama walipie kama ambavyo tunafanya kila siku tunapokwenda hospitali za watu binafsi.

Kwa Falsafa yake Kanisa katoliki haliwezi kuwabagua watu kwa misingi yoyote ile. Wote watalipa kiasi kile kile. Athari itakayofuatia hatua hii, hasa kwa kipindi cha muda mfupi na wa kati, ni kwamba lile lengo la kudhibiti magonjwa ya kuambukiza kwa kasi litapungua. Kwa maneno mengine kasi ya vita dhidi ya magonjwa yanayosumbua watu wengi hasa mahali ambapo serikali bado haijafikisha huduma hizo itapungua.

Ninafahamu zipo hospitali na shule zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu. Hizi nazo zimeingia makubaliano na serikali pia. Kadri ya ufahamu wangu kwa shule za sekondari za Kanisa ni juhudi ya Shirika, Parokia au Jimbo husika wakishirikiana na wazazi wanaojenga na kuendesha shule hizo. Serikali kama ina mchango wowote katika shule hizo hiyo itakuwa ni kwa shule zote bila kujali anayezimiliki. Sidhani kuwa ni asasi za kikatoliki tu ambazo hupendelewa kupewa ruzuku kama ipo.

Utamaduni na desturi ya kutoa huduma za elimu na afya kwa wanadamu ni wa zamani sana katika Kanisa Katoliki. Kwa kweli ni sehemu ya wito wake wa kuinjilisha wanadamu. Hata makubaliano yakivunjwa bado wataendelea kutekeleza wajibu huo. Kwa maneno mengine wataendelea kutoa huduma hizo kwa upana na weledi zaidi. Mwaka 2000 nilitembelea jimbo la Bamenda katika nchi ya Cameroon na kufahamishwa kuwa shule bora kabisa katika nchi ile zilikuwa mbili moja ya wavulana na nyingine ya wasichana na zote zilimilikiwa na Kanisa Katoliki. Kama utagundua sasa hivi Majimbo mengi ya Kanisa Katoliki yameanzisha shule nyingi sana za sekondari na hasa za wasichana.

Kwa kumalizia, majadiliano makali kuhusu makubaliano kati ya serikali na Wakritu pengine yanakuzwa sana. Mimi ningefikiri Waziri wa Elimu na Waziri wa Afya (ambao kwa bahati nzuri ni Waislamu) wangeulizwa kwa nini makubaliano hayo yanaendelea na ni kitu gani kitatokea kama yakisitishwa. Hakuna sababu ya kuyaelekeza mashambulizi haya kwa Viongozi wa Wakristu ilhali serikali iliyoanzisha utaratibu huo ipo.

Ninashauri sisi wengine tujitahidi sana kuchimbua ukweli na tujiepusha kutoa maelezo ambayo hata sisi wenyewe tunajua kuwa si sahihi.
 
Kuna maelezo mengine yatolewayo humu yakiachwa yabaki hivyo yalivyo yanapotosha ukweli uliopo. Wewe Bwana unayejiita Sideeq dhana yako kuwa Mahospitali, makanisa na shule zinazomilikiwa na Makanisa zilijengwa na Mkoloni kwa hela ya Watanganyika wote si ya kweli hata kidogo. Naomba nitoe maelezo ya Kanisa Katoliki. Makanisa, Hospitali, vituo vya afya, zahanati, shule za msingi na sekondari vilijengwa wakati wa Ukoloni wa Mwingereza katika Tanganyika. Katika kipindi hicho isingewezekana serikali ya kikoloni ya Waingereza ikawapa Wakatoloki fedha za kujenga majengo kwa ajili ya kutoa huduma nilizozitaja hapo juu. Ikumbukwe kuwa Waingereza (wakiwa na dhehebu lao la Anglikana) wasingetoa fedha kwa ajili ya washindani wa dhehebu lao.
Isikushangaze! Wakati Muingereza akija Tanganyika tayari kulikuwa na treaty kati ya nchi za Ulaya kwa jina la Ukristo (rejea historia ya tishio la Ottoman sultan, Selim 1 dhidi ya ukristo)!
Wakatoliki wakiongozwa na Pope, mfalme wa Ufaransa akiliongoza jeshi laWaspanish, Waportugal na madhehebu yote unayoweza kuyafikiria katika Ukristo yalishafunga mikataba ya ushirikiano.
 
Chama,
I respect you. Lakini kusema kuwa pesa za MOU zinatumika kujenga shule 100 za makanisa ni uwongo mtupu. Kwa hakika sijui ni hospitali ngapi ambazo serikali imeahidi kuzipa fedha kupitia MOU ambazo zinapokea fedha hizo, Kama alivyosema Sikonge, hospitali ya Moravian mpaka sasa inapokea zero money licha ya MOU. Na mimi naweza kukuthibitisha kuwa hospitali ya Shirati, as of July this year, ilikuwa haijapokea hata senti tano za serikali ingawa ni serikali hiyo hiyo iliomba hospitali ifanywe hospitali ya rufaa ya mkoa. Kwa hiyo dhana kwamba serikali inatoa MOU kwa taasisi za makanisa na makanisa kuzitumia kupanua himaya zake ni uwongo mtupu.
Jasusi mkuu wangu hizi zahanati msifikie kuzipa jina la Hospital. Hiyo Hospital ya Moravian inalaza wagonjwa wangapi na inatoa huduma zipi hasa hasi mkaipa masifa kemkem.. Je ipo ktk ubia na orodha ya CSSC ama ndio wameomba nawasubiri kukubaliwa kuwa chama maana hutujui ni zipi zinazo qualify kupata fedha za maendeleo. Kwa hiyo unaweza tu kuongezea kwa nini hii Hospital yaMoravian hawapewi lakini sii kwamba fedha haitolewi. Billioni 90 kwa mwaka unaweza fanya mengi sana kwa asasi moja.

Na ukitazama kwa jicho hilo nenda kwetu Ukerewe halafu nambie kuna Hospital ngapi, wananchi wanatembea mwendo gani kufuata huduma hii maana hata pale mjini Nansio hakuna Huduma hiyo kwa miaka sasa. hakuna Umeme tunailalamikia Tanesco ndivyo mfumo wetu ulivyojengwa na wala sii kosa la Mtanzania kusema Tanesco ivunjwe.
Swala zima tunailalamikia serikali na kwa undani wake tunaikuta CSSC na muafaka wa MoU kwa hiyo tunashindwa kupata majibu..
 
hapana MOU haivunjwi na haitavunjwa kwa shinikizo la imani na hisia fulani za watu,serikali yenyewe ya ccm hii kwa huduma zipi tutapata kwa serikali zembe na yenye rushwa chini ya utawala wa ccm?acha tu watu wawe katika MOU tupate nagalau huduma za afya na elimu kwa upana.
serikali ingekuwa makini kuendeleza miundombinu ya uchmi wetu hapo ingeeleweka
 
Huwezi kuhukumu kitu ambacho hakijatokea unasema hata kama MoU ikivunjwa ufisadi hauwezi kuisha halafu Tanzania kuna wilaya nyingi sana hakuna huduma za afya.

Serikali kwa nini wasitumie hizo Bilioni 90 kujenga vituo vya afya wilayani wanufaike watanzania wote kuliko hizo pesa kuwapa Makanisa halafu tunakwenda kutibiwa kwa kutoa pesa hakuna nafuu yoyote...kuna sehemu nyingi tu watu wanataabika tu wakipata ugonjwa hakuna hospital.

Nenda Iramba, Ikungi, Mkalama, Tandahimba, Lutubinga, Mwakiloba, Katunguru, Kayenze, Ukara, Kagunguri, Mwabuki, Nyanguge, Nyamisangura, watu hawana huduma za afya MoU ielekezwe huko.

Tunaongelea tu sijui Moravian ya Sikonge wanatibiwa bure kisa ya Kanisa hiyo hospital inalaza wagonjwa wa ngapi na inatibu watanzania wa ngapi..MoU ni ufisadi tu kama ufisadi mwingine hata wakiristo hawafaidiki na MoU.
 
Nafikiri hili tumeliandika sana. Kama huko hukuelewa, basi hata nikikujibu hapa, bado ntakuwa nafanya hii kazi.

Only-Goat-In-The-World-That-Enjoys-Punk-Rock1.jpg

kuna kanisa linasomesha bure waislam..au kwa bei nafuu ??! :confused2: kanisa gani hilo...? au shule gani hiyo ya kanisa inasomesha waislam bure/ kwa bei ya kawaida ..? naomba mfano ...

 
Chama,

Nilishasema mapema kuwa tunaongea jambo lilelile. Ukinisoma vizuri utakuwa nimelisema hili. Tatizo siyo MoU wala makanisa. Tatizo ni Serikali yetu ya Tanzania. Ukishambulia NGO yoyote utakuwa unafanya makosa.

Ni sawa na Tatizo la UMEME kwa Tanzania ambalo hadi sasa ndiyo Waziri amesema kuwa Tanzania haijawahi kuwa na tatizo la umeme. Huu mgawo wote upo ili watu WAIBE. Pia hizi NGO nyingi zipo ili watu waibe. Nakiri kabisa kuhusu hilo. Ila wao ili wafanikiwe hilo, walikuja na gia ya MoU ili kusaidia hospital za kweli kama ya SIKONGE. Ila cha ajabu, pesa zinakwenda kwenye hospital zao na za SIKONGE zinaachwa zijichunge zenyewe ingawa wanaambiwa watibiwe watu wote kwa bei nafuu - Maajabu maana Mkono Mtupu haulambwi (Changia JF - by SIKONGE).

Nafikiri ili tusolve hili, tusililie tu kusema tuvunje MoU. Tuanze kwanza na kubadili serikali maana ndiyo mzizi wa fitina. Ikija Serikali imara, MoU zitakufa zenyewe maana serikali haitazihitaji tena.
Mkuu Sikonge
Kwa pole sana kwa kumpoteza mzee wako kazi ya Mungu wote tupo njia moja Mungu amlaze mahala pema.
Turudi kwenye Mada husika; sijakataa hata siku moja taasisi iwe ya kidini au za kibinafsi; zisijitoleee; tunachokataa ni wizi wa rasimali zetu kwa kutumia mgongo wa dini; nilisema awali waathirika wa hizi pesa si waislamu tu; wapo wakristo wa madhebu mengine; waandishi wa MoU walikuwa ni watendaji wa serikalini kutoka madhehebu ya kikatoliki na waanglikana; jiulize kwanini Moravian na wasabato hawapewi? Mkuu binafsi kesho ukiniambia kuna mchango unahitajika wa kusaidia kuendesha hospitali ya Sikonge nitajitolea ni utashi binafsi; hata US nachangia shule kikatoliki ingawaje mimi si mkatoliki ipo kwenye maeneo ninayoishi na kuna wakati pia najitolea kwenye vijishughuli vidogo vidogo; mkuu sijawahi kuunga mkono wizi wa Marememeta; unakumbuka mzee jaji Warioba alivyozungukwa na kusaini kitu ambacho hakukijua hadi leo hana jibu kuhusu Merememeta; ndio hivyo hivyo mzee Mwinyi alivyozungukwa mkuu huu ni wizi nadhani unatetea kitu ambacho hukijui kaa chini tafuta data za hii kitu kinachoitwa MoU; mwanzoni nilikubaliana nazo baada ya kupata datas zake niliacha kinywa wazi; hapa hapana udini tunapigania maslahi ya taifa; yakishaundwa haya matabaka; zitakuwa vurugu ambazo kuzizima hatutaweza.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Kuna maelezo mengine yatolewayo humu yakiachwa yabaki hivyo yalivyo yanapotosha ukweli uliopo. Wewe Bwana unayejiita Sideeq dhana yako kuwa Mahospitali, makanisa na shule zinazomilikiwa na Makanisa zilijengwa na Mkoloni kwa hela ya Watanganyika wote si ya kweli hata kidogo. Naomba nitoe maelezo ya Kanisa Katoliki. Makanisa, Hospitali, vituo vya afya, zahanati, shule za msingi na sekondari vilijengwa wakati wa Ukoloni wa Mwingereza katika Tanganyika. Katika kipindi hicho isingewezekana serikali ya kikoloni ya Waingereza ikawapa Wakatoloki fedha za kujenga majengo kwa ajili ya kutoa huduma nilizozitaja hapo juu. Ikumbukwe kuwa Waingereza (wakiwa na dhehebu lao la Anglikana) wasingetoa fedha kwa ajili ya washindani wa dhehebu lao. Kitu kingine ambacho Bwana Sideeq unapaswa kujua ni kuwa wakati Wamisionari wa Kikatoliki walipokuja hapa Tanganyika walikuja chini ya miavuli ya mashirika yao ambayo ingawa kwa sheria za kanisa yalikuwa chini ya Papa, lakini yalikuwa tofauti. Kuna sehemu walikwenda Holy Ghost, sehemu nyingine walikwenda Wabenediktini, sehemu nyingine Wamisionari wa Afrika (White Fathers), Wakonsolata, Wajesuiti na kadhalika. Wengine kati yao walikuwa ni Wamonaki.

Hawa wote walikuwa na karama na misisitizo tofauti katika huduma zao za kimwili na kiroho kutegemea na shirika lenyewe. Mashirika mama yao huko Ulaya yaliwategemeza kwa kila kitu wakiwa hapa. Kipato cha Watanganyika wakati huo kilikuwa cha chini sana.

Makanisa yao na shule zao yalijengwa kwa fedha kutoka makao makuu ya mashirika hayo. Fedha walizopewa na makao makuu ya mashirika yao zilitolewa na waumini wa Ulaya kwa lengo la kuinjilisha nchi ambazo zilikuwa bado gizani kiimani. Hiyo desturi ya kupewa fedha kutoka Ulaya na Marekani haikuishia wakati wa ukoloni bali imeendelea hadi sasa. Katika maeneo ambayo watu wake wana umaskini wa kipato bado Wamisionari wameendelea kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule, makanisa na vituo vya afya.

Kadri ninavyofahamu mimi, hiyo MoU si kwamba inalazimishwa na Kanisa Katoliki. Kwa miaka mingi hata kabla ya utaratibu wa kuingia na makubaliano na serikali Kanisa Katoliki limekuwa likitoa huduma hizo kwa kutoza kiasi kidogo cha fedha. Lengo lilikuwa si kufanya biashara bali kurudisha gharama ili huduma iwe endelevu. Hata hivyo katika sera ya afya ya nchi hii kuna aina ya huduma za afya hutolewa na serikali bila malipo. Huduma hizo ni kama chanjo kwa watoto chini ya miaka 5, huduma kwa mama na mtoto, hiduma ya tiba kwa wazee, huduma za VVU/UKIMWI, na kadhalika. Katika maeneo ambayo hakuna hospitali au vituo vya afya vya serikali ambavyo vingetoa huduma hizo lakini kulikuwepo hospitali binafsi ( za makanisa na wengineo) serikali iliamua kushirikiana na asasi hizo binafsi ili kuisaidia serikali kutoa huduma hizo. Huwezi kuwa na ushirikiano bila kuwa na makubaliano yatakayoonyesha mipaka ya majukumu kwa kila mshirika. Huu ndiyo mwanzo wa MoU.

Inawezekana kufuta makubaliano haya ya MoU. Matokeo ni kwamba huduma zitakazotolewa na asasi hizi za Kikatoliki hazitakuwa bure tena. Watalazimika kutoza fedha kidogo ili huduma ziwe endelevu. Itabidi sasa watoto wadogo na akina mama walipie kama ambavyo tunafanya kila siku tunapokwenda hospitali za watu binafsi.

Kwa Falsafa yake Kanisa katoliki haliwezi kuwabagua watu kwa misingi yoyote ile. Wote watalipa kiasi kile kile. Athari itakayofuatia hatua hii, hasa kwa kipindi cha muda mfupi na wa kati, ni kwamba lile lengo la kudhibiti magonjwa ya kuambukiza kwa kasi litapungua. Kwa maneno mengine kasi ya vita dhidi ya magonjwa yanayosumbua watu wengi hasa mahali ambapo serikali bado haijafikisha huduma hizo itapungua.

Ninafahamu zipo hospitali na shule zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu. Hizi nazo zimeingia makubaliano na serikali pia. Kadri ya ufahamu wangu kwa shule za sekondari za Kanisa ni juhudi ya Shirika, Parokia au Jimbo husika wakishirikiana na wazazi wanaojenga na kuendesha shule hizo. Serikali kama ina mchango wowote katika shule hizo hiyo itakuwa ni kwa shule zote bila kujali anayezimiliki. Sidhani kuwa ni asasi za kikatoliki tu ambazo hupendelewa kupewa ruzuku kama ipo.

Utamaduni na desturi ya kutoa huduma za elimu na afya kwa wanadamu ni wa zamani sana katika Kanisa Katoliki. Kwa kweli ni sehemu ya wito wake wa kuinjilisha wanadamu. Hata makubaliano yakivunjwa bado wataendelea kutekeleza wajibu huo. Kwa maneno mengine wataendelea kutoa huduma hizo kwa upana na weledi zaidi. Mwaka 2000 nilitembelea jimbo la Bamenda katika nchi ya Cameroon na kufahamishwa kuwa shule bora kabisa katika nchi ile zilikuwa mbili moja ya wavulana na nyingine ya wasichana na zote zilimilikiwa na Kanisa Katoliki. Kama utagundua sasa hivi Majimbo mengi ya Kanisa Katoliki yameanzisha shule nyingi sana za sekondari na hasa za wasichana.

Kwa kumalizia, majadiliano makali kuhusu makubaliano kati ya serikali na Wakritu pengine yanakuzwa sana. Mimi ningefikiri Waziri wa Elimu na Waziri wa Afya (ambao kwa bahati nzuri ni Waislamu) wangeulizwa kwa nini makubaliano hayo yanaendelea na ni kitu gani kitatokea kama yakisitishwa. Hakuna sababu ya kuyaelekeza mashambulizi haya kwa Viongozi wa Wakristu ilhali serikali iliyoanzisha utaratibu huo ipo.

Ninashauri sisi wengine tujitahidi sana kuchimbua ukweli na tujiepusha kutoa maelezo ambayo hata sisi wenyewe tunajua kuwa si sahihi.
Hivi niulize kitu.. Kwa nini ndugu zangu wakristu mnapenda sana kutunga Uongo? Hivi kweli ndio mnaita ujanja wa waloelimika au mnataka tu kubishana..

Hivi kweli wewe uaamini shule zilijengwa wakati wa Muingereza tu ukasahau kwamba kulikuwa na Mjarumani kabla ya Muingereza? Sasa pengine pitia kipande hiki:-

In 1884 and 1885, Carl Peters and agents of the German East Africa Company made treaties with the Tanganyika main-land chiefs, and. in 1887 officials arrived to establish a colonial rule which lasted until 1914. The primary task of these administrators was to maintain law and order and develop communications which would open up the country to trade and commerce.
Missionaries proceeded the administrators and as education was an inevitable concomitant of evangelization, a system of rudimentary schools was quickly established. In 1900, there were 600 mission schools with 50,000 pupils accounting for 95% of the total school enrolment at the time, and by 1914 these figures had risen to 1000 schools with 150,000 pupils.
The Germans had no initial plans to establish an education system, but the need arose for them to train a junior and local civil service to staff their administrative machine. The purpose of their schools was thus defined in an official circular of 1903 as:
a. to enable the native to be used in government administration;
b. to inculcate a liking for order, cleanliness, diligence and dutifulness and a sound knowledge of German customs and patriotism
In single-minded fulfilment of these aims, they had established by 1914, 60 three-year village primary schools, 9 two-year central schools and one high school in Tanga providing clerical, industrial and teacher training for up to 500 pupils. The system was secular and strictly vocational but effective, and brought much favourable comment from British administrators who tried to rebuild the civil service in the 1920s.
Source
 
Hivi niulize kitu.. Kwa nini ndugu zangu wakristu mnapenda sana kutunga Uongo? Hivi kweli ndio mnaita ujanja wa waloelimika au mnataka tu kubishana..

Hivi kweli wewe uaamini shule zilijengwa wakati wa Muingereza tu ukasahau kwamba kulikuwa na Mjarumani kabla ya Muingereza? Sasa pengine pitia kipande hiki:-

In 1884 and 1885, Carl Peters and agents of the German East Africa Company made treaties with the Tanganyika main-land chiefs, and. in 1887 officials arrived to establish a colonial rule which lasted until 1914. The primary task of these administrators was to maintain law and order and develop communications which would open up the country to trade and commerce.
Missionaries proceeded the administrators and as education was an inevitable concomitant of evangelization, a system of rudimentary schools was quickly established. In 1900, there were 600 mission schools with 50,000 pupils accounting for 95% of the total school enrolment at the time, and by 1914 these figures had risen to 1000 schools with 150,000 pupils.
The Germans had no initial plans to establish an education system, but the need arose for them to train a junior and local civil service to staff their administrative machine. The purpose of their schools was thus defined in an official circular of 1903 as:
a. to enable the native to be used in government administration;
b. to inculcate a liking for order, cleanliness, diligence and dutifulness and a sound knowledge of German customs and patriotism
In single-minded fulfilment of these aims, they had established by 1914, 60 three-year village primary schools, 9 two-year central schools and one high school in Tanga providing clerical, industrial and teacher training for up to 500 pupils. The system was secular and strictly vocational but effective, and brought much favourable comment from British administrators who tried to rebuild the civil service in the 1920s.
Source

Mkandara,
Kazata hajasema uwongo. Hapo kwenye red unasoma mwenyewe kuwa missionaries proceeded the administrators lakini hii haina maana kwamba hela walizotumia administrators ndizo hizo hizo walizotumia wamishenari. Kumbuka nchi zote za Ulaya pamoja na Marekani zinafuata mfumo wa kutenganisha kanisa na serikali. Hizi misheni zilikuwa zinajitegemea. Uingereza na Marekani walikuwa na church mission societies ambazo zilichangisha hela zilizotumika kuanzisha makanisa, shule na hospitali katika makoloni walikokwenda. Hakuna hela ya serikali, ama ya mkoloni au ya koloni, kama anavyoamini Sadeeq, iliyotumika kuanzisha shule, makanisa na hospitali katika Tanzania. Hakuna. Kwa mfano kanisa letu pale Musoma, Mennonite, lilianzishwa na wamishenari kutoka Salunga, Pennsylvania, na mpaka leo wana kitengo cha Mennonite Church charities ambacho huchangisha hela zinazotumika popote pale duniani kunapokuwa na mahitaji ya kanisa lao. Sijui nimeeleweka?
 
Kuna mambo napenda niyaweke sawa kwa kuwa kwa namna fulani yameeleweka sivyo.

Serikali haitoi fedha zozote kwa ajili ya mashule yanayomilikiwa na kanisa.

Hospitali zinazopokea pesa kutoka serikalini ni Hospitali teule za wilaya na hospitali za rufaa ambazo serikali imeomba kuingia ubia na wamiliki wake. Si hospitali zote za kanisa.

Kila hospitali ya teule na ya rufaa iliyoombwa na serikali huingia mkataba na serikali. Vifuatavyo ni vipengele vilivyo katika mkataba.

1. The share of costs between the Diocese and Government: capital expenditure, development projects and staff housing on the one hand, and recurrent expenditure and ‘other related services' on the other.
Kuna majukumu ya kushirikiana gharama, na mambo yote yahusikayo na ujenzi/ukarabati na uendelezaji wa hospitali, pamoja na nyumba za wafanyakazi ni jukumu la mmiliki (kanisa), na gharama za uendeshaji na nyingine husika ni jukumu la serikali.

2. The mention of a ‘Board of Governors' (BOG) as the governing body of the hospital and its duty to act in accordance with ‘the medical ethics and policies of the Government' as well as with the ‘principle of the faith' fostered by the relevant religious body.


3. The composition of the BOG (a mix between diocese and government appointed members), the terms of its mandate, its function and duties and its meeting frequency. BOG authority delegation for day-to-day running of the hospital is foreseen.


4. The appointment, appointment authority and functions of the Medical Officer in charge of the hospital.


5. The creation of a Hospital Management Committee to assist the Medical Officer in the day-to-day running of the hospital, and the creation of an Advisory Committee whose function it is to advise the Management Committee. Both committees' composition is detailed.


6. The duty of the hospital to deliver health services, fulfill all medical functions and be staffed as any other, government managed district hospital.

7. A series of provisions related to hospital staffing: formerly employed staff remains employed by the Diocese; the diocese is responsible for staffing the hospital and the Government may attach additional staff upon request. The salary and other financial rights of employees is to be the same as for civil servants.


8. A series of provisions related to the funding of the hospital: the Government is responsible for funding running costs and approved services upon approval of estimates provided by the BOG for each financial year. Funding is paid quarterly and in advance. Charging fees from patients is allowed if in accordance with the applicable ministerial directives; tax-exemption for hospital supplies is provided as for Government hospitals.


9. Additional funding of recurrent expenditures, possibly resulting from an extension or improvement of the hospital, are subject to prior approval of the Government.


10.Auditing of accounts of expenditure is required yearly and to be performed by Government-approved auditors.


11. Amendments to the agreement are mentioned as a possibility, subject to joint approval by both parties (Diocese/Government)


Mpango wa kuingia makubaliano kwa ajili ya kutumia hospitali za binafsi kama DDH na Hospitali za wilaya umekuwepo kabla ya MoU, na terms zinazotumika ni za mkataba ambao dondoo zake zipo hapo juu, na si MoU. Nasisitiza tena MoU si mkataba, ni makubaliano ya ushirikiano.

Fedha hizo zinakuwa kwenye bajeti ya wizara ya afya, na ni fungu la afya kwa wilaya husika. Mf. Katika Wilaya ya Rombo Serikali imeingia mkataba na hospitali ya Huruma Rombo kuitumia Hospitali hiyo kama Hospitali teule ya wilaya. Wakati wa bajeti, fungu la tiba kwa ajili ya wilaya hiyo linapelekwa kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Huruma.

Fedha zinazopelekwa ni kwa ajili ya uendeshaji na si kwa ujenzi.

Fedha hizo zinakaguliwa na mkaguzi wa mahesabu ya serikali.
 
Mkandara,
Kazata hajasema uwongo. Hapo kwenye red unasoma mwenyewe kuwa missionaries proceeded the administrators lakini hii haina maana kwamba hela walizotumia administrators ndizo hizo hizo walizotumia wamishenari. Kumbuka nchi zote za Ulaya pamoja na Marekani zinafuata mfumo wa kutenganisha kanisa na serikali. Hizi misheni zilikuwa zinajitegemea. Uingereza na Marekani walikuwa na church mission societies ambazo zilichangisha hela zilizotumika kuanzisha makanisa, shule na hospitali katika makoloni walikokwenda. Hakuna hela ya serikali, ama ya mkoloni au ya koloni, kama anavyoamini Sadeeq, iliyotumika kuanzisha shule, makanisa na hospitali katika Tanzania. Hakuna. Kwa mfano kanisa letu pale Musoma, Mennonite, lilianzishwa na wamishenari kutoka Salunga, Pennsylvania, na mpaka leo wana kitengo cha Mennonite Church charities ambacho huchangisha hela zinazotumika popote pale duniani kunapokuwa na mahitaji ya kanisa lao. Sijui nimeeleweka?
Mkuu wangu unakuwa kama hujui kiingereza. Hivi inaposemwa Administrator ina maana ndiye alojenga au ku administor? Je unataka kunambia pasipo Utawala wa Mjarumani bado hawa wachungaji wangeweza kufungua hizo shule na Hospital au umesahau Historia mkuu wangu. Halafu kama unakumbuka mwanzoni waloingia nchini sio serikali isipokuwa wafanya biashara kina Carl Peters wakijita explorer na kampuni yao waliyoiita Germany East Africa wakaja kabidhi nchi kwa serikali ya Ujarumani mwaka 1891..

Maswal ya Marekani huwezi kuyalinganisha na hapa nyumbani huko ni kwao hivyo wakijenga wanajenga kwao kama vile shule alojenga Filbert Bay nyumbani. Na ukizisoma zote zina majina ya wafadhili na sio fedha kutoka vatican au Ujarumani..

halafu unazungumzia maswala ya kanisa lenu la Monnonite?, nani kaulizia makanisa yalijengwa na nani? au nani kasema hata makanisa yalijengwa na serikali au yalijengwa na serikali za mkoloni? Mkuuuwangu mbona mnajichanganya kiasi hiki jamani kwa nini hamtaki kukubali tu yaishe tusonge mbele..
 
Mkandara,
Kazata hajasema uwongo. Hapo kwenye red unasoma mwenyewe kuwa missionaries proceeded the administrators lakini hii haina maana kwamba hela walizotumia administrators ndizo hizo hizo walizotumia wamishenari. Kumbuka nchi zote za Ulaya pamoja na Marekani zinafuata mfumo wa kutenganisha kanisa na serikali. Hizi misheni zilikuwa zinajitegemea. Uingereza na Marekani walikuwa na church mission societies ambazo zilichangisha hela zilizotumika kuanzisha makanisa, shule na hospitali katika makoloni walikokwenda. Hakuna hela ya serikali, ama ya mkoloni au ya koloni, kama anavyoamini Sadeeq, iliyotumika kuanzisha shule, makanisa na hospitali katika Tanzania. Hakuna. Kwa mfano kanisa letu pale Musoma, Mennonite, lilianzishwa na wamishenari kutoka Salunga, Pennsylvania, na mpaka leo wana kitengo cha Mennonite Church charities ambacho huchangisha hela zinazotumika popote pale duniani kunapokuwa na mahitaji ya kanisa lao. Sijui nimeeleweka?
Mkuu wangu unakuwa kama hujui kiingereza. Hivi inaposemwa Administrator ina maana ndiye alojenga au ku administrate? Je unataka kunambia pasipo Utawala wa Mjarumani bado hawa wachungaji wangeweza kufungua hizo shule na Hospital au umesahau Historia mkuu wangu. Halafu kama unakumbuka mwanzoni waloingia nchini sio serikali isipokuwa wafanya biashara kina Carl Peters wakijita explorer na kampuni yao waliyoiita Germany East Africa wakaja kabidhi nchi kwa serikali ya Ujarumani mwaka 1891..

Maswala ya Marekani huwezi kuyalinganisha na hapa nyumbani huko ni kwao hivyo wakijenga wanajenga kwao kama vile shule alojenga Filbert Bay nyumbani. Na ukizisoma zote zina majina ya wafadhili na sio fedha kutoka vatican au Ujarumani na mfumo uliopo ni Private schools mimi Mkandara siwezi kuingia pasipo kufuata masharti yao.

Halafu unazungumzia maswala ya kanisa lenu la Monnonite hapo Musoma?, nani kaulizia makanisa yalijengwa na nani? au nani kasema hata makanisa yalijengwa na serikali au yalijengwa na serikali za mkoloni? Mkuu wangu mbona mnajichanganya kiasi hiki jamani kwa nini hamtaki kukubali tu yaishe tusonge mbele..
 
Back
Top Bottom