Maisha ya ndoa ni magumu sana

Maisha ya ndoa ni magumu sana

Pole Dada na hongera kwa moyo wako wa uvumilivu kile kitendo cha kusema ni mapito yataisha kunaonyesha unampenda mume wako na uko tayari kuendelea kuwa nae katika hali yoyote mpaka mapito hayo yatakapokwisha hongera sana Dada hongera Ila ukiweza tafuta mtaji au kazi msaidiane kuendesha familia yenu nzuri
 
Nashukuru kaka huyu mume wangu sijaona kasoro yoyote kwake ni mstaarabu msomi sema maisha yetu bado ni ya chini sanaaa na ndugu hawakubali maisha ninayoishi sasa sijui wanataka nifanyeje

Baki na mume wako
Endelea kumpenda kwa dhati Na ninaamini mambo eventually yatabadilika na mtafanikiwa
Kumbuka ukimwacha hao hao ndugu wataanza kukucheka
Mtangulize Mungu
 
Vumilia tu ni chaguo lako hilo, shikamana naye mjikwamue kutoka iyo hali.
 
Nashukuru kaka huyu mume wangu sijaona kasoro yoyote kwake ni mstaarabu msomi sema maisha yetu bado ni ya chini sanaaa na ndugu hawakubali maisha ninayoishi sasa sijui wanataka nifanyeje
Nilihisi tu kuwa unaongea kitu kinachokutatiza. Dada usikate tamaa, maisha huwa hayapangwi na mtu.

Mungu awe kipaumbele chako cha kwanza

Pendaneni kwa dhati na mheshimiane
Fanyeni kazi kwa bidii

Mafanikio katika maisha kwa baadhi ya hivyo vitatu hayakwepeki ingawa yahitaji muda na uvumilivu wenye staha
 
ndo maana wanasema kosea vyote ila sio mtu wa kukuoa au kumuoa ukibugi tu lazima uone ndoa ngumu sana
 
shikamana na mumeo kwa kuwa anakupenda pambana hakuna maisha marahisi muulize mama yako au ndugu zako hizo mali walizonazo zilishuka mbinguni? kama walipata hapa hapa duniani na walitafuta kama wengine basi na wewe utafute vyako na mumeo vinaheshima yake binti.......... halafu usipende sana ndugu zako wajue matatizo yako hata mkila ugali wa chumvi kula kunywa maji furahi lala usikumbuke ooh nyumbani leo wanaratiba ya kuku ningekuwa home ningekula kuku big nooo........ mshukuru Mungu .,....... ushauri mwingine mvumilie zikianza kuingia uwe unasave save hawachelewi kuchepuka na kutengenezwa huko na kukupiga chini wewe ila usiwe na mawazo hasi kuwa chanya kwamba anakupenda basi..
NB: ACHA KUWAPA MUDA NDUGU ZAKO KWA NINI WAJUE MATATIZO YENU? KWA NINI UENDE KUOMBA MSAADA KWA NDUGU ZAKO? KWANI ULITAKA KUFA?... WAPOTEZEE CHA MUHIMU NI WEWE KUWAHESHIMU BASI LAKINI SI KWENDA KUKINGA VIKOMBE HUKO.. JITAHIDI KUJITEGEMEA AISEEE
 
mtani wewe wengi tunajua kuolewa ni kugegedana na kulala

Kwa mwanamume mkamilifu na mtimilifu....hakuna jambo la aibu na la fedheha kama kuomba........
Kuomba ni jambo linalomfedhehesha sana mwanamume kiasi kwamba linamuathiri sana kisaikolojia.......
Na mwanamume yeyote ili kuepukana na kadhia hiyo ya fedheha....hana budi kupambana na kuhangaika kwa namna yoyote ili kukidhi mahitaji yake na ya wale wategemezi wake......ndio maana mwanamume hufikia hatua mpaka ana hatarisha maisha yake yote ni katika harakati za kukidhi mahitaji yake......

Katika taswira ya kawaida kumuona mwanamume amekaa na huku anaomba msaada kwa watu wanaovuja jasho kama yeye si jambo la kawaida.....ni jambo litakalompelekea mwanamke mwenye akili timamu akajiuliza kuwa nimeolewa na mwanamume wa aina gani...!!??

Kuomba msaada ni jambo la kawaida kwenye maisha kwani kati yetu hakuna aliyejikamilisha....unaweza ukawa na hiki na ukapungukiwa hiki....lakini kuna mazingira yake ya kuomba msaada na staha zake.....

Kwa mfano huyo kijana kama angeanzisha kajimradi ambako kangekuwa kanaendesha familia yake....ambako pengine baba mkwe angeona juhudi zake na kumuongezea mtaji na kukuza mradi wao....sidhani kama wangekataa ukizingatia unaishi na mtoto wao...na juhudi zinaonekana wazi ni katika kuhakikisha mtoto wao anaishi maisha mazuri.....

Kimsingi hakuna mtu mwenye uvumilivu wa kutoa misaada endelevu isiyo na mwisho.....na hilo ndilo lililotokea kwa huyo kijana.....ameukumbatia umaskini kana kwamba ni sifa nzuri.....anashindwa hata kutoka kutafuta vibarua kwenye masite ya ujenzi.....anashinda nyumbani huku akitumainia familia ya mwanamke itaweka mambo sawa.......

Hili ni tatizo kubwa kwa vijana wa sasa hivi ambapo uvivu na kutojituma ni sehemu ya miasha yao.....wanapenda mambo ya kiwepesi wepesi....mafanikio ya ghafla......hapo pengine aliunganisha dot kuwa nikimuoa huyu binti kwakuwa familia yao inajiweza....basi na mimi nitakula humo humo.......

Mwanamme ukishaingia katika majukumu unatakiwa uwe mpambanaji na sio goi goi....hayo ni majukumu yako....usiposhughulika na majukumu yako hakuna wa kushughulika nayo......usiwatupie watu majukumu yako.....

Jukumu la kumtunza mkeo ni lako haijalishi hali ya maisha ya familia ya mkeo.......
 
Kwa mwanamume mkamilifu na mtimilifu....hakuna jambo la aibu na la fedheha kama kuomba........
Kuomba ni jambo linalomfedhehesha sana mwanamume kiasi kwamba linamuathiri sana kisaikolojia.......
Na mwanamume yeyote ili kuepukana na kadhia hiyo ya fedheha....hana budi kupambana na kuhangaika kwa namna yoyote ili kukidhi mahitaji yake na ya wale wategemezi wake......ndio maana mwanamume hufikia hatua mpaka ana hatarisha maisha yake yote ni katika harakati za kukidhi mahitaji yake......

Katika taswira ya kawaida kumuona mwanamume amekaa na huku anaomba msaada kwa watu wanaovuja jasho kama yeye si jambo la kawaida.....ni jambo litakalompelekea mwanamke mwenye akili timamu akajiuliza kuwa nimeolewa na mwanamume wa aina gani...!!??

Kuomba msaada ni jambo la kawaida kwenye maisha kwani kati yetu hakuna aliyejikamilisha....unaweza ukawa na hiki na ukapungukiwa hiki....lakini kuna mazingira yake ya kuomba msaada na staha zake.....

Kwa mfano huyo kijana kama angeanzisha kajimradi ambako kangekuwa kanaendesha familia yake....ambako pengine baba mkwe angeona juhudi zake na kumuongezea mtaji na kukuza mradi wao....sidhani kama wangekataa ukizingatia unaishi na mtoto wao...na juhudi zinaonekana wazi ni katika kuhakikisha mtoto wao anaishi maisha mazuri.....

Kimsingi hakuna mtu mwenye uvumilivu wa kutoa misaada endelevu isiyo na mwisho.....na hilo ndilo lililotokea kwa huyo kijana.....ameukumbatia umaskini kana kwamba ni sifa nzuri.....anashindwa hata kutoka kutafuta vibarua kwenye masite ya ujenzi.....anashinda nyumbani huku akitumainia familia ya mwanamke itaweka mambo sawa.......

Hili ni tatizo kubwa kwa vijana wa sasa hivi ambapo uvivu na kutojituma ni sehemu ya miasha yao.....wanapenda mambo ya kiwepesi wepesi....mafanikio ya ghafla......hapo pengine aliunganisha dot kuwa nikimuoa huyu binti kwakuwa familia yao inajiweza....basi na mimi nitakula humo humo.......

Mwanamme ukishaingia katika majukumu unatakiwa uwe mpambanaji na sio goi goi....hayo ni majukumu yako....usiposhughulika na majukumu yako hakuna wa kushughulika nayo......usiwatupie watu majukumu yako.....

Jukumu la kumtunza mkeo ni lako haijalishi hali ya maisha ya familia ya mkeo.......
umenena vyema mtani vijana watajifunza jambo hapa
 
Inahitaji uvumiliv Sana,

Ila pia kuwa makini Sana huwa tunapozipata tunabalika Na kusahau shida.
 
Pole sana kwa hayo yakukutayo ila ndo maisha.....hayahitaji hasira kumbuka suluhisho au mwisho wa tatizo lolote lipo ni suala la muda tu...
 
Back
Top Bottom