Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Maskini Magufuli ana nia njema sana na nchi hii tatizo sijui ni mbinu anazotumia au ni wanaomshauri binafsi kuna vitu namuelewa sana ingawa hili la uhuru wa vyombo vya habari simuelewi kabisaaaaa
****
NINGEKUWA MAGUFULI VYOMBO VYA HABARI NINGEVIPA UHURU ZAIDI NA ULINZI MAALUM, MAANA NDIVYO VINAVYOFUNUA UOVU ULIO CHINI KABISA / AU KUJIFICHA.

unless otherwise tunashindwa tambua dhamira yake ya ndani.
 
Ili uthibitishe haya maneno yako kuwa Magufuli kachuja au lah nenda mtaani alafu ukikuta kikundi cha watu tamka haya maneno kuwa "Magufuli hafai".. Kitachokutokea kutoka kwa wananchi usisite kuja kutuambia ata kama ukiwa ICU.

Huko kitaani kwenu kwa washua nini?
 
Mwanzoni mwa utawala wake ilikuwa kila gazeti linamwandika yeye tena vizuri. Vijiwe vyote kuanzia vya kahawa, daladala, bar na maofisini story alikuwa ni yeye tena watu wakimsema kama malaika mkombozi.

Ghafla upepo ukabadilika, watumishi wakaanza kukosoa utumbuaji majipu, wafanyabiashara wakakosoa mbinyo wake kwenye kodi, wanasiasa wakahoji style yake ya uongozi. Wananchi wa kawaida wakanigwa na maisha magumu (ingawa hawa bado wamebakiza kaimani fulani). Vyombo vya habari wanalalamikia kuminywa uhuru wao.

Kiujumla upepo unavuma vibaya kwa JPM naye ameshakiri ugumu wa kiti chake mpaka akasema angejua asingegombea urais. Je, rais wetu amekosea wapi mpaka hali imegeuka mapema hivyo?

Nafuatilia kauli ya Nyerere ya Makabila ambayo hayawezi kushika urais Kama ilikuwa ya kweli. Mojawapo lilikuwa ni hili la Huyu Jamaa.
 
Mbona mtoa post na wachangiaji hamjielewi? kwa miezi 7 aliyoyafanya ni makubwa sana, lakini ni muda mfupi kubadilisha nchi na watu kufaidi au kupata ahueni ya maisha, halafu budget ndo hiyo kwanza hata haijapita mmeanza kelele, kumbukeni wafanyabiashara pia wanataka kua juu ya serikali kwa kuficha sukari ili wajipangie bei, JPM bado anajipanga kwa mambo mengi , utumbuaji ( kuwasimamisha watu Kazi) lazima iwe kazi endelee mpaka tuheshimiane.
 
Mlilipwa kumshambulia JPM kipindi cha kampeni mkashindwa,mlivyo na akili fupi mnadhani mtafanikiwa na mtu ameshakuwa Raisi??,kweli akili zenu fupi sana,ndo maana Mzee Mkapa aliwaita WAPUMBAVU NA MALOFA.,ndo maana Mlikuwa mkizungusha mikono kama wendawazimu,nimeanza kuelewa.

Povu la nini? Si ujibu tu hoja kisha jenga hoja ya kutokubaliana na hoja hiyo kwamba Rais wetu mtukufu utukufu wake na sifa zinazidi kupanda juu na si kushuka? Kadiri unavyotukana unaonyesha udhaifu wako
 
Mbona mtoa post na wachangiaji hamjielewi? kwa miezi 7 aliyoyafanya ni makubwa sana, lakini ni muda mfupi kubadilisha nchi na watu kufaidi au kupata ahueni ya maisha, halafu budget ndo hiyo kwanza hata haijapita mmeanza kelele, kumbukeni wafanyabiashara pia wanataka kua juu ya serikali kwa kuficha sukari ili wajipangie bei, JPM bado anajipanga kwa mambo mengi , utumbuaji ( kuwasimamisha watu Kazi) lazima iwe kazi endelee mpaka tuheshimiane.
....

.....njaa haina simile !!!
 
Dhulma ndo inamtafuna, na itaendelea kumtafutana hadi akwishe kabisa!
 
Hizi story nyingine nafikiri hapa sio mahali pake, hii ipeleke kijiweni kwenu utapata majibu haraka sana
 
Tatizo ni kuwa ameshindwa kufanya kazi kimfumo zaidi ya ziara za ghafla sasa zikikosekana anaonekana kama yupo hayupo. Ziara za ghafla ndio zimemtambulisha na yeye kajitambulisha nazo. Hivyo ni lazima aendelee kufanya ziara za ghafla ili watu wajue yupo shida ni kuwa sehemu za kwenda ghafla zikikosekana hapo itakuwa ni shida itabidi aanze hata kwenda mikoani
 
Kwa mjadala mzuri naomba unapochangia, jikite kwenye hoja sio kujikita kwenye itikadi za vyama. Mheshimiwa Magufuli Ni rais WA wote, akifanya vyema sote tunanufaika, ikitokea amefanya vibaya huwezi kukwepa sehemu ya matokeo hayo.
Lengo ni kutaka kuwa na nchi ambayo kila mmoja anatimiza majukumu na wajibu wake.
 
Back
Top Bottom