Mahakama yatupilia mbali Kesi ya Mbowe ya Kikatiba dhidi ya IGP, DPP na Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Nimesoma sababu za kufutwa kwa kesi ya kikatiba zilizotolewa
a mahakama Kuu ya Tanzania, naomba niseme poleni mnaosoma mkituaminisha mnakuja kufanya mabadiliko ya kifikra kwenye Taifa hili. Nawapa pole kwa sababu kwa Aina hii ya maamuzi sidhani Kama huko tuendako kutakuwa na kesi za miaka ya karibuni za kufanyia rejea. Mahakama iliondoka na akina Jaji Samatta.
Mahakamaba 23, 2021 imeifuta kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na, @freemanmbowetz, kutokana na kilichoelezwa kuwa kuwepo kwa kesi ya msingi katika Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, hivyo malalamiko yake ayawasilishe huko yataweza kushughulikiwa.
 


Wazee wa PGO kuna mchochozi huko Marekani nendeni mkamuarest Haraka anatupaka matope.



 
Kesi ya kikatiba iende uhujumu uchumi tena?
Hakuna tatizo la katiba, kuna tatizo la ki utaratibu, Mbowe anaamini taratibu hazikuafuatwa wakati anakamatwa, ana uwezo wa kupungua hilo ndani ya kesi yake kama wanavyo pinga saivi maelezo ya washtakiwi wengine yasikubuliwe kama ushahidi katika kesi ndogo inayo endelea. Kwa lugha rahisi, mawakili wa Mbowe walikurupuka ili kufurahisha genge na vigelegele vya watu wao.
 
Mahakama Kuu ya Tanzania imetupilia mbali kesi ya kikatiba ya mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, aliyekuwa akipinga namna alivyowekwa kizuizini na kulazwa sakafuni kwa siku tano bila kufikishwa mahakamani.

Mbowe alifungua kesi hiyo Julai 30, mwaka huu akilalamikia namna alivyotiwa mbaroni jijini Mwanza kuweka mahabusu ya polisi kwa siku tano bila kufikishwa mahakamani ndani ya saa 48 kama sheria inavyoelekeza.

Kiongozi huyo wa chama kikuu cha upinzania pia alikuwa akilalamika kiulazwa sakafuni bila matandiko uyoyote wakati akiwa mahabusu.

Katika kesi hiyo namba 21 ya 2021, Mbowe alikuwa akipinga kufikishwa mahakamani bila kuwajulisha mawakili wake au ndugu zake na kabla ya kujulishw kwa maandishi kuhsu mashtaka yaliyokuwa yakumkabili.

Katika kesi hiyo aliyoifungua dhidi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Mbowe alikuwa pia akipinga kusomewa mashtaka ya ugaidi yanayomkabilia bila kuwa na wakilia wala kupewa hati ya mashtaka.

Mbowe alikuwa akidai utaratibu huo ulikiuka haki zake za kikatiba, huku akiiomba mahakama hiyo itamke kuwa haki zake zilikiukwa.

Uamuzi wa kuitupa kesi hiyo umetolewa leo Alhamisi Septemba 23 na Jaji John Mgetta aliyesikikiza pingamizi hilo la Serikali kwa niaba ya jopo la majaji watatu waliokua wamepangwa kusikiliza kesi hiyo, akiwemo Jaji Leila Mgonya na Jaji Stephen Magoiga.

Majaji hao wamekubaliana na pingamizi la Serikali lililokuwa na hoja nne lililotaka kesi hiyo isisikilizwa kwa madai ya kuwa na kasoro nyingi za kisheria.

Mahakama Kuu imekataa hoja tatu za pingamizi la Serikali na kubaliana na hoja moja tu ya pingamizi la Serikali iliyodai kuwa Mbowe hakutumia njia nyingine zilizopo kutafuta haki anazodai kabla ya kufungua kesi ya kikatiba.

Mahakama amekubaliana na Serikali kupitia jopo la mawakili wa Serikali lililoongozwa na Wakili wa Serikali Hangi Chang'a kuwa kwa kuwa kuna kesi ya jinai dhidi yake (Mbowe), basi madai yake alipaswa kuyaibua katika Mahakama hiyo kwanza kabla ya kufungua kesi ya kikatiba.

"Kwa hiyo nakubaliana na pingamizi hili la wajibu maombi kwamba hii ni hoja ya kisheria na kama alivyoeleza Wakili Mkuu wa Serikali, Mussa Mbura katika hoja za maandishi, Mahakama inayosikilizwa kesi yake (Mbowe) ya uhujumu uchumi ndiyo mahakama sahihi. Hivyo alipaswa kutoa madai yake huko kwanza," amesema Jaji Mgetta.

Chanzo: Mwananchi
 
Toka kizazi cha majaji tajika kama Jaji Lugakingira,Jaji Kati,Jaji Mapigano,Jaji Mwalusanya,Jaji Chipeta na wengine wa aina hiyo waliokuwa real bold spirted judges,kwa sasa tuna kizazi cha majaji wasiojielewa na wasiomjua nguvu waliyonayo katika kusimamia Uhuru wa muhimili wa mahakama katika kutenda haki. Inasikitisha.
 

wakina mdude walivoachiwa muhimili ulikua vizuri ila alipowekwa hatiani mzee baba muhimili mbovu
 
Kumbe mahakama haijakataa hoja za Mbowe ila imeelekeza kwamba, kwa kuwa kesi ya msingi iko mahakama kuu, kitengo cha Uhujumu uchumi, basi huko ndiko mahali sahihi kupeleka madai yake...

On the other hand, kama Jaji angekubaliana na hoja za mleta pingamizi (ambazo obviously ziko sahihi), maana yake alikuwa anaifuta kabisa kesi ya Msingi iliyoko mahakama kuu kitengo cha makosa ya uhujumu uchumi...!

Ndiyo maana, Jamhuri wiki hii yote imesimama kuendelea na usikilizaji wa shauri hili ili kupima na kujadiliana namna ya kulimaliza pingamizi hilo...
 
Mhimili uko kazini

Mungu ibariki Tanzania
Unatakiwa pia kusema Mungu Mbariki Mbowe ili atoke mapema huko korokoroni! Maana hata wewe kada wa ccm, unatambua fika hii kesi ni ya kubambikiwa na polisi wakishirikiana na mfumo, kwa lengo tu la kumkomesha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…