Profesa katiririka vizuri.Ameonyesha ukongwe wa hali ya juu katika siasa.
Kwa watu wavivu wa kufikiri wanaweza kuona kama Prof. Mwandosya hapa katiririka lakini ukweli ni kwamba alichoongea ni utumbo mtupu! Mwandosya hajazunngumza hata chembe moja ya ukweli hapa.
Hivi Professor huyu wa Kinyachusa pamoja na majigambo yake hayo ya kubinafisha mashirika ya Umma anaweza kutuonyesha ni shirika gani linalofanya vizuri baada ya Ubinafsishaji? Liko wapi angalao moja tu atuambie.
Mimi ningependa kuanza na hili la TTCL. Nakumbuka vizuri sana nikiwa na akili timamu kuwa kabla ya Detecon/MSI hawajauziwa/kupewa TTCL kwa bei ya kutupa TTCL chini ya marehemu Adolar Mapunda(RIP) ilikuwa na kiasi cha Tshs. 90 Billion. Mkurugenzi Mkuu Adolar alikwenda mpaka Bungeni akaiambia Serikali kuwa TTCL inauwezo wa kuanzisha Kampuni ya Simu za Mkononi yenyewe na tayari ilishapewa leseni na BRELA kuanzisha Kampuni ya CELNET. Lakini Serikali kupitia Mwandosya wakamwabia Mapunda kuwa TTCL hawataruhusiwa kuanzisha huduma ya Mobile badala yake wamsubiri Mwekezaji DETECON/MSI.
Kila Mtanzania anajua jinsi mchakato wa uuzaji/Ubinasishaji wa TTCL ulivyokwenda. Mwekezaji huyu tapeli kwa kushirikiana na kina Mwandosya walikubaliana walipe USD 120m lakini badala yake wakalipa USD 60m kwa ahadi kwamba ile nusu iliyobaki 60m USD ingelipwa baada ya kuanza kazi. Matokeo yake ni kwamba walipoingia tu TTCL walichezea mahesabu ya TTCL na hela zote zile 90B Tshs wakazikomba na kuzipeleka kwenye Kampuni yao ya Celtel. Iumbukwe kwamba leseni ileile ya CELNET toka BRELA ndiyo waliyoitumia hawa jamaa kwa kufanya nabadiliko kidogo kwenye jina kutoka Celnet kwenda CELTEL.
Muda wa kulipa ile 60m USD iliyobaki ulipofika hawa wahuni wakadai kuwa baada ya kupitia mahesabu upya wamegundua kuwa TTCL haina fedha kabisa tofauti na walivyofikiria mwanzo na kwa hiyo wako tayari kulipa 4.5m USD tu badala ya 60m USD!
Ikumbukwe kuwa kabla ya hawa wakezaji uchwara hawajapewa TTCL kulifanyika upembuzi yakinifu wa kimiundo mbinu waliyokuwa nayo TTCL na kupitia mahesabu ya TTCL na ndiyo maana wakakubaliana na Serikali ya CCM chini ya Mkapa na Mwandosya kuwa watainunua TTCL kwa 120m USD na si vinginevo!
Kwa kutumia ulaghai na kucheza na mahesabu ndipo wakawaweka sawa kina Mwandosya kwa kuwapa RUSHWA ya fedha pamoja na kuwasomeshea watoto wao akiwemo huyo Binti wa Mwandosya aliyepelekwa Afrika Kusini kwa gharama za CELTEL. Watu wanajua chuo alichopelekwa na mpaka chumba alichokuwa nakaa huyo Binti wa Mwandosya huko SA.
Kwa hili la TTCL Prof. amedanganya kwa 100%.
Nitaendelea............now loading.....