Maisha haya acheni tu unaweza kukufuru

Maisha haya acheni tu unaweza kukufuru

Habari za jioni

Maisha mnayaonaje ndugu zangu,dada zangu,Kaka zangu.

Kila nilichopanga kufanya mwaka huu naona kabisa hakitimii.

Dada yangu mmoja hapa mtaani anasema nisijipe presha bado mdogo,nitafanikiwa tu kwa uwezo wa Mungu, lakini Mimi mwenyewe nina marafiki kibao,naona kama wanaendelea vizuri na mambo yao.

Na Mimi kila siku najiuliza nawezaje kufanikiwa na Elimu yangu ya kuunga unga ?

Kudanga siwezi,
Kutapeli ni mwiko kwangu,

Pamoja na hivi nilivoo naenjoy Kula pesa ya jasho halali iliyo na Baraka za Mungu. Je nitafanikiwa vipi.
Nawaombeni ushauri.
Maria D.
Njoo inbox nikupe jambo la kufanya nauhakika utatoka
 
Habari za jioni

Maisha mnayaonaje ndugu zangu,dada zangu,Kaka zangu.

Kila nilichopanga kufanya mwaka huu naona kabisa hakitimii.

Dada yangu mmoja hapa mtaani anasema nisijipe presha bado mdogo,nitafanikiwa tu kwa uwezo wa Mungu, lakini Mimi mwenyewe nina marafiki kibao,naona kama wanaendelea vizuri na mambo yao.

Na Mimi kila siku najiuliza nawezaje kufanikiwa na Elimu yangu ya kuunga unga ?

Kudanga siwezi,
Kutapeli ni mwiko kwangu,

Pamoja na hivi nilivoo naenjoy Kula pesa ya jasho halali iliyo na Baraka za Mungu. Je nitafanikiwa vipi.
Nawaombeni ushauri.
Maria D.
Kwanza, nikupe pongezi kwa kuwa na standards ambazo umejiwekea na unaishi kwa kuziheshimu hizo. Pili, nkuhakikishie kuwa mafanikio ni tafsiri pana ambayo unaweza kuielewa kwa ukweli wake kama utaitafsiri kwa kujitizama wewe wa sasa na wewe wa siku za nyuma na sio wewe ulivyo na wengine walivyo kwa hatua au vitu wanavyomiliki na wewe huna. Tatu, Hatua ya kwanza kufanikiwa ujue unataka nini katika maisha au unataka ufikie wapi ndani ya muda gani, kisha tambua kuwa unapaswa ujikane mwenyewe na kuamua kuachana na mambo fulani fulani, watu wa aina fulani na kuondoka pahali fulani ulipokulia n.k ili uweze kuona maisha katika mtazamo mwingine na uonavyo sasa. Hivyo, nkutakie safari njema ya kujitafuta na mtegemee Mungu utafanikiwa. Kila la Kheri Maria.
 
Back
Top Bottom