Makafara katika ujenzi wa magorofa

Makafara katika ujenzi wa magorofa

Upuuzi au viimani mshenzi tu ukiviendekeza hata usingizi utaukosa!

1451041382626.jpg baki hapo hapo
 
  • Thanks
Reactions: itv
Mimi yalinikuta hayo nilinunua site nilijenga fasta baada ya miezi 3 nikahamia, yaliyonikuta Mungu ndo anaejua. Kiukweli Nyumbani imenishinda nimeiacha ni majanga mpk Leo sijakaa Sawa.

Mkuu hayo maneno ni kweli au fix tu. Sijali nyumba iko sehem gani lakini kama huitaki niuzie. Ila kama unaitaka, mimi ni mjenzi nipe contract niimalizie kwa mkataba mzuri tu. Ni PM tuwasiliane. Natafuta majumba ka hayo yaliyokataliwa niwawezeshe wenye nazo kuingia. Wakiogopa, nipeni
 
Dawa pekee hapo ni kuita watumishi wa kuaminika washushe maombi


mshana jr;
Kila siku nashindwa kukuelewa. Maombi hayo ya hao watumishi ni ya dini gani? Hata kule siye twasomaga kisomo na mambo yakawa powa kabisa. Je unamtuma wapi sasa?
Ila kule, uvumba lazima
 
mshana jr;
Kila siku nashindwa kukuelewa. Maombi hayo ya hao watumishi ni ya dini gani? Hata kule siye twasomaga kisomo na mambo yakawa powa kabisa. Je unamtuma wapi sasa?
Ila kule, uvumba lazima

Atakapoona panafaa kaka
 
Kule pangani kuna majengo ya zamani mojawapo kuna nguzo inasemekana walifukiwa watu wakiwa hai..nadhani ndio inahusiana na hii..
 
Wenzetu ulaya ni wachawi sana kuliko unavofikiria lkn sio kama uchawi wa kiafrika. Mshana jr aliweka hapa mpaka vyuo wanasomesha.

Ni tofauti sana. Uchawi wao ni wa mazingaombwe na hayamdhuru mtu, na ni tofaiti na uchawi wa kutumia majini na mashetani. Nime kaa huku ulaya miaka 15 na sijawahi kumsikia mzungu akisema anaenda kwa mganga ili afanikiwe au anaenda kumkomesha mtu. Lakini Tanzania utasikia karibia kila siku
 
Kaka Mshana ushirikina upo kabisa nakumbuka 1998 nilienda kumtembelea kaka yangu maeneo ya bariadi ambayo kwa sasa ni simiyu nyege zangu ziliniponza nikamfuata demu mbali kidogo na nilipofikia wakati narudi saa saba za usiku nilifukuzwa na mienge ya moto iliyokuwa inapepea mithili imeshikwa na mtu nilifika kwa kaka yangu kwa mateso makubwa wazee Wa gamboshi walinikomesha uhuni.
 
Mengi, nilikosekana na ajali kama Mara 4,mpk siku moja nikapata ajali mbaya Kuna gari ikapanda juu ya gari yangu. tulikua tunalala mke wangu anakuta kitanda kila siku kinacheza, Kuna siKu Kuna mtu aliingia ndani akawa anataka kumuingiza Mtoto wangu kitu mke wangu akagimbana nae sana usingizini, asubuhi tunaamka mtoto amefanya mstari mweusi kwenye kifua.

Mbali ya hayo nilianza kuuza gari,niliuza kiwanja,niliuza duka, niliuza kila kitu.

Nikishtuka nilijua tayari Kuna Mambo siyaelewi na chanzo ni kuhamia Iyo sehemu mpk Leo bado naungaunga.

Ardhi ilikuwa na laana na maagano kiasi yoyote atakayetumia akubwe na majanga. Ndo mana inashauriwa ukinunua ardhi itakaye na kuiombea. Huwezi jua ardhi hyo kulifanyika maagano gani au mikafara
 
Hayo mambo yapo,tangia wadogo tumeyasikia sana.Vipi kuhusu ujenzi wa hospitali(theatre) za upaauaji na zenyewe kuna kafara?
 
Mimi yalinikuta hayo nilinunua site nilijenga fasta baada ya miezi 3 nikahamia, yaliyonikuta Mungu ndo anaejua. Kiukweli Nyumbani imenishinda nimeiacha ni majanga mpk Leo sijakaa Sawa.

Hiyo nyumbA ipo wapi!?
 
Ni tofauti sana. Uchawi wao ni wa mazingaombwe na hayamdhuru mtu, na ni tofaiti na uchawi wa kutumia majini na mashetani. Nime kaa huku ulaya miaka 15 na sijawahi kumsikia mzungu akisema anaenda kwa mganga ili afanikiwe au anaenda kumkomesha mtu. Lakini Tanzania utasikia karibia kila siku

Sasa ndugu yangu Brown73 unataka uchawi wa ulaya ufanane kila kitu na wa huku kwetu? Hii ni very wrong judgement... Kukaa ulaya miaka 15 haimaanishi unajua kila kitu cha huko... Kuna wahindi wa hapo Posta magorofani hawaijui tabata segerea wala kigodoro na maisha yao yote wapo hapahapa
Naona una notion ya kwamba wote tunaoandika hapa hatujawahi kufika au kuishi huko ulaya
Sasa kwa taarifa yako bwana Brown73 huko ulaya kuna na vyuo kabisa vya ushirikina na si mazingaombwe kama unavyotaka kutuaminisha hapa
 
Last edited by a moderator:
Hayo mambo yapo,tangia wadogo tumeyasikia sana.Vipi kuhusu ujenzi wa hospitali(theatre) za upaauaji na zenyewe kuna kafara?

Inategemea imejengwa na watu gani na wanaamini nini
 
mshana jr mimi nataka dawa ya kumuona mchawi na mwanga unayo?
 
mshana jr mimi nataka dawa ya kumuona mchawi na mwanga unayo?

Ninayo lakini siwezi kutupatia kwasababu hutawaona wao tuu, utaona na vingine vingi vya ajabu utapiga kelele au kukimbia.... Na watu watakukumata wakidhani tayari Homa imepanda kichwani... Utawashangaa lakini wao watakushangaa zaidi na mwishowe utaishia mirembe... Usidhani wote walioko kule ni wendawazimu kama tunavyodhani
 
ni jambo la kificho mno, lisilojulikana na wengine wengi lakini ukweli ni kwamba magorofa mengi uyaonayo yana roho za watu au imevunja mifupa ya watu kwa njia za ajali au yamekunywa damu ya kikafara
si mara zote wafanyao mambo haya ni wamiliki la hasha bali mambo haya hufanywa pia na wakandarasi na hata waliopewa tenda mbali mbali kwenye site husika... Nia na lengo ni moja tuu kupata zaidi au kujikinga kishirikina
kama tungekuwa na takwimu za kitaifa si ajabu kati ya kila magorofa kumi saba yamesababisha maafa vilema na makovu... Hili jambo lina level zake kuanzia kutoa kafara dogo la mtu mmoja mpaka ibada za makafara zifanywazo na makandarasi wakubwa kufikia viwango vya freemason
ndio maana kwenye ujenzi wa mahekalu makubwa ya ibada hufanyika ibada maalum za kumwomba mungu aepushe mbali mabaya yote kwenye ujenzi husika mpaka mwisho wa ujenzi wake.
Hata wewe kwa kutambua hili fanya hivyo kwenye ujenzi wako hata kama si ghorofa ili nyumba yako isije kuwa ni chanzo cha mabalaa na mitihani ya dunia

mshana jnr mimi nikiwa mbali na kwangu mambo yangu safi lakini kosa niende kwangu kisha niende kwenye mihangaiko yangu ni mabalaa kwenda mbele kama siyo ugomvi basi burst au biashara kugoma na mawasiliano yanakuwa mabaya nifanyeje?
 
mshana jnr mimi nikiwa mbali na kwangu mambo yangu safi lakini kosa niende kwangu kisha niende kwenye mihangaiko yangu ni mabalaa kwenda mbele kama siyo ugomvi basi burst au biashara kugoma na mawasiliano yanakuwa mabaya nifanyeje?

Ninavyodhani: Hapo kwako pamefanyiwa kafara la mikosi, ramli chonganishi nuksi na banyanyi naomba wasiliana na MziziMkavu
 
Last edited by a moderator:
Sasa ndugu yangu Brown73 unataka uchawi wa ulaya ufanane kila kitu na wa huku kwetu? Hii ni very wrong judgement... Kukaa ulaya miaka 15 haimaanishi unajua kila kitu cha huko... Kuna wahindi wa hapo Posta magorofani hawaijui tabata segerea wala kigodoro na maisha yao yote wapo hapahapa
Naona una notion ya kwamba wote tunaoandika hapa hatujawahi kufika au kuishi huko ulaya
Sasa kwa taarifa yako bwana Brown73 huko ulaya kuna na vyuo kabisa vya ushirikina na si mazingaombwe kama unavyotaka kutuaminisha hapa

Sija wahi kusikia vyuo vya Aina hiyo labda unitumie majina Yao na nchi zao, kila kitu siku hizi ziko wazi uki google tu utapata kila kitu
 
Sasa ndugu yangu Brown73 unataka uchawi wa ulaya ufanane kila kitu na wa huku kwetu? Hii ni very wrong judgement... Kukaa ulaya miaka 15 haimaanishi unajua kila kitu cha huko... Kuna wahindi wa hapo Posta magorofani hawaijui tabata segerea wala kigodoro na maisha yao yote wapo hapahapa
Naona una notion ya kwamba wote tunaoandika hapa hatujawahi kufika au kuishi huko ulaya
Sasa kwa taarifa yako bwana Brown73 huko ulaya kuna na vyuo kabisa vya ushirikina na si mazingaombwe kama unavyotaka kutuaminisha hapa

Sasa mbona wenzetu hawaongelei au hawajihusishi kama tunavto fanya huko TZ. Maana hapo Tz kila siku utasikia suala la uchawi
 
Sasa ndugu yangu Brown73 unataka uchawi wa ulaya ufanane kila kitu na wa huku kwetu? Hii ni very wrong judgement... Kukaa ulaya miaka 15 haimaanishi unajua kila kitu cha huko... Kuna wahindi wa hapo Posta magorofani hawaijui tabata segerea wala kigodoro na maisha yao yote wapo hapahapa
Naona una notion ya kwamba wote tunaoandika hapa hatujawahi kufika au kuishi huko ulaya
Sasa kwa taarifa yako bwana Brown73 huko ulaya kuna na vyuo kabisa vya ushirikina na si mazingaombwe kama unavyotaka kutuaminisha hapa

Sija wahi kusikia vyuo vya Aina hiyo labda unitumie majina Yao na nchi zao, kila kitu siku hizi ziko wazi uki google tu utapata kila kitu

1451050273172.jpg hii ni mada kuhusiana na hivyo vyuo baadhi lakini
 
Back
Top Bottom