Magufuli alipoinia madarakani kwa mjibu wa report ya BOT February 2016 Export Trade kwenye baadhi ya sector ilikuwa kama ifuatavyo Manufacturing $1.3 B,horticulture $960 M, Fish And Fish Products $402, Baada ya miaka 4 February 2020 Export. Manufacturing $794 M, Horticulture $167 M, Fish And Fish Products $155 M.
Ni miaka michache iliyopita niliwahi kushauri, nini kinaweza kufanyika.
Inawezekana mawazo yangu, hayakuwa perfect 100%, ila nilitegemea walau extracts za kilicho na tija zaidi mchakato wa kukifanyia kazi kwa haraka.
Tujikumbushe.
Wachumi wetu Hazina na BOT wanafanya nini kuiokoa shilingi yetu au mpaka Magufuli awape TOR ndipo “waamke” usingizini? - JamiiForums
Wachumi wetu Hazina na BOT wanafanya nini kuiokoa shilingi yetu au mpaka Magufuli awape TOR ndipo “waamke” usingizini? II - JamiiForums
Nguvu kubwa ya uzalishaji tukiamua kuifanya Tanzania ili kikidhi mahitaji ya soko la ndani na ku-export, hapo tutaotoba.
Fuatilia takwimu hapa chini, toka miaka ya '70 mpaka 2018; huko nyuma China hakuwa lolote, ila baada kuongeza uzalishaji na kuanza kuongeza exports, mbona tutapiga bao.
Wakati uchumi wa dunia umeanza kutikisika wakati wa COVID, mahitaji ya kuzalisha chakula duniani hayatakoma na soko lake lipo tu.
Ni wakati, BOT na hazina wakaacha kuja na analysis pekee; isipokuwa ni vema kuja na mfumo wa ku-guarantee investment projects zenye uhakika wa soko kubwa la ndani na nchi majirani.
Soko la Sukari lipo Tanzania na Kenya kwa zaidi ya tani laki 5. Hii mbona fursa nje nje.
Kuongeza uzalishaji wa alizeti, ufuta ili kuzalisha mafuta ya kula
Kuja na mkakati wa ku-process
Products kadhaa za pamba,
Products kadhaa za kahawa
Products kadhaa za korosho,
Products za kahawa
Pareto
Products kadhaa za Chai
Mchele
Unga mahindi
Asali
Nyama
Products za Ngozi
Products za samaki.
Vyote hivi tunaweza kuzalisha ndani kukidhi soko, na ziada tuka-export.
Waziri Mpango, chonde chote, hatuwezi kutumia njia za zamani kujenga uchumi wakati huu ambapo kila mmoja anapambana na hali yake.
Akili za kuzalisha na maandiko ya investment projects zipo, kuna projects zingine haziwezi kuhitaji fedha moja kwa moja toka local investment bank, zinahitaji Bank Guarantee tu toka BOT ili kujenga viwanda ambavyo pia zitatoa ajira.
Jamani, chonde chonde, huu sio wakati wa kutengena kifikra, ni wakati wa kufikiri pamoja na kuja na suluhisho la Tanzania bora kati ya Covid19 na baada ya Covid19