Mkuu maada yako ni tata sana! hasa ukidefine neno mamlaka na wajibu wa aliyepewa mamlaka! kama kwajibika kwa magufuli kwa mamlka aliyonayo ni tatizo then we have problem somewhere
Je unaweza kutoa mfano wa asiye na mamlaka na yet ni mpiganaji au mtetezi wa mali ya umma
Pili je ulitaka magufuli afanye nini bungeni ili aonekane kuwa anapigania haki na kufabya unavyotaka wewe?
Baada ya majibu hayo je ili uonekane mpiganaji lazima
1. uandike article sana
2. useme sana bungeni (kama mbunge)
3. Jamii yote ijue wewe ni mpiganaji?
Je wale wasio na nafasi ya kujulikana kwa vigezo utakavyoonyesha wanaweza kuwa wapiganaji?
Je unaweza kutoa mfano mmoja wa waziri mmoja wa sasa na serikali zilizopita ambaye ni mpiganaji from bungeni mpaka serikalini na OUTPUT yake imeonekana?
Magufuli ulivyo-m-rate umetumia standard gani? job descritption yake inasemaje?
cheers
mkuu, hapo kwenye red umenikuna hasaaaaa!Heshima Mkuu! Mimi nilivyomwelewa MM, ni vigumu sana kujua msimamo wa Magufuli, anasimamia nini hasa katika masuala ya kitaifa. sawa, anaonekana mchapa kazi sana, lakini so far ukipiga picha, anaonekana kufaulu akiwa katika madaraka tu. sasa MM amejenga hoja hapo, na binafsi nimeikubali. conclusion yake pia, kwamba kwa maana hiyo itakuwa ni vigumu sana Magufuli kujiuzulu, kwa sababu hawezi kusimama kama yeye na msimamo wake, aka-flourish. na hoja hii ya MM inakuwa urgent kwa sababu kama asemavyo MM, PM na JK wamemlima jamaa kisawasawa, kiasi kwamba unabaki unashangaa huyu jamaa bado yupo. nadhani kwa mtu mwenye msimamo hasa, alitakiwa ajiuzulu na kama ni mtu mwenye misimamo inayojitokeza kitaifa, bado anaweza kuwa relevant and effective katika kusimamia yale anayoyaamini katika taifa hili. ndivyo anavyofanya Dr. Slaa, kwa mfano. sasa hivi sio mbunge, lakini akisimama mahala akaongea, watu wanamsikiliza na serikali inatetemeka
Kiongozi anayeamini katika kanuni na sheria tunamhitaji katika nchi hii kwa sasa. Nchi yetu haihitaji kiongozi wa kuwafurahisha watu bali mwenye 'discipline, vision, goals and action'.
Binadamu tumetofautiana sana.kuna watu wanaweza kuhoji wakiwa tu hawana madaraka pindi wakiyapata huwA KIMYA.kuna watu wengine huwa kinyume chake.Nafikiri hapa cha msingi ni je alikuwa sahihi kwenye yale aliyofanya akiwa madarakani?kama alikuwa sahihi apongezwe kama hakuwa hivvyo atalaumiwa.
Kuhusu kufuata sheria, kwa kuwa anatambua kuwa watanzania wengi wana kiu ya kuona sheria zikifuatwa basi Magufuli hutumia kauli mbiu hiyo kujipigia chapuo lakini ukichunguza kwa makini yeye sio muumini mzuri wa utawala wa sheria na kanuni za utawala bora.
Ndugu MM, topic yako hii, inaweza kukuweka mahali pabaya hata wewe, kwa sababu inaonekana kama kumjadili mtu. Tukumbuke kuwa simple minds discuss people... .
a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.
b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.
Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:
a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.
b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.
my two cents plus the other fifty
Magufuli sio kiongozi wa Principle, na hii imejidhihiriasha sasa. Magufuli ni kama robbot unaliprogram halafu linafanya kazi kulingana na ulivyo liprogram, nasema hivyo kwa sababu kila wizara anayoenda anakariri sheria na miongozo yake na kuanza kutekeleza bila kuipa nafasi akili yake kupambanua. Na ndio maana nje ya uongozi hana kitu anachoweza kufanya. Hana principle zake anazozisimamia.you are right absolutely! Na mimi ni miongoni mwa watu ambao nilikuwa ninaamini Magufuli ni kiongozi wa principle... lakini hili bado linanisumbua.
Waberoya, umetoa maswali na hoja nzuri. Hatujatenda haki kwa huyo jamaa anayejaribu kutumikia jamii. Tena kuna kitu ambacho kimeniuma sana...yaani mtu anaomba kwa raisi aruhusiwe kutekeleza majukumu na sheria alizoapa? Yaani kutenda haki na wajibu sasa hivi mpaka ulambe miguu ya kiongozi wa mfumo unaotawala??? Hii ni hatari na hapo lazima nguvu itokayo juu iingilie kati
Magufuli sio kiongozi wa Principle, na hii imejidhihiriasha sasa. Magufuli ni kama robbot unaliprogram halafu linafanya kazi kulingana na ulivyo liprogram, nasema hivyo kwa sababu kila wizara anayoenda anakariri sheria na miongozo yake na kuanza kutekeleza bila kuipa nafasi akili yake kupambanua. Na ndio maana nje ya uongozi hana kitu anachoweza kufanya. Hana principle zake anazozisimamia.
Kimsingi hii inaonyesha kwa namna fulani viongozi anaowatumikia JPM hawana imani nae au hawakubaliani na jinsi anavyo endesha mambo yake, inapofikia kwamba kiongozi wako anaonyesha kutokubaliana na wewe hadharani ina maana aliisha kaa na wewe pembeni akakushauri na hukusikiliza ushauri wake. Sitaki kuamini kwamba JK na PM waliamua kumkosoa hadharani bila kuwa waliisha kaa nae na kumpa muongozo wao, huenda anachofanya JPM sicho walichokubaliana kwenye baraza la mawaziri na vikao vyo vingine na hivyo wameamua kumtolea uvivu hadharani. Kama kweli JPM is the man of principle ilibidi awaachie wizara yao, ili asije akaongo wizara kinyume na kile anacho amini.sn2139 - ndio maana naamini ya haya maswali na uchokozi wangu hapa.. of course tunajua mawaziri wanafanya kazi at the pleasure of the president.. kwa hiyo upande mmoja ni kuwa ili aweze kuendelea kuwa madarakani na kufanya anayotaka hana budi kulamba miguu ya bosi wake. Swali langu ambalo ndio msingi wa hoja (natumaini Waberoya naye ataliona) ni kuwa viongozi hawa wanapotofautiana hivi ni nani ajiuzulu on principle? Swali langu halihusiani na upiganaji n.k linahusu kutawala na kuwabika kama kiongozi pale tofauti za msingi zinapotokea.
Swali linakuja hivi: Je ni kazi yake kwenda frontline na kusimamia kama afanyavyo? Je katika kusimamia sera ( pamoja na Sheria) huyu waziri angeweza kuwa tofauti kiutendaji na akawa na tija? Kuna nafasi ipi itakayomwezesha kutenda effectively nje ya 'madaraka" yake?( madaraka ilivyotumiwa na MMKJJ ni sawa na mandate?)
Ninacho zungumzia ni kwamba nje ya madaraka hajawahi kuwa mwanaharakati/mkereketwa katika kuonyesha kuisukuma serikali iendeshe mambo kulingana na sheria zakeHapo kwenye bold, naomba ufafanue.
Nijuavyo mimi, Waziri ana majukumu 1. Kusimamia sera za serikali iliyomweka madarakani 2. Ni political commissar hivyo anasimamia sera za chama na ilani ya uchaguzi ya chama chake. Ina maana hawezi kutenda nje ya mandates hizi.
Swali linakuja hivi: Je ni kazi yake kwenda frontline na kusimamia kama afanyavyo? Je katika kusimamia sera ( pamoja na Sheria) huyu waziri angeweza kuwa tofauti kiutendaji na akawa na tija? Kuna nafasi ipi itakayomwezesha kutenda effectively nje ya 'madaraka" yake?( madaraka ilivyotumiwa na MMKJJ ni sawa na mandate?)
Dr. Magufuli atakumbukwa kwa misimamo ya KIJINGA eti anasimamia SHERIA kwa kuwafanya watu wazidi kuwa mafukara...tayari zaidi ya nusu yetu tunatumia CHINI YA DOLA MOJA kwa siku.....anampango sasa tutumiae CHINI YA NUSU DOLA kwa siku....
Kwa maelezo uliyoyatoa,he will make a good president pindi tukishabadili katiba...Kwasababu ameonyesha sifa nzuri ya usimamiaji wa sheria,then tubadili katiba halafu kama atasimama kwa sera nzuri,then he will make a good contender for presidency.Good kwa maana ya good for the country.Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?
Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?
Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?
Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?
Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?
Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:
a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.
b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.
Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:
a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.
b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.
my two cents plus the other fifty
Magufuli bado namfagilia kwa ushupavu wake wa kusimamia sheria kwa vitendo. Suala la je, anapokuwa hana madaraka yukoje, to me is irrelevant. Kwani kuna mijitu ndani ya serikali ya kifisadi ya ccm imepewa madaraka yote lakini imekaa kimya na kuacha nchi inachezewa kama haina mwenyewe. Kikwete anamweka magufuli madarakani kwa kinyongo.
Anachoogopa ni kunyoshewa vidole na watanzania endapo ataamua kumwacha kwa sababu utendaji wake wa kazi hakuna mtanzania asiyeujua. Aliwahi hata kumtia ndani kiongozi mmoja wa ccm kwa kukutwa na kokolo ya kuvulia samaki kwenye bwawa la nyumba ya Mungu.
a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.