Maisha yanaenda kasi, kweli timu ya Simba ni yakuzomewa kutoka Mtwara hadi Dar?

kukumsela

JF-Expert Member
Oct 13, 2018
721
907
Ameandika Ahmed Ally

===
Mara kadhaa utasikia shabiki anasema sisi tunaumia kuliko Wacheza ji au Viongozi.

Ndugu zangu ilimradi sote tuna damu ya Simba basi wote tunapitia maumivu, kinachotokea ni tofauti ya mtu na mtu kuhimili maumivu.

Ndo maana wengine wanalia, wengine wanazimia, Wengine wanashindwa kula, Wengine wanakasirika yote ni maumivu.

Leo tumezomewa kutoka Mtwara hadi Dar Es Salaaam hali ambayo nawaumiza zaidi wachezaji, hakuna mchezaji anaetaka kufungwa makusudi ili azomewe kuzomewa ni kitendo cha aibu sana.

Katika nyakati hizi ni vema kila mmoja akaheshimu maumivu ya mwenzie kwani hakuna anae jua mwenzie anaumia kiasi gani.

Tufanye yote lakini tuwaache viongozi wamalize kuugulia baada ya hapo wa je watutengenezee timu madhubuti kwa ajili ya msimu ujao.

Hakuna mtu anaekubali kuharibikiwa katika kazi yake, viongozi wetu wanapambana usiku na mchana kuhakikisha sisi mashabiki tunapata furaha.

Tuwaunge mkono kwenye kipindi hiki kigumu kwao kwani na wao wanaumia kama sisi na hawana mahala pa kupeleka lawama zao, lakini pia pamoja na kuumia kwao wanatakiwa warudi kazini kututengenezea Simba imara.


 
Ujinga Ujinga tu.

Zinafeli kuchukua makombe timu kubwa duniani kama Manchester, Liverpool na Chelsea halafu Simba iwe kitu cha ajabu.

KILA LA HERI SIMBA SC MSIMU UJAO.
 
Mashabiki wa Simba kuweni waungwana, hii si haki hata kidogo. Wachezaji wamewafanyia makubwa sana lakini shukrani mnayowapa si sawa!

 
Wazomewe tu timu kubwa haina taji lolote mm ndio maana kuwa na ushabiki sitaki maana washabiki wanaumizwa roho kila siku waacheni wawazomee wapunguze machungu yao
 
... Akiambatanisha picha za viongozi wa Simba, Mangungu na Try again, Ahmed Ally amesema LEO WAMEZOMEWA !

"Leo tumezomewa kutoka Mtwara hadi Dar, hali ambayo inawaumiza zaidi Wachezaji, hakuna mchezaji anayetaka kufungwa makusudi ili azOmewe. Kuzomewa ni kitendo cha aibu sana"

"Katika nyakati hizi ni vema kila mmoja akaheshimu maumivu ya mwenzie kwani hakuna anayejua mwenzie anaumia kiasi gani"

"Tufane yote lakini tuwaache viongozi wamalize kuugulia baada ya hapo waje watutengenezee timu madhubuti kwa ajili ya msimu ujao"

"Hakuna anayekubali kuharibikiwa katika kazi yake, viongozi wetu wanapambana usiku na mchana kuhakikisha sisi mashabiki tunapata furaha"

"Tuwaunge mkono kwenye kipindi hiki kigumu kwao kwani na wao wanaumia kama sisi na hawana mahala pa kupeleka lawama zao"

Ahmed Ally
 
Semaji la robo fainali
1683626466059.jpg
 
... Akiambatanisha picha za viongozi wa Simba, Mangungu na Try again, Ahmed Ally amesema LEO WAMEZOMEWA !

"Leo tumezomewa kutoka Mtwara hadi Dar, hali ambayo inawaumiza zaidi Wachezaji, hakuna mchezaji anayetaka kufungwa makusudi ili azOmewe. Kuzomewa ni kitendo cha aibu sana"

"Katika nyakati hizi ni vema kila mmoja akaheshimu maumivu ya mwenzie kwani hakuna anayejua mwenzie anaumia kiasi gani"

"Tufane yote lakini tuwaache viongozi wamalize kuugulia baada ya hapo waje watutengenezee timu madhubuti kwa ajili ya msimu ujao"

"Hakuna anayekubali kuharibikiwa katika kazi yake, viongozi wetu wanapambana usiku na mchana kuhakikisha sisi mashabiki tunapata furaha"

"Tuwaunge mkono kwenye kipindi hiki kigumu kwao kwani na wao wanaumia kama sisi na hawana mahala pa kupeleka lawama zao"

Ahmed Ally
Itakuwa malengo yao ya mwaka huu hawakuwashirikisha na mashabiki.
Kwa sababu malengo ilikuwa ni ROBO na kumfunga UTO na yote yamefikiwa.
 
Hakuna jipya. Hao viongozi watamleta Manzoki au Adebayor kwenye mkutano wa wanachama halafu watashangiliwa.
  • Kocha wa Wydad katimuliwa kwa sababu tu kaingia nusu fainali kwa taabu sana
  • Kiongozi wa Raja kajiuzulu kwa sababu wameshindwa kuingia nusu fainali.

Kwa Simba kufanya vibaya msimu wa pili mfululizo bila kombe lolote nani kajiuzulu/kawajibika mpaka sasa?
 
Back
Top Bottom