Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge

Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge

Magufuli.jpg

Magufuli amesema Serikali katika kupambana na foleni Jijini dar es Salaam wameamua Kujenga flyover maeneo ya daraja la salenda. Kasema daraja lililopo halitabomolewa bali daraja jipya litajengwa upande wa baharini.

Kasema mkataba wa awali umeshasainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Korea tayari kwa maandalizi ya Kujenga.

Daraja litakua na urefu wa zaidi ya km7.

Magufuli akiongea na TBC1 alisema;
Mia

HAPA ANAONGEZEA shiidda tu sidhani kama ndio ametatua tatizo. iangalie hiyo picha yake vizuri tu afu piga picha tu hiyo daraja linapoanzia na linapoishia na pia piga picha msururu kutoka ALIHASAN MWINYI RD changanya na msururu unaotokea OCEAN ROAD yote hii ije ikutane ni hilo daraja jipya inamaana ameongezea kipande kingine cha msururu wa foleni ambazo ndio ziatkuja kukutana hapo kwenye makutano na njia ya zamani karibia kwenye mataa ya kuelekea kinondoni. je huoni kuwa hapa kaongeza msongamano mkubwa zaidi??
TUNAPATA HAYA KWA HISANI YA WAHISANI. maumivu yakizidi tutoroke hospitalini
 
Wakati tukiwa tunaongea na wadau mmojawetu akanitumoa picha hii kwamba linaweza kuwa hivi endapo likiwa kamili.
Nikawaza au ni.propaganda kuekwa 2015.
 

Attachments

  • 1416486976538.jpg
    1416486976538.jpg
    2.5 KB · Views: 239
HAPA ANAONGEZEA shiidda tu sidhani kama ndio ametatua tatizo. iangalie hiyo picha yake vizuri tu afu piga picha tu hiyo daraja linapoanzia na linapoishia na pia piga picha msururu kutoka ALIHASAN MWINYI RD changanya na msururu unaotokea OCEAN ROAD yote hii ije ikutane ni hilo daraja jipya inamaana ameongezea kipande kingine cha msururu wa foleni ambazo ndio ziatkuja kukutana hapo kwenye makutano na njia ya zamani karibia kwenye mataa ya kuelekea kinondoni. je huoni kuwa hapa kaongeza msongamano mkubwa zaidi??
TUNAPATA HAYA KWA HISANI YA WAHISANI. maumivu yakizidi tutoroke hospitalini

Na bado kuna daraja la kutoka Ocean Road kwenda Kigamboni, tuliwachagua wenyewe, hivyo tulinywe togwa hilo kwa uvumilivu.
 
Kuna mpango mwaka 3000 tujenge daraja kutoka dar hadi zanzibar na zanzibar hadi tanga.
 
Naomba NYINYI WASHAURI WA MAGUFULI. HEBU MSHAURINI HIVII... ILI KUONDOA TATIZO LA MISONGAMANO YA FOLENI MIJINI. AFANYE MAAMUZI MAGUMU YA KUPASUA BARABARA MPYA KATIKA MAENEO YA MJI NA KATIKATI. SERIKALI IKUBALI KUINGIA GHARAMA KWA KUVUNJA NYUMBA ZA WANANCHI ILI KUTENGENEZA NJIA MPYA. MFANO MMOJA KUELEKEA MBAGALA NJIA NI MOJA TU IKITOKEA BALAA BASI WATU HAWAJI MJINI. NASHAURI KUANZIA KONGOWE AMA MBAGALA YENYEWE IPASULIWE NJIA KUELEKEA UKONGA KUPITIA TANDIKA N.K. HII NI MOJA TU YA USHAURI.
YOTE HAYA YANAWAJIA KWA HISANI YA WAHISANI.
 
Wanaohusika nina imani washaandaa UTARATIBU wa kupanua matumbo ili escrow ichukue nafasi yake...
 
Ni bora wakaweka flyover mataa ya mwenge,ubungo na tazara.Maeneo haya yana impact kubwa kuliko surrender.Kama kawa ile ni barabara ya wakubwa masaki,obey wanataka wawe kivyao.
 
yaani tangu ameanza kuzitaja hizo flyover sijaona hata moja ambayo imeshaanza kujengwa walau kuchimba msingi tu. au jamani mtuambie, ile ya ubungo aliyosema je, ile ya TAZARA je, ile ya fire je?, ya magomeni je? sasa anasema ya salanda....wanatudanganya au nini, tell us mr magufuli why should we believe what you are telling us?....
kuna lingine wanataka kujenga dar hadi zenji
 
Mwala wameshindwa njia za SINZA nzuri tu kuboreshswatu wapite ukatengeneze daraja wajukuu siwatakwita mwizi jmn
 
Nimeshangaa sana.Siamini kama Magufuli amefanya tathmini ya kutosha kujua kama hili daraja litakuwa na tija.kutoka Aghakan hadi Cockcock beach maana yake ni kwa wale wanaoelekea Masaki,Osterbay kidogo na Msasani kidogo. Sasa kwa kiasi cha mabilioni zaidi ya 100 sioni tija yake.
Lakini kwa kutengenezeka wakorea hilo daraja la km 7 kwao ni kazi ndogo mno.Korea kuna hadi daraja la km 20 na hili daraja limeshikiliwa na nguzo ndefu za kimo cha mita 70.hayo ya km 7,2,4,6 ni kitu cha kawaida sana kwa kuwa kule ni nchi ya vimilima.

Haina tija kabisa. Yaani badala ya kujenga fly overs pale junction ya UN/ OCEAN/ A.H MWINYI ROADS na kutanua barabara, pia kujenga nyingine pale Morroco na Mwenge unafikiria kujenga daraja la km7 kwa sifa tu ambazo ni baseless kwa mahitaji ya sasa. Daraja la salenda kamwe halisababish foleni. Foleni iko kwenye makutano ya barabara pale njia za Ocean, Umoja Mataifa na Muhimbil na ile ya A. H.Mwinyi. Na pia pale kona ya Kinondon na Pale Mbuyuni. Kamwe daraja halijawa tatizo la foleni pale Ubungo( Riverside na UDSM) halijawa tatizo pale Matumbi, halijawa tatizo pale Jangwani. Matatizo ya foleni kubwa ni kwenye makutano ya barabara kubwa hasa: Ubungo, Tazara, Moroco, Tabata, Mwenge, Kamata, VETA- Chang'ombe, Buguruni, Namanga, nk.

Sehemu kubwa ya maeneo ambayo barabara ziko mbili mbili ndani ya jiji la Dar na hamna makutano( ukiondoa pale Mbagala na Ukonga- Banana, asilimia kubwa hapo ni upuuz wa kupaki vibaya daladala), huwa foleni hamna kabisa.
 
Ni sawa, ila naona hata barabara juanzia moroko waongeze upana hadi hapo salenda, ila la muhimu ni fly over ya tazara na ubungo, wajenge hizo kwanza, sio salenda, mbona tunaishia kuonyeshwa mapicha tu, tuone na kazi.
Barabara ya morocco - mwenge imeshapanuliwa. Ujenzi fly-over ya Tazara umepamba moto, wa-Japan wako kazini pale. Ujenzi fly-over ya ubungo design zimeshakamilika, Mwenge fly over itafuata inshallah..
 
Pesa zipo tena cash.Wanaoleta fyokofyoko kuhusu madawa hospitalini ninawaona.Waache wajifanye wamejificha nyuma ya keyboard.
Hapakazitu.
 
Utafikiri wanakaribia kwenda mwezini. Is that the only problem that cause traffic in this area?


Nadhani wangeweka kipaumbele kwenye city exit roads, sijui kama wanajua kuwa kutoka Ubungo hadi Kibaha huchukua zaidi ya two hours nyakati za jioni
 
Back
Top Bottom