Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge

Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge

Gharama zitakazotumika ni 100bil, mkopo wa "masharti nafuu" kutoka serikali ya Korea, hivi hayo masharti ni siri ya nani na nani? Halafu kamradi kama hako ni kweli serikali imeshimdwa kukafinance mpaka wakope kwa wahisani??

Kweli Mkuu kama watu wanaweza kupiga b300 si bora wangeziweka hapo. Hii ndo Tanganyika zaidi ya uijuavyo!!!!
 

Mkuu daraja Litaanzia maeneo ya coco beach hadi mataa ya agha khan. Mia

Agakhan hadi Oysterbay ni 1.2kms kwa kunyoosha moja kwa moja. ukisema uendelee hadi coco hazizidi 3 kms.Ukisoma maelezo wamesema kutakuw ana barabara mpya yenye km 7.2,ukitazama picha inaonesha barabara na sehemu ya kukatiza majini, hapo hakuna kina kirefu wala umbali mrefu, ni kama km 1 tu,na kwenda chini pale hakuzidi m30,hii ni kazi nyepesi sana.

Miaka ya nyuma walitakakupajaza udongo hapo wajenge waterfront, ule mradi sijui umeishia wapi.
 
Agakhan hadi Oysterbay ni 1.2kms kwa kunyoosha moja kwa moja. ukisema uendelee hadi coco hazizidi 3 kms.Ukisoma maelezo wamesema kutakuw ana barabara mpya yenye km 7.2,ukitazama picha inaonesha barabara na sehemu ya kukatiza majini, hapo hakuna kina kirefu wala umbali mrefu, ni kama km 1 tu,na kwenda chini pale hakuzidi m30,hii ni kazi nyepesi sana.

Miaka ya nyuma walitakakupajaza udongo hapo wajenge waterfront, ule mradi sijui umeishia wapi.

Hahaa, eti waterfront.

Hivi hiyo barabara waliyoipa jina la Obama wameweza kui protect isimomonyolewe na bahari kwanza?
 
Naona maneno mengi na maramani, Kukamilika sijui lini. TZ noma sana, Wale wawekezaji wa Kijapan wa kampuni ya Honda walitaka kuja na mkataba mkasaini wametokomea wapi?
 
Magufuli ni janga la taifa

Nehemia ni Janga la taifa

Ogopa mijitu aina hii inaoenda sifa tu...

Hawajui gharama za majaribio yao kwa taifa letu
 
Siamini kama kurundika kila kitu katika mji uliochoka vile ni sahihi. Magari yakishajaa mjini katika mji usiotoa fursa ya upanukaji wala usiokuwa na parking halafu nini kitokee.Kujenga hiyo baraba ni gharama kubwa sana kuliko kutawanya mahitaji ya watu ili wote wasiwe na uelekeo mmoja kunapokucha na pia uelekeo mmoja inapofika jioni.Wizara zote zitoke mjini ikiwezekana zihamie Dodoma kama haiwezekani katika mji mpya wa kufikirika Luguruni. Reli ifufuliwe.Bandari za Tanga na Mtwara ziongezwe uwezo Dar kutakuwa kuna magari yenye kuhitaji hiyo flyovers kweli baada ya kivuko cha kwenda Bagamoyo kufanya kazi? Sijui kwa nini tunakuwa na hamu ya flyovers namna hii wakati si mahitaji yetu! Ama kweli hii ndio miradi bubu ya wazalendo
 
kwa hiyo daraja likipita juu ya maji ya bahari ni fly over?
 
Wadau haya ni maendeleo japo ni kwa taratiiiibu lakini safari bado inaendelea.
 

Attachments

  • 1416459453659.jpg
    1416459453659.jpg
    27 KB · Views: 671
Na hili ndo daraja jipya kwa mbaali kama unakuwa maeneo ya daraja zee la salenda na kupiga picha.
 

Attachments

  • 1416460983814.jpg
    1416460983814.jpg
    3.2 KB · Views: 910
Ni kweli maendeleo ila wanayataratibusha sana, after 50 years?Yaani nusu karne.

Renegade:
Unajua wanao taratibisha siyo wao ni upeo wa fikra za maendeleo to future days kwa wakati wao ndipo wanadhani na kuona wamechelewa sasa wakija kwenye bajeti kwa vitu kama hivo ndo wanakuta wamechelewa na kukimbilia kuomba misaada.
Kwani ili jipya lenyewe ni msaada kutoka serikali ya korea.
 
Renegade:
Unajua wanao taratibisha siyo wao ni upeo wa fikra za maendeleo to future days kwa wakati wao ndipo wanadhani na kuona wamechelewa sasa wakija kwenye bajeti kwa vitu kama hivo ndo wanakuta wamechelewa na kukimbilia kuomba misaada.
Kwani ili jipya lenyewe ni msaada kutoka serikali ya korea.
Mkuu naomba nifafanulie hapo kwenye nyekundu, ila mimi nachukia saana misaada na nafikri kuwa hii nchi inaendesheka bila misaada.
 
Mkuu naomba nifafanulie hapo kwenye nyekundu, ila mimi nachukia saana misaada na nafikri kuwa hii nchi inaendesheka bila misaada.


"UPEO WA FIKRA ZA MAENDELEO"
upeo unapokuwa uwezi panga kitu cha kesho na ndiyo maana unakuta jana/leo wanafikilia kupanua barabara ya Dar to Chalinze but matokeo ni miaka 20 ijayo. That's All Renegade.
 
Pale tazara + ubungo, vipi yako tayari? Na tren ya kisasa nilisikia mwisho wa mwaka itakuwa tayari!
 
Back
Top Bottom