Maisha ya ndoa ni magumu sana

Maisha ya ndoa ni magumu sana

nikuusie kitu kimoja tu. KATIKA HAYO UNAYO PITIA SHETANI NAE HUPENYEZA MAMBO YAKE USIJE SHANGAA LIKAJITOKEZA JITU LENYE MIPESA YAKE NA KUANZA KUKURUBUNI.

ila kwa kuwa umetambua ni mapito please usimsaliti mumeo kwa kisingizio cha kutafuta unafuu kwa kutoka na watu wa aina hiyo.....


Umempa angalizo muhimu...hope atazingatia ushauri wako
 
Maisha ya ndoa ni rahisi sana ikiwa mnajitambua kwamba hauja olewa kwaajili ya familia ya mume, na mke sio kitendea kazi.
Mwanamke anapaswa kujitambua na kuijua nafasi yake ndani ya familia, pia mume anatakiwa kujua na kutambua majukumu yake kama baba wa familia.
Utii na heshima ni nguzo madhubuti ndani ya ndoa. Upendo na uvumilivu ni chachu ya kudumisha ndoa.
 
Kwa mwanamume mkamilifu na mtimilifu....hakuna jambo la aibu na la fedheha kama kuomba........
Kuomba ni jambo linalomfedhehesha sana mwanamume kiasi kwamba linamuathiri sana kisaikolojia.......
Na mwanamume yeyote ili kuepukana na kadhia hiyo ya fedheha....hana budi kupambana na kuhangaika kwa namna yoyote ili kukidhi mahitaji yake na ya wale wategemezi wake......ndio maana mwanamume hufikia hatua mpaka ana hatarisha maisha yake yote ni katika harakati za kukidhi mahitaji yake......

Katika taswira ya kawaida kumuona mwanamume amekaa na huku anaomba msaada kwa watu wanaovuja jasho kama yeye si jambo la kawaida.....ni jambo litakalompelekea mwanamke mwenye akili timamu akajiuliza kuwa nimeolewa na mwanamume wa aina gani...!!??

Kuomba msaada ni jambo la kawaida kwenye maisha kwani kati yetu hakuna aliyejikamilisha....unaweza ukawa na hiki na ukapungukiwa hiki....lakini kuna mazingira yake ya kuomba msaada na staha zake.....

Kwa mfano huyo kijana kama angeanzisha kajimradi ambako kangekuwa kanaendesha familia yake....ambako pengine baba mkwe angeona juhudi zake na kumuongezea mtaji na kukuza mradi wao....sidhani kama wangekataa ukizingatia unaishi na mtoto wao...na juhudi zinaonekana wazi ni katika kuhakikisha mtoto wao anaishi maisha mazuri.....

Kimsingi hakuna mtu mwenye uvumilivu wa kutoa misaada endelevu isiyo na mwisho.....na hilo ndilo lililotokea kwa huyo kijana.....ameukumbatia umaskini kana kwamba ni sifa nzuri.....anashindwa hata kutoka kutafuta vibarua kwenye masite ya ujenzi.....anashinda nyumbani huku akitumainia familia ya mwanamke itaweka mambo sawa.......

Hili ni tatizo kubwa kwa vijana wa sasa hivi ambapo uvivu na kutojituma ni sehemu ya miasha yao.....wanapenda mambo ya kiwepesi wepesi....mafanikio ya ghafla......hapo pengine aliunganisha dot kuwa nikimuoa huyu binti kwakuwa familia yao inajiweza....basi na mimi nitakula humo humo.......

Mwanamme ukishaingia katika majukumu unatakiwa uwe mpambanaji na sio goi goi....hayo ni majukumu yako....usiposhughulika na majukumu yako hakuna wa kushughulika nayo......usiwatupie watu majukumu yako.....

Jukumu la kumtunza mkeo ni lako haijalishi hali ya maisha ya familia ya mkeo.......
Umeongea mambo ya msingi, kuna watu matatizo yao binafsi huwa wanataka kuyageuza kuwa matatizo ya jamii!!
 
Usitishike na masimango wala maneno yao. Endelea kushikamana na mumeo anahitaji

1. Saport yako
2. Ujasiri wako
3. Faraja yako

Wanaowadharau leo kesho watajirudi. Ni kipindi tu cha mpito kukamilisha kusudi fulani... Na hongera kwa moyo wako huo
 
Nashukuru kaka huyu mume wangu sijaona kasoro yoyote kwake ni mstaarabu msomi sema maisha yetu bado ni ya chini sanaaa na ndugu hawakubali maisha ninayoishi sasa sijui wanataka nifanyeje
Wanataka uishi maisha gani mada, waambie wakuoe wao
 
Na hapo ndugu wanarudi kwa kasi
mume anawasikiliza ndugu hao hao waliomdharau kupita mkewe
na ndugu sasa wanasema mke ndo mkorofi....

inaitwa fungu la kukosa....inatokea kwa wengi tu
Hata hayo ni mapito tu yatapita
 
kuolewa na mume maskini halafu mkipata shida anakuambia kaombe msaada kwenu......kwani yeye hawezi kusolve mambo ya nyumbani kwake? ndugu zako wapo sawa shida zako na mumeo zinawahusu nini?
ajipange hawezi akurudishe kwenu
Hata hayo nimapito yatapita tu
 
Unakuta binti unatoka familia ambayo ni bora kidogo unakutana na kijana ambaye kiuchumi yupo chini mnaoana lakini maneno yanakuwa Mengi ndugu hawamuheshimu mume wako wanamdharau wanaona kama ulikosea kuchagua.

Binti unadharaulika kwenye familia yenu kila unachoongea hakina maana, ndugu wanakutenga yaani ni mateso tupu hata ukiwapigia simu wakusaidie wanakuambia mwambie mumeo na wanajua kabisa mume hana kwa muda huo.

Haya ni mapito tu naamini yana mwisho
Muombe sana Mungu wako akupitishe katika mtihani huo.

lkn pia mhimize mmeo afanye kazi kwa bidii na kwa uchungu mkubwa huku akimtanguliza Mungu ili baadae waje kuomba msaada kwenu hao ndugu zako.

Kama uliamua kuolewa nae akiwa hana kitu basi kubali matokeo na shirikianeni katika kufanya kazi
 
Unakuta binti unatoka familia ambayo ni bora kidogo unakutana na kijana ambaye kiuchumi yupo chini mnaoana lakini maneno yanakuwa Mengi ndugu hawamuheshimu mume wako wanamdharau wanaona kama ulikosea kuchagua.
hii ipo kwa wachaga sana usiombe ukawa huna kitu alafu ukaoe kwenye hiyo familia lol

Binti unadharaulika kwenye familia yenu kila unachoongea hakina maana, ndugu wanakutenga yaani ni mateso tupu hata ukiwapigia simu wakusaidie wanakuambia mwambie mumeo na wanajua kabisa mume hana kwa muda huo.

Haya ni mapito tu naamini yana mwisho
 
Msiba wa kujitakia hauna kilio.Umelilia wembe sasa vumilia maumivu.
 
poleni, umenikumbusha jamaa mmoja anapitia ugumu wa maisha kashindwa kodi kahamia kwa wakwe,
sasa. mawifi na mamamkwe kila siku wanajisemesha tu, hapo chini kuna nyumba wanapangisha bei nafuu..
Muda mwingine don't let yourselves down.
hata muwe na ugumu gani jishikeni musimame pamoja.
usilielie kwa familia ni mwanzo wa dharau.
na hata wakikusaidia mkifanikiwa watajinadi wao ndiyo chanzo cha mafanikio.
 
Back
Top Bottom