Majambazi yapora Tanzanite ya billion 10

Majambazi yapora Tanzanite ya billion 10

Hao ndio wanaume! Sio mnakuja kutuibia vyupi vyetu uswazi bado mnatuua. Una silaha unamwibia maskini mwenzio na unamuua. Waibieni mafisadi kama hivyo. Huo mzigo unamkono wa mafisadi kibao,Safi sana majita.

Duh aisee are you sane?
 
Usijekuta kuna inside job maana walijuaje kuna mzigo na thamani. je kulikuwa na police escort

Hata Mimi naungana na Wewe kwasababu zifuatazo;
1. Hakuna mzigo wa thamani kiasi hiko usafirishwe unclassified..... Info zimekuwa leaked kimakusudi kabisa.
2. Na kubwa ni kwambazi huwa hawabakishi kama walivyofanya hao coz wamechukua 15kg kati ya kg Zaidi ya 30 zilizokuwa zinasafirishwa.
 
wachukue tu, hiyo ni safari moja tu kati ya maelfu ya tanzanite kuporwa. Mi sifikilii ujambazi Huo. Lakini unaona kwa nini tanzania ni kati ya inchi kumi bora zenye akili finyu. iweje tuna madini ya thamani ivo , yaani kilo 15 ni bilioni kumi halafu nchi masikini, kwani hivi ina laana gani jamani. wageni waje na kuwa matajiri na nchi kwenda chini, looh EE mungu wangu. ni aibu kuwa kiongozi katika nchi yenye mali ikiwa masikini. Kuna fahari gani kuendesha Ferrari kwenye vumbi, kupitisha range kwenye squeter,au kujifariji kuwa wewe ni tajiri kati ya fukara, hili haliwezekani tutaomba mungu tu. wafisadi kwa neno la bwana hawatakiwi kuishi zaidi ya nusu ya life spam yao, hilo ni andiko sio mimi, yaani kati ya miaka 35-40.sasa ni kuitekeleza hukumu kwa kutuma neno la mungu hilo ili malaika walitekeleze.

Kg 15=Ten 10 halafu ni Masikini........!
 
Hiyo issue ina wa2 wengi kuanzia ndani istoshe ucku ndio huwa wanatorosha madini,inakuja jet yao inatua kia wanaleta mzigo kimyakimya then wa2 wa tra wanahongwa ndege inaondoka.

Huo mzigo ni zaidi ya 15kg mana production yao huwa karibia 200kg so wakisort mawe masafi watapata c chini ya 50kg

kama si rushwa hii nchi tungekuwa mbali sana
 
Gram ya tanzanite ikiwa y top colour ni 1.5m so hpo wazungu wamedanganya mana walikua wanasafirisha kimagendo wasilipe kodi wajuba wakasoma dili,huwa wanasafirisha na escort na gari yenye bullet proof body
nafanya biashara ya tanzanite ulichoandika hapo sikweli kwanza tanzanite inauzwa kwa caret not gram na caret moja ya tanzanite top colour yani triple A nice usd 300 name gram 1 sawa na caret 5 so fanya hesabu utapata jibu
 
mimi nauza rough stone kwa wanao uza ambazo wameshafanya cutting ndio wanatumia caret c gram,wachimbaji wengi wanauza rough stones
 
OK kama unazungumzia rough nimekupata

Hata brokers wanadili na rough sana ila maofisini ndio wananunua then wanachonga kutegemeana na order,huwezi export roughstone lazima iwe imechongwa
 
embu tafuta hzo tetesi alafu utujuze

Wameiba mifuko mitatu ambayo ni zaida ya 75kg hpo wakisort wanaweza pata kma kg5 mpka 7kg,mana wameiba mifuko ambayo wanaweka production ina 25kg kila mfuko so hpo huwa ni mawe na mchana.
Ukichambua unaweza pata 15% mawe then 60% ikawa mchanga na mawe mabovu ndio miamba ya tanzanite ilivyo
 
Tanzanite.gif


Madini ya tanzanite ya Kampuni ya TanzaniteOne ya Mirerani, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara yenye uzito wa kilo 40 na thamani ya zaidi ya Sh bilioni 10 yameporwa na watu wanaosadikiwa ni majambazi.



Taarifa kutoka katika kampuni hiyo zilisema, uporaji huo ulitokea jana ndani ya kampuni hiyo saa tisa usiku.


Kwa mujibu Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Dauglas Swartz, tayari wafanyakazi watano wa kampuni hiyo wanashikiliwa na polisi katika kituo kidogo cha Mirerani kuhusu wizi huo.


Alisema jana kuwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Manyara (RCO), Benedict Msuya alifika eneo la tukio kwa uchunguzi wa wizi huo.
“Ni kweli tumeibiwa madini ya tanzanite na baadhi ya wafanyakazi wanaodaiwa kuhusika katika tukio hilo wameshakamatwa na upelelezi bado unaendelea, niache kwa sasa,’’
Taarifa zilizopatikana ndani ya kampuni hiyo zinadai kwamba madini hayo yaliyokuwa yamefungwa katika mifuko miwili tofauti yenye uzito wa kilo 15 na kilo 25 na yameporwa mita chache kutoka mgodini eneo la kuingia chumba cha ulinzi. -- via HabariLeo




Hapa mimi napata wasiwasi inamaana kama Kilo 40 tu ni Bilioni 10/= Je Tanzania inazalisha Kilo ngapi za Tanzanite kwa mwaka? Maana kama Kilo 40= 10Bilioni sasa Tanzania ingetakiwa hata South Africa tumeshawapiga Bao Kiuchumi Kupitia tu Madini Haya.



 
Hata brokers wanadili na rough sana ila maofisini ndio wananunua then wanachonga kutegemeana na order,huwezi export roughstone lazima iwe imechongwa
mimi huwa nauza finish products sifanyi rough
 
Hata brokers wanadili na rough sana ila maofisini ndio wananunua then wanachonga kutegemeana na order,huwezi export roughstone lazima iwe imechongwa
najua lazima ununue rough ufanye cutting uwezi kuuza nje rough kama mawe mengi mfano ruby ,suphire
 
Back
Top Bottom