PostGE2025 Makamu Mwenyekiti CHADEMA John Heche azidiwa, akimbizwa hosptali ya taifa ya Muhimbili

PostGE2025 Makamu Mwenyekiti CHADEMA John Heche azidiwa, akimbizwa hosptali ya taifa ya Muhimbili

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections
Chanzo cha Serikali kukosa haya ni Magufuli, ndiyo maana leo katiba inaitwa kijitabu, Magufuli ni source wa haya yote kuchezea katiba na ndio maana wengine hawa wanaona katiba haina maana

Be strong John Heche, Mungu akurejeshee afya na nguvu tele
Let's say uko sahihi kuwa chanzo cha haya yote ni Magufuli. So what? Twende Chato tukamfufue ama?

20251023_135323.png
 
Chanzo cha Serikali kukosa haya ni Magufuli, ndiyo maana leo katiba inaitwa kijitabu, Magufuli ni source wa haya yote kuchezea katiba na ndio maana wengine hawa wanaona katiba haina maana

Be strong John Heche, Mungu akurejeshee afya na nguvu tele
Acha kumshutumu Magu. Yeye anabeba ya kwake. Lakini haya ni upumbafu wetu tuliopo hai.

Kwani sisi ni wendawazimu? Kama Magu alikosea, ni lazima na sisi tukosee. Huu ni uvivu wa kufikiri kuwapelekea lawama marehemu ama watu wasio na mamlaka kwa wakati huu.

Tujibebe wenyewe. Kama tunazama acha tuzame, kama kuna namna ya kujiikoa tufanye hivyo.
 
Waombe mashetani wanayayaabudu asife. Maana akikata moto sijui nini au nani atatuliza ghadhabu za walimwengu.
tatizo lenu mnaichukulia serikali kama kituo cha daladala, Hata biblia inasema Heshimuni mamlaka ilipo juu
 
Kwa sasa katiba ya nchi haigeshimiwi.
CHAUMA walipata chini ya asilimia moja ya kura zote kwa mujibu wa yule jaji wa tume kandamizi. Iweje wapewe wabunge wawili wa kuteuliwa wa KIKE?
 
Kutoka mitandao ya kijamii ( not confirmed)

MAKAMU mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Heche, amekimbizwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam, baada ya hali yake ya kiafya kuripotiwa kudorora.

Taarifa hizi, zimethibitishwa na mmoja wa wanafamilia wa mwanasiasa huyo. Anasema, Heche alichukuliwa kutoka kituo cha polisi cha Mburahati, alikokuwa anashikiliwa na kukimbizwa hospitali, kutokana na hali yake ya kiafya kuendelea kuwa mbaya. Hajasema anasumbuliwa na maradhi gani.
 
Back
Top Bottom