Babe makasiriko ya nini sasa?Nenda zako huko bana
Ungefika basi mahakamani kutoa ushahidi namna huyo dada alivyonyanyaswaUnaamini vipi kama alichosema ni kweli.
Mosha ni katili. Ametunga uongo mwingi na kwasababu anapesa mnaamini kila anachosema.
Na kama kweli mke ameiba mimi nampongeza maana amemnyanyasa sana dada wa watu.
Lazima alisaidiwa na hawara kufanya hivyo.Shida mwanamke ni mwizi
Na cha ajabu hakukataa huo wizi
Yaani dollar karibu milioni 7 in total .... amechukua kwa signature za wizi
Huyu dada tamaa zilimzidi sana,mpaka kuiba pesa nyingi hivyo?
What a bad woman
Kiongoli ni watu wa wapi aisee?I know sio Mchagga kabisa,Mosha kiazi sana aisee,badala aoe kwao kuna wasichana wazuri na disciplined kaenda kuoa jambazi,yaani unafoji documaa unaiba madola mengi hivyo?
Huyo kama alivyosema haoni hatari kumuwekea sumu jamaa
Anayo magari anazo nyumba zipo kwa jina la mdogo wa mke anaitwa Steven yupo KigamboniUnaweza kuta Huyo mwanamke hapo alipo hajaachwa kizembe, utakuta hapo mke wa Davis mosha ana nyumba za kupangisha dar, magari, na nyumba ya ghorofa, biashara mbalimbali na assets kama ardhi, ila utakuta mke hapo kwenye hio kesi anatafta ziada tu Nifah
Ujanja kapewa na Jamaa anaitwa Athuman kufakunoga huyo ndiyo mchepuko wa huyo mwanamke kwa sasaNifah umesoma vizuri kweli?
Kaiba dollar 500,000..kaja dollar sijui 950,000....total ni kama dollar milioni 7 hivi na zote hizo hajabisha,jibu lake kasema "sijibu hii hoja ya wizi hizi sababu nampenda petitioner na nimekaa nae miaka 28" hilo ndio jibu la huyo dada.
Tatizo huyo dada ni mwizi anaiba kwa kufoji documents,anakopa benki bila knowledge ya mwenye kampuni na hela anazihamishia kwenye account zake binafsi anazila
Huyo hafai tena na ni very wrong
Wanaomtetea Mosha wanajidanganya sana ...Baada ya ndoa mali akichumq hata kama mke angekuwa mama wa nyumbani mali zinamuhusuNinavyojua mimi ni kuwa chochote kinacho chumwa ndani ya ndoa ni cha wanandoa pasu kwa pasu. Siwezi kuamini kuwa katika miaka 28 ya ndoa hamna kilichoingizwa au kununuliwa. Kama kuna kampuni imeanzishwa basi mke anakuwa na mgao wake. Tabia za huyo mwanamke katika ndoa hiyo hazina uhusiano wowote na haki yake.
Mike Tyson alitakiwa kumlipa mtalaka wake Robin Givens mamilioni ya dola ingawa ndoa yao ilidumu muda mfupi na Robin aliolewa wakati Tyson tayari ana mapesa. Mambo kama haya ndio yanayowafanya matajiri wengi kuingia katika makubaliano ya prenup kabla ya ndoa ambamo stahili za kila mmoja ikitokea divorce zinawekwa wazi.
Hapa Hakimu inaonekana ameyumbishwa na hizo simulizi za kutoka nje ya ndoa, uchawi, jaribio la kumuua n.k. Haikupaswa kuwa hivyo. Alipaswa kuhakikisha kuwa mke anapata mgao wake kwa sababu tu wamekaa katika ndoa kwa miaka 28. Kwenye hili hakutenda haki.
Amandla....
Labda sio akili zakeKama unamuonea sana huruma huyo mwanamke, unaonaje ukimpa wewe mali zako, au mgawane mali zako.
Dah!Mtu yeyote anayetumia maneno "nitty gritty" katika hukumu anatia wasiwasi. Na kwani huyo mama alikuwa anajiita Davis Mosha mpaka Hakimu aone kuna umuhimu wa kumzuia kulitumia?
Amandla...
Sasa hafai kwa lipi Yaani Jaji ulitaka apendelee kisa Ni maanamke, wanawake tunajidhalilisha Sana, Yaani Nancy alikiri kukimbia Nyumba yake mwenyewe, na Meseji za kutaka kuua zipo, Lakini Ushahidi wa wizi wa mabilioni upo na ndo Maana Nancy yeye kwa maandishi yake Instagram na Akaunti yake real na fake alikiri kuwa Mfanyabiashara Huyo Kwenye kampuni ana Madeni mengi, alibeza kampuni aliyokuwa anajua Siri zoote na ndo Maana mwanzoni alikubali Talaka na akaachana na kesi kwa Sababu alisema Kuna Madeni.Huyu Jaji Msafiri ni mla rushwa mkubwa, Ukiwa na kesi anakwambia kesi yako namaliza miezi mitatu nipe milioni 6. Yaaani nimesoma tu nikasema hapa kuna shida sana. Msafiri hafai
Na ungana na wewe kabisa kabisa umesema kweli..Davis Mtu sanaLuckily huyu Mwanamke hajamuua tajiri yangu wa zamani Davis kwa sumu au kwa umafia.
Nje ya mada: Kwa wale tuliopata kufanya kazi na Davis kama bosi wetu, Davis ni mtu wa kipekee sana.
Sio ajabu yule jamaa ni Bilionea.
Davis ni mtu mpaka akufukuze kazi anakuwa amekuvumilia sana na amekuonya sana.
Davis hawezi kumfokea mfanyakazi wake hadharani hata kama amekosea kwa kiasi gani.
Davis anapenda watu. Davis akifika ofisini atamsalimia kila mtu kwa kumpa mkono hata mkata majani.
Davis huwezi mwambia shida ukiwa kama mfanyakazi wake (Sijui kwa watu wengine) asikusaidie kama lipo ndani ya uwezo wake.
Ni mtu mwenye hekma, busara na maarifa. He's truly blessed.
Sio ajabu aliweza mvumilia mwanamke wake akiwa "Mwizi" na "Mzinzi".
One of a kind billionaire.
Nakazia: Nipo nje ya mada.
Huyu @NigelBaby ni nani naona anatomboka kweli kweliSasa hafai kwa lipi Yaani Jaji ulitaka apendelee kisa Ni maanamke, wanawake tunajidhalilisha Sana, Yaani Nancy alikiri kukimbia Nyumba yake mwenyewe, na Meseji za kutaka kuua zipo, Lakini Ushahidi wa wizi wa mabilioni upo na ndo Maana Nancy yeye kwa maandishi yake Instagram na Akaunti yake real na fake alikiri kuwa Mfanyabiashara Huyo Kwenye kampuni ana Madeni mengi, alibeza kampuni aliyokuwa anajua Siri zoote na ndo Maana mwanzoni alikubali Talaka na akaachana na kesi kwa Sababu alisema Kuna Madeni.
Leo Wewe unayetumia jina letu pendwa unasema HAKIMU mla rushwa Kweli, Wewe ndiye hakimu unaongozwa kwa Ushahidi na Ushahidi wa wizi, umalaya, uchawi, ushirikina, nk vyoote vilipelekwa mbele ya hakimu na hukumu ikatoka Sasa Rushwa hapo Ni nini? Au Nancy hajakupanga?
Au zile Bilion alizoiba bado zipo, alimjengea Nyumba Mpenzi wake Mtabibu Mitimingi, na uliishuhidia ilizinduliwa, ili waue Ushahidi haraka haraka alizindua Kiongozi Mkubwa wa jeshi la Polisi na Mtabibu akaoa haraka haraka, Lakini Ndugu Kafara za Afrikana Kwenye petrol Station ya Mfanyabiashara Huyo ukuziona Tembelea Akaunti ya @NigelBaby Instagram utaelewa mengi Mpaka sauti za Mipango ya kuua, wizi, na Ujinga.
Nancy ni mtu wa singida km sijakoseaNaomba kujua kabila la Nancy. Maana hii ya kutaka kuua ili ubaki na mali ni story za long time sana zilizowalenga dada zetu wa jamii fulani hivi
Ni tu Huyo Nancy na washirika wake ambao Ni mashoga kina Husein, Wamemtukana huyo Mfanyabiashara matusi yote mnayoyajua, waliunda Akaunti real na fake kumtukana Lakini jamani kanyamaza.Huyu Jaji Msafiri ni mla rushwa mkubwa, Ukiwa na kesi anakwambia kesi yako namaliza miezi mitatu nipe milioni 6. Yaaani nimesoma tu nikasema hapa kuna shida sana. Msafiri hafai
Hapo Sasa linamjia WAZO la kumrogaMfanyabiashara Davis Mosha ameacha na mke wake wa ndoa aliyeishi naye kwa miaka 28 amekwenda kufoji nyaraka za kampuni hukumu imetolewa mke hajapewa urithi hata pini.
Masikini ya Mungu Huyu Mkewe ndiye alikuwa muhasibu wa kampuni zote za huyu mfanyabiashara kwa miaka 20.
Majaji wetu hukumu kama hizi ni za ukandamizaji, mawakili tunaomba msaidie kama hii hukumu ni halali na mahakama zetu zinatoa haki nimeona uonevu mtupu humu Pesa imenunua haki.
Je hii ni sawa?
==========
MAAMUZI YA MAHAKAMA
- Ndoa kati mlalamikaji na mlalamikiwa imevunjwa na talaka imetoka.
- Hakuna mali zilizopatikana kwa pamoja kwenye ndoa.
- Uangalizi wa mtoto Daniela Davis Mosha unakuwa chini ya mlalamikaji(Baba)
- Mdaiwa anapewa ruhusa ya kuwa na mtoto kipindi cha likizo na siku yenye nafasi kwa mtoto
- Mdaiwa amekatazwa kutumia jina la mlalamikaji Davis Mosha na amerejeshewa majina yake ya awali
- Kila mmoja atabeba gharama za kesi
View attachment 2912748View attachment 2912749View attachment 2912750View attachment 2912751View attachment 2912752View attachment 2912753View attachment 2912754View attachment 2912755View attachment 2912756View attachment 2912757View attachment 2912758View attachment 2912759View attachment 2912760View attachment 2912761View attachment 2912762View attachment 2912763View attachment 2912764View attachment 2912765View attachment 2912766View attachment 2912767View attachment 2912768
Huyo Nancy ni tapeli kwanza hajawahi kuwa muhasibu miaka 20, Mfanyabiashara huyo alimpa biashara yake ubungo ya beurauDechange, Nancy Akapata mwanaume mkongo wakafilisi duka loote mnakumbuka jamani au mmesahau, Akapelekwa headquarter ndiyo akawa anaiba kwa kwenda mbele na wafanyakazi wanajua akatolewa toka 2017.Yupo na Othuman ndiyo anamfundisha mwanamke usumbufu wote
Nilikuwa nazungumzia utofauti kati yake na jackline mengi.
Hajaiba. Amechukua maana anastahili, amezifanyia kazi.
Alafu nasikia aligushi nyaraka pia! Ndiyo maana Mahakama imempiga chini,kwa kua alikua na nia ovuu kwa mwenzie!!Kama alitaka kumuua Mumewe..... Hapaswi Kupewa hata THUMUNI.
Mwizi apewe stahiki tena? Hivi unaanzaje kumuibia mme wako kama unapenda?Halafu utasikia wasio na akili wanamuita huyo mwanamke mdangaji. Mwanamke ameshiriki kwenye biashara zake miaka 20 sio mchezo, tena kitengo ambacho ni uti wa mgongo wa biashara.
Kuachana kupo lakini apewe stahiki zake.