Maisha ya uzeeni bila hela ni tabu sana

Maisha ya uzeeni bila hela ni tabu sana

Nina miaka 77 nakwenda 78 Desemba hii na ngoja nikwambie kitu kijana.

Pesa ndiyo ni muhimu sana huku uzeeni lakini cha muhimu zaidi ni afya yako. Ukizubaa ukajiachia ukakamata presha, kisukari, matatizo ya moyo na figo; na mengineyo; kila kitu kinakuwa kimeparaganyika na hizo hela hutazifaidi. Kwanza hata mtambo wako wa nyuklia utakuwa haufanyi kazi tena imagine!

Kijana Linda sana afya yako. Kama ni lazima unywe pombe basi kunywa kwa wastani (tunaambiwa na wataalamu kuwa usizidishe bia mbili kwa siku). Acha sigara maana hazina faida yo yote kwako. Punguza sukari na matumizi ya caffeine (kunywa kahawa na energy drinks kwa kiasi kidogo sana); na angalia sana mlo wako. Fanya vimazoezi karibu kila siku na kamwe usikubali ukanenepeana kama kifutu.

Kama miaka ingekuwa inarudishwa nyuma kwa hakika ningejitahidi sana kulinda afya yangu maana kuna mambo niliyafanya huko ujanani (hasa pombe, nyama choma sana, ulaji wa hovyo kwa ujumla ..) na mpaka leo nalipia gharama zake japo sina presha, kisukari wala matatizo mengine ya kawaida kwa wazee.

Hitimisho: Kijana tafuta pesa. Kula bata lakini kwa tahadhari na priority namba wani kwako iwe ni kulinda sana afya yako maana mambo unayoufanyia mwili wako kwa sasa madhara yake utaanza kuyaona miaka 15+ huko mbele ya safari; na inaweza kuwa ni too late ukajikuta umeshaharibu kila kitu.

➡️➡️➡️ NB: Hata hizi shida zenu za nguvu za kiume vijana wadogo miaka 35 mnafakamia mivayagra kuna mambo ukiyazingatia, hata huku uzeeni utakuwa sawa tu na wala hutahitaji haya madawa yenu. Wewe hakikisha tu cardiovascular system yako iko sawa na mengine yote ni marahisi. Ongeeni na wazee mjifunze 😁😁😁🏃🏿‍♂️🏃🏿‍♂️🏃🏿‍♂️🖐
Shikamoo babu naomba hela nikanunue ice cream
 
Binadamu huwa hazeeki

Binadamu huendeshwa na AKILI. Na AKILI haizeeki .

Mimi mambo ambayo huwa siyazingatii ni umri.


Kuitwa babu
Kuitwa kijana
Kuitwa mzee

Sio swala Ila swala ni kuwa smart kichwani na kuwa na "sense of who you are" that all.
 
Unafikia umri umemtamani mtoto wa kike mrembo 18+ kumwita tu anakusalimia shkamoo babu au shkamoo baba.
Ujue bora akusalimie tu shkamoo
Hapo ujue bado upo
Ila akimalizia tu .
Una hali mbaya. Sitaki uzee aisee ngoja nitafute hela
"ngoja nitafute hela" hili ndo neno.. kila kitu kitakuja chenyewe hata ukiwa na mika buku.. niko na 58yrs ila girls 22 to 25 ndo natumia mkuu [emoji3][emoji3]
 
Unafikia umri umemtamani mtoto wa kike mrembo 18+ kumwita tu anakusalimia shkamoo babu au shkamoo baba.
Ujue bora akusalimie tu shkamoo
Hapo ujue bado upo
Ila akimalizia tu .
Una hali mbaya. Sitaki uzee aisee ngoja nitafute hela
Hauutaki uzee!

Nadhani una tatizo la kisaikolojia linalohitaji wataalamu kukusaidia.

Ujana unaweza kukudanganya na ukajisahau sana kumbe?

Lakini nikuhakikishie, miaka ishiri ama thelathini iloyoko mbele yako ya kuuanza uzee ni michache sana ni kama dakika thelathini kwenye mzunguko wa saa.

Kama Mungu hajakuua na kubaki hai na afya njema, kuuingia uzee ni kufumba na kufumbua tu.

Kama akili zako umezielekeza kwenye ukiruka njia wa kutongoza wasichana, kweli waweza ukateseka, lakini ni mateso ya kujitakia ya kusaikolojia kwa sababu wasichana warembo ni kama matoleo ya magazeti, ukiishalisoma asiyelisoma atatamani alisome na akishalikulisoma hatalihitaji aendelee nalo, hulitupa pembeni.

'Shikamoo zao' ni kelele za chura zisizoweza kuzuia tembo kunywa maji, nadhani umenielewa.

Nihitimishe kwa kusema usijivunie chochote ambacho binadamu unamiliki sasa hivi: ujana, afya, michongo ya pesa na mali na kupelekea kuwaona wasivyonavyo ni mafala, hapana ni mfumo.

Mshukuru tu Mungu wako kwa kukuwezesha uwe hivyo ulivyo leo, lakini mipango ya kesho yako pamoja na mabadiliko ya chochote kizuri unachokimiliki kuwa virse versi chaweza kukutokea wakati wowote ukae ukijua hilo.
 
Nina miaka 77 nakwenda 78 Desemba hii na ngoja nikwambie kitu kijana.

Pesa ndiyo ni muhimu sana huku uzeeni lakini cha muhimu zaidi ni afya yako. Ukizubaa ukajiachia mpaka ukajisababishia presha, kisukari, matatizo ya moyo na figo; na mengineyo; kila kitu kinakuwa kimeparaganyika na hizo hela hutazifaidi. Kwanza hata mtambo wako wa nyuklia utakuwa haufanyi kazi tena imagine. Hata kula yenyewe itakuwa shida tupu!

Kijana Linda sana afya yako. Kama ni lazima unywe pombe basi kunywa kwa wastani (tunaambiwa na wataalamu kuwa usizidishe bia mbili kwa siku). Acha sigara maana hazina faida yo yote kwako. Punguza sukari na matumizi ya caffeine (kunywa kahawa na energy drinks kwa kiasi kidogo sana); na angalia sana mlo wako. Fanya vimazoezi karibu kila siku na kamwe usikubali ukanenepeana kama kifutu.

Kama miaka ingekuwa inarudishwa nyuma kwa hakika ningejitahidi sana kulinda afya yangu maana kuna mambo niliyafanya huko ujanani (hasa pombe, nyama choma sana, ulaji wa hovyo kwa ujumla ..) na mpaka leo nalipia gharama zake japo sina presha, kisukari wala matatizo mengine ya kawaida kwa wazee.

Kwa hiyo kijana tafuta pesa. Kula bata lakini kwa tahadhari na priority namba wani kwako iwe ni kulinda sana afya yako maana mambo unayoufanyia mwili wako kwa sasa madhara yake utaanza kuyaona miaka 15+ huko mbele ya safari; na inaweza kuwa ni too late ukajikuta umeshaharibu kila kitu.

➡️➡️➡️ NB: Hata hizi shida zenu za nguvu za kiume vijana wadogo miaka 35 mnafakamia mivayagra kuna mambo ukiyazingatia, hata huku uzeeni utakuwa sawa tu na wala hutahitaji haya madawa yenu. Ndiyo maana mpaka miaka ya 70, 80 na 90 hapa ilikuwa kawaida tu kukuta mzee wa miaka 78 bado anaendelea kuoa vibinti vibichi; na anavizalisha! Wewe hakikisha tu cardiovascular system yako iko sawa na mengine yote ni marahisi. Ongeeni na wazee mjifunze 😁😁😁🏃🏿‍♂️🏃🏿‍♂️🏃🏿‍♂️🖐
Mkuu umetema madini yenye ujazo wa hatari Sana.
Hakika vijana tunatakiwa tuuzingatie Sana huu ushauri wako na tuufanyie kazi.
 
Mkuu umetema madini yenye ujazo wa hatari Sana.
Hakika vijana tunatakiwa tuuzingatie Sana huu ushauri wako na tuufanyie kazi.
Thanks nimeongea kitu halisi ila baadhi wanaleta fantasy Kuna Raha eg wa age Yako kuwa na mwanamke wa 30's as mahusiano sio tu ngono Kuna mengi sana
Mwanamke akiwa under age anakunyima mambo mengi sana
Kwanza hana cha kukushauri
 
Unafikia umri umemtamani mtoto wa kike mrembo 18+ kumwita tu anakusalimia shkamoo babu au shkamoo baba.
Ujue bora akusalimie tu shkamoo
Hapo ujue bado upo
Ila akimalizia tu .
Una hali mbaya. Sitaki uzee aisee ngoja nitafute hela
isisahau kujiwekee akiba sasa, ya kila kitu, nguvu za mwili, pesa, afya n.k ikusaidie uzeeni :whatBlink:
 
Back
Top Bottom