Makafara yanatumaliza wafanyakazi benki ya Posta

Makafara yanatumaliza wafanyakazi benki ya Posta

Mkuu huna nyumbani kwani....omba kalikizo kafupi mji mzito huu
 
Mwamini Yesu Kristu utaishi kwa amani kweli mkuu
 
mtakufa kweli wewe huoni kila ofisi akichaguliwa kibosile mpya lazima anunue sofa set mpya na kila kitu kipa unadhani wajinga wale au wanataka tu vitu vipya , yale masofa aliyoyakuta hata kama mapya yanatolewa analeta yake.
Hii yakubadili vipya nimeona mkuu.
 
Hapo umejitafutia matatizo kabisa maana wengi wanaotoa hii Siri huwa wanakufa
 
Sisi wafanyakazi wa benki ya posta tunafanya kazi kwa hofu kubwa ya kufa.
Kwa mwezi wa tano na wa sita wanakufa wafanyakazi zaidi ya wanne.
Kila anayekufa lazima amwage damu.
Yaani hali ni mbaya sana.
Jana Kuna Dada wa HR kafa akiwa anafanyiwa upasuaji wa nyonga, hip bone.
Mkuu angalia Avatar yako isije ikakuletea matatizo, umejianika sana
 
Acha kupotosha umma huyo dada aliefariki ni kutokana na uzembe wa madaktari wa hospital ya Hindu Mandal kum overdose nusu kaputi... wakuu tuwe makini na hizi hospitali ni janga aisee bora uende Muhimbili tuu
Hizi case hizi alafu Ni kwenye hospital za private Mara nyingi cjui kwanini.........

Miaka kadhaa iliyopita Kuna Dada tulimzika aliacha twins wake kwa uzembe huuhuu na ilikua Ni private hospital Arusha iyooi
 
Hahaha hahahahahaha uchawi upo me nawaangalia tu hawa wanaoongea shit hapa yakiwakuta wataondoa huu ubishi wao......


Kuna mwalimu mmoja shule fulani huku kusini alikuwa na tabia ya kupiga wanafunzi vibaya mnooo siku hiyo kalala ndani kwake asubuhi wanamkuta juu ya simtank amelazwa huko.... Wenzie wakamshtua we jamaa vipi akashushwa pale toka siku hiyo alikuwa hapigi wanafunzi kama anauwa nyoka na bila sababu
Mimi shule niliyosoma O Level watu walikua wanakufa jamani. Yani kila mwezi anakufa mwanafunzi. Wengine wanapandisha mapepo darasani. Alianza dogo wa form one kwa kutoa mimba. Alikufa mwezi wa kwanza mwishoni. Akaja wa form two kwa kugongwa na gari wakati tunatoka kwenye michezo Lushoto. Tukapumzika kidogo. Kuanzia mwezi wa 10 mambo yakarudi upyaaa. Kila mwezi form one mpaka form 3 anakufa mtu. Kuna familia walikufa watoto wao wawili ndani ya miezi mitatu. Walivyofika wanafunzi 10 ndani ya miezi 6 nikamwambia mama nihamishe shule naona kabisa mambo yatahamia form four. Ikabidi wazazi wakae kikao wakatafuta wachungaji na wachungaji. Baadae nikasikia walichinja mbuzi mbele ya mti uliokuaga assembly ndio vifo vikapotea. Madam mmoja alikuaga kaokoa akasema kulikua na agano la damu ndio sababu ya vifo vyote vile.
Kweli watu tunakufa ila vifo vya kila mwezi tena wanafunzi sio kitu cha kawaida
 
ofisi zote au makampuni yote au taasisi zote kubwa kubwa lazima mtu 1 au zaidi aondoke kila mwaka hata kam ani kibarua lazima ujue hilo. IPP Media huwa unaonaje kila mwaka, na mengine mengi fuatilia
 
Back
Top Bottom