Makaidi atoboa siri urais UKAWA

Makaidi atoboa siri urais UKAWA

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Mwenyekiti mwenza wa UKAWA Dr Emmanuel Makaidi amewataka wafuasi wa UKAWA kote nchini kutojishughulisha na mchakato wa kumpata mgombea Urais ndani ya CCM.

Dr Makaidi ambaye pia ni Mwenyekiti wa NLD amesema badala yake wanachama wote waendelee kuijenga UKAWA huku wakisubiri kutangazwa mgombea mmoja atayepeperusha bendera ya UKAWA kugombea Urais ambaye pia akishatangazwa kuna uwezekano mkubwa wa kuwa Rais wa Tanzania.

Dr Makaidi aliyekuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Masasi ametangaza pia nia ya kugombea Ubunge Masasi mjini kwa tiketi ya UKAWA.

Ikumbukwe Watanzania wana Imani kubwa na UKAWA na pia wanaamini umoja huo unaoundwa na vyama vya NLD,CHADEMA,NCCR na CUF utapendekeza mgombea mwenye ushawishi mkubwa na uwezo wa kupambana na rushwa na kuwaondolea umaskini.

Chanzo: Chanel ten Habari.
 
Hii ni habari njema sana .........Wacha Vibaka wa CCM Waendelee na mchakato wa kutafuta kibaka bora .....atakuja kupambana na UKAWA imara
Uzuri wa Hawa watangazania wa kila leo Watanzania wamewaona wanacheza mchezo wa futuhi tuu
 
Hizi siyo habari njema kwa mafisadi wa CCM...
 
Sasa mbona magazeti walisema UKAWA hakukaliki? Ooo urais unaigawa UKAWA Sasa itakuwaje jamani ccm hoye!
 
Ndio uzuri wa UKAWA, hatugombei vyeo kama Ma-CCM.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom