Majungu na kukwamishana Buboka Mjini vyamliza Mbunge Byabato. Apiga magoti na kutoa machozi mbele ya wanabukoba

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Mbunge wa Bukoba wa Mjini na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa anaongea na wakazi wa jimbo wakati akikabidhi mkataba wa ujenzi wa Standi Kuu ya Mabasi hilo amelalamikia majungu yanayoendelea Bukoba Mjini ambayo yanakwamisha maendeleo ya manispaa hiyo kwa miaka nenda rudi.

Baadhi ya miradi ambayo imekuwa ikikwamishwa na wanasiasa kwa maslahi binafsi ni pamoja na Stendi Kuu ya Mabasi Bukoba na Barabara ya Nyangoye ambayo imekuwa ikisababisha vifo na vilema kwa miaka nenda rudi.

Akiongea kwa machungu sana mpaka kupelekea kulia na kupiga magoti anadai kusaidia Bukoba kutekeleza hiyo miradi kwanini iwe NONGWA kwake? Kwanini aanze kupigwa majungu. Ameendelea kudai kuwa atahakikisha miradi hiyo inatekelezwa hata akinyimwa Ubunge 2025 lakini wananchi wakiona miradi hiyo watamkumbuka 'Ni Byabato Omsigazi Tukamwima Obubunge, chonka akabikola'(Ni kijana Byabato Tulimnyima Ubunge lakini aliifanya kazi)

Amesema aliomba ujenzi wa barabara ya Nyangoye, wataalamu wakaja wakafanya upembuzi yakinifu na kupendekezwa upanuzi wa barabara njia nne, na kaya 20 zitalipwa fidia ili kutekeleza mradi huo. Anashangaa kwanini anapigwa majungu!

Amesema kama ni Ubunge 2025 wauchukue lakini wanabukoba wasikwamishane bila Sababu. Ili kuonesha msisitizo wa anachokisema, Naibu Waziri huyo aliamua kupiga magoti na kulia, kabla ya kunyanyuliwa na wananchi.

Amezidi kusema wanabukoba tulimpa ubunge miaka mitano basi tumwamini tuache afanye kazi, hawezi kuacha kujenga Stendi, Barabara na Soko kisa atakosa Ubunge 2025. Anasema bora atekeleze hiyo miradi ili akose ubunge 2025 lakini atakumbukwa na wanabukoba. Kama shida ni ujenzi wa Stendi nzuri Bukoba Mjini.

 
Mkuu wa mkoa chalamila aliwahi kulalamika mkoa wa Kagera na MAJUNGU huu ndiyo mkoa unaongoza Kwa unafiki kutokana na WENYEJI WA MKOA HUU WA KAGERA..... Omba MUNGU jirani yako asiwe MHAYA hawa jamaa ni za HAMAS
Bukoba kuna majungu sana miaka na miaka. Sina hakika kama Byabato atarudi 2025. Cha msingi akomae atukamilishie hiyo miradi
 
Mbunge wa Bukoba wa Mjini na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa anaongea na wakazi wa jimbo wakati akikabidhi mkataba wa ujenzi wa Standi Kuu ya Mabasi hilo amelalamikia majungu yanayoendelea Bukoba Mjini ambayo yanakwamisha maendeleo ya manispaa hiyo kwa miaka nenda rudi.

Baadhi ya miradi ambayo imekuwa ikikwamishwa na wanasiasa kwa maslahi binafsi ni pamoja na Stendi Kuu ya Mabasi Bukoba na Barabara ya Nyangoye ambayo imekuwa ikisababisha vifo na vilema kwa miaka nenda rudi.

Akiongea kwa machungu sana mpaka kupelekea kulia na kupiga magoti anadai kusaidia Bukoba kutekeleza hiyo miradi kwanini iwe NONGWA kwake? Kwanini aanze kupigwa majungu. Ameendelea kudai kuwa atahakikisha miradi hiyo inatekelezwa hata akinyimwa Ubunge 2025 lakini wananchi wakiona miradi hiyo watamkumbuka 'Ni Byabato Omsigazi Tukamwima Obubunge, chonka akabikola'(Ni kijana Byabato Tulimnyima Ubunge lakini aliifanya kazi)

Amesema aliomba ujenzi wa barabara ya Nyangoye, wataalamu wakaja wakafanya upembuzi yakinifu na kupendekezwa upanuzi wa barabara njia nne, na kaya 20 zitalipwa fidia ili kutekeleza mradi huo. Anashangaa kwanini anapigwa majungu!

Amesema kama ni Ubunge 2025 wauchukue lakini wanabukoba wasikwamishane bila Sababu. Ili kuonesha msisitizo wa anachokisema, Naibu Waziri huyo aliamua kupiga magoti na kulia, kabla ya kunyanyuliwa na wananchi.

Amezidi kusema wanabukoba tulimpa ubunge miaka mitano basi tumwamini tuache afanye kazi, hawezi kuacha kujenga Stendi, Barabara na Soko kisa atakosa Ubunge 2025. Anasema bora atekeleze hiyo miradi ili akose ubunge 2025 lakini atakumbukwa na wanabukoba. Kama shida ni ujenzi wa Stendi nzuri Bukoba Mjini.

View attachment 2784184
Anazunguka tu, aseme Wazi tu kwamba ni CCM wenzake.
 
Lakini huyo huyo ndo alishiriki kusaini mkataba wa kyakailabwa uliopingwa na mkuu wa mkoa baada ya kukuta upigaji
Naona bajeti ya mwaka huu....Barabara ya njia nne bukoba kutoka Rwamishenye hadi bandarini...vip walishaanza ujenzi?
Vip watu wamekubali kuvunja nyumba zao?

Kulinganisha na wabunge waliopita bora huyu...at least anaonekana hata hapo Bukoba...


Barabara ya njia nne ikijengwa aiss itaubadilisha completely mji wa Bukoba
 
Mbona hayo ni kawaida kote dunia...
Kumbuka hata wakati wakazi wa kimara wakivunjiwa nyumba zao ule mtiti haukuwa wa nchi hii...

Isingekuwa ukali wa magufuli hata barabara ya kimara isingejengwa..

Ndo yanayotokea bukoba...barabara ya uganda inapaswa kuwa njia nne lakini bado watu wanalamika walio ndani ya hifadhi ya barabara
 
Back
Top Bottom