Majibu ya Prof Mwandosya kwa Zitto

Majibu ya Prof Mwandosya kwa Zitto

ameendesha wizara ya maji kwa ufanisi wa kutukuka alivoumwa ndio ikapewa hawa wababaishaji. jamaa wanasema ni mpiga kazi usiku na mchana ,he is capable
Imebaki kizazi kimoja tu ili Tanzania tubaki wafu
 
Prof blah blah nyingi kama kawaida yao!Mtoto wake Sekela alisomeshwa na MSI na gazeti la Rai mwaka 2001 lilisema na Prof Mwandosya hakukanusha wala kulipeleka Mahakamani gazeti hilo
 
Mkuu Mkandara, hawa jamaa ni wahuni tu. Walikuwa na sababu gani kuuza benki (NBC), Kiwanda cha sigara, Kampuni ya pombe TBL...mashirika yaliyokuwa yakijiendesha kwa tija! Hapa prof. anaimba wimbo wa kipumbavu na kushangiliwa la watu wanaomchukia Zito.
Ni wa chache saana wataona na kukumbuka hili maana hakika imebaki kizazi kimoja tanzania soon watatembea wafu
 
Kumbe ndio maana proffessor anaheshimika na kina membe .Hii kitu imenifanya nimkubali katika wagombea wote wa CCM ni kichwa ,anakupa vielelezo huku anakutukana bila neno la tusi aisee jamaa ni big brain, mnaosema mnaakili kuliko watu wengine jifunzeni kwa prof na huwa haongei sana short and clear

Huyo ndo profesa high Quality Tanzania kaka, Mathew Luhanga, Lipumba , Muhongo , na Sarungi ila zingine za kupewa tu hakunA lolote.

Yani huyo mzee muogopeni angefundisha CoET vichwa vingi vingetokea Tz sema ndo ivyo siasa inalipa
 
We mwandosya si ndiye uliyemuambia zitto asijibu tuhuma za kipuuzi kwenye escrow. Naona dogo kakugeuka sasa, tamaa za urais zilikuongoza kutoa kauli ya ajabu sana,.
 

Nianze na hili la ubinafsishaji kwa ujumla wake. Inawezekana ulikuwa badi shule, pamoja na nia njema ya kuanzisha mashirika ya umma, hatimaye yalikuja kuwa mzigo mkubwa kwa hazina yetu, maana yake kwa wananchi. Asilimia kubwa yalitegemea ruzuku ya serikali na baadhi yalikuwa mufilisi. Teknolojia ilikuwa imebadilika sana na ili kuyafungua ingeigharimu serikali na umma wa Tanzania kiasi kikubwa sana. Uchumi wa nchi wakati ule usingeweza kubeba mzigo huo. Ndipo Chama, wakati ule kiliporidhia Serikali ibakie na shughuli zake za msingi za Utawala, Ulinzi na Usalama, na Usimamizi wa ujumla wa uchumi.


MAELEZO HAYO HAPO JUU KWA MWENYE akilli timamu yanatosha kwamba Mwandosya ni kiongozi mwepesi kushindwa, kwa kauli hiyo ya kuogopa ushindani ni ishara kwamba hata viwanda karibu vyote vimekufa kwa sababu ya uoga wa wanaCCM. Pia kwa maelezo hayo ya Mwandosya kuogopa risk, watanzania wasitegemee kufufuliwa kwa viwanda Mwandosya akiwa kocha wa CCM.

Basi Watanzania, tuelewe kwamba mafanikio ya China na kuwa taifa kubwa kiuchumi duniani imetokana na uwezo wa Deng Xiaoping ambaye alilibadili taifa hilo kwa kuboresha mashirika ya umma, kufungua viwanda vipya na kwenda sambamba na mapinduzi ya teknolojia duniani. SASA tuna Mwandosya na wanaCCM wenzake wanaona teknolojia ni adui wa kumkimbia na kutelekeza mashirika ya serikali badala ya kuwa rafiki wa kumkimbilia.

Nimalizie tu, kwa uelewa mdogo na ushabiki wa wanaJF kwa majibu ya Mwandosya na kuyachukulia kijumla jumla bila kushirikisha ubongo, to find if there is any substance in his counterargument, then we are doomed as a nation and overal we lack human potential for the future of this nation.

Kama nimekupata vizuri unamaana kuwa njia pekee ya maendeleo ni serikali kufanya biashara, maana serikali ikifufua viwanda, ikaviendesha maana yake imeingia kushindana na sekta binafsi wakati ikiwa pia msimamizi,conflict of interest.Namna ya kufanikisha unalosema ni kujenga uchumi wa kijamaa, kurudisha uhodhi wa serikali kwenye shughuli za kiuchumi.Serikali iendeshe viwanda, iendeshe mashirika kwa pesa zake, hapa MWandosya anasema ugumu wa hilo

"pamoja na nia njema ya kuanzisha mashirika ya umma, hatimaye yalikuja kuwa mzigo mkubwa kwa hazina yetu, maana yake kwa wananchi. Asilimia kubwa yalitegemea ruzuku ya serikali na baadhi yalikuwa mufilisi. Teknolojia ilikuwa imebadilika sana na ili kuyafungua ingeigharimu serikali na umma wa Tanzania kiasi kikubwa sana. Uchumi wa nchi wakati ule usingeweza kubeba mzigo huo. Ndipo Chama, wakati ule kiliporidhia Serikali ibakie na shughuli zake za msingi za Utawala, Ulinzi na Usalama, na Usimamizi wa ujumla wa uchumi"

Huu ni uamuzi wa serikali kujiondoa kwenye shughuli za kibiashara na kubaki kuwa msimamizi, huu ni uamuzi wa kuingia rasmi kwenye uchumi wa kibepari.Kupanga ni kuchagua, kuna nchi nyingi za kibepari pia ambazo zina mwelekeo mzuri wa maendeleo, hivyo lazima serikali iwe na mentality za kijamaa ili kuendelea, katika ubepari serikali hazifanyi biashara, hazina kampuni wala kiwanda,hivyo vyote vinafanywa na sekta binafsi.

Na ninakubaliana na serikali kuwa huu uamuzi sahihi kufanyika, issue ni utekelezaji wake kwenye baadhi ya maeneo hasa kwenye upande wa baadhi ya viongozi wasio waaminifu kupiga deal zao wakati huo.
 
Ni wa chache saana wataona na kukumbuka hili maana hakika imebaki kizazi kimoja tanzania soon watatembea wafu

Ndio maana Prof ametoa jibu la jumla kwamba huenda mlikuwa shuleni , anamaanisha mlikuwa hamjitambui kwa kuwa hata ungalikua shule ungalikua unajitambua ungekumbuka kuwa Kiwanda cha bia kilikumbwa na tatizo sugu la kushindwa kuzalisha kadiri ya mahitaji ya soko. Mmi mwenyewe nimewahi kupewa jukumu la kwenda kufanya mipango ili tupata kreti nane kwa ajili ya sherehe ndogo tu nyumbani ilikuwa" issue" sikufanikiwa, na mipango hapo inamaanisha kujuana.sababu ya hiyo hali ni maswala ya kuyumba kwa uchumi wa kijamaa -unakosa mitaji, unakosa ingridients, unafeli kwenye ushindani. Kumbuka bia za kenya ziliingizwa kwa njia za panya kutokea Kitobo.


Kampuni ya sigara nayo iliyumba sana ,ikawa haiwezi kutengeneza baadhi ya products kwaiyo mvutaji wa SM angeweza kulazimika kuvuta sport ama zote zinakosekana wanavuta sonyo. Kwaiyo kuna kuyaishi haya mambo na kuna kujifunza mashuleni, kama mtu atakwenda kuwakumbusha wanachi hali ile halafu ukamwambia kuna chama kinataka kuirudisha utakuwa umejimaliza mwenyewe. Kwa ufupi mwandosya anawaona watu wana utoto ila kistaarabu katumia neno mlikua shule.kasome political and economic liberalization na ujikite kwenye privatization in tz.
 
Naona zitto ameamua rasmi kufanya kazi ya 4umovement.......alianza n Membe sasa kafuatia Prof Mwandosya........soon atatuambia Makongoro aliiba microphone EAC...unafiki wa hali ya juu......Zitto kuwa team Lowasa ni aibu
 
Imebaki kizazi kimoja tu ili Tanzania tubaki wafu

Bavicha bana wakati mwingine mnachekesha mko tayari kuwatetea MAFISADI ILI TU ZITTO AONEKANE NI WA HOVYO HOVYO au alichokiandika hakina mashiko
 
zito anaakili za vijiweni wakati mashirika yanaingiza hasara yeye alikuwa bado ananyonya kwahiyo kumfafanulia mtoto kama huyo ni kuumiza kichwa
 
Nacheka sana leo Chadema wote wameamia CCM halafu mnajindanganya UKAWA watachukua nchi.

teh teh teh Tanzania hamna upinzani.

Mkuu nadhani unawawaza sana Chadema unnecessarily hadi mnatoa watu nje ya mada.
 
Huyo ndo profesa high Quality Tanzania kaka, Mathew Luhanga, Lipumba , Muhongo , na Sarungi ila zingine za kupewa tu hakunA lolote.

Yani huyo mzee muogopeni angefundisha CoET vichwa vingi vingetokea Tz sema ndo ivyo siasa inalipa
Hivi, ni kitu kipi cha ajabu amefanya CoET? Cha kuweza kujivunia, zaidi ya kubatizwa jina handsome boy, kwa kupenda utunda
 
Back
Top Bottom