Mahakama: BAKWATA si Chombo cha Waislam wote

Mahakama: BAKWATA si Chombo cha Waislam wote

Nipo upande wa Sheihk Ponda toka Bakwata walivyouza eneo la waislamu pale Keko niliona ni wahuni tu aisee na eneo lenyewe pana mwislamu alitoa ili hilo enjoy lijengwe msikiti mkubwa Daslm Viongozi wa Bakwata waliliuza kwa hela ndogo sana kisa walipewa rushwa kubwa hakuna taasisi ya Waislamu hapo ni wahuni tu.
Achana na Hilo dogo:
Lile la Chang'ombe kalibu na Kibasila:
Bora wangelikodisha:
 
Bakwata walivyouza eneo la waislamu pale Keko niliona ni wahuni tu aisee na eneo lenyewe pana mwislamu alitoa ili hilo enjoy lijengwe msikiti mkubwa Daslm Viongozi wa Bakwata waliliuza kwa hela ndogo sana kisa walipewa rushwa kubwa hakuna taasisi ya Waislamu hapo ni wahuni tu.
Hao wala hawakupewa rushwa kama unavyojidanganya hao waliigawa kwa mahaba yao kwa muislam mwenzao,usually hao alimradi amenunua muislam mwenzao au kitu kafanya muislam mwenzao basi inakuwa siyo nongwa.

Kama hivi,Watanganyika wameuliwa hapa but hao hao wanaitisha press kumsafisha aliyesaini order eti anaonewa kwa sababu muislam,hovyo kabisa.
 
Hao wala hawakupewa rushwa kama unavyojidanganya hao waliigawa kwa mahaba yao kwa muislam mwenzao,usually hao alimradi amenunua muislam mwenzao au kitu kafanya muislam mwenzao basi inakuwa siyo nongwa.

Kama hivi,Watanganyika wameuliwa hapa but hao hao wanaitisha press kumsafisha aliyesaini order eti anaonewa kwa sababu muislam,hovyo kabisa.
BAKWATA taasisi ya ovyo
 
Nahisi hao Bakwata ndio wanaopiga pesa nyingi zinazotakiwa kwenda kwenye miradi ya kiislamu, pesa zikitoka hutoka za waislamu kumbe wanapewa Bakwata wanazipiga hahaha, always huwa nafikiria kwenye huu mtizamo maana sioni cha maana wanachofanya zaidi ya blah blah, wao husema ni chombo cha waislamu, waislamu kwenye mambo gani?...Taasisi nyingine za kidini athari zao zinaonekana wazi kabisa Wana vitu vinavyoweza kusaidia jamii, Bakwata utawaona kwenye mambo ya mwezi sijui umetoka Zanzibar nk.. Nadhani Wana ofisi Kila mkoa na wilaya, tija Haionekani zaidi ya kualikwa kwenye sherehe au vikao kupiga Dua na Kula ubwabwa.
 
mnashangilia lkn hamjui kwamba you are creating a monster, bakwata ndiyo chombo pekee kinachoweka muslims at bay, wakiua bakwata kitakachofwatia ni islamic state, and believe me kama wewe ni Christian basi haujui unachoshangilia.

punchline, muslims hasa hawa wa third world countries hawaioni dunia jinsi ninyi mnavyoiona, muslims wako vitani against the so called ''mfumo Kristo'', na bakwata is standing in the way, wakiondoa bakwata kinachofwatia ni jihadists na caliphate mpaka mwisho hata kama yakibakia majivu, shehe ponda anapigania uislamu na kamwe hapiganii demokrasia kama mnavyojiaminisha ila yuko na nyie kwa sababu anaweza kuwatumia kama daraja tu lkn hana lengo lolote la kuleta katiba wala haki kwa wote, kama hamuamini mpeni ofa ya kuwa na mwanachama wa chadema halafu muone kama atakubali, kuna sababu kwa nini yuko cuf au act.

be careful with what you wish for, alisema wise man ....
 
mnashangilia lkn hamjui kwamba you are creating a monster, bakwata ndiyo chombo pekee kinachoweka muslims at bay, wakiua bakwata kitakachofwatia ni islamic state, and believe me kama wewe ni Christian basi haujui unachoshangilia.

punchline, muslims hasa hawa wa third world hawaioni dunia jinsi ninyi mnavyoiona, muslims wako vitani against the so called ''mfumo Kristo'', na bakwata is standing in the way, wakiondoa bakwata kinachofwatia ni jihadists na caliphate.

be careful with what you wish for, alisema wise man ....
Safi kabisa
Naona umetupata vizuri sana
Hapa hakuna kulala
Wazungu huko wanasherehekea krismas roho mkononi
Globalise the Intifada
 
Ukombozi mzuri. Sasa twende na kwenye mpira wa miguu, mbio na sehemu zote ambako kuna umonopoly wa kihuni. TFF isimamie mpira wa waliohiari kuwa chini ya TFF. Mi nikianzisha ligi na sitaki kuwa kwenye chain ya TFF-CAF-FIFA nianzishe.
 
Hata hamjaelewa maamuzi BAKWATA kosa lao ni kutaka kila muislamu anapotaka kufanya jambo lake labda kuanzisha Taasisi yake lazima aanzie bakwata ambalo sio jambo sahih Bakwata ni taasis kama taasis nyingine zilizosajiliwa...

Katika suala la amani ya nchi hii na kinachoendelea kupambana na huu udini unaondelea ktk hii nchi waislamu wote msimamo wao ni mmoja kaeni mkilijua hili wagalatia...
Hiyo vita ipo wapi na ipo kwenye nini? Maana siono chochote tangile, zaidi watu wanabwabwaja tu wakishashiba kande
 
Tena ingekuwa ni jambo hema kama waislam wasuni wangeikataa BAKWATA ili waanzishe taasisi yao badala ya hii BAKWATA jumuia ya CCM. Waislam wasuni wanatakiwa wao wenyewe kuanzisha taasisi yao inayoendana na imani yao na itakayokuwa chini yao kuliko hii iliyoanzishwa na TANU/CCM ambayo kwa kweli inamsikiliza mmiliki wake, yaani CCM. Kwa hali ya sasa ambapo CCM.imeamua kwa nguvu zake zote kumtumikia shetani, na hizi taasisi zake zote, UVCC, UWT, BAKWATA, Jumuiya ya wazee, zote zinalazimika kumtumikia shetani.
 
Leo waislam wameshinda kesi waliofungua dhidi ya BAKWATA kujipa mamlaka ya kuwaongelea waislam na kukwamisha miradi Kwa ukiritimba ati wao ndo watoe vibali Kwa taasisi zingine za kiislam

Shehe Ponda amesema mahakama katika hukumu hiyo, mahakama imeitamka kuwa BAKWATA sio taasisi inayosimamia Waislam wote Bali wale waliohiari kuwa chini ya taasisi ya BAKWATA

Pia Shehe Ponda ameahidi kuandaa kongamano kutoa elimu juu ya umuhimu wa hukumu ya Leo Kwa waislam
Assalam Alyekum
=============
Kufuatia hukumu ya Mahakama Kuu, Masijala ya Dar es Salaam, iliyotolewa leo Desemba 24, 2025 imebainishwa rasmi kuwa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) si chombo kinachowakilisha Waislamu wote nchini. Katika uamuzi huo, Mahakama imerejea Katiba ya BAKWATA yenyewe ambayo inatambua dhehebu moja pekee la Ahlus Sunnah Wal Jama’ah (maarufu kama Sunni).

Uamuzi huu unaliweka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) katika hadhi sawa na vyombo vingine vya kidini, kama vile Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC). Hii ina maana kuwa madhehebu mengine ya Kiislamu, yakiwemo Shia, Ibadhi, Salafi (Mawahabi), na Ahmadiyya, kisheria hayatabanwa tena na mamlaka ya BAKWATA katika kujisimamia. Madhehebu haya sasa yana uhuru wa kisheria kuratibu mambo yao yenyewe, ikiwemo kutangaza mwandamo wa mwezi kwa ajili ya kuanza au kumaliza funga, kusimamia masuala ya ndoa, talaka, na mirathi, pamoja na kupata uwakilishi wa moja kwa moja katika shughuli rasmi za kijamii na kiserikali. Aidha, uamuzi huu unazipa taasisi hizo uwezo wa kusajili jumuiya zao bila kuhitaji ridhaa au udhamini wa BAKWATA kama ilivyokuwa hapo awali.

Kwa maelezo rahisi, kama ambavyo Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) hutoa matamko kwa niaba ya waumini wa Kanisa Katoliki pekee, ndivyo BAKWATA inavyopaswa sasa kutoa matamko kwa niaba ya Waislamu wa Sunni. Jambo linalobaki kuwa swali la msingi ni ikiwa BAKWATA italazimika kubadili jina lake ili liendane na uhalisia huo wa kisheria, kwa kuitwa Baraza la Waislamu wa Kisunni Tanzania au Baraza Kuu la Masunni Tanzania, ili kuondoa mkanganyiko wa uwakilishi wa Waislamu wote nchini.
View attachment 3520003
Hii ni habari mbaya sana kwa CCM, chawa wao(jumuia yao) kakatwa mapembe.
 
Back
Top Bottom