Maige aichana serikali ya JK

Maige aichana serikali ya JK

It is too late Maige, wewe ni sawa tu na Ngeleja alivyo kuwa mwehu na mhanga wa kuachishwa uwaziri na kuchangia bungeni kwa hasira na kuishambulia CDM.
 
Mhhh!...kwa hiyo kwa maneno haya huyu Waziri mpya wa Nishati na Madini hana maisha marefu katika wizara hiyo. Wanaweza kabisa kumtafutia la kumtafutia kisha wamtose.

Kwanini hakuyasema haya alipokuwa Waziri huku akijua kulikuwa na malalamiko chungu nzima toka kwa Watanzania kuhusu utendaji wa DHAIFU na Serikali yake yote? asubiri kuyasema baada ya kutoswa?


Aliyekuwa waziri wa JK ambae alitoswa kwenye reshuffle, akichangia bajeti ya wizara ya nishati na madini amesema


  1. mawaziri wanaofanya maamuzi wako hatarini sana kwa sababu kama maamuzi yataenda kinyume na maslahi ya mafisadi basi inaweza ikala kwa waziri

  2. akimpa ushauri naibu waziri masele, amemwambia aende kahama kurekebisha mambo maana huko vitalu wamepewa mabwenyenye ila awe makini maana maauzi ya kutetea wanyonge yana gharama zake, na ushahidi upo na akamaliza kwa kusema 'najua wewe ni mtu mzima, nafikiri utakua umenielewa!'
 
Maige huna aibu, na wewe unakemea wala rushwa. Mpaka leo hujawaeleza watanzania dola 700,000 US$ za kujenga hekalu Mbezi beach ulizipata wapi!!! Twiga wetu walipita KIA. UMEPATA WAPI MORAL AUTHORITY ! SHAME UPON YOU!!!

US$ 700,000 amedumbuliza kwa muda mrefu pamoja na kukopa kama alivyosema, lakini wizi wa TShs. 6 billion kwa mwezi wewe CHUAKACHARA unaoni ni ufisadi wa kawaida?
 
Last edited by a moderator:
Huyu Waziri mstaafu mwaka jana nilitoa maoni yangu on facebook kuhusu madudu ya serikali ya CCM ndani na nje ya bunge; aliponisoma, akaenda mwambia mtu mmoja ambae ninamfahamu kwamba huyu mtoa maoni ni mtu wa ajabu sana, na kwamba hoja zangu hazina mashiko na badala yake ninakisingizia tu chama na serikali yake. Lakini kauli za waziri huyu mstaafu tangia ametoka kwenye uwaziri hazina tofauti na zangu mwananchi na mwanachama wa kawaida wa CCM ambae (na wengien wengi pia mitaani) nimechoshwa na mwenende wa CCM katika kuliongoza taifa letu. Sasa sijui kwanini waziri huyu mstaafu alipokuwa na wadhifa wa uwaziri aliona maoni yangu hayana maana, na sijui ni kwanini sasa hivi mtazamo wake hautofautiani na makabwela kama mimi.
 
Maige hasomi alama za nyakati. Hajajua kuwa kwa sasa hana nafasi ya kuushauri umma kuwa ana hata punje ya busara. Akae kimya angoje msimu wake wa ubunge uishe wengine wapokee jimbo lake
 
Imemchukua muda kuamka sasa anatakiwa kuendelea alipoanzia ingawa bado koti lake nyuma lina harufu ya ufisadi
 
Atasema yote ila hatakana kuwa nafasi ya uwaziri wa Nishati na Madini ulimpa utajiri wa kunuka hadi akanunua hekalu kwa kashi ya dola 700,000. Hata hivyo ndivyo walivyo. Wakibwagwa chini wanajifanya wana uchungu na nchi wakati ukweli ni kwamba wana uchungu na ulaji tu. Tanzania tunajua tulishageuzwa shamba la bibi na watu kama Maige na hao mabwanyenye wake.
 
Typical Tanzanian politician. Baada a kutoswa sasa amegeuka na kuwa mtetezi wa ''wanonge'' huku akiwashauri mawaziri nini cha kufanya
 
Aliyekuwa waziri wa maliasili na utalii, akichangia katika bajeti ya wizara nishati na madini muda mfupi kabla kupitishwa, amemtahadhalisha Naibu Waziri wa Nishati na madini (Masele) huku akimuita mdogo wake kuwa awe makini katika kurejesha miradi hiyo ya wakubwa kwa wajasilimali wadogowadogo ili matatizo yasije yakamfika.

Hii ni baada ya wabunge wengi kudai kuwa maeneo mengi ya uchimbaji madini wamekabidhiwa kwa wachimbaji wakubwa huku wadogo wakibaki hawana kitu. Akahitimisha kwa kumwambia Masele kuwa yeye ni mtu mzima na atakuwa amemwelewa!

Swali: Ni matatizo yapi yanayoweza kumfika huyo mheshimiwa? Anamaanisha yaliyomkuta (kuenguliwa ktk uwaziri) ilitokana na yeye (Maige) kugusa maslahi ya wakubwa?
 
Jamani,huyu mtu yawezekama kaathirika kisaikolojia,hata hajui atamkalo!
 
Maige kama vile Karai la magamba lililotupwa baada ya nyumba kukamilika.

Swadaktaaaaa! Duuuu, lazima utakuwa jiniasi kwa namna ulivyotumia lugha. Ningekuwa karibu nawe, ningekuuliza unatumia kinywaji gani.
 
Mchambuzi

Hii mikitu mzee ni kama mchezo wa draft,ukiwa nje huchezi unaona sana kete za kucheza lakini ukiingia wewe kucheza unakua huzuioni kete
 
Last edited by a moderator:
Huyu Waziri mstaafu mwaka jana nilitoa maoni yangu on facebook kuhusu madudu ya serikali ya CCM ndani na nje ya bunge; aliponisoma, akaenda mwambia mtu mmoja ambae ninamfahamu kwamba huyu mtoa maoni ni mtu wa ajabu sana, na kwamba hoja zangu hazina mashiko na badala yake ninakisingizia tu chama na serikali yake.

Mkuu naomba ufafanuzi kwenye red hapo. Maana naona siku hizi kiongozi akivuliwa uongozi kutokana na kashfa tunamwita mstaafu. Kwa maana hii pia hata akina Jairo na Muhando na wao ni wastaafu!
 
Typical Tanzanian politician. Baada a kutoswa sasa amegeuka na kuwa mtetezi wa ''wanonge'' huku akiwashauri mawaziri nini cha kufanya

na ni dharau kwa waTZ, hawa jamaa wanafikiri sie tuna vichwa vya kuku, kwamba tunasahu kilichotokea dakika moja iliyopita?

 
wote mnatoka mkoa mmoja, na inawezekana huwa mnaonana kila mara, so nilidhani ushauri huu ulitakiwa umwambie mkiwa peke yenu, na si lazima utokee kwenye hansard? pole sana
 
Back
Top Bottom