Mkandara,
Kwanza lazima nitangaze upande. Mie ni MKRISTO wa Moravian. Ila zaidi ya nusu ya familia ni Waislaam. Siwezi kuwatukana kwa sababu kwa Mama na kwa baba wamejaa Waislaam.
Nashukuru kuwa walau unakiri kwamba hizi Taasisi za dini zinasaidia na kuwa Wewe, Kikwete, Lipumba na wengine wengi ambao ni Waislaam, mmesaidiwa/kusomeshwa na hizi taasisi.
Marehemu Baba yangu mdogo, alichaguliwa kwenda kusoma shule za Wamission wakati wa ukoloni. Akiwa njiani kwenye gari, aliruka na kurudi nyumbani. Niliambiwa na wazee wengi kuwa darasani alikuwa moto wa kuotea mbali na kama angeliendelea, basi kuna kila dalili angelikuja kuwa ni mmoja wa Wasomi wa Mwanzo wa Sikonge.
Kisa cha kuruka kwenye gari ilikuwa ni kuogopa kwenda kulishwa Nguruwe. Ila Baba yake mdogo, alikwenda kusoma na alipomaliza shule, ingawa alikuwa kabatizwa, alirudia dini yake na kujiolea wake kadhaa.......
Enzi hizo, huwezi kufanya kazi Moravian kama wewe si Moravian. Kuwa Mkristo tu haikuwa inasaidia ila lazima uwe Moravian. Kwa sasa hivi hakuna tena anayejali na nakumbuka wakati Katibu wa hospital alikuwa Muislaam. Sasa hivi wanajitahidi kusomesha watu wao kwenye uongozi.
Inapokuja kutibiwa, hakuna swali kama hilo. Hizi hospital zinafanya kazi kwa shida sana. Hizo zinazoneemeka kwa fedha ya Serikali ni chache sana. Sikonge nimeshasema hata mishahara sasa Serikali imegoma kutoa tangu mwaka 2006. Wanajiendesha kwa misaada ya Wakristo kutoka nje na Wasamaria wengine wema ninaamini wapo wasio na dini na hata Waislaam walioko nchi za WEST.
Mkuu Mkandara, nakubaliana na maneno yako kuwa ni SERIKALI inabidi iwe inatoa huduma kama za MAJI, UMEME, Usafiri kama UDA, Matibabu, Shule nk. Hiyo ndiyo kazi ya Serikali. Ila kwa sababu walishindwa na hasa enzi ya Mwinyi, hapo ndipo mambo yalianza kubadilika. Mikataba kama hii ikaanza kuandikwa. Hapa tatizo liko wapi? Kanisani au Serikalini?
Huwezi kuanza kumtibu mtu aliyeumia kwenye moto kwa kumfunga Bandeji huku akiwa bado motoni. Inabidi kwanza umtowe motoni na umuweke kivulini na ndiyo uanze kumuwekea vitambaa. Serikali ilishindwa kuhudumia na ikaomba Makanisa yasaidie. Hapa ili kubadilisha hili, Serikali kwanza ianze kuchukua Majukumu yake kwa kujipanga vizuri. Kidogo kidogo ianze kuchukua majukumu ya kuhudumia Watu wake na mwisho itafika wakati, Serikali haihitaji tena huduma za kanisa na itavunja mkataba.
Nitamuelewa sana mtu atakayeipigia Makelele Serikali na siyo makanisa. Ila kama unakuja na story kuwa SERIKALI ya TANZANIA inafilisika kwa kuwalipia Wanafunzi ada na kuzilipa taasisi za makanisa pesa, basi ni au wewe kweli unatakiwa kupewa huduma ya kwanza au unajifanya tu hilo hulioni.
Kama Waislaam mkianzisha juhudi za kuilazimisha SERIKALI ichukuwe Majukumu yake, basi ni mie MNIHESABU.
Mkuu wangu kwanza nashukuru umewaletea watu kitu hiki ambacho nimekisoma na kuwasoma baadhi ya watu na kwa uhakika imethibitisha UDINI uliopo nchini hauwezi kuzimwa kirahisi. wadanganyika ni WABINAFSI sijapata kuona maishani..
Mmejaribu sana kujenga hoja na hata kuendelea kuwatukana waislaam lakini, Je sii mawazo haya haya wana CCM husema kuhusu Chadema?..Iweje leo inapofikia swala la dini nyie wenyewe wana Chadema mnabadilika wakati mnajua fika CCM inawakandamiza wananchi japokuwa wapo watu watajiri na wanaofanya vizuri.. Majority ni maskini. Mbona sioni matusi haya kwa maskini wakulima na wafanyakazi ya kwamba hata wakikamatwa mafisadi bado mtaendelea kulalamika!..Nilikuwa nawaamini sana vijana wa Chadema kuwa wasomi na wenye kuelewa lakini sasa naanza kuingiwa na shaka kubwa sana..
Nimemsoma Jasusi, Mtu wangu na amenisikitisha sana kwa sababu swala sio waislaam wanataka nini isipokuwa jambo lililofanyika ni kinyume cha sheria. CSSC ni shirikisho la dini tofauti kabisa na NSSF ambalo ni shirika la Taifa na board yake inatokana na serikali iliyopo madarakani sio kama CSSC ya makanisa. Halafu maneno ya kujilinda anaposema hata MoU ikivunjwa Waislaam wataendelea kulalamika! kumbe mnajua hawa sii kama nyie eeeh! hatuko pamoja ila kuna wao na sisi. Bila shaka wataendelea kulalamika ikiwa kuna makundi na kutakuwa na jambo jingine maana nijuavyo hawajarudishiwa shule zao.
All am asking for ni fairplay. iwepo policy moja kwa wote na sio kundi la watu. kama tuna Private schools sheria zake ziwahusu shule zote za Private, ikiwa kuna ruzuku zitapewa zote kulingana na aidha wananfunzi wanaosoma pale, na muhimu zaidi serikali yetu ijikite ktk kuwalipia ada na matuzmizi wanafunzi badala ya kuziendesha shule hizo. Hivyo kila shule zita compete na real market price itajitokeza wakati huo huo serikali ikiziboresha shule zake...
Binafsi yangu naamini kabisa Tambaza ya wakati wa Nyerere sio Tambaza ya leo kiwango cha Elimu nchini kimeshuka kiasi kwamba wanafunzi wanamaliza darasa la saba wengine hawajui kusoma wala kuandika na hii ni across the board..Shule na Hospital zimekuwa utapeli mwingine ambako madawa na huduma fake zinapatikana kwa wale wasiokuwa na uwezo..