Mkandara,
Lukolo,
..unajua hii hoja yako inaweza kututoa nje ya mjadala.
..tukiendeleza hizi hoja zako tunaweza kuita shule nyingi sana, karibu zote, zilizojengwa tangu enzi za Waarabu, Wajerumani, na Waingereza, kuwa ni shule za wakoloni.
..halafu tukidai kwamba shule ni za wakoloni, what about Makanisa na Misikiti?? Je, tutakuwa tumekosea kusema kwamba kuna Misikiti na Makanisa ya wakoloni??
..for the sake of this discussion, tukubaliane tu kwamba shule za serikali ni zile zilizokuwa zikiendeshwa na serikali na kuitwa "goverment schools. Mfano wa shule hizo ni shule ya Tabora. Halafu kulikuwepo na shule za makanisa, pamoja na madhehebu mengine ya dini.
..Mwisho, kuna shule zilijengwa na madhehebu ya dini baada ya UHURU ambazo zilikuja kutaifishwa. Ndiyo maana nikaeleza kwamba utakuwa huutendei mjadala huu haki ukidai kwamba shule zilizotaifishwa zilikuwa shule za "mkoloni."
NB:
..kuna shule za madhehebu ya dini zilijengwa kwa njia ya kujitolea na waumini wa eneo husika.