Wakuu nawasalimu wote,
Kwanza kabisa poleni kwa majukumu naamini wote mnapambana ili kuhakikisha hili taifa linasonga mbele.
Pili, nipende kutoa shukrani zangu za dhati kwa wote walionishauli.
Ni Juzi tu nilileta uzi hapa nikiwa nalalamika kuwa kuna mpenzi wangu namhudumia kila kitu lakini yeye hataki kunipa haki ya wapendao.
Huu hapa;
Mahitaji yake nampa lakini yeye hataki kunipa
Ndugu wanajukwaa ushauri wenu nimejaribu kuutumia na nimeona matunda ya ushauri wenu. Kuna wengine walinambia msimtafute, ni kweli jana asubuhi sijamtafuta, cha kushangaza mchana akanitumia SMS nikamshaushia. Usiku amenitafuta nikaendelea kubana vyuma.
Cha kushangaza leo asubuhi na mapema amenifuata kazini kwangu analia, ananibembeleza anasema turudiane.
Wanajukwaa msichoke kunishauri, mimi msimamo ni kwamba tuachane, lakini analia.
Naomba mtazamo wenu wakuu kuhusu hili suala, ukizingatia nimetumia gharama kubwa kumhudumia ndani ya wiki moja halafu sijalamba kitu.
Niendelee kubana vyuma?.