Makanisa yavunje MoU na Serikali...

Makanisa yavunje MoU na Serikali...

Mdondoaji ni CCM ndiyo imefanya haya yote; mwaka 2010 kundi la watu (wakiwemo Waislamu wengi tu) walitaka CCM irudi madarakani. Sasa hilo la MoU siyo la Wakristu ni la serikali ya CCM. Imeshaoneshwa huko nyuma ni Ally Hassan Mwinyi (Muislamu) ambaye aliingia mkataba huo na wakati wanaingia na kanisa walifanya pia na Imam Aga Khan (Muislamu). Hicho kilichoingiwa kwa Kanisa kiliingiwa na kwa Aga Khan na taasisi yake inafanya karibu mambo yale yale ambayo yanafanywa na makanisa (elimu, shule n.k).

Ni kweli wakiamua kuvunja hii MoU isiwe nusu nusu; ihusishe na hizi taasisi nyingine lakini kama watu kweli wanataka an absolute secularization ya serikali yetu wasiishie hapo waende mbele zaidi.

Pia kuna taasisi inaitwa ithnaasheri nayo inakula shavu.
 
Mdondoaji ni CCM ndiyo imefanya haya yote; mwaka 2010 kundi la watu (wakiwemo Waislamu wengi tu) walitaka CCM irudi madarakani. Sasa hilo la MoU siyo la Wakristu ni la serikali ya CCM. Imeshaoneshwa huko nyuma ni Ally Hassan Mwinyi (Muislamu) ambaye aliingia mkataba huo na wakati wanaingia na kanisa walifanya pia na Imam Aga Khan (Muislamu). Hicho kilichoingiwa kwa Kanisa kiliingiwa na kwa Aga Khan na taasisi yake inafanya karibu mambo yale yale ambayo yanafanywa na makanisa (elimu, shule n.k).

Ni kweli wakiamua kuvunja hii MoU isiwe nusu nusu; ihusishe na hizi taasisi nyingine lakini kama watu kweli wanataka an absolute secularization ya serikali yetu wasiishie hapo waende mbele zaidi.

Mzee Mwanakijiji,
Umesema Waislam wengi ndio walitaka CCM irudi madarakani, unataka kutuambia Wakiristu wengi nao walitaka Chadema wachukuwe dola.
 
Last edited by a moderator:
..hebu nieleze ni wapi hapa Tanganyika ambapo Waarabu walieneza Ukristo, Uyahudi, au Upagani, ili tuweze kuwanasibisha na imani hizo..
Mkuu! si lazima Myahudi,Mpagani au Mkristo aeneze dini yake popote anapokwenda!
JokaKuu said:
..kuhusu Sultani na kuhamia Zanzibar, bila shaka alifanya hivyo kutokana na kishawishi cha biashara ya WATUMWA pamoja na pembe za ndovu
Ulijuaje hilo la ushawishi wakati umeambiwa hapa kuwa alihamia baada ya kuitwa na Wakilwa?
 
Sikonge, kwa nini wavunje? Mimi naona kuwa hili ni Hannity zuri linalofaa kuigwa. Hivyo ushauri wangu ni Huu-nendeni shule mkapate elimu ya kuweza kuandika proposal kuomba makubaliano na serikali.
Wow!
Waislamu "tukienda shule" na kujipatia MoU yetu na Serikali wakati Wakristo tayari wana ya kwao na Serikali, Wapagani nao "wataenda shule" na kujipatia MoU yao na Serikali, kwa mbali naona Baniani nao "wataenda shule" na kujipatia MoU yao ..tartiibu tunai isolate Serikali! mwisho wa siku tunaona kuwa hatuna haja nayo, serikali ya nini wakati mambo muhimu ya Afya na Elimu tunaweza kuyafanya wenyewe...kinachofuatia tunagawana nchi!
 
Sideeq,

..ndugu yangu, hata Tanzania tuliitwa Ushelisheli kuwasaidia wakati makaburu walipojaribu kuwavamia. Lakini hukusikia Mwalimu Nyerere akihamisha makao makuu toka Dodoma kupeleka Port Victoria baada ya JWTZ kuwatimua makaburu.

..zaidi, Muarabu alijimilikisha eneo zima la pwani ya Afrika Mashariki mpaka alipokuja kuporwa na wazungu. Vilevile Waarabu alikuwa wakifanya vurugu[terror] kubwa sana ktk interior of Tanganyika mpaka Congo ambapo walikuwa vinara/wamiliki wa njia za kusafirisha WATUMWA.

..NOW, tunaweza tusikubaliane ktk mambo mengi, lakini nadhani hakuna mashaka yoyote kwamba DINI hizi mbili zililetwa katika zama za UKATILI na UDHALILISHAJI mkubwa kwetu sisi WAAFRIKA. Wakati mwingine huwa nawaza kama kweli MUNGU alikua na nia Waafrika nao wawe waumini wa dini hizi.

Asante sana kwa kufikiri ukiwa nje ya boksi la imani za dini za kikoloni(paragrafu ya mwisho). Dini za kikoloni ni utumwa mkubwa sana kwa mwafrika. Dini hizi zimesokota mnyonyoro mkubwa na mzito dhidi ya fikra za mwafrika na kumfanya mtumwa wa kutupwa kifkra. Ni vigumu sana kumkomboa mwafrika kutoka katika mnyonyoro wa utumwa wa kifikra uletwao na imani za dini za kikoloni
 
Last edited by a moderator:
Mdondoaji ni CCM ndiyo imefanya haya yote; mwaka 2010 kundi la watu (wakiwemo Waislamu wengi tu) walitaka CCM irudi madarakani. Sasa hilo la MoU siyo la Wakristu ni la serikali ya CCM. Imeshaoneshwa huko nyuma ni Ally Hassan Mwinyi (Muislamu) ambaye aliingia mkataba huo na wakati wanaingia na kanisa walifanya pia na Imam Aga Khan (Muislamu). Hicho kilichoingiwa kwa Kanisa kiliingiwa na kwa Aga Khan na taasisi yake inafanya karibu mambo yale yale ambayo yanafanywa na makanisa (elimu, shule n.k).

Ni kweli wakiamua kuvunja hii MoU isiwe nusu nusu; ihusishe na hizi taasisi nyingine lakini kama watu kweli wanataka an absolute secularization ya serikali yetu wasiishie hapo waende mbele zaidi.

Mwanakijiji,

Je una una uhakika na hicho nilicho BLUE. Kuwa The Aga Khan Foundation wanakula Pesa ya MoU? Je unajuwa fedha za MoU zinatumika kufanyia nini kwa maana majengo au hata wataalamu na vifaa?

NB. Kumbuka Pesa za MoU ni tofauti kabisa na Pesa za misamaha ya Kodi.

naomba uthibitisho wako.

 
Kwa nini Pro-Chadema wengi uwa wanakuwa upande wa CCM linapokuja suala la MoU... halafu hapo hapo eti wana mawazo ya kuing'oa CCM madarakani wanachekesha sana.


Kwani ulijui hilo. Hii ni Crusade kwao.
 
Boko haram wanapochoma makanisa huko Nigeria ni kwa Sababu ya MOU?????

Don't argue with a ful!
Boko haramu, uamusho, alkaida na wengine wote wa aina hiyo wanawaza kwa kutumia makamasi badala ya ubongo.
 
Tatizo la waislamu lipo karibu kwa watu wote, WALIOSOMA NA WASIOSOMA. Wakati unategemea waliosoma wawasaidie ambao hawajasoma unakuta na wao wakiwa kwenye vikao vyao wote wanawaza vilevile. Mapendekezo ya mtoa mada siyo tu ni ya kitoto bali pia yanaonesha ni ya mtu aliye soma lakini ameamua kufikiri kama wasio soma.

NI KAMA ANAPENDEKEZA KUWAWALIO ENDELEA WAWASUBIRI WALIO NYUMA KIMAENDELEO.

Waislamu walio wengi elimu kwao ni kama anasa. Ukiangalia maeneo yaliyo na waislamu wengi mahudhurio ya watoto wao shuleni yako chini ya asilimia 50. Ukienda BAGAMOYO, CHALINZE, LINDI YOTE, MTWARA YOTE KASORO MASASI, siku mvua ikinyesha tu asubuhi mahudhurio yanashuka hadi asilimia 25!! Hali kama hiyo huwezi kuikuta Kilimanjaro, Mbeya, Shinyanga, Iringa, Ruvuma, na maeneo yote ya wakristo wengi.

Kama wakitambua kuwa elimu ni ufunguo wa maisha basi ungetegemea kuona wanajenga shule nyingi zenye ubora wa hali ya juu na kuimarisha uongozi wa shule zao sambamba na kutafuta walimu wenye sifa nzuri kitaaluma na siyo kiroho tu. Shule zao siyo tu zinatia huruma lakini pia nyingi zinaendeshwa kimagumashi. Karibu zote wastani wa kufaulisha watoto kwenda kidato cha tano ni asilimia kati ya 2 hadi 5 tu.

USHARI WANGU NI wajitathini wenyewe kwanza.
Ndg yangu mikoa yote uliyoitaja imedidimizwa makusudi na mfumo K, kwa sababu hata huduma za kijamii tu we angalia, ile mikoa yenye waislam wengi hata barax2, zimeanza kujengwa hivi karibuni tu. kwa hiyo hayo yote ni matokeo ya mfumo K, na ndo maana waislam wanataka usawa, kama ilivyo wanawake walivyokandamizwa na mfumo dume walikuja wakaanza kudai haki zao na sasa hivi wameanza kuzipata, the same to Muslim kudai wanaonewa si dhambi, wapewe haki zao, na niwakumbushe tu wakatoliki wenzangu, kwamba waislam tumewastua wenyewe kutoka usingizini, kwa sababu, pale wanapodai haki zao sisi tumekuwa wakwanza kutoa matamko mazito kupitia kwa viongozi wetu wa kiroho, wakati wao wanaidai serikali, na hata kwenye katiba munafanya hivyox2, sasa naombeni muwaache waislamu waidai serikali yao haki zao, na ninyi bakini na mambo yenu, lkn vinginevyo ninaona hatari tu. na naomba mungu atuepushe na balaa hili. Ameeeeeen.
 
Kwanza nashukuru kwa kufunguka kuwa upo USA na siyo Gongolamboto kama unavyotuandikia.

Kwa kuwa unaishi huko, yanayotokea huku SIKONGE kwa kweli huyafahamu na unafikiri ni kama USA. Ni sawa na yule binti wa mfalme aliyesema "Kama watu wana njaa, si wale keki?"

Nilimjibu Barubaru kuwa kwa Sikonge hospital, Serikali inabidi ipeleke Tsh.20 milioni kwa mwezi ambazo ni sawa na Euro 10,000 sawa na mshahara wa Gavana wa BoT. Ila kwa sasa Sikonge Hospital inapokea Tsh. 00,000 milioni kwa mwezi.

Kwa hiyo unaona hapo jinsi Moravian Church wanavyoibia Serikali? Na hadi leo hii wametajirika sana kwa hizo hela nyingi sana wanazozipokea kila mwezi.

Taasisi za dini zinafanya kazi ya kujitolea kwa sana tu. Mfano ni Mchungaji (mama Mgonela) ambaye ni Mmarekani mweusi. Alipokuja Sikonge kama Muuguzi, akaishia kuukataa mshahara wake na nyumba ya hospital. Akajenga nyumba yake na kwa sababu alikuwa kweye kitengo cha watoto wachanga, akaagiza hela USA na akajenga Ward ya watoto wachanga pekee. Mwisho akawa ndiyo mfadhili wa timu ya Afya ya Sikonge (Football) kwa kuwaletea vifaa vyote vya michezo.
Ukiacha mama, alishakuwepo Dr kutoka Uholanzi ambaye na yeye alikuwa anajitolea hadi chakula cha watu masikini ambao wanakuwa wamefanyiwa upasuaji na hawajiwezi kula vyakula laini. Mke wake alipika na wakawapa chakula hawa watu - BUREE.

Bruda wa Tabora mjini na timu yake ya Chipukizi, ndiyo aliyewavumbua akina Saidi Mwamba Kizota (RIP) na Amasha. Walifanya mazoezi na kupikwa vizuri hadi wakaja kununuliwa na Simba/Yanga. Walipewa hadi vifaa vya michezo bure.

Nakubaliana na wewe kuwa MoU inabidi ZIFE. Ila huwezi kuziuwa leo hivi hivi. Hebu fikiri Bugando, KCMC, Sikonge, Peramiho, nk zinasitisha kuhudumia watu wasio wa dini yao. Wengi sana wataumia. Watu wanaishi kwa Dola moja kwa siku na kitanda pekee utaambiwa ulipie Dola 50 kwa siku, unafikiri nani ataweza?

Naona umekaa sana MAJUU kijana. Shuka chini na uone hali halisi ya Tanzania. Ukiweza basi kama kweli mwenzetu una hela, hebu ADOPT kijiji kimoja cha SIKONGE.

Soma hapa na URITHI kijiji huku kwetu SIKONGE: AIDS Ministry * Moravian Board of World Mission
Mkuu Sikonge,

Kwa labda nikusahihishe hizi MoU ni kwa taasisi zote ambazo si za kiserikali ziwe za kidini au kipagani inabidi zivunjwe kwa manufaa ya Taifa letu najua wadau wengi wamechangia labda nitakuwa narudia

1. MoU ni wizi tu rasiamali zetu kwa kutumia mgongo wa dini; taasisi husika zimekuwa zipokea free handout kutoka serikalini kwa kisingizio cha kupunguza gharama Za matibabu je ni kweli gharama zao ni nafuu? Si kweli hata kidogo hawana tofauti na hospitali za binafsi, ikiwa waislamu wanamudu kwenda hospitali za binafsi basi elewa fika hawatashindwa kulipia huduma za hospitali za taasisi husika.

2. Pesa wanazolipishwa wananchi zinakwenda wapi? Ni kweli pesa wanazolipa wananchi na pesa wanazopokea kutoka MoU zote zinakwenda kwenye kupunguza gharama za matibabu? Hayo si kweli taasisi husika zinatumia udhaifu wa serikali pesa hizo hizo ndizo zinazotumika kwenye miradi mengine ya elimu; ukichunguza kwa makini taasisi husika zimeweza kuongeza idadi ya mashule na vyuo baada ya mfumuko wa pesa MoU tusidanganyane eti ni pesa za sadaka za waumini.

3. Ikiwa hizi ni taasisi za kidini zinafanya kazi ya Mungu kuna ulazima gani wa wao kuchukua pesa kutoka serikalini? Hapo thawabu inapata serikali au taasisi husika? Yaani ni sawa kwa muumini aliyeshindwa kwenda kwenye sala na kumupa pesa jirani akamtolee sadaka.

3. Ukirudi kwenye hizi handout waathirika sio waislamu pekee wapo wakristo wengi tu waathirika wa wizi huu; inakuwaje taasisi husika zinachangia kujenga matabaka kwenye jamii? Ni kichekesho kwani hata hapa US upuuzi huu uliachwa siku nyingi zipo taasisi za kweli za kidini hatozi ada yoyote kwenye matibabu;inakuaje Tanzania tumeuzwa wajinga kiasi hiki kutetea upuuzi ambao athari zake ni kuja kuuana uvumilivu una kikomo; wana historia someni mapinduzi ya ulaya yalitokana na nini?

Niwahi kufanya kazi kwenye taasisi ya kidini hapa US kila mwisho mwaka kila mfanyakazi anapewa bonus kati dola 1000-700 baada yakutoa gharama zote kinachobaki kinagiwa wafanyakazi kwasababu zipo chini not for profit organization je hicho ndicho kinachoafanyika hapo Tanzania!Ningeomba nyie washabiki wakubwa mmoja wenu ende kwenye hospitali mnazozitetea aombe kutibiwa bila pesa halafu arudi hapa jamvini atueleze hatima yake.

Chama
Gongo lamboto DSM
 
Serikali ijenge kwa pesa gani wakati mabilioni ya pesa za serikali zinakwenda Kanisani kupitia MoU.
Unataka serikali ikachukuwe mkopo wenye riba kujenga hizo hospitali na Vyuo bora, mkopo na riba ambazo baadae zitawaumiza wananchi wenyewe wakati hela zao zipo zinakwenda Kanisani?
...ivunjwe MoU kwanza!
Yai na kuku nini kimetangulia!!! Unaondoa ruzuku gharama zipande watu wafe kwa kukosa matibabu wakati unajenga hospitali? Zote zingekuwa za serikali bado ruzuku ingetolewa na bado ingeendelea kujenga hospitali mpya!!
 
Kenya, Somalia na kwingineko Waislamu wanalalamika tu!!! Huko nao kuna MOU????
Hawa hata huko kwenye nchi ambazo ni za dini yao, huwa hawaishi kulalamika. Hapa kwetu Ukristo ni ajenda yao ya kudumu ili ufutwe. Hata ukiufuta watatafuta sababu nyingine. Je, nini kinatokea Iran, ambako alitokea kiongozi wao na hata kuwa na uwezo wa kutangaza hukumu ya kifo kwa mtu ye yote ( Ref Salimin Rushdie). Wanalalamikia MoU ya Wakristo, nani wao kawazuia kujenga shule na hospitali za kwao. Rais Mkapa aliwapa chuo cha Tanesco Morogoro, badala ya kuwa Chuo Kikuu sasa ni uchochoro wa dini. Chuo hicho kilikuwa ni amli ya umma, iweje wapewe kundi la watu wenye imani moja. Mbona Wakristo na wasoi wakristo hawalalamiki. Hawa watu inafaa kuwajibu bila mafumbo maana wanazidisha uwongo, na uwongo ukirudiwa mara nyingi huweza kuonekana kama ukweli. Hili wanalijua ndio maana wanarudia rudia ili uwogo ugeuke ukweli. Tuwaombe wale ambao ni Waislam na wana elimu ya kutosha wasaidie taasisi zao kujenga vyuo, shule na hospitali. Huwezi kuvunja MoU, bila kuumiza watu wengi wakiwemo wao pia, maana pamoja na kelele zote hizo bado wanatibiwa huko huko na hawabaguliwi. Kelele zote ni chuki ya ukristo, basi.
 
Sideeq,

..Waarabu wananasibishwa na Uislamu kwasababu asilimia kubwa ni waumini wa dini hiyo.

..mfano mwingine ni ZNZ, ambapo tunasema ni taifa la Waislamu kwasababu asilimia kubwa ya raia wake ni Waislamu.
 
Last edited by a moderator:
Mleta hoja aeleze ni vipi waislam wanabaguliwa wakati wa kupatiwa huduma na zile taasisi zilizoainishwa katika MOU ya makanisa na serikali. Kuzungumza kijumlajumla tu hakusaidii sana. Aidha aeleze ni jinsi gani huduma zimeshuka kutokana na makanisa kutumia vibaya rasilimali zinazopewa kwa ajili ya kuhudumia jamii tena kwa vilelezo sahihi. Vinginevyo hoja bado haijakamilika kwa vile vigezo vya kutekeleza anavyoshauri havitoshelezi.
 
Mkuu Sikonge
Tabora naifahamu vizuri sana mimi nilikuwa mmoja wa vinara wa Gongoni Stars; huu mjadala MoU ulianza kiasi cha mwaka hivi mwanzoni niliuunga mkono kwasababu sikufahamu undani niliangalia zaidi dhana ya kusaidia watanzania wote bila kujali dini; na huo ndio utaifa wetu; naunga mkono sana kwa taasisi ziwe za kidini na NGO kujitolea kuwasaidia watanzania kwenye nyanja ya elimu na afya; nadhani unafahamu nini maana ya neno KUJITOLEA ukidai pesa huko si kujitolea ni biashara; nimeshakuambia hizi pesa MoU hazitumiki kwenye huduma za afya kama wengi mnavyodai; na ndio zimechangia kwa kiasi kikubwa mfumuko wa mashule na vyuo; ikiwa kama makanisa ya pesa ya kujenga mashule na vyuo kama ambavyo wengi mnavyodai iweje yashindwe kuhuduma hospitali zake? Hebu nionyeshe ni hospitali gani ya kanisa utakayokwenda kupewa matibabu bila pesa; Nimekupa mfano hata hapa Marekani zipo hospitali zakujitolea za kiisalamu zinawasaidia sana waumini wa dini zote hawakutozi hata senti moja kutoa utatoa wewe mwenyewe kusaidia kuendesha hospitali na kama utahitajika kupata matibabu zaidi wao wanakusaidia kupata matibabu karibu na bure huwezi kuniambia hizi taasisi zinapokea mamilioni kwa mwaka halafu eti wanajitolea tusidanganyane huo ni wizi sawa na ile mikataba ya madini. Hebu nenda Agakhan Hospitali na hospitali yoyote ile hapo Dar ya kanisa omba matibabu bila pesa tuone kujitolea kwao.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Hawa hata huko kwenye nchi ambazo ni za dini yao, huwa hawaishi kulalamika. Hapa kwetu Ukristo ni ajenda yao ya kudumu ili ufutwe. Hata ukiufuta watatafuta sababu nyingine. Je, nini kinatokea Iran, ambako alitokea kiongozi wao na hata kuwa na uwezo wa kutangaza hukumu ya kifo kwa mtu ye yote ( Ref Salimin Rushdie). Wanalalamikia MoU ya Wakristo, nani wao kawazuia kujenga shule na hospitali za kwao. Rais Mkapa aliwapa chuo cha Tanesco Morogoro, badala ya kuwa Chuo Kikuu sasa ni uchochoro wa dini. Chuo hicho kilikuwa ni amli ya umma, iweje wapewe kundi la watu wenye imani moja. Mbona Wakristo na wasoi wakristo hawalalamiki. Hawa watu inafaa kuwajibu bila mafumbo maana wanazidisha uwongo, na uwongo ukirudiwa mara nyingi huweza kuonekana kama ukweli. Hili wanalijua ndio maana wanarudia rudia ili uwogo ugeuke ukweli. Tuwaombe wale ambao ni Waislam na wana elimu ya kutosha wasaidie taasisi zao kujenga vyuo, shule na hospitali. Huwezi kuvunja MoU, bila kuumiza watu wengi wakiwemo wao pia, maana pamoja na kelele zote hizo bado wanatibiwa huko huko na hawabaguliwi. Kelele zote ni chuki ya ukristo, basi.

Mkuu Mkapa alitoa chuo cha Tanesco kama kiini macho pesa aliwapa makanisa kupitia pesa za Mou zinajenga yale kama 100
bila ya wasiwasi wowote na nyingine zikabaki.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Memorandum ilifanywa kwa siri mpaka ilipo fichuliwa na wanaharakati wa kiislam ,serikali walikua wakikanusha kuwepo kwake mpaka ushahidi ulipotolewa.
Hakika katika nchi yenye madhehebu ya dini tofauti ambayo yamekumekuwa yakisababisha misuguano ya hapa na pale basi kufanya makubaliano au mikataba kama hii inaweza kuleta matatizo makubwa ya kutoaminiana basina ya serikali na waumini wa kislam na wakristo.ukweli hili lilikua ni kosa
Waislam wanaiona serikali yao imefanya upendeleo wa wazi kwa madhehebu ya kikristo,
NINI CHA KUFANYA
serikali makini yenye kufata katiba na kulinda misingi ya umoja walio jiwekea inatakiwa ifanye mambo yake bila ya upendeleo na “all inclusive” isiokua na upendeleo na viongozi wake wasiendeshe shughuli za serikali kwa misingi ya dini ,
basi kwa vile serikali inatambua umuhimu wa dini katika kuleta maendeleo ingeandaa kitu kama 'general policy on religious institutions and assistance'
hii ndio ingekuwa white paper kwa ajili ya kuzisaidia taasisi za dini kutoa huduma, mfano kama hii memorandum ingegeuzwa na kufanyiwa marekibisho ikawa sera ya kitaifa kwa dini zote,
na si vibaya serikali kuingiza katika bileteral talk kuomba misaada kwa ajili ya taasisi za dini.
umuhimu ni uwazi na kufanya haya kwa maslahi ya nchi, ikijulikana wazi faida itayopatikana ni kwa ajili ya taifa na sio kwa ajili ya taasisi moja kujifagilia dhidi ya mwenziwe.
leo tukiwa na white paper kama hii tungeona wakati rais labda alipoenda Oman juzi labda bakwata wangefatana na rais na wao wangeondoka na project ambayo serikali inairidhia , naamini ingetusaidia sana ,
ama Rais anapokwenda Germany angeweza kufatana na wachungaji wa kanisa nao pia wangekuja na project zao labda ya kujenga hiospital kule sumbawanga , basi naamini chance ya kupata ni kubwa.
Hivyo hata katika bilateral agreement serikali ingeingiza mipango na project za taasisi za dini .zingesaidia sana kuleta maendeleo katika nchii hii, haya lakini yanataka umakini na Utanzania kwanza.

hivyo ni jambo la kuimbia serikali kwamba ilichofanya sio kibaya lakini ni cha upendelo, hivyo serikali ifute hii memorandum na badala yake itengeneze national policy ama sera kuhusu misaada kwa taasisi za dini.
kwa waislam:
Na upande wa ngugu zangu waislam , taasisi zetu ukweli zinahitaji kufanyiwa marekebisho makubwa ya kiutendaji.taasisi zetu nyingi zinaendeshwa na wanaharakati , sasa ni wakati wa wasomi wa kiislam kujitokeza na kupewa nafasi za kuongoza taasisi hizi.maulamaa na masheikh washughulike na mambo ya kiroho na propagation ya dini.mambo ya maendeleo wapewe wasomi .
Ama baada ya hapo tunaweza kuweka pressure au kuwa na constructive arguments ili serikali iweze kubadili hii memorandum na badala yake itengeneze sera ya taifa kuhusu misaada ya taasisi za dini.
bakwata ambao mie binafsi ni mmoja kati ya wanaolipinga sana kutokana na uhafidhina na ubadhirifu wake basi at least wakati huu ambapo waislam wengi wamekosa na imani nalo likubali kubadilika.
Mpaka hapo tutapo kubali kubadilika kinyume chake tutakuwa tunapiga kelele ambazo ambazo hakuna ataetusikiliza
 
nadhani unafahamu nini maana ya neno KUJITOLEA ukidai pesa huko si kujitolea ni biashara; nimeshakuambia hizi pesa MoU hazitumiki kwenye huduma za afya kama wengi mnavyodai; na ndio zimechangia kwa kiasi kikubwa mfumuko wa mashule na vyuo;
ikiwa kama makanisa ya pesa ya kujenga mashule na vyuo kama ambavyo wengi mnavyodai iweje yashindwe kuhuduma hospitali zake? Hebu nionyeshe ni hospitali gani ya kanisa utakayokwenda kupewa matibabu bila pesa;
Hebu nenda Agakhan Hospitali na hospitali yoyote ile hapo Dar ya kanisa omba matibabu bila pesa tuone kujitolea kwao.
Point taken.
 
NGOJA NIKUANDIKIE TENA:

Nilimjibu Barubaru kuwa kwa Sikonge hospital, Serikali inabidi ipeleke Tsh.20 milioni kwa mwezi ambazo ni sawa na Euro 10,000 sawa na mshahara wa Gavana wa BoT.Kwa sasaSikonge Hospital inapokea Tsh. 00,000 milioni kwa mwezi.

Kwa hiyo unaona hapo jinsi Moravian Church wanavyoibia Serikali? Na hadi leo hii wametajirika sana kwa hizo hela nyingi sana wanazozipokea kila mwezi.

Pesa unayolipa hapo Sikonge Hospital huwa ndogo sana. Pia kwa mfano Marehemu baba yangu alipouguwa moyo na wakamkataza kufanya kazi nzito, walimuandikia dawa ambazo alikuwa akichukua BURE. Gharama ya kitanda kwa siku hapo hospital ni sawa na bure. Ukienda Agha Khan ndiyo utajua nini maana ya kitanda cha hospital.

Huwezi kufananisha NGO na hizi hospital Mkuu. Zimetibu watu wengi sana na zinaendelea kutibu na wengine hata kwa mkopo. Kama umekaa Gongoni basi usiseme unafahamu Tabora. Mie nasema SIKONGE, wewe unasema Gongoni........

full.jpg
full.jpg


Mkuu Sikonge
Tabora naifahamu vizuri sana mimi nilikuwa mmoja wa vinara wa Gongoni Stars; huu mjadala MoU ulianza kiasi cha mwaka hivi mwanzoni niliuunga mkono kwasababu sikufahamu undani niliangalia zaidi dhana ya kusaidia watanzania wote bila kujali dini; na huo ndio utaifa wetu; naunga mkono sana kwa taasisi ziwe za kidini na NGO kujitolea kuwasaidia watanzania kwenye nyanja ya elimu na afya; nadhani unafahamu nini maana ya neno KUJITOLEA ukidai pesa huko si kujitolea ni biashara; nimeshakuambia hizi pesa MoU hazitumiki kwenye huduma za afya kama wengi mnavyodai; na ndio zimechangia kwa kiasi kikubwa mfumuko wa mashule na vyuo; ikiwa kama makanisa ya pesa ya kujenga mashule na vyuo kama ambavyo wengi mnavyodai iweje yashindwe kuhuduma hospitali zake? Hebu nionyeshe ni hospitali gani ya kanisa utakayokwenda kupewa matibabu bila pesa; Nimekupa mfano hata hapa Marekani zipo hospitali zakujitolea za kiisalamu zinawasaidia sana waumini wa dini zote hawakutozi hata senti moja kutoa utatoa wewe mwenyewe kusaidia kuendesha hospitali na kama utahitajika kupata matibabu zaidi wao wanakusaidia kupata matibabu karibu na bure huwezi kuniambia hizi taasisi zinapokea mamilioni kwa mwaka halafu eti wanajitolea tusidanganyane huo ni wizi sawa na ile mikataba ya madini. Hebu nenda Agakhan Hospitali na hospitali yoyote ile hapo Dar ya kanisa omba matibabu bila pesa tuone kujitolea kwao.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Back
Top Bottom