Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge

Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge

Hizi ahadi ambazo mnatutangazia kila siku halafu hatuoni mnachofanya mmetuchosha sana ccm.naomba kuanzia sasa msitangazie wananchi nyie fanyeni tu kimyakimya tutaona tu.
 
Akili za kuambiwa changanya na za kwako
 
Katika hali inayoonyesha kukabiliana na msongamano katika Jiji la Dar es Salaam, jana Dk.Magufuli ameshuhudia hafla ya utiaji saini Mkataba wa Muhtasari wa Majadiliano ambapo Serikali ya Korea ya Kusini watafadhili ujenzi wa daraja jipya pembezoni na lile la Selander.

Waziri wa Ujenzi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu ujenzi wa daraja lenye urefu wa kilometa 7.5 litakaloanzia eneo la Aghakani na kuishia Coco beach, ujenzi huo unaotarajiwa kuanza mapema mwakani na unafadhiliwa na Serikali ya watu wa Korea Kusini ,lengo ni kupunguza msongamano wa magari katika daraja la Selander.



1.jpg
Waziri wa Ujenzi Dkt.Magufuli akionesha sehemu ambazo daraja hilo jipya litakapojengwa pembezoni mwa daraja daraja Selander kuanzia hospitali ya Aghakan hadi barabara Kenyatta. Sehemu ya Daraja hilo pekee litakuwa na urefu wa kilomita 1.03
2.jpg
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt.Servacius Likwelile akiwa na ujumbe kutoka Serikali ya Korea Kusini pamoja na Wizara ya Ujenzi mara baada ya kusaini Mkataba wa Muhtasari wa Majadiliano.

3.jpg
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt.Servacius Likwelile kulia akimushukuru Waziri wa Ujenzi Dkt.Magufuli mara baada ya hafla ya utiaji sahihi
4.jpg
Tukio la utiaji sahihi likiendelea

5.jpg
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Mhandisi Patrick Mfugale akionesha mchoro wa nguzo kubwa za daraja hilo litakalopita baharini pembezoni mwa daraja la Selander huku waziri Magufuli na Katibu Mkuu wake Mhandisi Mussa Iyombe wakifuatilia.
6.jpg
Dkt.Magufuli akifafanua jambo kuhusu ujenzi wa daraja hilo.​
 
wameamua kujiwekea huko mjini ili wapite kwa raha,unaacha kuweka fly over bugurun tazara,mawasiliano river side kimara baruti shekilango unaweka huko mjini tu.
 
Yaani hii serikali ndio typical ya mifano ya vitabu vya literature z post independence, yaani wanajifikiria wao tu wa Obay na Masaki, 2015 ifike haraka.
 
Wamekopa tena ili kujenga dar wakati kuna barabara za mikoa/wilaya hazina lami,mikoani hospitali ni mbovu kupita maelezo lakini wao wanajenga dar tu kana kwamba matatizo ya watz ni dar ..nakumbuka Jk aliahidi meli mpya Kagera yenye thamani ya 40bn lakini mpaka leo si pesa wala meli ambacho wamekifanya juu ya meli hii na hivi juzi imezimika ziwani kwa masaa 6 watu wakiwa majini,hiyo haingolewi ila wako busy na kujenga dar kuwaonesha wazungu eti Tz nzuri wakati mikoani umaskini wa kutisha ..kwa hali hii ndo maana naunga mkono sera ya majimbo ili maendeleo yafike kote kuliko kuichuma mikoa alafu kodi zote ziishie dar
 
Dar itakuwa nzuri sana

Jiulize kwanini lijengwe Aga Khan mpaka Coco..? Kwanini lisijengwe mpaka Kunduchi ili kusaidia maelfu ya Wakazi wanaopoteza muda wao kwenye foleni..

Hilo Daraja nilapitisha Vigogo na mafisadi wanaoishi Masaki..
 
Wamekopa tena ili kujenga dar wakati kuna barabara za mikoa/wilaya hazina lami,mikoani hospitali ni mbovu kupita maelezo lakini wao wanajenga dar tu kana kwamba matatizo ya watz ni dar ..nakumbuka Jk aliahidi meli mpya Kagera yenye thamani ya 40bn lakini mpaka leo si pesa wala meli ambacho wamekifanya juu ya meli hii na hivi juzi imezimika ziwani kwa masaa 6 watu wakiwa majini,hiyo haingolewi ila wako busy na kujenga dar kuwaonesha wazungu eti Tz nzuri wakati mikoani umaskini wa kutisha ..kwa hali hii ndo maana naunga mkono sera ya majimbo ili maendeleo yafike kote kuliko kuichuma mikoa alafu kodi zote ziishie dar

Mkuu umenena.
Siku hizi Tanzania inaangaliwa kwa jicho la kutokea Dar huku kwingine sio kipaumbele ndio maana hata wabunge karibu wote waaishi huko kwani huku kwetu hakuna "maisha"

Nilikuwa natoka Bukoba siku ile meli ya Mv Victoria ilipokaribia kuzama, abiria hawakupewa maelezo ya nini kitafuata baada ya meli kupatahitilafu huku wengine wakitakiwa kufika mwaka siku ya Jumapili kwa ajili ya kupanda dge saa 1.30 asubuhi.

basi nililopanda tulikuwa na abiria kadhaa ambao walilazimika kuingia gharama nyingine ya kubadili usafiri lakini basi hilo, lilipata hitilafu mara kadhaa na tukafika kivuko cha Busisi saa tano kasorobo usiku, ambapo tuliambiwa hatuwezi kuvuka kwa kuwa muda wa kufanya kazi umekwisha!

Jitihada za kuwashawishi hazikufanikiwa na tukalazimika kulala Busisi, kwa kushindwa kuvuka katika eneo la umbali wa sio zaidi ya kilomita moja, leo tunaambiwa huko "Mjini" kunajengwa daraja lenye urefu wa Km 7.5. Tanzania!
 
Hivi daraja la bahari ndo lina flyover? kwa hiyo na lile kigamboni ni flyover????????
Jana nilimsikiliza kwa makini na kugundua hana tafsiri sahihi ya daraja na "flyover"hata kule kigamboni amesema kutakuwa na "flyover" tatu
 
Magufuli.jpg


Nimeiangalia hiyo picha kwa makini na kugundua kuwa anapo panyooshea kidole ni Oyesterbay pale kwenye mbuyu kafara. Kwa maana hiyo hiyo fyover or whatever it is itaanzia Agha Khan mpaka mwanzo wa Coco Beach kupitia hapo mbuyu kafara.
 
Magufuli.jpg

Magufuli amesema Serikali katika kupambana na foleni Jijini dar es Salaam wameamua Kujenga flyover maeneo ya daraja la salenda. Kasema daraja lililopo halitabomolewa bali daraja jipya litajengwa upande wa baharini.

Kasema mkataba wa awali umeshasainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Korea tayari kwa maandalizi ya Kujenga.

Daraja litakua na urefu wa zaidi ya km7.

Magufuli akiongea na TBC1 alisema;
Mia

Umbali wa Selander hadi COCO sio 7km, kuna makosa ya namba hapo, labda 700m, maximum pale ni 1km.Gharama haziwezi kuwa kubwa sana kwa kuwa pale hakuna kina kirefu.hivyo nguzo ambazo ndio sehemu kubwa ya gharama za daraja hazitakuwa ndefu sana.
 
Nimeshangaa sana.Siamini kama Magufuli amefanya tathmini ya kutosha kujua kama hili daraja litakuwa na tija.kutoka Aghakan hadi Cockcock beach maana yake ni kwa wale wanaoelekea Masaki,Osterbay kidogo na Msasani kidogo. Sasa kwa kiasi cha mabilioni zaidi ya 100 sioni tija yake.
Lakini kwa kutengenezeka wakorea hilo daraja la km 7 kwao ni kazi ndogo mno.Korea kuna hadi daraja la km 20 na hili daraja limeshikiliwa na nguzo ndefu za kimo cha mita 70.hayo ya km 7,2,4,6 ni kitu cha kawaida sana kwa kuwa kule ni nchi ya vimilima.
Kwanza miradi ya kitanzania huwa ya kukurupuka, pili, nilidhani kama kusudio lilikuwa ni kuondoa foleni "basing kwenye hoja yako kuwa huu mradi ni mdogo sana kwa wakorea japo sijajua ni kwa nini" basi serikali ingefikiria hio flyover ingeanzia kwenye makutano ya Barbara za Mandela na Kilwa na ipitie huko huko baharini na utokee hapo aghakhan hadi huko Toure Drive/ koko beach, kwa mradi huu naona kama umekusudia kuwa favour watumishi wa magogoni wawahi majumbani kwao,Tatu, jana saa 2 usiku TBC walisema huyu mradi unafadhiliwa na Korea Kaskazini ila vyombo vingine vinasema Korea kusini.
 
Uhai ndio utakaojenga Flyover?

Na hilo ndo sulujisho la foleni dar?

Nchi hii ina viazi vingi sijui kwanini tusiviuze china na uturuki.

Unakuza maneno
Mimi nimeandika kuwa
IPo siku tutapita hilo daraja, muhimu uhai, ikiwa na maana kuwa bila uhai hatutapita hapo hata kama likijengwa

Wameongelea foleni pale Salender na sio Dar nzima

Wewe ni mmoja wa hao viazi
 
Umbali wa Selander hadi COCO sio 7km, kuna makosa ya namba hapo, labda 700m, maximum pale ni 1km.Gharama haziwezi kuwa kubwa sana kwa kuwa pale hakuna kina kirefu.hivyo nguzo ambazo ndio sehemu kubwa ya gharama za daraja hazitakuwa ndefu sana.
Mkuu daraja Litaanzia maeneo ya coco beach hadi mataa ya agha khan. Mia
 
Back
Top Bottom