Makafara katika ujenzi wa magorofa

Makafara katika ujenzi wa magorofa

Mengi, nilikosekana na ajali kama Mara 4,mpk siku moja nikapata ajali mbaya Kuna gari ikapanda juu ya gari yangu. tulikua tunalala mke wangu anakuta kitanda kila siku kinacheza, Kuna siKu Kuna mtu aliingia ndani akawa anataka kumuingiza Mtoto wangu kitu mke wangu akagimbana nae sana usingizini, asubuhi tunaamka mtoto amefanya mstari mweusi kwenye kifua.

Mbali ya hayo nilianza kuuza gari,niliuza kiwanja,niliuza duka, niliuza kila kitu.

Nikishtuka nilijua tayari Kuna Mambo siyaelewi na chanzo ni kuhamia Iyo sehemu mpk Leo bado naungaunga.

Daaah....pole ndg....Tatizo lako linawakuta watu wengi sana....Ila wengi hawajui namna yakupambana nahiyo hali Kwakawaida ARDHI ni Lango hicho kiwanja aliekuuzia Alikifanyia Zindiko sasa hilo zindiko ndio limeleta hayo yote Inatakiwa kila unaponunua Kiwanja au Kipande chochote cha Ardhi lazima ukitakase Kumbuka Habari za Musa alipoambiwa na MUNGU avue Viatu....daah....Mkuu nakusikitikia pia nakupa Pole lkn maarifa yakushinda majanga kama hayo wekeza kwa Mungu kwa kumaanisha...utatoka tu hata mimi nilikuwa naishi hovyohovyo tu lkn yaliponikuta nikautafuta USO wa Mungu sasa hivi najua mengi khs hayo mambo yakishirikina
 
hakuna kitu kama hicho , ni imani yenu tu, hutegemea malezi yako, jamiii uliokulia na kulelewa, elimu, mazingira unamoishi , imani potofu sana hizo

Usiishi kwa kukariri ndg Jifunze utaelewa inaonekana unaishi Dunia ya peke yako
 
mshana jr speaking of magadi hapo, naomba unambie kuhusu issue ya kuogea magadi huwa inasaidia nn exactly?
 
Last edited by a moderator:
Mtu asikudanganye, dunia hii ina pande mbili ulimwengu tunauona na ule tunauhisi/ hatuuoni. lakini hizi zote zinafanya kazi kwa kutegemeana, mambo yote yanaanza kufanyika kwenye ulimwengu tusiouna kwanza halafu matokeo yake ndiyo tunayaona mwilini, yaani phyisical world. mtu akipata kitu alikipata kizuri au kibaya, kilikuwepo rohoni kwanza ndipo kikaja mwili.

Wapo wanaoona mambo haya, wachawi waganga wa kienyeji, watakatifu, baadhi ya viongozi wa dini zenye muunganiko wa kweli na Mungu wanaona.Hivyo ndiyo maana ni rahisi kumwambia mtu fanya hivi au hivi utashinda. mfano anayesema chumvi na mfupa wakitimoto alipata wapi hayo maneno? lazima aliambiawa na waona fahamu eimu hii. ni elimu njema kuijua maana ndiyo chimbuko la kufanikiwa kwetu.

Mtu akikwambia uongo mambo haya hayapo. either yeye anafaidika na upande huo na hataki wewe ujue ili usimpinge, au hajui kwa maana ni kipofu au anatumiwa aseme hivyo ili usifahamu. Kwa kawaidaa binadamu akifahamu kitu ukombozi unakaribia maana ataanza kupambani ili atoke, hivyo anayefaidika na ujinga wako hatapenda ujue ukweli.

Ndoto ni kigezo kikubwa cha kujua upande ulioko, kama unaota mabaya tu ujue jambo baya lipo upenuni linakuja, na kama unaota mema, ujue pia jambo jema lipo upenuni linakuja pia. ukiwa na maarifa unaweza kuyapinga mabaya na yasije, na ukiwa na maarifa unaweza kuyaita mema na yakaja.

Hivyo ni vyema sana kutafuta nafsi na kujifunza juu ya jambo hili kwani ndimo ufanisi wa ubinadamu ulimo. Kuna watu wamejaliwa kabisa wanaona mambo haya, japo inaweza kuwa kwa kipindi fulani kisha uwezo unapotea kulingana na alivyo jipanda na source ya uwezo huo.

Ndugu asante kwa hii uliyoandika....Kwanza kupitia ndoto MTU unaujua kitu gani kitakuja kukutokea kama nikibaya au kizuri sasa wengi wanajifanya kutojali Badae yanawakuta wakiwa wamechelewa kuyazuia
 
Hapana si kweli kabisa wee huoni huko kwa wenzetu mpaka serikali imekubali uwepo wa wachawi lakini huku kwetu bado

Huyo jamaa ni miongoni mwa watu wanaoamini Mzungu ni Binadamu tofauti....Pamoja nakumuwekea hizo picha bado haelewi
 
Mimi namshukuru mungu kwenye kanyumba kangu sijafanya chochote hila sijawai pata tatizo lolote watoto wako poa na kakipato nakapata kama sio hii kasi ya hapa kazi tu ningenunu kakiwanja kengine panda hizi watu wastarabu mpaka basi
 
Huyo kuku aliliwa. Changa la macho. Nenda uone kama utakuta hata bawa!. Waganga wanawadanganya sana watu. Pole zenu
 
Mtoa mada hii inauhusiano na matukio ya kimiujiza katika Maghorofa tuyaonayo hapa mjini.Nisingependa kutaja ni ghorofa gani ila nina pokea matukio mengi ya Wafanyakazi hasa wanafanya usafi na maid wa Maghorofa .mara nyingi wanapandisha mapepo/mashetani na wanatulia bila hata ya kunywa dawa yoyote...
 
Mtoa mada hii inauhusiano na matukio ya kimiujiza katika Maghorofa tuyaonayo hapa mjini.Nisingependa kutaja ni ghorofa gani ila nina pokea matukio mengi ya Wafanyakazi hasa wanafanya usafi na maid wa Maghorofa .mara nyingi wanapandisha mapepo/mashetani na wanatulia bila hata ya kunywa dawa yoyote...

Posta muhimbili na kariakoo hivyo visa vipo sana
 
Ni jambo la kificho mno, lisilojulikana na wengine wengi lakini ukweli ni kwamba magorofa mengi uyaonayo yana roho za watu au imevunja mifupa ya watu kwa njia za ajali au yamekunywa damu ya kikafara
Si mara zote wafanyao mambo haya ni wamiliki la hasha bali mambo haya hufanywa pia na wakandarasi na hata waliopewa tenda mbali mbali kwenye site husika... Nia na lengo ni moja tuu kupata zaidi au kujikinga kishirikina
Kama tungekuwa na takwimu za kitaifa si ajabu kati ya kila magorofa kumi saba yamesababisha maafa vilema na makovu... Hili jambo lina level zake kuanzia kutoa kafara dogo la mtu mmoja mpaka ibada za makafara zifanywazo na makandarasi wakubwa kufikia viwango vya freemason
Ndio maana kwenye ujenzi wa mahekalu makubwa ya ibada hufanyika ibada maalum za kumwomba Mungu aepushe mbali mabaya yote kwenye ujenzi husika mpaka mwisho wa ujenzi wake.
Hata wewe kwa kutambua hili fanya hivyo kwenye ujenzi wako hata kama si ghorofa ili nyumba yako isije kuwa ni chanzo cha mabalaa na mitihani ya dunia
Mkuu mshana jr Ninakubaliana na wewe kuwa inapojengwa

nyumba ya gorofa lazima itolewe Kafara ya mtu au watu zaidi ya 2 na kuendelea ili hiyo nyumba ipate kuishi muda

mrefu huku nje Ughaibuni huwa wanatowa watu wengi utakuta wanasema hayaleo tunataka tunafunguwe duka au

nyumba mpya ya biashara gorofa 20 njooni Wananchi kuja kuchukuwa vitu bure leo basi utakuta wananchi

wankwenda wengi kupita kiasi na wakifika katika hiyo nyumba ya gorofa ya biashara wanapanda lift wengi basi

utakuta hiyo lif inakatika minyororo na utasikia watu 10 au zaidi ya hapo wamefariki ndio kafara yenyewe

inavyofanyika hivyo. huko kwetu Afrika kuna baahi ya nchi katika kila kituo cha polisi mlangoni mwake aakuwa

amezikwa kichwa cha mtu wana imani kuwa kukizika kichwa cha mtu kunafanya kila siku wawe wanakuja watu hapo

kituoni imani za kishikirikina hizo zipo hata huko kwetu nyumbani.


mshana jnr mimi nikiwa mbali na kwangu mambo yangu safi lakini kosa niende kwangu kisha niende kwenye mihangaiko yangu ni mabalaa kwenda mbele kama siyo ugomvi basi burst au biashara kugoma na mawasiliano yanakuwa mabaya nifanyeje?
Mkuu CARBON 14 Umefanyiwa mambo ya kiuchawi nitafute mimi kwa wakati wako nipate kukutibia ukihitaji matibabu yangu unawezakunitafuta kw akubonyeza hapa.
Mawasiliano

Ninavyodhani: Hapo kwako pamefanyiwa kafara la mikosi, ramli chonganishi nuksi na banyanyi naomba wasiliana na
Mkuu mshana jr ni kweli Mkuu CARBON 14 amefanyiwa uchawi nyumbani kwake ili asiweze kuwa na amani na utulivu akinitafuta nitaweza kumtibiana mambo yake yatakuwa yapo poa nimeshampa contact zangu Mkuu CARBON 14.
 
Last edited by a moderator:
Pole ndg kama ni Mkristo...chukua mchana....nenda kwa Mchungaji wako ukafanye toba ya a
ARDHI simamia Neno kutoka 2nyakati 7:14 INASEMA IKIWA WATU WANGU WALIOITWA KWA JINA LANGU WATAJINYENYEKESHA KUNIYAFUTA USO NITASIKIA TOKA MBINGUNI NITAPONYA NCHI YAO...ukimaanisha hayo Maombi utaishi hapo bila Zengwe kila la Heri ndg

Nashkuru mkuu wangu na nitayazingatia haya maombi mm mwenyewe sasa
 
Mimi namshukuru mungu kwenye kanyumba kangu sijafanya chochote hila sijawai pata tatizo lolote watoto wako poa na kakipato nakapata kama sio hii kasi ya hapa kazi tu ningenunu kakiwanja kengine panda hizi watu wastarabu mpaka basi

uko pande zipi mkuu kwenye nafuu kidogo kwakua hapa dar sidhani kama kuna sehemu utapata kuishi 100pacent
 
Daaah....pole ndg....Tatizo lako linawakuta watu wengi sana....Ila wengi hawajui namna yakupambana nahiyo hali Kwakawaida ARDHI ni Lango hicho kiwanja aliekuuzia Alikifanyia Zindiko sasa hilo zindiko ndio limeleta hayo yote Inatakiwa kila unaponunua Kiwanja au Kipande chochote cha Ardhi lazima ukitakase Kumbuka Habari za Musa alipoambiwa na MUNGU avue Viatu....daah....Mkuu nakusikitikia pia nakupa Pole lkn maarifa yakushinda majanga kama hayo wekeza kwa Mungu kwa kumaanisha...utatoka tu hata mimi nilikuwa naishi hovyohovyo tu lkn yaliponikuta nikautafuta USO wa Mungu sasa hivi najua mengi khs hayo mambo yakishirikina

Ni kweli wengi wamerudi kijijini na kulaumiwa sana na jamii, kumbe kuna tusiyoyaona yanatusumbua. Lakini kupata mitihani ndio kusoma maisha bila ya kupitia huku kila mtu unaweza kumdharau na ukawafanya wengine ni wajinga.. Nimesoma mengi niliyokua sikuwahi kuyajua katika kipindi changu kigumu cha maisha. Ahsante sana tutakiane dua
 
Nashkuru mkuu wangu na nitayazingatia haya maombi mm mwenyewe sasa

Yaap....ukiombea mwenyewe ni safi zaidi...cz ww unajua mazingira halisi ya hilo eneo...Chukua mchanga weka kwenye Kiganja kunja ngumi....Ukishamaliza kumuomba Mungu akusamehe Dhambi zako uamrishe ule Mchanga vile unavyotaka Kwa sababu huo mchanga ni Roho inayosikia utauamrisha nautakutii kwa Jina la YESU hutaona shida tena....
 
Ni kweli wengi wamerudi kijijini na kulaumiwa sana na jamii, kumbe kuna tusiyoyaona yanatusumbua. Lakini kupata mitihani ndio kusoma maisha bila ya kupitia huku kila mtu unaweza kumdharau na ukawafanya wengine ni wajinga.. Nimesoma mengi niliyokua sikuwahi kuyajua katika kipindi changu kigumu cha maisha. Ahsante sana tutakiane dua

Amina....ndugu yaah...kuhusu hiyo watu kulaumu ipo sana Kwamfano.....Umaskini wakati mwingine sikwamba MTU anapenda kuwa maskini ila MTU unatengenezewa utataabika km hujajishughulisha kuitafuta sababu.....MTU unabaki historia maisha utayaona sio kabisa Acha ndg yangu nimepitia hiyo misukosuko yakurogwa wacha kabisa....
 
Kuna baadhi ya nyakati mmiliki mjenzi/mkandarasi na hata mafundi hawana tatizo bali tatizo linakuwa ni kipande chenyewe cha ardhi... Pengine hapo kilikuwepo kilinge cha wachawi au Pengine palifanyiwa kitu kibaya cha kishirikina au Pengine kuna watu walishawahi kufa au kuawawa hapo na roho zao zikabaki hapo zikisubiri kisasi

Wewe kijana Kuna kikubwa sana unacho, ila uhuni umeweka mbele.
 
Back
Top Bottom