Magufuli: Tutajenga flyover Salender Bridge

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,888
Magufuli.jpg

Magufuli amesema Serikali katika kupambana na foleni Jijini dar es Salaam wameamua Kujenga flyover maeneo ya daraja la salenda. Kasema daraja lililopo halitabomolewa bali daraja jipya litajengwa upande wa baharini.

Kasema mkataba wa awali umeshasainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Korea tayari kwa maandalizi ya Kujenga.

Daraja litakua na urefu wa zaidi ya km7.

Magufuli akiongea na TBC1 alisema;
Tuliwatuma wataalamu hawa, na bahati nzuri Chief Executive wa TANROADs hivi karibuni na wataalamu wenzake walienda South Korea.. Serikali ya South Korea imekubali kutufadhili kujenga flyover nyingine pale.. na barabara yenyewe itakuwa na urefu wa karibu kilomita 7.2 na barabara itaanzia Coco Beach, itapita baharini itakuja kutokea Agakhan Hospital na kuja ku-join na barabara nyingine hii ya Alli Hassan Mwinyi…"


".. Tumepanua maeneo pengine kote.. tuna mradi wa BRT ambao una-involve kilometa zaidi ya ishirini na moja na karibu sasa hivi unaisha chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia, lakini tunapofika pale Salenda pamekuwa na tatizo kubwa na kwa sasa hivi katika traffic count ya magari yanayopita pale kwa siku yamezidi zaidi ya magari hamsini na moja elfu kwa hiyo hawawezi wakaya-accommodate magari yote yanayoweza kupita sehemu hiyo.
Mia
 
Ni sawa, ila naona hata barabara juanzia moroko waongeze upana hadi hapo salenda, ila la muhimu ni fly over ya tazara na ubungo, wajenge hizo kwanza, sio salenda, mbona tunaishia kuonyeshwa mapicha tu, tuone na kazi.
 
Magufuli amesema Serikali katika kupambana na foleni Jijini dar es Salaam wameamua Kujenga flyover maeneo ya daraja la salenda. Kasema daraja lililopo halitabomolewa bali daraja jipya litajengwa upande wa baharini. Mia
Hizi ni porojo tu! CCM hawana jipya.
 
Kinachosababisha msongamano wa watu na magari Dar es salaam ni sera mbovu za CCM. Vijiji vimesahaulika. Hakuna fursa ya vipato kwa vijana huko vijijini. Hivyo, melfu kwa maelfu ya vijana kutoka kila kona ya Tanzania wanakimbilia Dar es salaam.

Halafu CCM wanakuja na porojo eti ya kujenga barabara kama suluhisho la msongamano. Huu ni ukame wa mang'amuzi.
 
Hiyo flyover atatumia nani wakati hapo itakapokamilika Watangayika wote watakuwa wameteketea kwa kukosa matibabu! Weka dawa hosipitali kwanza ndio ufikirie kujenga flyovers. This is another corruption and politically calculated project.

Magufuli amesema Serikali katika kupambana na foleni Jijini dar es Salaam wameamua Kujenga flyover maeneo ya daraja la salenda. Kasema daraja lililopo halitabomolewa bali daraja jipya litajengwa upande wa baharini.

Kasema mkataba wa awali umeshasainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Korea tayari kwa maandalizi ya Kujenga.

Daraja litakua na urefu wa zaidi ya km1. Mia
 
Nimeshangaa sana.Siamini kama Magufuli amefanya tathmini ya kutosha kujua kama hili daraja litakuwa na tija.kutoka Aghakan hadi Cockcock beach maana yake ni kwa wale wanaoelekea Masaki,Osterbay kidogo na Msasani kidogo. Sasa kwa kiasi cha mabilioni zaidi ya 100 sioni tija yake.
Lakini kwa kutengenezeka wakorea hilo daraja la km 7 kwao ni kazi ndogo mno.Korea kuna hadi daraja la km 20 na hili daraja limeshikiliwa na nguzo ndefu za kimo cha mita 70.hayo ya km 7,2,4,6 ni kitu cha kawaida sana kwa kuwa kule ni nchi ya vimilima.
 
Wabongo tunadanganywa kiraisi. Serekali ya CCM siiamini ahadi zake mpaka nione kitu kikifanya kazi. Hata daraja la kigamboni japo kunaaina ya ujenzi, siamini mpaka nitakapoona magari yanapita kwa mwaka mzima bila ajali maana inawezekana wamejenga kivuko cha bomba au umeme alafu wakatudangaya ni daraja la kuvuka magari. Usicheze na CCM na uchaguzi 2015 maana waweza kuaidi hata nyumba za bure
 
Magufuli amesema Serikali katika kupambana na foleni Jijini dar es Salaam wameamua Kujenga flyover maeneo ya daraja la salenda. Kasema daraja lililopo halitabomolewa bali daraja jipya litajengwa upande wa baharini.

Kasema mkataba wa awali umeshasainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Korea tayari kwa maandalizi ya Kujenga.

Daraja litakua na urefu wa zaidi ya km1. Mia

Hivi daraja la bahari ndo lina flyover? kwa hiyo na lile kigamboni ni flyover????????
 
Tazara ni shida kubwa lakini hawajapafikiria
Kwa kweli kama serekali yetu ingekuwa inasikiliza maoni ya watu nadhani wasingekuwa wanaingia gharama kubwa bila kuwa na impact ya wanachokifanya!! Ssasa najiuliza kwa nini wanaingia gharama kubwa kwenda baharini? Nchi Kavu Kumejaa!! Kupunguza msongamano wa kuingia Mjini ningewashauri waweke Daraja kutokeo kinondoni makaburini kuunga upanga na kuongeza ukubwa wa barabara maeneo ya upanga.
Upande wa sallender bridge Waongeze Upana wa lanes ziwe 3 na barabara ya barrack Obama iongezwe upana iwe na lanes 2 na kuwe na under pass
 
Gharama zitakazotumika ni 100bil, mkopo wa "masharti nafuu" kutoka serikali ya Korea, hivi hayo masharti ni siri ya nani na nani? Halafu kamradi kama hako ni kweli serikali imeshimdwa kukafinance mpaka wakope kwa wahisani??
 
Back
Top Bottom