Makanisa ya kiroho mnatupeleka wapi?

Makanisa ya kiroho mnatupeleka wapi?

Ndo mana nitabakigi kwenye madhehehu yaliyokuwepo miaka na miaka. Nishaapa kanisa la mtu binafsi sihamii ng’oooo!!!
 
Mimi nilishaachana na hizo habari kitambo sana tu.

Sadaka nitatoa mwenyewe kwa jambo ninaloona mwenyewe linafaa.

Nilikuwa nasikiliza BBC World Service kama kawaida yangu, wakawa wanaongelea habari mpya nilikuwa sijawahi kuisikia.

Kawaida huwa kuna watu wanapenda kuwa dominated katika mahusiano, wanapenda kuna na ma "dominatrix", usually it is about the use of force and humiliation.

Sasa siku hizi kuna mpaka ma "financial dominatrix", kwa mfano mwanamke ana m control mwanamme anam dominate mpaka kwenye mambo ya fedha, mwanamme anampa pesa zake zote mwanamke (wengine mtasema mganga wake mzuri huyo mwanamke, lakini hamna uganga hapo)

Ulivyosema hiyo habari, nikakumbuka hawa "dominatrix", hao Wachungaji nao wanaweza kuwa katika kundi moja na ma"financial dominatrix".

The Wwashington Post did an article on this.

- The Washington Post

Meet the dominatrixes who control men where it really hurts: Their wallets

In a pastel-colored French patisserie in Beverly Hills, Mistress Harley sips on a Bellini topped with raspberries and scrolls through surveillance monitors on her Android. “Oh, look, there’s Ben!” she says, tapping on the screen with her long magenta nails. “He’s naked.”

Speaking into the microphone on the app Nest, which is usually used for things like home security and pet monitoring, Mistress Harley instructs the man to kneel on the floor and bow down to her. He obeys. “You can see that I’ve made him sell all his stuff and even his bed, so he sleeps on the floor,” Mistress Harley explains. “He lives in Sacramento. I’ve actually been considering buying a house in Sacramento and making him rent it from me.”

Mistress Harley — who, like many in this article, refuses to reveal her legal name citing privacy and safety concerns — isn’t forcing Ben to do anything he doesn’t want to do. He is paying her a weekly salary to monitor him throughout the day. Sometimes she likes to cackle at him in the middle of the night via speakers installed in his bedroom. Other times, she’ll demand that he eat only meals that resemble dog food and send her photos as proof.

Read more here - - The Washington Post

I thought wewe ni atheist..
 
I thought wewe ni atheist..
Atheists ndio wanaoongoza kutoa sadaka kusaidia watu wenzao.

Kwa sababu hawaamini Mungu atasaidia.

Wanaoamini Mungu yupo wanaweza kujibalaguza tu kwa kusema "Tuombe, Mungu atajibu na kusaidia"
 
Atheists ndio wanaoongoza kutoa sadaka kusaidia watu wenzao.

Kwa sababu hawaamini Mungu atasaidia.

Wanaoamini Mungu yupo wanaweza kujibalaguza tu kwa kusema "Tuombe, Mungu atajibu na kusaidia"

Sasa kama hawaamini Mungu how do you call it “sadaka” badala ya labda mchango au msaada wa kawaida???
Sadaka ina relate na imani. ‍♀️
 
Umetoka nyumbani unaamua kuingia kanisani japo kupunguza stress za ugumu wa maisha na matatizo mbalimbali lakini humo kanisani unakutana na michango isiyoisha tena kwa lazima.
Nijuavyo mimi sadaka ni kile ambacho mtu amejaaliwa kukipata
Sasa eti kuna makanisa mpaka wameweka viwango sadaka isiwe chini ya kiasi flani, bado shukrani, bado fungu la 10, bado sadaka ya utumishi, bado sadaka ya madhabahu, bado sadaka ya malimbuko sijui nini. !
Mbaya zaidi kila mahubiri ni kusisitiza utoaji sadaka na michango tu.
Sio siri makanisa yetu mnakatisha tamaa kabisa ukute mtu ni mama wa nyumbani atapataje pesa yote hiyo kama sio mwanzo wa kugombana na mmewe.
Mungu atusaidie.

Bado kwenye jumuiya zetu zile.......
 
Hapo nilicho gundua wewe unazungumzia majengo mazur na sio kanisa zur
wewe unajifariji, ulichoandika NI TOFAUTI kabisa , uko nje kabisa ya nilichoandik, na kuendelea kubishana na wewe ni kupoteza muda, Yesu aliwahi kuwalalamikia mafarisayo kwa kuwawekea watu sheria NZITO ambazo hata wao hawatimizi , MIMI mtu hanitishi hata siku moja na hizo sadaka za kuinuliwa , NA NAAMINI MNAZITUMIAA kujilimbikia mali na si msingi wa kwenda mbinguni.
Nnacho faham Mimi kanisa zur Ni lile lenye kumcha Mungu katika misingi ya amli 10 tu nasio habar cha Tass
 
Ukweli ndio huo,kama hautaki endelea kujidanganya.

Yesu alipokua hapa duniani alifanya vitu vikuu vitano(5).1 alihubiri,2.alifundisha,3.alitoa pepo ,4.aliponya wagonjwa na 5. alifanya miujiza.

Kanisa lolote lisilofanya hayo mambo matano hata kama likiwa kubwa kiasi gani,kanisa hilo limekufa.Na watu wake wanakua wamekufa kiroho.

Mengi ya hayo makanisa uliyoyataja hapo ni mafu.Mengine uliyoandika hapo sina haja ya kujibu coz naona ni ujinga tuu utatoka taratibu taratibu kadiri unavyojitahidi kujua
Ndugu, Yesu aliwalalamika kwa wanasheria , kuwatwisha watu MIZIGO ambayo wao HATA kiduchu hawaibebi, MNAWATWISHA mama zetu na dada zetu mizigo ya sadaka, ambayo nyinyi hambebi ! HILO ni tatizo , hata kwenye mitandao ya kijamii wahubiri wazungu wanawalalamikia sana waafrika kwa mahubiri ya SADAKA na miujiza ! SISI tutawambia ukweli , HUBIRINI INJILI SIO KILA SIKU MNAWATWISHA DADA ZETU MIZIGO YA SADAKA TU. MAHUBIRI YA KUTAJIRIKA TU KILA SIKU , KUPATA KAZI NZURI UKITOA SADAKA
 
Kutoa kulitakiwa kuwe hiari,sio lazima. Hili La baadhi ya viongozi wa dini kumiliki utajiri kufuru hali waumini wao dhoofu hali lina ukakasi kidogo japo utajiri si dhambi.
 
Sasa kama hawaamini Mungu how do you call it “sadaka” badala ya labda mchango au msaada wa kawaida???
Sadaka ina relate na imani. ‍♀️

Kwanza tuone baadhi ya definitions zinasemaje

the definition of alms
alms
ä(l)mz/
noun
plural noun: alms
  1. (in historical contexts) money or food given to poor people.
    synonyms: gift(s), donation(s), handout(s), offering(s), charity, baksheesh, largesse
    "alms for the poor"
Origin
Old English ælmysse, ælmesse, from Christian Latin eleemosyna, from Greek eleēmosunē ‘compassion,’ from eleēmōn ‘compassionate,’ from eleos ‘mercy.’

Sadaqah or Sadaka (Arabic: صدقة‎, IPA: [sˤɑdæqɐ], "charity", "benevolence", plural ṣadaqāt صدقات) in the modern context has come to signify "voluntary charity". According to the Quran, the word means voluntary offering, whose amount is at the will of the "benefactor".

Etymology and meaning[edit]
'Sadaqa' literally means 'righteousness' and refers to the voluntary giving of alms or charity.[4] But in Islamic terminology; Sadaqah has been defined as an act of "Giving something to somebody without seeking a substitute in return and with the intention of pleasing Allah."[5] Meanwhile, according to Ar-Rageeb al-Asfahaani “Sadaqa is what the person gives from what he possesses, like Zakat, hoping to get closer to Allah."

Upo sawa, sadaka ina relate na imani, lakini imani sio lazima iwe kwa Mungu.

Juu hapo wanaongelea kwamba sadaka ni righteousness hususan kutoa kwa ukarimu bila kulazimishwa

Mtu anaweza kuwa na imani tu kwamba jua litachomoza kesho asubuhi, hivyo anyooshe nguo za kuvaa kesho kwenda kazini, bila kuamini Mungu yupo.

Mtu anaweza kuwa na imani ya kuwa kusaidia watu wenzake, bila kutegemea malipo ya mbinguni au kuogopa moto wa Jehanam ni jambo zuri, bila kuamini Mungu yupo.

Na kwa kweli, ukifuata definition ya kwamba sadaka ni kutoa bila kulazimishwa, mtu asiyeamini Mungu yupo, halafu akatoa msaada kusaidia watu wenzake, anatoa sadaka ya kweli kuliko mtu anayeamini Mungu yupo. Kuna ma atheists wengi sana ma philanthropists.

Maana, kama sadaka ni kutoa bila kulazimishwa, huyu anayemuamini Mungu kuna uwezekano mkubwa sana anatoa kwa sababu kalazimishwa na dini, anatoa sadaka kwa sababu analazimishwa na maandiko, kwa sababu anaogopa kwenda motoni, kwa sababu ana tamaa ya kwenda mbinguni.

Unanikumbusha mazungumzo fulani nilifanya na dada yangu mmoja mdogo mlokole (sio dada yangu mdogo Rebeca 83 , huyo ni mwingine). Yeye ni mlokole sana. Tulikuwa na msiba, tuna reflect maisha na kama kuna afterlife. Mimi muda wote niko philosophical. Namjua mlokole. Nikamuuliza, wewe ni mlokole, unafanya mengi mazuri, kwa imani ya kwamba Mungu anapenda ufanye mazuri na atakuzawadia mbingu kwa mazuriu nayofanya.

Je, ukihakikishiwa kwamba Mungu hayupo na mbingu haipo, na hakuna moto, halafu ukaambiwa uendelee tu kufanya mazuri hivyo hivyo kama unavyofanya leo kwa kuamini kuna Mungu na mbingu, utaweza?

Lilikuwa swali gumu sana kwa dada yangu, nikaona nisimuulize sana maswali mazito msibani, nikamuacha hajajibu swali.

Kama sadaka ni kutoa bila kulazimishwa, hao wote wanaotoa sadaka kwa kulazimishwa na wachungaji hawatoi sadaka, wanatoa mchango wa kulazimishwa.

Kama sadaka ni kutoa bila kulazimishwa, mtu asiyeamini Mungu ambaye anasaidia watu kwa kutaka tu mwenyewe, anayesaidia bila kuamini kwamba asiposaidia ataenda motoni wala kuamini kwamba akisaidia ataongeza nafasi za kwenda mbinguni, anatoa sadaka zaidi ya mtu anayeamini Mungu na kutoa kwa kuangalia anavyolazimishwa, au kwa kutamani mbingu, au kwa kuogopa moto.

This is where the ungodly atheist can be more godly than the believers.

Kuna dhana ya kwamba ukiwa huamini Mungu wewe ni mtu mbaya, hupendi watu, husaidii, hufanyi mema etc.

Hi ni dhana potofu.

Kuna watu tumeamua kuwa atheists kwa sababu tunaona kuamini Mungu kunatoa mwanya wa kufanya mabaya, ambayo hatuyataki (kwa mfano, kuua kwenye vita za kidini, kubagua watu wa dini tofauti etc).

Kuna watu ambao tumeamua kuwa atheists kwa sababu tunaona ukiwa unasaidia watu kwa sababu unaona kusaidia kutakuongezea nafasi ya kwenda mbinguni na kukupunguzia nafasi ya kwenda motoni,huko si kusaidia watu wengine, nikujisaidia mwenyewe.

Uko sawa kwamba kutoa sadaka ni jambo la imani, lakini, hujagusia zaidi kuona kwamba imani si lazima iwe ya Mungu.

Kuna Buddhists wanatoa sana sadaka, lakini hawamini kuwa kuna Mungu. Wanaamini mtu yeyote anaweza kuwa Buddha.

Kuna article wameandika kuhusu atheist philanthropists
Atheists are the most generous—even without heavenly reward!
 
Kutoa kulitakiwa kuwe hiari,sio lazima. Hili La baadhi ya viongozi wa dini kumiliki utajiri kufuru hali waumini wao dhoofu hali lina ukakasi kidogo japo utajiri si dhambi.
Ndiyo maana wengine tunasema hizi dinini siasa tu, watu wanashikiwa vichwa kwa sababu za kiuchumi na kisiasa.

Sasa mimi masikini nakuja kanisani kujumuika na wenzangu nipate msaada wa kiroho, kwa sababu siwezi kwenda kwa therapist kulipia sessions na wala siwezi kwenda Gymkhana kupoteza mawazo nikicheza golf na hata hela ya bia bara sina.

Halafu kanisani nakuta nikijumlisha michango ya lazima, kuanzia fungu la kumi mpaka hizo sadaka zisizo na kichwa wala mguu, napigwa kuliko ada ya Gymkhana au gharamaza bar.

Ndiyo maana watu wanajaa bar tu.
 
Kazi kwako kama utaendelea kukumbalia hizo roho zidanganyazo au utaamua kutubu,nakushauri utubu na uanze kumtolea Mungu na kusimama na kazi yake.
Sikiliza wewe kipofu wa imani, MUNGU haitaji pesa, wala sadaka, MUNGU anahitaji watu kutenda mema kwa kuzishika Amri zake zote pasipo kuzivunja hata moja. MUNGU anahitaji mioyo iliyopondeka, MUNGU anahitaji UPENDO na REHEMA. Kama unatoa sadaka wakati huna upendo kwa binadamu wenzako, sadaka yako ni bure kabisa! Kama utanatoa mamilioni ya sadaka kanisani, lakini huzishiki Amri Kumi za MUNGU sadaka zako ni bure kabisa!

Soma 1 SAMWELI 15:22 imeandikwa hivi;
"Je! BWANA huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu sawa sawa na kutii sauti ya BWANA?
Angalia kutii ni bora kuliko dhabihu, na kusikia kuliko mafuta ya beberu".

MITHALI 21:3 imeandikwa hivi;
"Kutenda haki na hukumu humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka".

HOSEA 6:6 imeandikwa hivi;
"Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua MUNGU kuliko sadaka za kuteketezwa".

ISAYA 1:11 imeandikwa hivi;
"Huu wingi wa sadaka zenu mnazonitolea una faida gani? Asema BWANA".

YEREMIA 7:22 imeandikwa hivi;
"Maana sikusema na baba zenu wala sikuwaamuru kwa habari za sadaka za kuteketezwa na dhabihu siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri; lakini naliwaamuru neno hili nikisema, sikilizeni sauti yangu nami nitakuwa MUNGU wenu nanyi mtakuwa watu wangu mkaende katika njia ile yote nitakayowaamuru mpate kufanikiwa.

MIKA 6:6-8 imeandikwa hivi;
Nimkaribie BWANA na kitu gani na kuinama mbele za MUNGU aliye juu? Je! nimkaribie na sadaka za kuteketezwa na ndama za umri wa mwaka mmoja? Je! BWANA atapendezwa na elfu za kondoo waume au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu? Eeh Mwanadamu Yeye amekuonesha yaliyo mema na BWANA anataka nini kwako; ila kutenda haki na kupenda rehema na kwenda kwa unyenyekevu na MUNGU wako!

WAEBRANIA 10:6 imeandikwa hivi;
Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo, ndipo niliposema tazama nimekuja niyafanye mapenzi yako MUNGU.

Mkuu Conspiracy theorist unapaswa kuwa na akili na busara kujua MUNGU anataka nini kutoka kwako, sadaka ni muhimu lakini siyo kipaumbele cha BWANA MUNGU, dini ya kweli na imani ya kweli siyo kutoa sadaka kanisani, dini iliyo safi isiyo na taka mbele za BABA MUNGU ni hii; kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao na kujilinda na dunia pasipo mawaa. UPENDO kwa Binadamu wenzako ni bora kuliko sadaka yako kanisani.

Mwenye masikio na asikie!
 
Sadaka Ni Ibada. Kuna Aina Kadhaa Za Sadaka, Sadaka Ya Hiari, Sadaka Ya Shukrani Na Fungu La Kumi/ Zaka. Halafu Kuna Malimbuko. Sadaka Hizi Hutolewa Kwa Imani. Kama Huna Imani Huwezi Kutoa. Utoaji Ni Moyo, Hata Kama Unacho Kidogo Kama Una Moyo Wa Utoaji Na Imani Unatoa Tu. By The Way Utoaji Si Pekee Kwa Makanisa Ya Kiroho Tu Hata Hayo Makanisa Mengine Nayo Waumini Wake Hutoa, Tena Wana Visanduku Vya Kuweka Bahasha Zenye Fedha Na Vina Namba Kabisa. Ni Rahisi Kumtambua Muumini Ambaye Si Mtoaji Na Rekodi Zake Za Utoaji Zaka Zinawekwa. Akipata Shida Itakoyohusu Msaada Wa Kanisa Rekodi Zake Za Utoaji Zitaangaliwa Kwanza Ndiyo Msaada Utolewe Kwa Kiwango Kinachostahili. Kama Si Mtoaji Unaweza Ukasusiwa Shughuli Zako Ufanye Mwenyewe. Utoaji Ndiyo Ushirika Wenyewe. Utoaji Uko Kila Kanisa Mpaka Jumuiya Zake Za Mitaani. Utoaji Ni Imani Kama Huna Imani Ni Ngumu Kutoa. Unaamini Nini Katika Kutoa ? Labda Hoja Ingekuwa Kutoa Ni Fedha Pekee Tu ? Kwa Nini Iwe Fedha Pekee Tu ? Sifa Kuu Ya Mshirika/muumini Ni Utoaji Sadaka.
 
Inakatisha tamaa kwenda church unajifikiria mara 2,2. Siku hizi uwe na angalau 15000/=kwenye wallet ndo uingie church
 
Toa Sadaka kwa Yatima,Wajane,Masikini,Wasiojiweza,Wenye mahitaji maalumu,Kamwe usitoe sadaka kwa wachungaji wa kileo ambao sadaka yako anaenda kujenga Jumba la bil 1.5,anaenda kununua gari la mil 200 na vitu vinavyofanana na hivyo,mtu ambaye anaifata dini kweli hauwezi kujilimbikizia mali kwa kuwanyonya masikini.
 
Msikitini hata usipotoa hakuna anaekulaumu
yaan waislamu nawakubali hapo tu, mhubiri wa kiislamu anaweza toka zanzibar akaenda kigoma kuhubiri akajigharamia mwenyew kila kitu na akarudi zake zenhi kuendelea na shughuli zake za kujenga taifa ila kwa sisi wakristu hakuna hilo mtu hawez fanya lolote kama hakuna michango yaan kila kitu ni pesa, yaan unakuta waumin maskini wanajuhudi kweli ya kutoa mchango hata kula yao ni mtihani ila mchungaji ana mpango wa kununua private jet yaan ni mambo ya ajabu sana
 
Binafsi si mjuvi sana wa haya mambo ila ukweli ni kwamba Kanisa za leo dhana ya sadaka haiko ktk uhalisia wake tena, wakristo wa leo haswa Waafrika SADAKA tumeinyumbua sana hadi tukatoka kwenye uhalisia wake na hatima yake tunaanza kuimithilisha na wizi kwa kivuli cha sadaka.
 
Umetoka nyumbani unaamua kuingia kanisani japo kupunguza stress za ugumu wa maisha na matatizo mbalimbali lakini humo kanisani unakutana na michango isiyoisha tena kwa lazima.
Nijuavyo mimi sadaka ni kile ambacho mtu amejaaliwa kukipata
Sasa eti kuna makanisa mpaka wameweka viwango sadaka isiwe chini ya kiasi flani, bado shukrani, bado fungu la 10, bado sadaka ya utumishi, bado sadaka ya madhabahu, bado sadaka ya malimbuko sijui nini. !
Mbaya zaidi kila mahubiri ni kusisitiza utoaji sadaka na michango tu.
Sio siri makanisa yetu mnakatisha tamaa kabisa ukute mtu ni mama wa nyumbani atapataje pesa yote hiyo kama sio mwanzo wa kugombana na mmewe.
Mungu atusaidie.
 
Back
Top Bottom