Maisha ya ndoa ni magumu sana

Maisha ya ndoa ni magumu sana

Unakuta binti unatoka familia ambayo ni bora kidogo unakutana na kijana ambaye kiuchumi yupo chini mnaoana lakini maneno yanakuwa Mengi ndugu hawamuheshimu mume wako wanamdharau wanaona kama ulikosea kuchagua.

Binti unadharaulika kwenye familia yenu kila unachoongea hakina maana, ndugu wanakutenga yaani ni mateso tupu hata ukiwapigia simu wakusaidie wanakuambia mwambie mumeo na wanajua kabisa mume hana kwa muda huo.

Haya ni mapito tu naamini yana mwisho
simama mbele ya kioo kisha uambie moyo wako kwa kutamka maneno haya "HILI NI GUMU ,LAKINI NALO LITAPITA,NITAPAMBANA, NINAWEZA KUIBADILISHA HALI HII" .Kisha kaa na mumeo chini muangalie humo ndani mwenu mna kitu gani ambacho hamkitumii au ni redundant , mkishavipata basi hivyo mnaweza kuvigeuza mtaji. na kwa mtaji huo huo mdogo pambaneni kuukuza na kusonga mbele. SAHAU kuhusu neno KUSAIDIWA , pambaneni nyinyi wawili na zidisheni upendo kati yenu.
 
kuolewa na mume maskini halafu mkipata shida anakuambia kaombe msaada kwenu......kwani yeye hawezi kusolve mambo ya nyumbani kwake? ndugu zako wapo sawa shida zako na mumeo zinawahusu nini?
ajipange hawezi akurudishe kwenu

Sio akurudishe bali urudi kwenu na hili ni kosa wanalofanya wanawake wote hata akiwa amezeeka anawaza kurudi kwao.

Yaani huko kwao sijui mwisho ni mda gani wa kurudi huko.
 
kuolewa na mume maskini halafu mkipata shida anakuambia kaombe msaada kwenu......kwani yeye hawezi kusolve mambo ya nyumbani kwake? ndugu zako wapo sawa shida zako na mumeo zinawahusu nini?
ajipange hawezi akurudishe kwenu
Hiyo imekaaje,, amrudishe kwao wakat ameshamtumia!!! mimi naona wakomae wote tu hadi kifo ndio ushauri.
 
Back
Top Bottom