Majambazi wamerudi upya, sasa hivi wananyonga hawaulizi

mtoto wa mchungaji

JF-Expert Member
Oct 24, 2020
279
480
Matukio ambayo tulishayasahau kitambo sasa yameamza kuibuka upya tena kivingine, kwani zamani majambazi walikuwa hata wanauliza au hata kutishia silaha au kupiga hewani risasi, lakini safari hii wananyonga yaani wamechoka, na kupiga risasi hewani wanaona kama hasara ni mwilini tu.

Kwa mujibu wa taarifa kupitia vyombo vya habari tayari majambazi wamenyonga mlinzi wa benki. Na mpaka sasa tayari kumeanza kuripotiwa matukio mbali mbali ya ujambazi na kupoteza maisha ya watu hata arobaini bado haijaisha.

Aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Dr. Magufuli yeye aliwahi kuwaita wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama na kuwaambia kuwa ni bora niendelee kusikia majambazi wameiba au wameua lakini sitaki kusikia jambazi kafikishwa Polisi au Mahakamani naomba muwanyang'anye silaha, mwisho wa kunukuu. (na hapo hata mimi sichangii zaidi).
 
Inabidi tumlaumu Magufuli yeye kama kiongozi Bora alitakiwa kuandaa system ambayo itafanya kazi kwa weledi bila hata uwepo wake maana siku za mwanadamu duniani ni chache zinahesabika.

Watu wa maana siku zote wanaandaa mfumo ambao utajiendesha bila hata uwepo wake sio mfumo tegemezi ambao hauna ufanisi bila uwepo wake.

Alaaniwe yeyote yule amtegemeae mwanadamu.
 
Ndo ujue kwamba magufuli alikuwa ni rahisi wa hovyo, aliendesha nchi ktk namna ya watu kumuogopa yeye pasipo kujenga mifumo imara.

Angejenga mifumo imara suala la majambazi kutoweka lingekuwa la jumla jumla.
Jengeni mfumo nyie sasa, yeye aliweza tatua tatizo tukalisahau, hayo ya mfumo ni ya kwenu na porojo kibao, kazi sifuri.
 
Inabidi tumlaumu magufuli yeye kama kiongozi Bora alitakiwa kuandaa system ambayo itafanya kazi kwa weledi bila hata uwepo wake maana siku za mwanadamu duniani ni chache zinahesabika.

Watu wa maana siku zote wanaandaa mfumo ambao utajiendesha bila hata uwepo wake sio mfumo tegemezi ambao hauna ufanisi bila uwepo wake.

Alaaniwe yeyote yule amtegemeae mwanadamu.
Appreciate bhac hata kwa hili jmn.
 
Ndo ujue kwamba magufuli alikuwa ni rahisi wa hovyo, aliendesha nchi ktk namna ya watu kumuogopa yeye pasipo kujenga mifumo imara.

Angejenga mifumo imara suala la majambazi kutoweka lingekuwa la jumla jumla.
Nyumbu watu wa hovyo sana.
 
Inabidi tumlaumu magufuli yeye kama kiongozi Bora alitakiwa kuandaa system ambayo itafanya kazi kwa weledi bila hata uwepo wake maana siku za mwanadamu duniani ni chache zinahesabika.

Watu wa maana siku zote wanaandaa mfumo ambao utajiendesha bila hata uwepo wake sio mfumo tegemezi ambao hauna ufanisi bila uwepo wake.

Alaaniwe yeyote yule amtegemeae mwanadamu.
System hata iwe bora vipi, kama hakuna utashi wa ku-inforce hiyo system hata iwekwe na nani haiana maana. enforcers wetu hawapo. PoliCCM
 
Ati wana uchungu jambazi mwenzao kawatoka ghafla.
Ukweli ni kwamba ulikuwa ukituhumuwa jambazi tuunapigwa risasi kichwani/unauawa, kwahiyo jambazi alikuwa hafikishwi polisi au mahakamani.

Je kama umetuhumiwa kwa chuki binafsi utajitetea saa ngapi wakati hufikishwi polisi au mahakamani!

Wengi waliuawa bila hatia kwa kisingizio cha ujambazi.
 
Hivi hizi maneno za mfumo aka system ni zipi bandugu munieleweshe. Yaan twende Kwa mifano. Kua kuteketeza ujambazi mfumo gani uwepo. Maana naona watu tuko general Sana.
Mifumo ipo tangia hapo ila msimamizi wa mfumo aliwa legelege nao mfumo utalegea na akiwa imara basi mfumo utakuwa imara.
 
Ndo ujue kwamba ... alikuwa ni rahisi wa ..., aliendesha nchi ktk namna ya watu kumuogopa yeye pasipo kujenga mifumo imara.

Angejenga mifumo imara suala la majambazi kutoweka lingekuwa la jumla jumla.
Nimerudi
===
Asante sana kwa bandiko lako murua.

Nina maswali kadhaa kutokana na bandiko lako hili.

1. Mfumo imara ni nini hasa? Yaani ni kitugani, jambo gani, hali gani na kiko, liko, ikoje?
2. Naomba unipe na kunifafanulia kinagaubaga tabia/desturi/tamaduni za "mfumo imara". Naomba pia katika kufafanua hili utumie mifano halisi ili kunirahisishia uelewa wa hii " mfumo imara"
===
Natanguliza shukrani kwa majibu ya maswali yangu.

Nakutakia asubuhi njema.

Nimebaki nikiwa TUJITEGEMEE.
 
Back
Top Bottom